Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,495
- 51,089
Kwako Dada Halima Mdee.
Sikupi pole kwa misukosuko iliyokukuta kwa sababu naamini unaistahili kutokana na kitendo ulichokifanya.
Nitakuwa mnafiki kujifanya nakuonea huruma, wakati kiukweli kabisa sikuonei huruma hata kidogo, maana naamini kuwa tamaa ya fedha kuliko Kuheshimu imani ya wananchi uliyopewa ni ubinafsi wa hali ya juu kupitiliza na lolote lililokukuta baada ya usaliti huo hupaswi kufutwa machozi, maana umeshiriki dhambi kubwa mno ya kutaka kufifisha ndoto za mamilioni ya wananchi walioweka imani katika upinzani na kwako binafsi wakiamini tuko pamoja bega kwa bega katika jitihada za kujenga Taifa la demokrasia zaidi, utawala bora zaidi, haki zaidi n. k
IIa nataka niongee na wewe mambo yafuatayo kukusaidia tu kiroho safi.
1. Tunaheshimu mchango wako kwa upinzani, tunakuomba usiendelee kushiriki kumnyonga mtoto uliyesaidia kumlea
Uongo mbaya, Halima unaomchango mkubwa, tena mkubwa kabisa kwenye kukua kwa upinzani nchini, Hiyo credit kamwe hatutokuondolea kwa sababu ni sehemu ya jasho lako. Kwa muktadha huo nakuomba sana, usikubali CCM wakugeuza kombora la kuibomoa kazi yako uliyoifanya kwa zaidi ya miaka 15, Usichana wako, the best years ya maisha yako uliitumia kwenye kujenga upinzani, japo umenikera kishenzi na naamini adhabu uliyopata ni haki yako, lakini nakuomba usikubali njama za CCM kukugeuza askari wa kuibomoa kazi yako mwenyewe.
CCM wanataka uvunje nyumba uliyoijenga, Usikubali, wewe waambie kuwa siyo kazi yangu kupambana na CHADEMA, hiyo ni kazi yenu. Wakatalie katakata, hao wanataka kukuchoresha na kuplay divide and rule.
2. Kula huo mpunga wa bure wa Ndugai, kisha tulia, lakini usikubali wakugeuze snitch
Halima kuna maisha baada ya migogoro, huko mbeleni utakuja kukaa na wapinzani kwenye kujadili issues, ni kama tu juzi akina Ndugai wamekutesa Bungeni, kukudhalilisha, kukuweka mahabusu, na kukufanyia kila aina ya ghilba lakini leo eti wanajifanya ni wema kwako. Halima hii ngoma usiichukulie personal, wewe kuwa low profile, usiwe kama yule mvulana Lijualikali, anapayuka na kuongea ujinga baada ya kufukuzwa, hiyo haikumsaidia yeye wala kutikisa CHADEMA.
Sasa wewe una akili kuliko Lijualikali, usifuate nyayo zake. Wewe kula huo mpunga wa Ndugai, buy time kisha uone siasa zitakunjuka vipi huko mbeleni, Lakini achana na kuiattack CHADEMA.
CHADEMA ya sasa hivi ni wananchi na siyo Mbowe, ni kupoteza muda kumshambulia Mbowe. Sisi wananchi tumesimama na maamuzi ya kamati kuu, kwa hiyo wewe kausha tu, kula hizo hela, tukutane huko mbele ya safari tuyajenge maana siasa haina rafiki wa kudumu au adui wa kudumu bali maslahi, Tatizo wewe uliweka mbele maslahi yako binafsi zaidi kuliko sisi wananchi ndo maana tunakuona fala
3. Kama Ndugai atakulindia ubunge wako achana na ishu za mahakama
Kwa sasa huaminiki ndani ya chama, hata ukipewa huo uanachama wa mahakama haikusaidii chochote kisiasa, Itakuwa ni mbinu tu ya hao handlers wako kuleta mgogoro tu ndani ya chama chako cha zamani ulichokipenda sana.
Wanaweza kukupa masharti kuwa ili wakulindie ubunge wako sharti uende mahakamani kupigania uanachama wako, Sasa ngoja nikuibie siri, yaani jinsi wewe unavyoutaka huo Ubunge ili upige hela, ndivyo jinsi na wao wanavyotamani wewe na wazinguaji wenzako wengine 18 muendelee kubaki Bungeni, maana kamwe hawatoweza kuwatoa Bungeni kwa hoja eti nyie siyo wanachama tena wa CHADEMA, wakifanya hivyo nao watajivua nguo mbele ya umma kuwa walibariki mchakato haramu wa kuwaapisheni kuwa Wabunge.
Kwa hiyo msiwe na wasiwasi, Ndugai atake asitake lazima atawalinda tu ili kulinda heshima ya taasisi yake. Kwa hiyo msikubali kwenda mahakamani maana mtazidi kuwakasirisha wananchi zaidi, mtadharaulika zaidi, mtachukiwa zaidi.
Sasa akili ni hivi, wewe nyuti, kula huo mpunga wa CCM, achana na mahakama, huna haja ya kwenda mahakamani maana nina uhakika mpunga wako huko bungeni uko palepale. Usishiriki kuwasaidia hao waliokuibia kura na kukudhalisha kwa kukupa pipi ya Viti Maalum, yale ni matusi!
4. Wewe ni mpinzani wa asili, endelea kupiga kazi huenda tukakufikiriafikiria
Sasa kwa kuwa wewe siyo mwanachama tena wa CHADEMA, lakini tunatambua mchango wako kwenye upinzani, unayo nafasi ya kumend ties na wananchi. Lazima uwe na subira sana kwenye hili, lazima uombe msamaha kwa wananchi kwa vitendo. Japo umekula haramu, umejirahisisha mbele ya madhalimu kwa sababu ya njaa yako ambayo kwa namna moja au nyingine imekuwa engineered makusudi na watesi wenu ambao leo hii wanajidanya kuwapendeni kumbe ni unafiki mtupu.
Mtesi wenu aligundua kuwa kuwachapa risasi ni counterproductive na inabackfire, sasa njia nzuri ni kuwachapa kiuchumi na kimahakama na hiyo ndo modus operandi yake, na kweli amefanikiwa ndiyo maana wengi katika kambi yenu wameunga mkono juhudi kutokana na njaa, na bahati mbaya na wewe Dada Halima hii teknic ya "njaa" imekusomba hata wewe.
Sasa iko hivi pambana sana kurudisha credibility kwetu, humohumo bungeni endelea kuzungumzia issues za wananchi. Kama ukitukosha huenda tukakufikiria kidogokidogo, lakini ukigeuka na kuwa mwanasiasa "malayamalaya", hakuna atakayekuwa na time wewe tena!
5. Jifunze wewe Dada, mafanikio ni zaidi ya pesa
Usaliti ni kansa, ondoa hii kansa once and for all. Hata ukienda CCM, kama una mentality hizi za kusalitisaliti sababu ya vijipesa na fursa, kamwe huwezi kuwa msaada kwa Taifa. Sellouts hawana nafasi kwenye mabaraza ya watu wa heshima. Jirekebishe!
Sikupi pole kwa misukosuko iliyokukuta kwa sababu naamini unaistahili kutokana na kitendo ulichokifanya.
Nitakuwa mnafiki kujifanya nakuonea huruma, wakati kiukweli kabisa sikuonei huruma hata kidogo, maana naamini kuwa tamaa ya fedha kuliko Kuheshimu imani ya wananchi uliyopewa ni ubinafsi wa hali ya juu kupitiliza na lolote lililokukuta baada ya usaliti huo hupaswi kufutwa machozi, maana umeshiriki dhambi kubwa mno ya kutaka kufifisha ndoto za mamilioni ya wananchi walioweka imani katika upinzani na kwako binafsi wakiamini tuko pamoja bega kwa bega katika jitihada za kujenga Taifa la demokrasia zaidi, utawala bora zaidi, haki zaidi n. k
IIa nataka niongee na wewe mambo yafuatayo kukusaidia tu kiroho safi.
1. Tunaheshimu mchango wako kwa upinzani, tunakuomba usiendelee kushiriki kumnyonga mtoto uliyesaidia kumlea
Uongo mbaya, Halima unaomchango mkubwa, tena mkubwa kabisa kwenye kukua kwa upinzani nchini, Hiyo credit kamwe hatutokuondolea kwa sababu ni sehemu ya jasho lako. Kwa muktadha huo nakuomba sana, usikubali CCM wakugeuza kombora la kuibomoa kazi yako uliyoifanya kwa zaidi ya miaka 15, Usichana wako, the best years ya maisha yako uliitumia kwenye kujenga upinzani, japo umenikera kishenzi na naamini adhabu uliyopata ni haki yako, lakini nakuomba usikubali njama za CCM kukugeuza askari wa kuibomoa kazi yako mwenyewe.
CCM wanataka uvunje nyumba uliyoijenga, Usikubali, wewe waambie kuwa siyo kazi yangu kupambana na CHADEMA, hiyo ni kazi yenu. Wakatalie katakata, hao wanataka kukuchoresha na kuplay divide and rule.
2. Kula huo mpunga wa bure wa Ndugai, kisha tulia, lakini usikubali wakugeuze snitch
Halima kuna maisha baada ya migogoro, huko mbeleni utakuja kukaa na wapinzani kwenye kujadili issues, ni kama tu juzi akina Ndugai wamekutesa Bungeni, kukudhalilisha, kukuweka mahabusu, na kukufanyia kila aina ya ghilba lakini leo eti wanajifanya ni wema kwako. Halima hii ngoma usiichukulie personal, wewe kuwa low profile, usiwe kama yule mvulana Lijualikali, anapayuka na kuongea ujinga baada ya kufukuzwa, hiyo haikumsaidia yeye wala kutikisa CHADEMA.
Sasa wewe una akili kuliko Lijualikali, usifuate nyayo zake. Wewe kula huo mpunga wa Ndugai, buy time kisha uone siasa zitakunjuka vipi huko mbeleni, Lakini achana na kuiattack CHADEMA.
CHADEMA ya sasa hivi ni wananchi na siyo Mbowe, ni kupoteza muda kumshambulia Mbowe. Sisi wananchi tumesimama na maamuzi ya kamati kuu, kwa hiyo wewe kausha tu, kula hizo hela, tukutane huko mbele ya safari tuyajenge maana siasa haina rafiki wa kudumu au adui wa kudumu bali maslahi, Tatizo wewe uliweka mbele maslahi yako binafsi zaidi kuliko sisi wananchi ndo maana tunakuona fala
3. Kama Ndugai atakulindia ubunge wako achana na ishu za mahakama
Kwa sasa huaminiki ndani ya chama, hata ukipewa huo uanachama wa mahakama haikusaidii chochote kisiasa, Itakuwa ni mbinu tu ya hao handlers wako kuleta mgogoro tu ndani ya chama chako cha zamani ulichokipenda sana.
Wanaweza kukupa masharti kuwa ili wakulindie ubunge wako sharti uende mahakamani kupigania uanachama wako, Sasa ngoja nikuibie siri, yaani jinsi wewe unavyoutaka huo Ubunge ili upige hela, ndivyo jinsi na wao wanavyotamani wewe na wazinguaji wenzako wengine 18 muendelee kubaki Bungeni, maana kamwe hawatoweza kuwatoa Bungeni kwa hoja eti nyie siyo wanachama tena wa CHADEMA, wakifanya hivyo nao watajivua nguo mbele ya umma kuwa walibariki mchakato haramu wa kuwaapisheni kuwa Wabunge.
Kwa hiyo msiwe na wasiwasi, Ndugai atake asitake lazima atawalinda tu ili kulinda heshima ya taasisi yake. Kwa hiyo msikubali kwenda mahakamani maana mtazidi kuwakasirisha wananchi zaidi, mtadharaulika zaidi, mtachukiwa zaidi.
Sasa akili ni hivi, wewe nyuti, kula huo mpunga wa CCM, achana na mahakama, huna haja ya kwenda mahakamani maana nina uhakika mpunga wako huko bungeni uko palepale. Usishiriki kuwasaidia hao waliokuibia kura na kukudhalisha kwa kukupa pipi ya Viti Maalum, yale ni matusi!
4. Wewe ni mpinzani wa asili, endelea kupiga kazi huenda tukakufikiriafikiria
Sasa kwa kuwa wewe siyo mwanachama tena wa CHADEMA, lakini tunatambua mchango wako kwenye upinzani, unayo nafasi ya kumend ties na wananchi. Lazima uwe na subira sana kwenye hili, lazima uombe msamaha kwa wananchi kwa vitendo. Japo umekula haramu, umejirahisisha mbele ya madhalimu kwa sababu ya njaa yako ambayo kwa namna moja au nyingine imekuwa engineered makusudi na watesi wenu ambao leo hii wanajidanya kuwapendeni kumbe ni unafiki mtupu.
Mtesi wenu aligundua kuwa kuwachapa risasi ni counterproductive na inabackfire, sasa njia nzuri ni kuwachapa kiuchumi na kimahakama na hiyo ndo modus operandi yake, na kweli amefanikiwa ndiyo maana wengi katika kambi yenu wameunga mkono juhudi kutokana na njaa, na bahati mbaya na wewe Dada Halima hii teknic ya "njaa" imekusomba hata wewe.
Sasa iko hivi pambana sana kurudisha credibility kwetu, humohumo bungeni endelea kuzungumzia issues za wananchi. Kama ukitukosha huenda tukakufikiria kidogokidogo, lakini ukigeuka na kuwa mwanasiasa "malayamalaya", hakuna atakayekuwa na time wewe tena!
5. Jifunze wewe Dada, mafanikio ni zaidi ya pesa
Usaliti ni kansa, ondoa hii kansa once and for all. Hata ukienda CCM, kama una mentality hizi za kusalitisaliti sababu ya vijipesa na fursa, kamwe huwezi kuwa msaada kwa Taifa. Sellouts hawana nafasi kwenye mabaraza ya watu wa heshima. Jirekebishe!