Barua ya wazi kwa meneja wa DAWASA

mohal

Member
Sep 22, 2018
40
32
Husika na kichwa cha habari,kwa heshima na taadhima sisi wananchi wa Kifuru tunakuandikia barua hii kwa meneja wa DAWASA ya kwamba sisi wakazi wa kifuru na viunga vyake,tunapenda kukumbushia swala letu LA maji,tunaomba utisambazie maji,ili kukidhi mahitaji yetu,na fedha tutakazolipa zitaongeza pato LA taifa.
Kwa taarifa tulizonazo mabomba yameshafika hapa malamba mawili,ni imani yetu kuwa kutokea hapo ni rahisi sana kwa sisi wakazi wa kifuru kusambaziwa,naomba tumuunge mkono Muheshimiwa Raisi kwenye utekelezaji huduma kwa sisi Wananchi.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Mbariki Raisi wa Tanzania
Mungu Atubariki Watanzania

Sent using Jamii Forums mobile app

=====

MAJIBU:

DAWASA said:
Maji yamefika malamba mawili, Kifuru ni eneo la Mkoa wa Tabata, na kazi ya usambazaji maji itafanywa kwa kushirikiana na Mkoa wa Dawasa Tabata na Mkoa wa Dawasa Kimara kihuduma. Kazi ya survey itaanza hivi karibuni ili kuona vifaa vinavyohitajika ili wakazi wa kifuru waanze na wao kunufaika na miradi. Aidha katika mpango wa muda wa kati Tenki kubwa la kuhifadhi maji linatarajiwa kujengwa eneo la malamba mawili ili kumaliza kabisa changamoto hiyo.
 
Binafsi nashukuru kwa majibu mazuri,na ya kutia moyo.
Tunawatakia kila LA heri,kwenye kufanikisha mradi huu muhimu,kwa sisi wakazi wa kifuru.
Mungu Ibariki Tanzania.
Mungu Mbariki Rais wa Tanzania
Mungu Atubariki Wa Tanzania
 
Hongereni sana DAWASA. Ila isije ikawa ni kwa awamu ya Tano na ikishamalizika tunarudi kule kiangazi cha maji. Jueni Bill zetu ndiyo maisha yenu.
 
Back
Top Bottom