Barua ya wazi kwa Mkuu wa Mkoa Tanga

Deshbhakt

JF-Expert Member
Jan 22, 2008
375
189
Kwa niaba ya rafiki wangu huko Tanga na-share hii uzi

Barua wazi kwa mkuu wa mkoa tanga.

Mheshimiwa mkuu wa mkoa Tanga,

Ni kwa masikitiko makubwa tunakueletea malalamiko dhidhi ya club ya Ben Bistro hapa wilayani Tanga, kati ya mtaa wa Ekcenforde na ring - Guinea Street

Club hii iliyoanzishwa miaka miwili ilioypita inaendelea kututesa kwa kuleta mazingira ya mateso mengi sana kwa sisi tunaoishi kwenye maeneo haya! Tabia za kihuni kwa kucheza muziki hadi usiku wa manane pamoja na wateja wao kuhudumiwa pombe kwenye magari zao barabarani na kukutwa wamesinzia hadi asubuhi pamoja na kutoa huduma za shisha, wadada wanauza mwili zao pia wapo na kufanya mambo zao kwenye magari n.K asubuhi hukosi kuona machupa za pombe barabarani au kwenye mataro na ukuta zinanuka na mkojo.

Huo mtaa unatumika sana na wanafunzi wanaopita kuelekea mashule mengi zilizo jirani na huwa wanashuhudia haya mazingira kila siku. Pia kuna kanisa na misikiti mawili na waumini wengi nao wanashuhudia haya matatizo.

Siku ya jumamosi tarehe saba mwezi huu wamezuia mabarara nne za mitaa na kufunga jukwaa. Jumapili kuanzia saa 11 jioni wameanza tamasha ya bendi iliyoendelea hadi 12 alfajiri.

Mheshimiwa, sisi tulishindwa kupumzika kabisa maana kelele ilikuwa mkubwa mno na hadi vitu vya ndani, ufa n.K. Za manyumba zetu zilikuwa zinatetemeka.

Mara nyingi asubuhi waumini waonaoelekea msikitini wamekuta watu wameelewa na kulala juu ya meza, kwenye magari na chupa za pombe zimetupwa barabarani.

Mwenyekiti wa mtaa naye hataki kutusaidia na insemekana biashara zake ni kukodisha vifaa wa bendi na vilitumika siku hiyo. Mwenye hiyo biashara aitwaye beny nae inasemekana kuwa anafahamia na 'viongozi wa juu' na hakuna atakaemsumbua?

Je hii ni haki? Mtaa wetu miaka nenda nyuma ilikuwa na utulivu na heshima wa hali ya juu ila leo hii tunateseka sana.

Tafadhali angalia video hizi.

Mheshimiwa, tunakuomba utusaidie.


 
Sema uandishi huu si wa kufika kwa mkuu wa mkoa. Acha watu waburudike maana ndo tulizo lao. We mtu analala kwenye gari, familia anayo kweli?
 
Sidhani kama ni uungwana kupiga makelele kwenye makazi ya watu, tunashida sana Tanzania hivi sasa na hizi pubs, clubs na mabar mitaani kwenye makazi ya watu.

Ufuska, Ulevi nk hufanyika kwenye macho ya watoto na watu wengine wenye imani zao, Kuna haja kuwa na maeneo maalum kwa ajili ya hizi Starehe.

Binafsi naijua Tanga na naijua ile club, iko kwenye makazi ya watu kabisa na ni maeneo ambayo kweli asubuhi kuna shule karibu na ni njia yakupita vijana wetu kuelekea shule.
 
Kama vipi wasogezwe/wahamishwe kama wale wa loliondo ..manake Mr Beny ni mwekezaji na alipewa vibali vyote na mamlaka husika... na hiyo ndio tatizo la maendeleo,yakikufuata inabidi ubadirike nayo ..kwa mfano miaka 15-20 iliyopita nyumba nyingi za shekilango Rd zilikua ni makazi ya watu but with time wenyewe wamezigeuza shops,bars, garages, carwash, Fuel station,saloons, nightclubs na Bus stands..na automatically hakuna watu wanaishi nyumba hizo coz of noise pollution na vitu kama hivyo..na uking'ang'ania kuishi mitaa kama hiyo unakua unafanya hivyo at your own inconvenience..huu mtaa anaoulalamikia member mwenzetu naufahamu na nimetembelea twice, ni mtaa wa migahawa na starehe za evening outing. Na nyumba nyingi ni Mali ya shirika la nyumba la Taifa ( NHC) sasa usitegemee kulipa rent ya 45,000/ month halafu upate kelele za ndege na breezes za bahari ya Hindi.
 
Halmashauri zijitahidi kujenga maeneo kwa ajili ya watu kujenga kumbi za starehe kama pubs, bar, clubs nk. Otherwise yawe maeneo ambayo usiku sio makazi ya watu.
Therefore tatizo sio la mwenye club, tatizo ni la mamlaka zilizompatia kibali...hii issue inabidi haipereke kwa Diwani wa eneo hili,manake Baraza la madiwani ndio haswa Wana uwezo wa kutoa au kutengua vibali katika maeneo ya halmashauri,manispaa au Jiji.... kupanga ni kuchagua
 
Kama vipi wasogezwe/wahamishwe kama wale wa loliondo ..manake Mr Beny ni mwekezaji na alipewa vibali vyote na mamlaka husika... na hiyo ndio tatizo la maendeleo,yakikufuata inabidi ubadirike nayo ..kwa mfano miaka 15-20 iliyopita nyumba nyingi za shekilango Rd zilikua ni makazi ya watu but with time wenyewe wamezigeuza shops,bars, garages, carwash, Fuel station,saloons, nightclubs na Bus stands..na automatically hakuna watu wanaishi nyumba hizo coz of noise pollution na vitu kama hivyo..na uking'ang'ania kuishi mitaa kama hiyo unakua unafanya hivyo at your own inconvenience..huu mtaa anaoulalamikia member mwenzetu naufahamu na nimetembelea twice, ni mtaa wa migahawa na starehe za evening outing. Na nyumba nyingi ni Mali ya shirika la nyumba la Taifa ( NHC) sasa usitegemee kulipa rent ya 45,000/ month halafu upate kelele za ndege na breezes za bahari ya Hindi.
Aanze na kelele za misikiti kwanza
 
Kwa niaba ya rafiki wangu huko Tanga na-share hii uzi

Barua wazi kwa mkuu wa mkoa tanga.

Mheshimiwa mkuu wa mkoa Tanga,

Ni kwa masikitiko makubwa tunakueletea malalamiko dhidhi ya club ya Ben Bistro hapa wilayani Tanga, kati ya mtaa wa Ekcenforde na ring - Guinea Street

Club hii iliyoanzishwa miaka miwili ilioypita inaendelea kututesa kwa kuleta mazingira ya mateso mengi sana kwa sisi tunaoishi kwenye maeneo haya! Tabia za kihuni kwa kucheza muziki hadi usiku wa manane pamoja na wateja wao kuhudumiwa pombe kwenye magari zao barabarani na kukutwa wamesinzia hadi asubuhi pamoja na kutoa huduma za shisha, wadada wanauza mwili zao pia wapo na kufanya mambo zao kwenye magari n.K asubuhi hukosi kuona machupa za pombe barabarani au kwenye mataro na ukuta zinanuka na mkojo.

Huo mtaa unatumika sana na wanafunzi wanaopita kuelekea mashule mengi zilizo jirani na huwa wanashuhudia haya mazingira kila siku. Pia kuna kanisa na misikiti mawili na waumini wengi nao wanashuhudia haya matatizo.

Siku ya jumamosi tarehe saba mwezi huu wamezuia mabarara nne za mitaa na kufunga jukwaa. Jumapili kuanzia saa 11 jioni wameanza tamasha ya bendi iliyoendelea hadi 12 alfajiri.

Mheshimiwa, sisi tulishindwa kupumzika kabisa maana kelele ilikuwa mkubwa mno na hadi vitu vya ndani, ufa n.K. Za manyumba zetu zilikuwa zinatetemeka.

Mara nyingi asubuhi waumini waonaoelekea msikitini wamekuta watu wameelewa na kulala juu ya meza, kwenye magari na chupa za pombe zimetupwa barabarani.

Mwenyekiti wa mtaa naye hataki kutusaidia na insemekana biashara zake ni kukodisha vifaa wa bendi na vilitumika siku hiyo. Mwenye hiyo biashara aitwaye beny nae inasemekana kuwa anafahamia na 'viongozi wa juu' na hakuna atakaemsumbua?

Je hii ni haki? Mtaa wetu miaka nenda nyuma ilikuwa na utulivu na heshima wa hali ya juu ila leo hii tunateseka sana.

Tafadhali angalia video hizi.

Mheshimiwa, tunakuomba utusaidie.

View attachment 2324800
View attachment 2324802
Kwa huu uandishi ni Dhahiri bila Mawaa kuwa wewe sio M Tanzania
Rudi kwenu Mombasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom