Barua ya Malcom X: Huko Makka Saudi Arabia

Katika kusafir kwangu hakuna watu mashetan kama waarabu. Na hakuna watu wanajiona cku zote wao wako juu kwa kila kitu kama wazungu. na hakuna watu wanaotafute hela kwa namna yoyote kama muasia. Waafrica cc sio watu wa kujifunza. Ni wazee wa lawama. Ni kama vile hawatak kukubali walishawahiwa so wajipange ili wajikomboe hilo hawalitak kila cku ni kulaumu tu mwanzo mwisho. Tumeshindwa kujifunza kwa japan. Maana baada ya kichapo walijipanga sasa hiv wako juu.
Hahaha kwahyo waafrika inshu yao ni blaming tu😂
 
Malcolm X au (Al-Hajj Malik El-Shabazz) huyu wengi wetu tunamjua wengineo wakimwiga na kufata matendo yake, na itikadi zake. Huyu mmarekani mweusi ambaye Alisiliimu na kuitwa jina maliki el shaabaz

Baada ya kufika MAKKA kama ilivyo amri hii kwenye vitabu vya dini ya kiislamu ni nguzo moja kati ya nguzo zinazojenga uislamu kuhiji makka , kwa mwenye uwezo.

Naye alilitimiza hili na ndani ya ibada hii akapata kuandika aliyojifunza na kuyapata huko 1964, huko alipata kuandika Barua juu ya aliyojifunza na kushuhudia huko

Barua yake aliyoiandika kutoka kwa Makka alipokuwa Hija Makkah, al-Hajj Malik El-Shabazz aliandika barua kwa wasaidizi wake waaminifu wa Harlem ...
View attachment 1711213

Na haya ni baadhi ya yaliyoandikwa katika

Barua ipo kama ifuatavyo

"Kamwe sikuwahi kushuhudia, Ukarimu wa dhati wa namna ile Na roho ya ukweli ya undugu ambao umefanywa na watu wa Rangi zote, Katika mji huu mkongwe na mtakatifu, Nyumbani kwa Ibrahim ,Muhammad na mitume wote , waliotajwa katika maandiko matukufu.

"Kwa wiki iliyopita nimekuwa kimya kutafakari , huku nikishuhudia neema ambayo nimeioona imeonyeshwa kila mahali na watu wa rangi zote"

"Nimepata bahati ya kutembelea mji mtukufu wa makka, nmekamilisha mizunguko yangu saba kuizunguka Al kaaba, nikiongozwa na kijana mdogo aitwaye Muhammad, Nmekunywa Maji kutoka katika visima vya ZamZam"

Nilikimbia mara saba nyuma kwenye vilima vya Safa na Marwah. Nikaswali na kuomba katika mji mtukufu wa kale wa Mina, na nikaswali juu ya Mlima Arafat.

" Kulikuwa na makumi na maelfu ya mahujaji, kutoka duniani kote. Walikuwa wa rangi zote, weupe kwa Waafrika wenye rangi nyeusi.
Lakini sisi wote tulishiriki katika ibada hiyo hiyo, tukiwa na roho ya umoja na udugu

kwamba katika uzoefu wangu wote nlipoishi huko Amerika uliniongoza kuamini haiwezekanii kuwepo mchanganyiko kati ya nyeupe na isiyo nyeupe.

" Amerika inahitaji kuuelewa Uislamu, kwa sababu hii ni dini ambayo inapinga na kuondoa katika jamii yake tatizo la utaifa. Katika safari zangu katika ulimwengu wa Kiislamu, nimekutana, nimezungumza na hata kula pamoja na watu ambao huko Amerika wangechukuliwa kama ni weupe lakini mtazamo wa rangi uliondolewa kwenye mawazo yao na dini ya Uislam"

"Sijawahi kuona udugu wa kweli uliofanywa na rangi zote pamoja, bila kujali rangi yao. "

Unaweza kushangazwa na maneno haya yanayotoka kwangu. Lakini juu ya safari hii, yale niliyoyaona, na uzoefu wangu, vimenifanya tena niweke upya mawazo yangu iyokuwa nayo hapo awali, na kutupa kando baadhi ya fikra za awali.

Hii haikuwa vigumu sana kwangu. Licha ya imani yangu imara, sikuzote nimekuwa mtu ambaye anajaribu kukabiliana na ukweli, na kukubali ukweli wa maisha kwa kupokea mafunzo mapya na ujuzi mpya unaomfumbua mtu.

Nimekuwa na akili ya wazi, ambayo ni muhimu inapaswa kwenda nayo pamoja ili kutafuta kubadilika.

"Katika siku kumi na moja hapa katika ulimwengu wa Kiislam, nimekula kwenye sahani , na kunywa katika kikombe kimoja, na kulala katika sakafu moja, huku tukimuabudu Mungu mmoja na waislamu wenzangu Weupe,
Nilihisi kuwa na uaminifu nilihisi kati ya Waislamu wa Afrika wa Nigeria, Sudan na hata Ghana. "

Tulikuwa ndugu kwa sababu imani yao katika Mungu mmoja iliondoa matabaka ya Rangi.


Niliweza kuona kutokana na hili, labda Wamarekani wazungu wanaweza kukubali Mungu mmoja basi labda, pia, wangeweza kukubali kwa kweli umoja katika Ubinadamu - na kusitisha ubaguzi, na kuzuia, na kuwadhuru wengine kwa suala la 'tofauti' zao katika rangi

Kwa ubaguzi , marekani ni sawa na Cancer isiyoponyeka, waamerika weupe wanapaswa kuopokea suluhisho

Labda inaweza kuokoa Amerika kutokana na maafa ya karibu ,uharibifu kama huo uliiletea Ujerumani Shida juu ya ubaguzi wa rangi ambao hatimaye ukawaangamiza Wajerumani wenyewe.

"Kila saa hapa katika Nchi Takatifu inaniwezesha kuwa na ufahamu mkubwa wa kiroho katika kile kinachotokea Amerika kati ya weusi na weupe.

Negro wa Marekani hawezi kuhukumiwa kwa chuki za kibaguzi- anajaribu kupinga miaka mia nne ya ubaguzi wa rangi wa wazungu wa Marekani. Lakini kama ubaguzi wa rangi unaongoza Amerika juu ya njia ya kujidhuru

Naamini, kutokana na uzoefu ambao nimekuwa nao, wazungu hawa kizazi cha vijana, katika vyuo vikuu na mashuleni wataona maandiko juu ya kuta na wengi wao watageuka njia ya kiroho na kufuata haki ya kweli

Kamwe sijawahi kuheshimiwa sana namna hii

Kamwe sijawahi kufanywa kujisikia mnyenyekevu zaidi.

Nani angeamini baraka ambazo zimefanywa juu ya mtu mweusi wa Amerika?

Siku chache zilizopita, mtu ambaye huko marekani angeitwa mzungu au mwanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa, balozi, au rafiki wa wafalme,yeye alinipa hoteli yake, na kitanda chake.

Kamwe nisingeweza hata kufikiria au kuota kwamba ningewahi kuwa mpokeaji wa heshima kama hizo - heshima ambazo huko Amerika zitapewa Mfalme , mtu mweupe na- sio mtu mweusi"

Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu wote.







(kutoka kwa Autobiography ya Malcolm X kwa msaada kutoka kwa Alex Haley, mwandishi wa ROOTS)

Malcolm X alifundisha mengi na kuona Mengi

Nyuzi hii ni baadhi ya yaliyoandikwa kwenye barua hio

UKIACHANA NA UDINI KUNA LA KUJIFUNZA hapa






DA VINCI XV
Kosa analofanya Malcom X ni kuchanganya DINI na Race!! Yaani anafungamanisha ukristo na uzungu/Caucasians afu Uislam na Uarabu!! As if Ukristo ulianzia marekani.

Tukienda kibiblia na Quran hakuna kitabu mojawapo kinachokubali ubaguzi wa rangi per se, vyote vinataka usawa kwa jamii zote.

Ni sawa na mtu aukosoe ujamaa kisa tu vitendo vya viongozi wa CCM au China!! Its wrong. Ukristo ulianzia mashariki ya kati huko huko ulikoanzia uislam so alipaswa aupime ukristo kwa maandiko na sio wazungu ambao wengi wao ni wakristo.
Mbona waafrika tuna ukarimu naturally ingawa walituita wapagani na washenzi? Ina maana kutokuwa na dini ni kuzuri kisa tu waafrika wana ukarimu na hatukuwa na ubaguzi? Je waarabu kma wazungu walivyotumika kwenye biashara ya utumwa ndio tuuchukie uislam au ukristo kisa ya kutufanyisha watumwa?

Vipe crusade za both waislam na wakristo walizotumia kusambaza dini zao je kwa kuwa walitubadili dini kwa kutumia upanga ndio tukatae imani zao?

Tusifungamanishe Tabia za wapractice dini na Vitabu vya dini!! ni kutengeneza incosistency zisizokuwepo.

NB: Mimi ni shabiki wa kutupwa wa Malcom X na wapigania usawa wote wa diaspora.
 
Kosa analofanya Malcom X ni kuchanganya DINI na Race!! Yaani anafungamanisha ukristo na uzungu/Caucasians afu Uislam na Uarabu!! As if Ukristo ulianzia marekani.

Tukienda kibiblia na Quran hakuna kitabu mojawapo kinachokubali ubaguzi wa rangi per se, vyote vinataka usawa kwa jamii zote.

Ni sawa na mtu aukosoe ujamaa kisa tu vitendo vya viongozi wa CCM au China!! Its wrong. Ukristo ulianzia mashariki ya kati huko huko ulikoanzia uislam so alipaswa aupime ukristo kwa maandiko na sio wazungu ambao wengi wao ni wakristo.
Mbona waafrika tuna ukarimu naturally ingawa walituita wapagani na washenzi? Ina maana kutokuwa na dini ni kuzuri kisa tu waafrika wana ukarimu na hatukuwa na ubaguzi? Je waarabu kma wazungu walivyotumika kwenye biashara ya utumwa ndio tuuchukie uislam au ukristo kisa ya kutufanyisha watumwa?

Vipe crusade za both waislam na wakristo walizotumia kusambaza dini zao je kwa kuwa walitubadili dini kwa kutumia upanga ndio tukatae imani zao?

Tusifungamanishe Tabia za wapractice dini na Vitabu vya dini!! ni kutengeneza incosistency zisizokuwepo.

NB: Mimi ni shabiki wa kutupwa wa Malcom X na wapigania usawa wote wa diaspora.
Shukraani kwa mchango mkuu🙏
 
Ndiyo tatizo la sisi ngozi nyeusi tunatapatapa sana ina maana huko uarabuni hakuna ubaguzi? Mbona walivyo tuletea dini zao walitufanya watumwa na kutuuza kama nazi.sasa jamaa kaenda kule tu akapewa kalimati na kachori akasahau matatizo yake yote.
Mi namuonaga tu kama snitch.

Historia za primary bado zinaendelea kuwapotosha,
 
Kwa hiyo upumbavu wake ni kuingia kwenye uislam au unataka kumasanisha nn?
Nadhani ungesoma maoni yangu mara mbilimbili kijana ungenielewa.

Au una maanisha wanao fuata dini ya uislam ni wapuuzi ila wanaofiata ukirsto ni werevu?
Sababu za baguzi kubwa lililofahamika kama Malcolm X kuanza kuamini kitu kinachoitwa Mungu ni kwamba "America kulikuwa kuna Makanisa, Usafiri na vinginevyo vya wazungu ila Makkah watu wanasali kwa races zote"

Pale mnapompondaga mawe shetani.
Sasa kwa mtu mwenye akili ataona na kutambua kuwa Malcom hakuwa na ufahamu wowote wa Biblia na wala hakuwa Mkristo na huu ndio ukweli.
Ebu fafanua kosa lake ni lipi mpaka uamue kumvunjia heshima kiasi hicho.
Simuheshimu na haitotokea nimuheshimu alishakufa imeisha habari yake.

Ni moja ya viongozi wa kimarekani ambao hawana heshima yoyote embu jaribu kutembelea America utajifunza historia ya Marekani vizuri kabisa mdogo wangu ukipata kumsikia huyo bogus njoo nihukumu
 
Watumwa kutoka Africa waliopelekwa uarabuni waliishia wapi? Mbona katika mataifa ya kiarabu hakuna kizazi cha watu weusi ambacho kinatokana na watumwa waliopelekwa huko enzi za biashara ya utumwa?

Hizi habari huwa mnaziokotoea wapi lakini!!!! Wewe na wenzio mnajuwaje waarabu walihusika na utumwa!!!! Nyie ndio walee mnaendeleza gurudumu la kuwakaririsha na kuwapandikiza watoto, wajukuu mpaka watukuu wenu chuki dhidi ya jamii hiyo.
 
Nadhani ungesoma maoni yangu mara mbilimbili kijana ungenielewa.


Sababu za baguzi kubwa lililofahamika kama Malcolm X kuanza kuamini kitu kinachoitwa Mungu ni kwamba "America kulikuwa kuna Makanisa, Usafiri na vinginevyo vya wazungu ila Makkah watu wanasali kwa races zote"

Pale mnapompondaga mawe shetani.
Sasa kwa mtu mwenye akili ataona na kutambua kuwa Malcom hakuwa na ufahamu wowote wa Biblia na wala hakuwa Mkristo na huu ndio ukweli.

Simuheshimu na haitotokea nimuheshimu alishakufa imeisha habari yake.

Ni moja ya viongozi wa kimarekani ambao hawana heshima yoyote embu jaribu kutembelea America utajifunza historia ya Marekani vizuri kabisa mdogo wangu ukipata kumsikia huyo bogus njoo nihukumu
Kwanza ww ni nani mpaka umpangie mtu aamini katika dini ipi?
Unacho takiwa kuangalia ni kile alicho kuwa ana pigania na si alikuwa anaamini katika dini gani, na ndio maana nyerere ni baba wa taifa ambalo lina utitiri wa dini.
Nyerere hapewi heshima ya baba wa taifa sababu ya ukatoriki wake bali amepata heshima hiyo kwa sababu ya alicho kuwa ana pigania ambacho ni sisi kuwa huru.
Huyu jamaa amewapigania watu weusi kiasi cha kifikia kuuawa kwa sababu ya harakati zake.
Yaan mtu aliye utoa sadaka uhai wake kwa ajili ya kupigania heshima ya mtu mweusi akiwemo wewe hapo, eti leo hii kawa mpumbavu kwa sababu tu alikuwa ahamini katika ulokore wenu ?

Pili ww ni mtu mwenye chuki dhidi ya waislamu na mm mtu mwenye chuki dhidi ya jamii nyingine hua namchukulia kama mpumbavu na asiye kuwa na akili hasa ukizingatia dunia ya sasa tunaishi kwa kutegemeana sana.
Mm huwa naamini katika kuheshimu kila mtu bila kujali kile anacho kiamini kwa sababu sijui ni nani atakuja kuwa msaada kwangu au kwa mtoto wangu au kwa ndugu yangu yeyote.
 
Kwanza ww ni nani mpaka umpangie mtu aamini katika dini ipi?
Binadamu mwenye msimamo mkali sana dhidi ya wajinga.
Unacho takiwa kuangalia ni kile alicho kuwa ana pigania na si alikuwa anaamini katika dini gani,
Umeuliza mimi ni nani hadi nimpangie mtu awe muumini wa dini gani ni nini hiki umeandika hapa?
na ndio maana nyerere ni baba wa taifa ambalo lina utitiri wa dini.
LOL! 😑
Nyerere hapewi heshima ya baba wa taifa sababu ya ukatoriki wake bali amepata heshima hiyo kwa sababu ya alicho kuwa ana pigania ambacho ni sisi kuwa huru.
Ahahahaha! Pole sana mdogo wangu.
Huyu jamaa amewapigania watu weusi kiasi cha kifikia kuuawa kwa sababu ya harakati zake.
Hujui chochote kuhusu Malcom ni kheri ungekaa kimya.
Yaan mtu aliye utoa sadaka uhai wake kwa ajili ya kupigania heshima ya mtu mweusi akiwemo wewe hapo,
Jesus Christ! Haufahamu chochote nje ya kuamini kwake juu ya dini kutoka kwenye upagani.
eti leo hii kawa mpumbavu kwa sababu tu alikuwa ahamini katika ulokore wenu ?
Ahamini 😢
Pili ww ni mtu mwenye chuki dhidi ya waislamu
Ni maoni yako
na mm mtu mwenye chuki dhidi ya jamii nyingine hua namchukulia kama mpumbavu na asiye kuwa na akili hasa ukizingatia dunia ya sasa tunaishi kwa kutegemeana sana.
Christians don't depend on Muslims but Moslems depend on Christians!
Kuanzia kwenye maandiko hadi maisha ya kila siku!

Am sorry for this!
Mm huwa naamini katika kuheshimu kila mtu bila kujali kile anacho kiamini kwa sababu sijui ni nani atakuja kuwa msaada kwangu au kwa mtoto wangu au kwa ndugu yangu yeyote.
Ni wewe keep it up
 
Hizi habari huwa mnaziokotoea wapi lakini!!!! Wewe na wenzio mnajuwaje waarabu walihusika na utumwa!!!! Nyie ndio walee mnaendeleza gurudumu la kuwakaririsha na kuwapandikiza watoto, wajukuu mpaka watukuu wenu chuki dhidi ya jamii hiyo.
Nenda hapo sudan leo hii. Utake kuoa mwarabu utapata jibu lake. Waarabu ni mashetan mkuu. Nimezunguka sana nchi zao sio watu wale.
 
Ndiyo maana alitwangwa shaba, uislamu ulishaingiliwa na wahuni, amerika waliona huyu mhuni akiachwa atakuja leta jihadi, wakafyeka mzizi.


Na Reverend (mchungaji) Martn luther king jr naye walihisi Ukristo umeingiliwa na Muhuni anayepinga ubaguzi na kutetea haki zilizokuwazikipingwa na Wakristo weupe naye akatwangwa shaba na hao wakristo wabaguzi.
 
Kuna Watu duniani wapuuzi sana,
Kumpuuza malcolm ni utovu tu wa nidhamu,alafu inawezekana hata uwepo wao huko,ni 7bu za struggle za Huyu jamaa,ile autobiography nimeisoma,Mimi ni mkatoliki,nimetembe sehemu nyingi duniani,jamaa ni exceptional,ni vile hakusoma sana,ila alikuwa gifted sana kwenye public speaking..
Kifo cha Malcolm,au harakati Zake zimefanya black Americans wengi kujivunia kuwa among Americans,
Malcolm amefundisha kuhusu equality,justice vitu hivyo si vya kuviomba,ni kuvichukua,haki haiombwi etc
Namna ya ufundishaji wake tu ilikuwa aggressive,lakini ni kwa sababu,unakuwa kushuhudia baba Yako mzazi akiuwawa kwa kufungwa kwenye rail ya train,chuki hiyo ni wachache sana kuigeuza kuwa upendo,
Walikuwa wakitofautiana kidogo tu na martin Luther king,namna ya Ku approach matatizo ya black americans those times,Mmoja ni mchungaji,mwingine ni raia tu wa kawaida,aliyekuwa akipitia struggle zote Za black americans to survive,in the end,Ile struggle ikamfanya maarufu dunia nzima,Watu wa namna yake wako wengi tu,bob marley(mwanamuziki),mandela (politician),hata nyerere alimtaja katika kitabu chake,Btw mwanangu wa kwanza I named after him..
 
Ndiyo tatizo la sisi ngozi nyeusi tunatapatapa sana ina maana huko uarabuni hakuna ubaguzi? Mbona walivyo tuletea dini zao walitufanya watumwa na kutuuza kama nazi.sasa jamaa kaenda kule tu akapewa kalimati na kachori akasahau matatizo yake yote.
Mi namuonaga tu kama snitch.
Umeongea point, sasa tujiulize mimi na ww chief, unadhani kila muarabu ni muislam!? Na kila muislam ana imani ya kweli!? Wapo waislam halafu wanatenda yale ambayo dini yao inakataza.. Akifanya jambo mkristo usiutoe maana ukristu sababu eti kafanya mkristu, kikubwa ni je ukristu ndio unavyotaka au huyu kapuyanga hilo 1.

Pili uislam ni njia ama tuseme namna ya kuishi kuanzia unaamka mpka unaenda kulala umefundisha kila kitu, hao waarabu wapo wengi tu washenzi, ndio maana walipelekewa mitume mingi ili ipate kuwaonya maovu yao.
Halafu kuleta dini huku si tatzo inawezekana walioleta dini walikuwa ni wale makanjanja.. Hiv hujawai kuona mtu anatongozea mistar ya biblia ili tu ampate demu(azini) au lake liende japo ni kinyume na mafundisho, leo unakuta muislam kapiga kanzu saafi, anaomba msaada wa ujenzi wa msikiti sehemu kumbe tapeli.. Huyo tusemaje..

Kuna vingi vya kujifunza.. Tusome kwanza tufaidi chief.. Dini ni imani.

Shukrani
 
Huwezi kutofautisha tabia za wanazi wa dini na dini zao, ukitaka kuilewa dini vizuri watazame wafuasi wake jinsi walivyoenenda na wanavyoendelea kuenenda.
Kosa analofanya Malcom X ni kuchanganya DINI na Race!! Yaani anafungamanisha ukristo na uzungu/Caucasians afu Uislam na Uarabu!! As if Ukristo ulianzia marekani.

Tukienda kibiblia na Quran hakuna kitabu mojawapo kinachokubali ubaguzi wa rangi per se, vyote vinataka usawa kwa jamii zote.

Ni sawa na mtu aukosoe ujamaa kisa tu vitendo vya viongozi wa CCM au China!! Its wrong. Ukristo ulianzia mashariki ya kati huko huko ulikoanzia uislam so alipaswa aupime ukristo kwa maandiko na sio wazungu ambao wengi wao ni wakristo.
Mbona waafrika tuna ukarimu naturally ingawa walituita wapagani na washenzi? Ina maana kutokuwa na dini ni kuzuri kisa tu waafrika wana ukarimu na hatukuwa na ubaguzi? Je waarabu kma wazungu walivyotumika kwenye biashara ya utumwa ndio tuuchukie uislam au ukristo kisa ya kutufanyisha watumwa?

Vipe crusade za both waislam na wakristo walizotumia kusambaza dini zao je kwa kuwa walitubadili dini kwa kutumia upanga ndio tukatae imani zao?

Tusifungamanishe Tabia za wapractice dini na Vitabu vya dini!! ni kutengeneza incosistency zisizokuwepo.

NB: Mimi ni shabiki wa kutupwa wa Malcom X na wapigania usawa wote wa diaspora.
 
Nimesoma darasani katika elimu ya sekondari.
Umefanikiwa kupata elimu angalau ya kidato cha nne?
Hizi habari huwa mnaziokotoea wapi lakini!!!! Wewe na wenzio mnajuwaje waarabu walihusika na utumwa!!!! Nyie ndio walee mnaendeleza gurudumu la kuwakaririsha na kuwapandikiza watoto, wajukuu mpaka watukuu wenu chuki dhidi ya jamii hiyo.
 
Jikite kwenye nyuzi za kula tunda kimasihara na za kumtafuta baba yake Diamond.
Aisee! kweli jf imejaa majitu ambayo ni broke sana, mtu kashasema ameleta uzi sio kwa ajili ya majibizano yenye mlengo wa kidini lakini kuna mangedere tayari yameanza kukuru kakara za kuharibu malengo ya mleta mada.
 
Back
Top Bottom