CalvinKimaro
JF-Expert Member
- Sep 11, 2017
- 244
- 312
Amani iwe kwako!
Mimi nikiwa kama muumini wa Kanisa lako la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki nimeshangazwa na ujumbe ulioutuma katika barua ya wazi kwa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwani umeacha jukumu la msingi uliloitiwa na Mungu la kutuhubiria wananchi ili tuokoke na kumrudia Mungu.
Inafikirisha kukuona Askofu wangu ukiacha majukumu yako na kuanza kufanya siasa, najiuliza huo wito aliopewa na Mungu ni kwa ajili ya kuhubiri neno au kufanya siasa?
Nawaomba Mhe.Rais Magufuli pamoja na washauri wake na Watanzania kwa ujumla wenu muupuuze ujumbe huo alioutoa kwani hauna nia njema ya kutujenga Wananchi zaidi ya kutugawa.
Askofu wangu Mwamakula umesema kuwa unataka kufanya "Matembezi ya Hiyari" nchi nzima yenye lengo la kuuhamasisha Umma wa Tanzania kuhusu Kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandika Katiba Mpya. Najiuliza tu hivi nilishawahi kukusikia au kukuona ukifanya matembezi ya hiyari kuhamasisha watu kumjua Mungu na kuokoka? Jibu ni hapana!.
Kwanini ufanye matembezi hayo wakati matembezi ya kiimani hujawahi kufanya!? Hapo ndipo napata jibu kuwa matembezi hayo hayajaandaliwa na wewe bali wanasiasa ambao wanakutumia kutuvuruga wananchi baada ya kushindwa kutimiza azma yao ya kuvuruga uchaguzi Mkuu na kuiingiza nchi katika machafuko kipindi cha uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba 2020.
Matembezi hayo unayoyaita "Matembezi ya Hiyari" yanalenga kuhamasisha Wananchi kuandamana katika mikoa yote ya Tanzania na wilaya zake zote katika kipindi chote cha mwaka 2021 kufanya fujo kinyume na sheria za nchi.
Ikumbukwe kuwa mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa 28 Oktoba 2020, vyama vya upinzani pamoja na wewe Askofu mlitoa tamko kupitia Vyombo vya Habari kuwa Uchaguzi haukuwa huru na haki, mlihamasisha Wananchi kufanya maandamano kupinga matokeo ya uchaguzi, kudai kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kutaka Uchaguzi urudiwe.
Ni dhahiri Wananchi walishangazwa na madai hayo na wakayapuuza kwa kutojitokeza kufanya maandamano hayo ambayo ndani yake mliandaa vikundi vya wahuni kuchoma matairi ya magari barabarani, kuvunja maduka ya watu, kuchoma moto vituo vya mafuta na kufanya vurungu kwa Wananchi wengine ambao wasingekuwa tayari kuwaunga mkono.
Pia nasikia kuwa katika Matembezi hayo vikundi hivyo vya kufanya fujo mmeviandaa ili kutimiza yale mliyokusudia kuyafanya baada ya matokeo ya uchaguzi. Mmeandaa vijana wa kufanya fujo ili kuwalazimisha Polisi kutumia nguvu kuwadhibiti.
Ninapenda Askofu wangu Mwamakula utambue kuwa kwa mtazamo wangu, tangu matokeo ya Uchaguzi yalivyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamekuwa na juhudi kubwa ya vyama vya upinzani nchini kuwatumia viongozi wa dini ukiwemo wewe kujenga chuki na uhasama miongoni mwa Watanzania! kwa lengo la kulinda maslahi ya watu binafsi ambao ni Tundu Lissu na Freeman Mbowe.
Hali hii ya uhasama, chuki na kuwagawa Watanzania kwa ajili ya maslahi ya watu binafsi katika nchi haiwezi kuachwa kuendelea. Ni lazima sote kwa pamoja tukemee tabia hii mpya ambayo imeanza kujitokeza nchini, yakuwatumia viongozi wa dini kufanya siasa.
Ni kwa sababu hiyo, naamini kuwa "Matembezi ya Hiyari" yatatoa fursa kwa wafuasi wa upinzani kuanzisha mijadala ya kulilaumu Jeshi la Polisi kwani mtakapokatazwa kufanya matembezi mtaanza kulalamika kuwa mnaonewa na kunyimwa Uhuru jambo ambao si kweli. Kwa ujumla matembezi hayo yatahatarisha amani, suala la Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandikwa kwa Katiba Mpya unalitumia tu kama kisingizio cha kuhalalisha vurugu mlizopanga kuzifanya.
"Matembezi ya Hiyari" yatasimamisha shughuli za uzalishaji katika nchi, kwani mmepanga kufunga barabara na shughuli za kijamii kwa wakati huo.
Matembezi hayo yatavilazimu Vyombo vya Dola kutumia nguvu kuzuia au kuvuruga vikundi vya wahuni mliowaandaa kufanya vurugu wakati wa matembezi hayo.
Hivyo kuvifanya vyombo vya usalama kuonekana kuwa havitendi haki.
Mwisho ninapenda nikusihi Askofu wangu Mwamakula kutumia njia sahihi za kudai haki yako ambayo kwa namna moja au nyingine unahisi inaporwa badala ya kufanya matembezi ambayo yatazalisha vurugu na kutugawa Wananchi.
Ni imani yangu kuwa Mungu atasema na nafsi yako kuitii mamlaka kwani hata neno la Mungu katika biblia limetuagiza kutii mamlaka iliyo Kuu (Warumi 13:1) "Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu na ile iliyopo imeamriwa na Mungu".
Pia nawasihii Watanzania wenzangu kupuuza matembezi hayo na kujikita katika shughuli za ujenzi wa Taifa letu.
Mungu atusaidie kutambua mema na mabaya na atufanye kuwa nguzo za kudumisha amani na umoja. Waovu wasipate nafasi ya kuharibu nchi yetu iliyojaa amani na utulivu!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Lusajo Mwakanyamale.
Mimi nikiwa kama muumini wa Kanisa lako la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki nimeshangazwa na ujumbe ulioutuma katika barua ya wazi kwa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwani umeacha jukumu la msingi uliloitiwa na Mungu la kutuhubiria wananchi ili tuokoke na kumrudia Mungu.
Inafikirisha kukuona Askofu wangu ukiacha majukumu yako na kuanza kufanya siasa, najiuliza huo wito aliopewa na Mungu ni kwa ajili ya kuhubiri neno au kufanya siasa?
Nawaomba Mhe.Rais Magufuli pamoja na washauri wake na Watanzania kwa ujumla wenu muupuuze ujumbe huo alioutoa kwani hauna nia njema ya kutujenga Wananchi zaidi ya kutugawa.
Askofu wangu Mwamakula umesema kuwa unataka kufanya "Matembezi ya Hiyari" nchi nzima yenye lengo la kuuhamasisha Umma wa Tanzania kuhusu Kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandika Katiba Mpya. Najiuliza tu hivi nilishawahi kukusikia au kukuona ukifanya matembezi ya hiyari kuhamasisha watu kumjua Mungu na kuokoka? Jibu ni hapana!.
Kwanini ufanye matembezi hayo wakati matembezi ya kiimani hujawahi kufanya!? Hapo ndipo napata jibu kuwa matembezi hayo hayajaandaliwa na wewe bali wanasiasa ambao wanakutumia kutuvuruga wananchi baada ya kushindwa kutimiza azma yao ya kuvuruga uchaguzi Mkuu na kuiingiza nchi katika machafuko kipindi cha uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba 2020.
Matembezi hayo unayoyaita "Matembezi ya Hiyari" yanalenga kuhamasisha Wananchi kuandamana katika mikoa yote ya Tanzania na wilaya zake zote katika kipindi chote cha mwaka 2021 kufanya fujo kinyume na sheria za nchi.
Ikumbukwe kuwa mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa 28 Oktoba 2020, vyama vya upinzani pamoja na wewe Askofu mlitoa tamko kupitia Vyombo vya Habari kuwa Uchaguzi haukuwa huru na haki, mlihamasisha Wananchi kufanya maandamano kupinga matokeo ya uchaguzi, kudai kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kutaka Uchaguzi urudiwe.
Ni dhahiri Wananchi walishangazwa na madai hayo na wakayapuuza kwa kutojitokeza kufanya maandamano hayo ambayo ndani yake mliandaa vikundi vya wahuni kuchoma matairi ya magari barabarani, kuvunja maduka ya watu, kuchoma moto vituo vya mafuta na kufanya vurungu kwa Wananchi wengine ambao wasingekuwa tayari kuwaunga mkono.
Pia nasikia kuwa katika Matembezi hayo vikundi hivyo vya kufanya fujo mmeviandaa ili kutimiza yale mliyokusudia kuyafanya baada ya matokeo ya uchaguzi. Mmeandaa vijana wa kufanya fujo ili kuwalazimisha Polisi kutumia nguvu kuwadhibiti.
Ninapenda Askofu wangu Mwamakula utambue kuwa kwa mtazamo wangu, tangu matokeo ya Uchaguzi yalivyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamekuwa na juhudi kubwa ya vyama vya upinzani nchini kuwatumia viongozi wa dini ukiwemo wewe kujenga chuki na uhasama miongoni mwa Watanzania! kwa lengo la kulinda maslahi ya watu binafsi ambao ni Tundu Lissu na Freeman Mbowe.
Hali hii ya uhasama, chuki na kuwagawa Watanzania kwa ajili ya maslahi ya watu binafsi katika nchi haiwezi kuachwa kuendelea. Ni lazima sote kwa pamoja tukemee tabia hii mpya ambayo imeanza kujitokeza nchini, yakuwatumia viongozi wa dini kufanya siasa.
Ni kwa sababu hiyo, naamini kuwa "Matembezi ya Hiyari" yatatoa fursa kwa wafuasi wa upinzani kuanzisha mijadala ya kulilaumu Jeshi la Polisi kwani mtakapokatazwa kufanya matembezi mtaanza kulalamika kuwa mnaonewa na kunyimwa Uhuru jambo ambao si kweli. Kwa ujumla matembezi hayo yatahatarisha amani, suala la Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandikwa kwa Katiba Mpya unalitumia tu kama kisingizio cha kuhalalisha vurugu mlizopanga kuzifanya.
"Matembezi ya Hiyari" yatasimamisha shughuli za uzalishaji katika nchi, kwani mmepanga kufunga barabara na shughuli za kijamii kwa wakati huo.
Matembezi hayo yatavilazimu Vyombo vya Dola kutumia nguvu kuzuia au kuvuruga vikundi vya wahuni mliowaandaa kufanya vurugu wakati wa matembezi hayo.
Hivyo kuvifanya vyombo vya usalama kuonekana kuwa havitendi haki.
Mwisho ninapenda nikusihi Askofu wangu Mwamakula kutumia njia sahihi za kudai haki yako ambayo kwa namna moja au nyingine unahisi inaporwa badala ya kufanya matembezi ambayo yatazalisha vurugu na kutugawa Wananchi.
Ni imani yangu kuwa Mungu atasema na nafsi yako kuitii mamlaka kwani hata neno la Mungu katika biblia limetuagiza kutii mamlaka iliyo Kuu (Warumi 13:1) "Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu na ile iliyopo imeamriwa na Mungu".
Pia nawasihii Watanzania wenzangu kupuuza matembezi hayo na kujikita katika shughuli za ujenzi wa Taifa letu.
Mungu atusaidie kutambua mema na mabaya na atufanye kuwa nguzo za kudumisha amani na umoja. Waovu wasipate nafasi ya kuharibu nchi yetu iliyojaa amani na utulivu!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Lusajo Mwakanyamale.