Binti Maria
Senior Member
- Jun 26, 2007
- 158
- 33
Sijui kama mmeshaiona hii barua ya Issa Shivji kuhusu yaliyotokea na yanayoendelea kutokea Kenya. Soma jinsi huyu Profesa mahiri na mzalendo alivyomkoma nyani gladi. Hamumunyi maneno, anaweka vitu hadharani. Haya jisomee sasa mwenyewe.
_______________________________________________________________
2-01-2008
Barua ya wazi kwa Marais Kikwete, Kagame na Kiguta juu ya hali ya Wakenya
Waheshemiwa Marais:
Ninashindwa kuwasalimia kwa kheri za mwaka mpya. Katika eneo letu hili la Afrika, hakuna heri, kuna shari tu. Waafrika wenzetu huko Kenya wanakufa bila sababu. Sababu ni moja tu uchu wa madaraka. Inanishangaza sana kwamba nyie kama viongozi wa nchi za Afrika zinazoshirikiana katika Jumuiya ya Afrika Mashariki yenye lengo la kujenga msingi wa Shirikisho la Afrika, mko kimya. Hi sio wakati wa kucheza mchezo wa kidiplomasia. Hatutaki, hatutaki kabisa kuona tena jangwa la mauaji ya halaiki yatokee barani Afrika. Tumechoka kuona wanaadamu, Waafrika wenzetu, wakiuawa kama wanyama mitaani na hao wanaojiita eti vyombo vya usalama. Usalama wa nani kama sio wa wananchi?
Jukumu la awali kabisa la vyombo hivyo ni kulinda usalama wa raia; kutuliza ghasia sio kuchochea ghasia au chuki. Wakiwakuta waandamaji bila silaha wawalinde, wawashauri kufanya maandamano yao kwa amani, wawapatie nafasi ya kuonyesha madukuduku yao kuhusu uchaguzi. Uchaguzi wa rais na wananchi kutokuridhika na jinsi ulivyoendeshwa ni suala la kisiasa, sio la kivita. Kama wananchi wana hisia za dhati kabisa kwamba watawala wameiba kura, wamepokonya haki yao ya kuchagua viongozi wao, wanahaki kabisa kuonyesha hisia zao. Kuwazuia wahalifu ni sawa; kuwazuia wezi ni sawa, lakini kuwaua wananchi wa kawaida kabisa kwa sababu wameandamana au wanaelekea kwenye mikutano ya kisiasa ni dhuluma. Haikubaliki na tusikubali kamwe. Kutawala sio haki ya kuzaliwa ya mtu fulani, au rika fulani, au ukoo fulani, au kabila fulani. Ni chaguo la wananchi.
Sasa nyie viongozi wetu mmesema nini kuhusu hali hio? Kwanza, kuhusu uwizi wa kura wa waziwazi kabisa. Mkikaa kimya maana yake mnamuoneya haya mwenzenu mtawala hata kama anatawala kwa mabavu bila ya ridhaa ya wananchi. Pili, mkikaa kimya juu ya mauaji yanayofanywa na vyombo vya usalama kwa niaba ya mtawala haramu, mnaweka mfano mbaya mno na mfano huo unaweza ukaugeukia kwenu, na kwetu pia. Tatu, mkifikiri kwamba jambo hili ni jambo la kidiplomasia, jambo la kusuluhisha chinichini au katika faragha ya Ikulu, mnachanganya jambo la msingi la haki ya wananchi kuishi na kujitawala, na mambo ya kiitifaki. Tumieni, mkitaka, lugha zenu za kidiplomasia. Tumieni njia zozote zinazowezekana kutuliza hali ya nchi hiyo ili wananchi wasiona hatia wasiendelee kupoteza maisha yao. Lakini kamwe msikubali utawala wa mabavu bila ya ridhaa ya wananchi.
Juu ya jambo hili la utawala wa mabavu, ukiwa wa kijeshi au wa kiraia wa uwizi bila ya ridhaa ya wananchi, semeni kwa sauti kubwa bila kutafuna maneno. Mkishindwa kufanya hivyo, sisi raia hatutawaelewa.
Wananchi wanataka amani; wao ni wa kwanza kutaka na kulinda amani. Lakini amani halisi hujengwa katika msingi wa haki, haki ya kisiasa na haki ya kijamii. Suala sasa ni nini la kufanya? Kwa maoni yangu, kama raia wa kawaida, naona hatua zifuatazo (katika lugha na njia mtakayaona inafaa kidiplomasia) zinaweza kuchukuliwa mara moja:
Mosi, iwekwe wazi kabisa kwamba nchi zetu hazikotayari kutambua utawala wowote ule ambao uhalali wake unatiliwa shaka na wananchi na watazamaji na watu wa kawaida ambao walikuwa wanafuatilia uchaguzi huu wa Kenya.
Pili, Mwai Kibaki awaamrishe mara moja jeshi na polisi wake kutokutumia silaha zozote za moto kuwatuliza wananchi isipokuwa pale to ambapo hakuna njia nyingine yoyote ya kutuliza machafuko.
Tatu, Kibaki akubali moja kwa moja bila masharti, kamati ya uchunguzi ulioteuliwa na Marais wa Afrika Mashariki wakishirikiana na Umoja wa Afrika, kuchunguza uchaguzi wa rais na kusimamia kuhesabiwa kura tena (recount) na kutangazwa hadharani.
Nne, wagombea urais wote kwa pamoja na mbele yenu wakubali kwa maandishi kwamba yeyote atakayeonekana ameshinda urais baada ya kura kuhesabiwa:
a) Maramoja ataunda serikali ya umoja wa kitaifa na rais na mawaziri waapishwe kwa wakati moja;
b) Ataliitisha Bunge na kupendekeza Azimio itakayoweka taratibu za Rais na Baraza la Mawaziri kuapa kwamba watailinda, kuikuuza na kuiendesha serikali ya umoja wa kitaifa kwa maslahi ya taifa bila kujali itikadi za chama, na kwamba kamwe hawatatumia ukabila, kwa vitendo au maneno, kama njia, chombo au jinsi ya kubaki katika au kugombea vyeo vya kisiasa. Serikali ya umoja wa kitaifa iendelee mpaka uchaguzi mkuu ujao.
Haya ni hatua za kisiasa; sio za kisheria. Zikikubalika kisiasa, njia za kitaalamu za kisheria zinaweza kubuniwa. Msikubali visingizio vya kisheria. Makubaliano ya awali, na yaliyo magumu, ni ya kisiasa. Sheria inafuata siasa, sio kuitangulia.
Wenu,
Raia Issa Shivji
Mwananchi 03-01-2008
_______________________________________________________________
2-01-2008
Barua ya wazi kwa Marais Kikwete, Kagame na Kiguta juu ya hali ya Wakenya
Waheshemiwa Marais:
Ninashindwa kuwasalimia kwa kheri za mwaka mpya. Katika eneo letu hili la Afrika, hakuna heri, kuna shari tu. Waafrika wenzetu huko Kenya wanakufa bila sababu. Sababu ni moja tu uchu wa madaraka. Inanishangaza sana kwamba nyie kama viongozi wa nchi za Afrika zinazoshirikiana katika Jumuiya ya Afrika Mashariki yenye lengo la kujenga msingi wa Shirikisho la Afrika, mko kimya. Hi sio wakati wa kucheza mchezo wa kidiplomasia. Hatutaki, hatutaki kabisa kuona tena jangwa la mauaji ya halaiki yatokee barani Afrika. Tumechoka kuona wanaadamu, Waafrika wenzetu, wakiuawa kama wanyama mitaani na hao wanaojiita eti vyombo vya usalama. Usalama wa nani kama sio wa wananchi?
Jukumu la awali kabisa la vyombo hivyo ni kulinda usalama wa raia; kutuliza ghasia sio kuchochea ghasia au chuki. Wakiwakuta waandamaji bila silaha wawalinde, wawashauri kufanya maandamano yao kwa amani, wawapatie nafasi ya kuonyesha madukuduku yao kuhusu uchaguzi. Uchaguzi wa rais na wananchi kutokuridhika na jinsi ulivyoendeshwa ni suala la kisiasa, sio la kivita. Kama wananchi wana hisia za dhati kabisa kwamba watawala wameiba kura, wamepokonya haki yao ya kuchagua viongozi wao, wanahaki kabisa kuonyesha hisia zao. Kuwazuia wahalifu ni sawa; kuwazuia wezi ni sawa, lakini kuwaua wananchi wa kawaida kabisa kwa sababu wameandamana au wanaelekea kwenye mikutano ya kisiasa ni dhuluma. Haikubaliki na tusikubali kamwe. Kutawala sio haki ya kuzaliwa ya mtu fulani, au rika fulani, au ukoo fulani, au kabila fulani. Ni chaguo la wananchi.
Sasa nyie viongozi wetu mmesema nini kuhusu hali hio? Kwanza, kuhusu uwizi wa kura wa waziwazi kabisa. Mkikaa kimya maana yake mnamuoneya haya mwenzenu mtawala hata kama anatawala kwa mabavu bila ya ridhaa ya wananchi. Pili, mkikaa kimya juu ya mauaji yanayofanywa na vyombo vya usalama kwa niaba ya mtawala haramu, mnaweka mfano mbaya mno na mfano huo unaweza ukaugeukia kwenu, na kwetu pia. Tatu, mkifikiri kwamba jambo hili ni jambo la kidiplomasia, jambo la kusuluhisha chinichini au katika faragha ya Ikulu, mnachanganya jambo la msingi la haki ya wananchi kuishi na kujitawala, na mambo ya kiitifaki. Tumieni, mkitaka, lugha zenu za kidiplomasia. Tumieni njia zozote zinazowezekana kutuliza hali ya nchi hiyo ili wananchi wasiona hatia wasiendelee kupoteza maisha yao. Lakini kamwe msikubali utawala wa mabavu bila ya ridhaa ya wananchi.
Juu ya jambo hili la utawala wa mabavu, ukiwa wa kijeshi au wa kiraia wa uwizi bila ya ridhaa ya wananchi, semeni kwa sauti kubwa bila kutafuna maneno. Mkishindwa kufanya hivyo, sisi raia hatutawaelewa.
Wananchi wanataka amani; wao ni wa kwanza kutaka na kulinda amani. Lakini amani halisi hujengwa katika msingi wa haki, haki ya kisiasa na haki ya kijamii. Suala sasa ni nini la kufanya? Kwa maoni yangu, kama raia wa kawaida, naona hatua zifuatazo (katika lugha na njia mtakayaona inafaa kidiplomasia) zinaweza kuchukuliwa mara moja:
Mosi, iwekwe wazi kabisa kwamba nchi zetu hazikotayari kutambua utawala wowote ule ambao uhalali wake unatiliwa shaka na wananchi na watazamaji na watu wa kawaida ambao walikuwa wanafuatilia uchaguzi huu wa Kenya.
Pili, Mwai Kibaki awaamrishe mara moja jeshi na polisi wake kutokutumia silaha zozote za moto kuwatuliza wananchi isipokuwa pale to ambapo hakuna njia nyingine yoyote ya kutuliza machafuko.
Tatu, Kibaki akubali moja kwa moja bila masharti, kamati ya uchunguzi ulioteuliwa na Marais wa Afrika Mashariki wakishirikiana na Umoja wa Afrika, kuchunguza uchaguzi wa rais na kusimamia kuhesabiwa kura tena (recount) na kutangazwa hadharani.
Nne, wagombea urais wote kwa pamoja na mbele yenu wakubali kwa maandishi kwamba yeyote atakayeonekana ameshinda urais baada ya kura kuhesabiwa:
a) Maramoja ataunda serikali ya umoja wa kitaifa na rais na mawaziri waapishwe kwa wakati moja;
b) Ataliitisha Bunge na kupendekeza Azimio itakayoweka taratibu za Rais na Baraza la Mawaziri kuapa kwamba watailinda, kuikuuza na kuiendesha serikali ya umoja wa kitaifa kwa maslahi ya taifa bila kujali itikadi za chama, na kwamba kamwe hawatatumia ukabila, kwa vitendo au maneno, kama njia, chombo au jinsi ya kubaki katika au kugombea vyeo vya kisiasa. Serikali ya umoja wa kitaifa iendelee mpaka uchaguzi mkuu ujao.
Haya ni hatua za kisiasa; sio za kisheria. Zikikubalika kisiasa, njia za kitaalamu za kisheria zinaweza kubuniwa. Msikubali visingizio vya kisheria. Makubaliano ya awali, na yaliyo magumu, ni ya kisiasa. Sheria inafuata siasa, sio kuitangulia.
Wenu,
Raia Issa Shivji
Mwananchi 03-01-2008