JERUSALEMU
JF-Expert Member
- Sep 19, 2012
- 3,106
- 3,523
Habari wana jamvi!
Naam, baada ya waraka namba moja,nimewiwa tena kuandika waraka namba mbili. Lengo ni lile lie kuzisaka kura kwa udi na uvumba. Kwa maoni yangu mheshimiwa Rais mtarajiwa nakuomba siku zilizo baki kila siku usikose kuyazungumzia masuala mtambuka yafuatayo kwani yanawagusa watanzania wote wa mjini na vijijini.Nitayabainisha kama ifuatavyo;
Mosi, Kwamba awamu ya tano imesababisa biashara nyingi kufungwa au kudorora kwasababu ya kodi nyingi zisizo lipika. Wafanya biashara hawana raha Nchini mwao na wengine wamepeleka biashara Nchi Jirani. Kodi zisizo lipika ni shida.
Pili, viwanda vingi vimekufa au kulazimika kufunga shughuli zake kwasababu ya mazingira magumu ya biashara.Morogoro peke yake viwanda vinne vilivyo kuwa viaajiri wafanyakazi zaidi ya 5000 vimefungwa. Kati ya hivyo viwili ni vya tumbaku. Kufungwa kwa viwanda vya tumbaku kumeathiri ununuzi wa zao la tumbaku Tabora na Ruvuma hivyo kuwasababishia watu wa maeneo hayo ugumu wa maisha kwasababu biashara ya zao la tumbaku imeharibika.
Tatu, dhiki ya mlo mmoja kwa siku imekuwa wimbo wa Taifa. Mijini tatizo hili ni kubwa kupindukia. Watu wanashindia mhogo Wa kuchoma na nyanya masaro wakisindikizia na maji mengi ya viroba. Maisha yamekuwa magumu kwelikweli. Hii imesababishwa na ukosefu Wa ajira kwa vijana, biashara kubwanwa, wakandarasi kuto kulipwa pesa, na wafanyakazi kutokuongezewa mishahara kwa muda wa miaka mitano.
Mwisho waombe watanzania wakapige kura tarehe 28.10.2020 na wazilinde. WAKUMBUSHE WATANZANIA KUWA HATA WALE AMBAO HAWAKWENDA KUBORESHA TAARIFA ZAO, MAJINA YAO YAPO KWENYE DAFTARI LA MPIGA KURA KWENYE VITUO VYAO VILE VILE VYA ZAMANI. Nakutakia Afya njema na kampeni kabambe za lala salama. Ni yeye 2020.
Naam, baada ya waraka namba moja,nimewiwa tena kuandika waraka namba mbili. Lengo ni lile lie kuzisaka kura kwa udi na uvumba. Kwa maoni yangu mheshimiwa Rais mtarajiwa nakuomba siku zilizo baki kila siku usikose kuyazungumzia masuala mtambuka yafuatayo kwani yanawagusa watanzania wote wa mjini na vijijini.Nitayabainisha kama ifuatavyo;
Mosi, Kwamba awamu ya tano imesababisa biashara nyingi kufungwa au kudorora kwasababu ya kodi nyingi zisizo lipika. Wafanya biashara hawana raha Nchini mwao na wengine wamepeleka biashara Nchi Jirani. Kodi zisizo lipika ni shida.
Pili, viwanda vingi vimekufa au kulazimika kufunga shughuli zake kwasababu ya mazingira magumu ya biashara.Morogoro peke yake viwanda vinne vilivyo kuwa viaajiri wafanyakazi zaidi ya 5000 vimefungwa. Kati ya hivyo viwili ni vya tumbaku. Kufungwa kwa viwanda vya tumbaku kumeathiri ununuzi wa zao la tumbaku Tabora na Ruvuma hivyo kuwasababishia watu wa maeneo hayo ugumu wa maisha kwasababu biashara ya zao la tumbaku imeharibika.
Tatu, dhiki ya mlo mmoja kwa siku imekuwa wimbo wa Taifa. Mijini tatizo hili ni kubwa kupindukia. Watu wanashindia mhogo Wa kuchoma na nyanya masaro wakisindikizia na maji mengi ya viroba. Maisha yamekuwa magumu kwelikweli. Hii imesababishwa na ukosefu Wa ajira kwa vijana, biashara kubwanwa, wakandarasi kuto kulipwa pesa, na wafanyakazi kutokuongezewa mishahara kwa muda wa miaka mitano.
Mwisho waombe watanzania wakapige kura tarehe 28.10.2020 na wazilinde. WAKUMBUSHE WATANZANIA KUWA HATA WALE AMBAO HAWAKWENDA KUBORESHA TAARIFA ZAO, MAJINA YAO YAPO KWENYE DAFTARI LA MPIGA KURA KWENYE VITUO VYAO VILE VILE VYA ZAMANI. Nakutakia Afya njema na kampeni kabambe za lala salama. Ni yeye 2020.