Barua ya wazi kwa Mbowe & CHADEMA: Kajipangeni Upya

Stuxnet

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
10,369
17,935
Kwako Freeman Mbowe,
Mwenyekiti wa CHADEMA

Ni wazi CDM mnapoteza focus maana Kama alivyosema E Lowassa mwaka 2015 kuwa Chama chenu ni wana harakati zaidi kuliko wanasiasa. Wanaharakati huenda na matukio wakati wanasiasa huenda na mikakati.

Kuna mabadiliko makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi ambayo yamefanywa ndani ya kipindi cha miezi 3 au siku 100 katika utawala wa Rais SSH. Watanzania wote wanajuwa na wanaona nafuu ya maisha katika nyanja zote na wana matumaini na Rais. Sina haja ya kuyataja hapa ambayo Rais SSH amefanya kwa kuwa mengine hata Mbowe binafsi ni mnufaika wa moja kwa moja.

Sijapendezewa na Uongozi wenu wa juu wa CDM namna mnavyotaka KIUMSHURUTISHA Rais afuate VIPUMBELE vyenu badala ya vipaumbele vyake na Chama chake.

Hata kama kuna mapungufu katika vipaumbele vya Rais, naamini kuna namna ya kufikisha ujumbe kwa Rais kwa maadili na nidhamu. Kumbukeni Rais ni Taaaisi

Najuwa CHADEMA mumeomba kukutana na Rais, na Rais bado hajaonyesha atakutana nanyi lini. Hili nalo linakuwa shida kwa kuwa nyinyi akina Mbowe mnaona alipaswa aonane na CHADEMA kwanza kabla ya makundi mengine ambayo Rais amekutana nayo.

Juzi mwanachama wenu mmoja (MDUDE) ameachiwa na Mahakama ya Mbeya kwa makosa ya kusafirisha cocaine. Badala mumuache kwanza apumzike ili aboreshe saikolojia na afya ya akili, nyie mumemempandisha kwenye majukwaa na ameanza kumtishia Rais SSH.

Jana mkutano wa dinner wa akina Mama wa BAWACHA uliopangwa kufanyika pale Hekima Garden ulivunjwa na Jeshi la Polisi. Naomba mjue kuwa Serikali ipo, na hai hezewi.

USHAURI WANGU:
CHADEMA wakumbuke kuwa Rais SSH siyo Kiongozi wa CCM na CHADEMA pekee bali ni Kiongozi wa Watanzania wote walio kwenye vyama na wasio na vyama. Kazi ya Samia tumeiona kwa muda mfupi na tuna matumaini kuwa yuko kwenye MSTARI SAHIHI na kuna makubwa nchi yetu itapata chini ya Uongozi wake.

Ametupa Uhuru wa kuongea na kushauri kwa mujibu wa Katiba, tuutumie vizuri kwa masilahi mapana na nchi yetu.

Katiba Nzuri kweli tunaitaka na Rais SSH kasema tumpe muda kwanza aratibu mipango yake ya uchumi, then suala la Katiba litakuja. Kwa nini tusimpe benefit of doubt Rais wetu kwa hilo? Maana mtangulizi wake (Magufuli) alisema "Kwenye Kampeni zangu sikuahidi Katiba". Ila huyu Samia anasema tumpe muda tu, nyinyi hamutaki.

Na kwa miaka 5 CHADEMA walikuwa wanaongelea Tume Huru Ya Uchaguzi, kuibiwa kura za uchaguzi na kesi za kubambikizwa. Sasa ndiyo wameanza kudai Katiba naada ya DIKTETA Magufuli kufariki.

Nawashauri CHADEMA, waitishe Mkutano wao Mkuu ili waweke mkakati wa nini wanachokitaka na siyo kila mwenye kusimama jukwaani anataka cha kwake. Wawatumie vijana wao wasomi waandike dira yao na miongozo ya vitu gani wadai kutoka Seikalini.
 
CDM wanazingua mama kaanza vizuri hafu hata hyo katiba wanayolilia ndo itabadilisha umaskini,Bora basi wangekuja na kipaumbele Cha kuondoa umaskini na ajira kwa vijana ambao ni wengi kwenye hili taifa. Waje na agenda ya kugusa watu wengi ila blah blah za katiba tu bila kuondoa umaskini it doesn't make sense.
 
Kwahiyo vyama vya siasa KAZI Yao ni kudai mambo Kwa serikali.

Tafsiri mpya hii.

Mimi ninavyoelewa vyama visivyokuwa na Dola kazi yake ni kuonesha mbadala wa Yale yanayofanywa na chama kinachoongoza serikali.

Kwa tafsiri Yako ndio maana Chadema imebakia kuwa chama Cha wanaharakati kwani wanaharakati ndio hudai mambo Kwa serikali.

Msingi wa vyama vya upinzani umepotoshwa na Chadema,

Chadema bila kujua wanaharibu siasa za nchi hii.
 
We pimbi, rais anawajibika kufuata vipa umbele vya umma/wananchi, siyo vyake yeye binafsi na kikundi kidogo Cha watu wa chama chake🙄

Kwani ile nafasi amejiweka pale mwenyewe?!!!
Usimwite Pimbi mwenzio bila kuwa na hoja.

Hebu leta andiko linalosema Katiba Mpya ni kipaumbele cha wananchi!!

Mimi ni mwana mitandao ya jamii mzuri nipo Twitter, FB na hapa JF. Katiba Mpya inaongelewa sana kwenye hiyo mitandao na mikutano ya CDM. Katika maisha ya kawaida kipaumbele chao ni UCHUMI tu??

Kila mwananchi anafikiria mishe mishe za kipato, ujasiriamali, Kodi za TRA, Bei za mafuta, kilimo gani afanye, bidhaa gani alete.

Sasa kama RAIS SAMIA anasema aanze na UCHUMI nafikiri anakidhi kiu ya Watanzania walio wengi
 
Rais anawajibika kufuata vipa umbele vya umma/wananchi, siyo vyake yeye binafsi na kikundi kidogo Cha watu wa chama chake🙄

Kwani ile nafasi amejiweka pale mwenyewe?!!!
Hivi akifuata vipaumbele vya kila mtu anachotaka kweli hata wewe unaweza kutawala nchi kwa mtindo mhuo? acheni ushenzi wenu mtavumiliwa mwishowe mtachokwa hata hiyo ya ndani mikutano mtyakuwa hamfanyi nyoko nyie msifikiri mnaogopwa sana nyie ni kama mavitu hakuna mtu anaye wajali maana hamna akili mngekuwa na akili hata kidogo tu za kuvukia barabara mngesikilizwa lakini hamna akili kenge nyie wa chadema
 
With all due respect, hii barua yako inatakiwa iishie mezani kwa secretary, haistahili kufika kwa Mbowe.

Mambo mengi uliyoandika unauelewa finyu juu yake, hili andiko lako simply linathibitisha vile wajinga wakiwa wengi kwenye jamii wanaweza kutuchagulia Rais mjinga pia.

Mosi: Unazungumzia masuala mengi yaliyofanywa na Samia kwenye madaraka yake kielimu, kijamii, na kiuchumi, sasa ni kwa vipi hayo masuala yanawazuia Chadema kuhitaji mambo mengine pia yenye uhitaji kwa wananchi?

Pili: Unasema hujapendezwa na namna Chadema wanavyomshurutisha Rais kwenye nafasi yake, ujue fika, kumshurutisha au kumpigia magoti ni option ambazo zipo ndani ya Chadema provided hawavunji sheria za nchi, above all, kumshurutisha mtu afuate sheria sioni kosa.

Huu ujinga wenu wa kuona sheria za nchi zinavunjwa wazi na bado mnataka mvunjaji apigiwe magoti kubembelezwa sijui mmeutoa wapi, sijajua bado, kwanini mnakuwa wepesi kuwalaumu Chadema kwa hatua wanazochukua kulinda haki zao, badala ya kumlaumu yule anayevunja haki hizo? huu ni ujinga tu.

Tatu: Umepeleka malalamiko yako kwenye hoja kwamba Rais anatakiwa kuelekeza majukumu yake kwenye makundi mengine na hao Chadema wanatakiwa kusubiri, sawa.

Lakini vipi kwenye hayo makundi mengine haki zinazopiganiwa na Chadema haziyahusu? naamini kwenye hayo makundi utawala bora na haki za binadamu vinawahusu, hili taka usitake, na hayo makundi mara nyingi hayajaweza kujisimamia yenyewe kudai hizo haki, wanasiasa ndio wamekuwa viongozi wao.

Mwisho, umewazungumzia Chadema na uanaharakati, kama una akili timamu ungetakiwa kwanza ujue chanzo cha huo "uanaharakati" wa Chadema ambao mimi siouni, kama ungekuwa wewe ungefanyaje kama unashindana na chama cha siasa kinachojiita "chama dola"?

Sheria zinavunjwa wazi Chadema wakipigania haki yao kwa njia ya maandamano tena njia inayotambulika kisheria mnawaona wabaya, hii mentality yenu ya kizee ndio inawafanya CCM na viongozi wake waendelee kuvunja sheria wapendavyo.

Nikwambie tu, Chadema sio wanaharakati, ni mazingira ya kisiasa wanayokabiliana nayo ndio yanayowafanya waonekane "wanaharakati" na wale wenye uwezo finyu wa kufikiri kama wewe, kama CCM wangekuwa chama cha siasa wanaotii sheria, wasijiite chama dola pasingeharibika kitu.
 
Kwako Freeman Mbowe,
Mwenyekiti wa CHADEMA

Ni wazi CDM mnapoteza focus maana Kama alivyosema E Lowassa mwaka 2015 kuwa Chama chenu ni wana harakati zaidi kuliko wanasiasa. Wanaharakati huenda na matukio wakati wanasiasa huenda na mikakati...
Kwa nini usiwashauri ccm waondoe kodi kwenye mafuta ili maisha yawe nafuu?

Madai ya katiba ni endelevu toka mwisho wa miaka ya 80, huenda ilikuwa hujazaliwa
Tutaungana na CDM kudai katiba mpya popote na wakati wowote
 
Kwako Freeman Mbowe,
Mwenyekiti wa CHADEMA

Ni wazi CDM mnapoteza focus maana Kama alivyosema E Lowassa mwaka 2015 kuwa Chama chenu ni wana harakati zaidi kuliko wanasiasa. Wanaharakati huenda na matukio wakati wanasiasa huenda na mikakati....

Hapa umebwabwaja tu mkubwa, umepiga propaganda za ujinga wa siasa majitaka za maCCM ukidhani sote ni wajinga kama mlivyo huko.

Sijaona hoja yako. Hujui usemalo wala uzungumzalo.

Kwa namna gani hasa Rais Samia Suluhu awe ameleta nafuu ya maisha ktk miezi mitatu hii tangu mwenzake Mwendazake John P. Magufuli utawala wake ukataliwe na kuhitimishwa na Mungu mwenyewe?

Hivi unafahamu kuwa miezi mitatu nyuma nishati ya mafuta ya petrol ilikuwa TZS 2,000 na sasa ni almost 2,600..?

Kwa ishara (indicator) hii ya kasi ya kupanda nishati ya petrol, basi elewa maisha ni magumu kote vijijini na mijini.

Unafahamu umuhimu wa nishati ya mafuta kwenye maisha ya wananchi wa kawaida walio wengi vijijini kote na mijini..?
 
Kwako Freeman Mbowe,
Mwenyekiti wa CHADEMA

Ni wazi CDM mnapoteza focus maana Kama alivyosema E Lowassa mwaka 2015 kuwa Chama chenu ni wana harakati zaidi kuliko wanasiasa. Wanaharakati huenda na matukio wakati wanasiasa huenda na mikakati...
Nadhan yote umeyasema na mwenye akili akuelewe!
 
CDM wanazingua mama kaanza vizuri hafu hata hyo katiba wanayolilia ndo itabadilisha umaskini,Bora basi wangekuja na kipaumbele Cha kuondoa umaskini na ajira kwa vijana ambao ni wengi kwenye hili taifa. Waje na agenda ya kugusa watu wengi ila blah blah za katiba tu bila kuondoa umaskini it doesn't make sense.
Ajenda walikuwa nazo oct. 2020 .mkaiba kura na kumtangaza yule mwehu kashinda
 
We pimbi, rais anawajibika kufuata vipa umbele vya umma/wananchi, siyo vyake yeye binafsi na kikundi kidogo Cha watu wa chama chake🙄

Kwani ile nafasi amejiweka pale mwenyewe?!!!
Mimi siyo pimbi. Pimbi hawezi kushika simu na kuandika kwenye key board. Njoo na hoja nitakujibi
 
Kwahiyo vyama vya siasa KAZI Yao ni kudai mambo Kwa serikali.

Tafsiri mpya hii.

Mimi ninavyoelewa vyama visivyokuwa na Dola kazi yake ni kuonesha mbadala wa Yale yanayofanywa na chama kinachoongoza serikali...
CCM wameharibu zaidi siasa za nchi hii wakati wa yule mwehu, wameharibu uchumi, wameharibu diplomasia, bado hawataki kutoka madarakani mpaka mungu anawatoa taratibu.
 
Kwa nini usiwashauri ccm waondoe kodi kwenye mafuta ili maisha yawe nafuu?

Madai ya katiba ni endelevu toka mwisho wa miaka ya 80, huenda ilikuwa hujazaliwa
Tutaungana na CDM kudai katiba mpya popote na wakati wowote
Niko toka Uhuru na najuwa Tume ya Jaji Nyalali kwenye miaka ya 1990-91 juu ya Sheria mbaya 40, moja ya mapendekezo yake ilikuwa ni kuachana na Katiba ya 1977 na kuandika mpya
 
Niko toka Uhuru na najuwa Tume ya Jaji Nyalali kwenye miaka ya 1990-91 juu ya Sheria mbaya 40, moja ya mapendekezo yake ilikuwa ni kuachana na Katiba ya 1977 na kuandika mpya
Ok Sasa kipi cha ajabu kwa CDM kudai katiba mpya?? Mpaka ukaamua kuwananga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom