Barua ya Papii Kocha kwa JK

Sanda Matuta

JF-Expert Member
May 9, 2007
949
134
Wakulu nimeiona hii ikizagaa za gaa kule kwa JayDee, naona kama watu wameogopa kuileta huku kwa haraka kama wafanyavyo kwa zengine. Labda kwa sababu ya history.

Hapa ni kwake mahara muafaka kwani ninaamini watu wengi wanasoma
JF (nadhani) hata mushemiwa rais.

Pia (siku moja kwenye taarifa ya habari ya TBC niliona akisoma habari furani kwenye page ya jf wakisisitiza habari kutoka kwenye chombo cha habari).

Sasa muheshimiwa kabla haijaja rasmi mezani kwako hii hapa barua.


MF/NA: 836'04 Johnson Nguza (Papii Kocha)
Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es Salaam


Mh. Rais Jamuhuri ya Muungano Tanzania

YAH: MAOMBI YA KUPEWA MSAADA (MSAMAHA) WA KUFUTIWA ADHABU YA KIFUNGO NILIYOPEWA NA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU.

Husika na somo hilo hapo juu. Mimi ni mfungwa katika gereza kuu Ukonga.
Kwa heshma na taadhima na kwa kutambua utu na huruma yako ya ki MUNGU ulionayo dhidi ya binadamu wenzako pamoja na mamlaka uliokabidhiwa na jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

Naanguka na kushika miguu yako mitukufu muheshimiwa rais. Na kuomba msaada (msamaha) kwako muheshimiwa rais
Kwa njia hii ya maandishi kusudi niweze kuondolewa adhabu ya kifungo cha maisha gerezani, niliyohukumiwa na mahakama tajwa hapo juu.

Mh.Rais mimi nimefungwa nikiwa bado kijana mwenye umri mdogo. Mpaka sasa natambua wazi hatima pamoja na dhamana ya maisha yangu ipo katika mikono yako mitukufu Mh. Rais.

Naomba huruma yako muheshimiwa Rais maana mimi ni mtoto wako ninaehitaji huruma yako wewe mzazi.
Natumaini kauli yako ya mwisho ndio itakayoleta pumzi ya uhai nafsini mwangu

Nakutakia kazi njema, afya njema na maisha marefu.
Mungu akubariki!

Wako mtiifu
NO:836'04
JOHNSON NGUZA (PAPII KOCHA)

Tahadhari:
Inaruhusiwa kuinakili hii story kama ilivyo ( i wont mind), ila sio vibaya pia mkitoa credit na sio kusema eti ni kutokana na vyanzo vyenu vya habari.
Walengwa mnajijua sio lazima nitaje majina (jaydee)
 
Sasa kama ni barua ya kwenda kwa Mkulu, kwa nini mumeianika hadharani?
Au ndio njia aliyoiomba mwenyewe Papii?
 
Thank sanda matuta kwa kutuletea hiyo barua, ila je umeomba ruhusa kwa Dada JIDE
 
Inagusa!..

Lakini kwanini iwekwe kwa Jaydee kwanza?

Jaydee ana mawsasiliano gani na Ikulu, au MKULU wa nchi husoma sana blogu ya JD?
HAPO NIFAFANULIWE!
 
Hiyo sio lugha ya Papii Kocha na barua rasmi haiandikwi hivyo - Wewe Paka Jimmy hujui JD ako kwenye System Gani - Chunguza utagundua kitu
 
Inagusa!..

Lakini kwanini iwekwe kwa Jaydee kwanza?

Jaydee ana mawsasiliano gani na Ikulu, au MKULU wa nchi husoma sana blogu ya JD?
HAPO NIFAFANULIWE!

Nadhani Jaydee alikwenda kumtembelea ndio akampa hiyo barua amsaidie kuifikisha kwa Mheshimiwa, ukiingia kwenye blog ya Jaydee utaiona imeandika kwa mkono, Jaydee akaipiga picha na kuiweka kwenye blog yake na baada ya kuona maandishi yanaonekana kwa mbali ndio akaamua kuiandika upya ili watu waweze kuisoma na walio karibu na Mh. Rais waweze kumfikishia ujumbe wakati yeye (Jaydee) anaendelea kutafuta taratibu za kumuona mh.Rais ampatie barua yake.
 
Hiyo sio lugha ya Papii Kocha na barua rasmi haiandikwi hivyo - Wewe Paka Jimmy hujui JD ako kwenye System Gani - Chunguza utagundua kitu
...Hivi huyo Papii amekwenda shule angalau hata darasa la 7? Barua haina kichwa, mwili wala mkia.....Mh! Huenda watu mnataka kutupisha baraza la kahawa tu humu....
 
BARUA YENYEWE INASOMEKA KAMA IFUATATAVYO:


MF/NA: 836'04 Johnson Nguza (Papii Kocha)
Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es Salaam


Mh. Rais Jamuhuri ya Muungano Tanzania


YAH: MAOMBI YA KUPEWA MSAADA (MSAMAHA) WA KUFUTIWA ADHABU YA KIFUNGO NILIYOPEWA NA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU.


Husika na somo hilo hapo juu. Mimi ni mfungwa katika gereza kuu Ukonga.
Kwa heshma na taadhima na kwa kutambua utu na huruma yako ya ki MUNGU ulionayo dhidi ya binadamu wenzako pamoja na mamlaka uliokabidhiwa na jamuhuri ya muungano wa Tanzania.


Naanguka na kushika miguu yako mitukufu muheshimiwa rais.
Na kuomba msaada (msamaha) kwako muheshimiwa rais
Kwa njia hii ya maandishi kusudi niweze kuondolewa adhabu ya kifungo cha maisha gerezani, niliyohukumiwa na mahakama tajwa hapo juu.


Mh.Rais mimi nimefungwa nikiwa bado kijana mwenye umri mdogo. Mpaka sasa natambua wazi hatima pamoja na dhamana ya maisha yangu ipo katika mikono yako mitukufu Mh. Rais.


Naomba huruma yako muheshimiwa Rais maana mimi ni mtoto wako ninaehitaji huruma yako wewe mzazi.
Natumaini kauli yako ya mwisho ndio itakayoleta pumzi ya uhai nafsini mwangu


Nakutakia kazi njema, afya njema na maisha marefu.
Mungu akubariki


Wako mtiifu
NO:836'04
JOHNSON NGUZA (PAPII KOCHA)


Na huo ndio mwisho wa barua alionitumia Papii ili imfikie Mh. Rais
 
Mkiisoma taratibu mtaelewa barua imetoka kwa nani kwenda kwanani,kumpitia nani?na maelezo yangu ya mwanzo kabla ya barua yanajieleza
 
Hivi kesi ya kubaka watoto huwa inahitaji msamaha wa Raisi??? naomba kuelimishwaaa
 
Hiyo sio lugha ya Papii Kocha na barua rasmi haiandikwi hivyo - Wewe Paka Jimmy hujui JD ako kwenye System Gani - Chunguza utagundua kitu

For sure sijui- Lakini si ungeweka wazi hapa Mkuu..kwani nini bana!
 
Nadhani Jaydee alikwenda kumtembelea ndio akampa hiyo barua amsaidie kuifikisha kwa Mheshimiwa, ukiingia kwenye blog ya Jaydee utaiona imeandika kwa mkono, Jaydee akaipiga picha na kuiweka kwenye blog yake na baada ya kuona maandishi yanaonekana kwa mbali ndio akaamua kuiandika upya ili watu waweze kuisoma na walio karibu na Mh. Rais waweze kumfikishia ujumbe wakati yeye (Jaydee) anaendelea kutafuta taratibu za kumuona mh.Rais ampatie barua yake.
Lakini ameshasema ni barua ya MKUU sio ujumbe
Ingekuwa ujumbe wa mkuu ingeeleweka kuwa ameuweka pale ili watu wamfikishie ujumbe wake sasa barua??? Ilipaswa iende moja kwa moja kwa mheshimiwa na si kuitundika pale- je siku mheshimiwa akitoa msamaha kwa wafungwa na Papii akisamehewa ndo tujue kuwa amesamehewa kwa vile aliomba msamaha hadharani?
 
waarabu wa pemba hao wajuana kwa vilemba, mara walilawiti mara wachache wamepata wameshinda kesi mara hivi mara vile, mazingira ya kesi hii yanawapa watu maswali mengi kuliko majibu, mimi binafsi sipendi sana kuamini kama kweli nguza na wanae wote walikuwa na uwezo wa kufanya uchafu huo kwa watoto, na halafu mazingira ya mwalimu wa watoto wale kutokukutwa na hatia vyote hiivyo kwangu ni kama comedy flani hivi! pole sana papiii we mic your music
 
Lakini ameshasema ni barua ya MKUU sio ujumbe
Ingekuwa ujumbe wa mkuu ingeeleweka kuwa ameuweka pale ili watu wamfikishie ujumbe wake sasa barua??? Ilipaswa iende moja kwa moja kwa mheshimiwa na si kuitundika pale- je siku mheshimiwa akitoa msamaha kwa wafungwa na Papii akisamehewa ndo tujue kuwa amesamehewa kwa vile aliomba msamaha hadharani?

Kuomba Huruma ya Rais sio siri....binti kaona kusubiri mpk apate nafasi ya kuonana na Mheshimiwa Rais itachukua muda sana, hivyo akaona njia nyepesi ni kuiweka barua kwenye blog yake.... na nina uhakika wengi wanasoma inawezena Rais huwa naperuz, hata kama sio yeye kuna watu wake wa karibu, watoto wake huwa wanapitia hiyo blog wakiiona watampa habari kwamba kuna barua yake soon itamfikia na dondoo watampa au kuprintia kabisa....
 
Hivi kesi ya kubaka watoto huwa inahitaji msamaha wa Raisi??? naomba kuelimishwaaa

Mara nyigi sana msamaha wa rais ukitoka kuwa hauwafikii watu wenye makosa kama mauaji, ubakaji, madawa ya kulevya n.k labda otherwise kwa mazingira kama ya uzee au ugonjwa..,kwa case ya Babu Seya sijui..,hebu tuendelee kusikilizia maana picha halijaisha bado na ukizingatia huu mwaka wa uchaguzi kila kitu kinawezekana.
 
Hivi huyu jamaa ni kweli alitenda hayo makosa? Mbona hazungumzii lolote kuhusu hilo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom