Barua kwa Waziri wa Katiba na Sheria: Tamko la uhalali wa ndoa ya Kiislamu

Sep 19, 2019
43
383
Bismillahir Rahmanir Rahiim

JUMUIYA NA TAASISI ZA
KIISLAMU TANZANIA
Barua Pepe- jtkt.tz@gmail.com
S.L.B, 2055, Dar es Salaam

Kumb: JTKT/WKS/B1/21/F-SHR. 31. 08. 2021.

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
WAZIRI WA SHERIA NA MAMBO YA KATIBA
S.L.P. 315, DODOMA.

YAH: TAMKO LA UHALALI WA NDOA YA KIISLAMU
Ndugu Waziri hivi karibuni umetoa kauli ya kuelekeza ndoa halali na haramu Tanzania. Miongoni mwa ndoa hizo ni ndoa ya Kiislamu. Katika hotuba yako umesema:

“Kiongozi wa Dini ambaye hajapata (idhini au), hajatambuliwa (au) kuruhusiwa na RITA kuwa msajili wa ndoa, ndoa anayoifunga kisheria ni batili”.

Katika maelezo hayo umeeleza kwamba ndoa itakayofungwa na mtu ambaye hajasajiliwa na serikali ndoa hiyo ni haramu. Ukifafanua zaidi ulisema ndoa hiyo inabatilishwa na sheria ya nchi.

Ndugu Waziri maelezo yako si sahihi kwa mizani ya Dini, Itifaki na Sharia ya nchi.

Kidini: Tunapenda uzingatie yafuatayo:

Ndoa ya Kiislamu ni ibada iliyoshushwa na Mwenyezi Mungu kwa Mtume Muhammad (SAW). Aya za ibada hiyo zimebainisha kila kitu kuhusu ndoa, tanzu zake na zimehifadhiwa vizuri ndani ya kitabu kitakatifu cha Qur’an na vile vile Sunna ya Mtume (SAW).

Ndoa ya Kiislamu inapofungwa kwa kuzingatia misingi hiyo ya Qur’ani Tukufu na Sunna ya Mtume (SAW), inakuwa halali. Kwa hiyo kiasili ndoa ya Kiislamu ni halali toka iliposhushwa na haijaharamishwa kwa Waislamu katika mazingira au zama zozote zile.

Katika misingi hiyo Mitukufu ya Qur,an na Sunna, hakuna kipengele cha cheti cha ndoa wala kipengele cha usajili wa mfungishaji. Bali kuna sifa za Maharusi na hao wafungishaji wa ndoa. Ndoa inapofungwa na Walii au Wakala muadilifu, ndoa hiyo inakua halali bila ya shaka yoyote. Itadumu kuwa halali mpaka pale itakapo koma au kuvunjika kwa misingi hiyohiyo ya Qur’an na Sunna.

Itifaki: Katika taifa letu kuna ndoa kubwa nne: Ndoa ya Kiislamu, ndoa ya Kikristo, ndoa ya Kimila na ndoa ya Serikali. Ndoa hizo zina wenyewe na wenyewe ndio wenye kauli na mamlaka kwa mujibu wa misingi ya ndoa hizo na Katiba ya nchi. Sheikh anapotoa kauli kuhusu ndoa ya Kikristo, au Padri anapotoa kauli kuhusu ndoa ya Kiislamu au Waziri anapotoa Fatwa kuhusu ndoa ya Kiislamu au ya Kikristo, mtu huyo anakuwa amechupa mipaka na kwenda kinyume na itifaki ya ustawi wa jamii.

Sheria: Kuhusu mtazamo wa sheria tunalo Bunge la kutunga sheria. Bunge hilo limeundwa na Wananchi. Makusudio ya wananchi kwa bunge lao ni kupanga na kuweka nidhamu ya mambo yao kwa pamoja. Kubwa miongoni mwa hayo ni kulinda haki zao za msingi kupitia sheria. Kwa muktadha huo bunge halina makusudio wala mamlaka ya kubadilisha Aya za Qur’an Tukufu au Biblia.

Katika dhana hiyo ya sheria na itifaki, bunge limetunga kanuni ya usajili wa ndoa zinazofungwa katika jamii. Lengo halisi la kanuni hiyo ni serikali kutambua kila ndoa na vilevile kuwa na takwimu za jambo hilo kubwa la kitaifa. Lengo la sheria ya tasjila kwa ndoa si sheria hiyo kuhalalisha au kuharamisha ndoa. Bali ni kufanya sensa itakayoiwezesha serikali kuwa na picha halisi ya jambo hilo pale itakapotaka kupanga au kutoa huduma stahiki katika jambo hilo.

Ndugu Waziri, tunakubaliana na wewe kwamba mtu ambaye atakayefungisha ndoa bila ya kusajiliwa RITA atakuwa amefanya kosa kwa mujibu wa sheria ya nchi. Ndugu Waziri jambo ambalo unatakiwa kuzingatia hapo ni kwamba kosa hilo halizuwii ndoa iliyofungwa chini ya misingi yake kuwa halali. Ndoa itakua halali hata kama mfungishaji hakusajiliwa na serikali. Kwa hiyo sheria uliyoitaja haiwezi kutengeneza adhabu kwa ndoa bali itatengeneza adhabu kwa yule aliyefungisha ndoa bila ya kusajiliwa. Maelezo yako kwamba: “…Ndoa anayoifungisha mtu huyo kisheria ni batili” yanatoa adhabu kwa ndoa na maharusi badala ya mfungishaji.

Kwa mujibu wa madhumuni ya sheria hiyo ulitakiwa utamke “wafungishaji batili wa ndoa wataadhibiwa”. Au “Ndoa iliyofungishwa na mfungishaji batili haitasajiliwa RITA”. Ni kinyume na sheria kutamka “ndoa hiyo ni batili”. Sheria uliyoitaja haina madhumuni wala mamlaka ya kuhalalisha na kubatilisha chochote katika Qur’an na Sunna.

Tumalizie kwa kukutakia kheri na utendaji mwema katika majukumu yako. Hata hivyo kuteleza ni jambo linalotokea kwa binadamu. Ni muhimu ukasimama tena kwenye vyombo vya habari kwaajili ya kusahihisha kasoro hiyo kubwa.

Tunatanguliza shukrani:
Wako katika utumishi wa Umma

* Sheikh PONDA ISSA PONDA
KATIBU MKUU*
Nakala:
• Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania (BARAZA KUU).
• Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
• Baraza la Sunna Tanzania (BASUTA).
• Shura ya Maimamu Tanzania.
• Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu (Hayatul-Ulamaa Tanzania).
• Tanzania Islamic Foundation (TIF).
• Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Tanzania.
• Chama cha Wanataaluma wa Kiislamu (TAMPRO).
• Alhikma Foundation.
• Jumuiya ya Wahadiri wa Kiislamu (ALMALID).
• Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
• Baraza la Wakristo Tanzania (CCT).
• Kanisa la Kilutheri Tanzania (KKKT).
• Uongozi wa Walokole (Tanzania).
• Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Matatizo makubwa katika Nchi iitwayo Tanzania ni watu wanaopewa mamlaka yauongozi kwa kisingizio cha elimu ya kisekula tu, hawana maono kwenye elimu ya dini hasa dini ya kiislamu Tanzania wamekuwa wakidharau kwenye nafasi kama hizi nyeti.,

Hawa kina Kabudi ndio mara huwapeleka watu Beijing waende wakadai haki zao huko mana ufinyu wao wakielimu hudhani hapa duniani tupo tupo tu kila kitu inabidi kipangwe na mwanadamu ambaye asili yake ameumbwa na Mungu, baadaE Mungu akampa miongozo kupitia kitabu chake.,

Ndoza za kiislamu iwe ni sahihi au imevunjia hakuna uhusiano wowote na sharia za kitwaghuti., Ndio mana kwenye bunge la katiba waislamu walitaka kuwe na Mahakama ya Kadhi kwa mambo kama haya leo mtu kama Kabudi anapata wapi mdogo kuwasemea waislamu kwenye ndoa zao.

Waislamu mambo yetu yapo katika kitabu kitakatifu (Quran).
 
Tatizo linaanzia juu kabisa.
Anaepaswa kuwakanya hawa wa chini yake yupo busy kujifanya tour guide na mmbongo movie.
Ni swala la wakati tutasikia viongozi wakiharamisha hata uvutaji pumzi kama hujasajiliwa nao.
 
Me mwenyewe nilishangaa sana et unasema huna uhalali wa kushika ugoni. Yaani niishi na mwanamke 5 years then atokee muhuni nimshuhudie anamtomba mie nimchekee tu et kisa sijafunga ndoa? Akiliza za mawaziri wengine ni upuuzi mtupu.
 
Bismillahir Rahmanir Rahiim

JUMUIYA NA TAASISI ZA
KIISLAMU TANZANIA
Barua Pepe- jtkt.tz@gmail.com
S.L.B, 2055, Dar es Salaam

Kumb: JTKT/WKS/B1/21/F-SHR. 31. 08. 2021.

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
WAZIRI WA SHERIA NA MAMBO YA KATIBA
S.L.P. 315, DODOMA.

YAH: TAMKO LA UHALALI WA NDOA YA KIISLAMU
Ndugu Waziri hivi karibuni umetoa kauli ya kuelekeza ndoa halali na haramu Tanzania. Miongoni mwa ndoa hizo ni ndoa ya Kiislamu. Katika hotuba yako umesema:

“Kiongozi wa Dini ambaye hajapata (idhini au), hajatambuliwa (au) kuruhusiwa na RITA kuwa msajili wa ndoa, ndoa anayoifunga kisheria ni batili”.

Katika maelezo hayo umeeleza kwamba ndoa itakayofungwa na mtu ambaye hajasajiliwa na serikali ndoa hiyo ni haramu. Ukifafanua zaidi ulisema ndoa hiyo inabatilishwa na sheria ya nchi.

Ndugu Waziri maelezo yako si sahihi kwa mizani ya Dini, Itifaki na Sharia ya nchi.

Kidini: Tunapenda uzingatie yafuatayo:

Ndoa ya Kiislamu ni ibada iliyoshushwa na Mwenyezi Mungu kwa Mtume Muhammad (SAW). Aya za ibada hiyo zimebainisha kila kitu kuhusu ndoa, tanzu zake na zimehifadhiwa vizuri ndani ya kitabu kitakatifu cha Qur’an na vile vile Sunna ya Mtume (SAW).

Ndoa ya Kiislamu inapofungwa kwa kuzingatia misingi hiyo ya Qur’ani Tukufu na Sunna ya Mtume (SAW), inakuwa halali. Kwa hiyo kiasili ndoa ya Kiislamu ni halali toka iliposhushwa na haijaharamishwa kwa Waislamu katika mazingira au zama zozote zile.

Katika misingi hiyo Mitukufu ya Qur,an na Sunna, hakuna kipengele cha cheti cha ndoa wala kipengele cha usajili wa mfungishaji. Bali kuna sifa za Maharusi na hao wafungishaji wa ndoa. Ndoa inapofungwa na Walii au Wakala muadilifu, ndoa hiyo inakua halali bila ya shaka yoyote. Itadumu kuwa halali mpaka pale itakapo koma au kuvunjika kwa misingi hiyohiyo ya Qur’an na Sunna.

Itifaki: Katika taifa letu kuna ndoa kubwa nne: Ndoa ya Kiislamu, ndoa ya Kikristo, ndoa ya Kimila na ndoa ya Serikali. Ndoa hizo zina wenyewe na wenyewe ndio wenye kauli na mamlaka kwa mujibu wa misingi ya ndoa hizo na Katiba ya nchi. Sheikh anapotoa kauli kuhusu ndoa ya Kikristo, au Padri anapotoa kauli kuhusu ndoa ya Kiislamu au Waziri anapotoa Fatwa kuhusu ndoa ya Kiislamu au ya Kikristo, mtu huyo anakuwa amechupa mipaka na kwenda kinyume na itifaki ya ustawi wa jamii.

Sheria: Kuhusu mtazamo wa sheria tunalo Bunge la kutunga sheria. Bunge hilo limeundwa na Wananchi. Makusudio ya wananchi kwa bunge lao ni kupanga na kuweka nidhamu ya mambo yao kwa pamoja. Kubwa miongoni mwa hayo ni kulinda haki zao za msingi kupitia sheria. Kwa muktadha huo bunge halina makusudio wala mamlaka ya kubadilisha Aya za Qur’an Tukufu au Biblia.

Katika dhana hiyo ya sheria na itifaki, bunge limetunga kanuni ya usajili wa ndoa zinazofungwa katika jamii. Lengo halisi la kanuni hiyo ni serikali kutambua kila ndoa na vilevile kuwa na takwimu za jambo hilo kubwa la kitaifa. Lengo la sheria ya tasjila kwa ndoa si sheria hiyo kuhalalisha au kuharamisha ndoa. Bali ni kufanya sensa itakayoiwezesha serikali kuwa na picha halisi ya jambo hilo pale itakapotaka kupanga au kutoa huduma stahiki katika jambo hilo.

Ndugu Waziri, tunakubaliana na wewe kwamba mtu ambaye atakayefungisha ndoa bila ya kusajiliwa RITA atakuwa amefanya kosa kwa mujibu wa sheria ya nchi. Ndugu Waziri jambo ambalo unatakiwa kuzingatia hapo ni kwamba kosa hilo halizuwii ndoa iliyofungwa chini ya misingi yake kuwa halali. Ndoa itakua halali hata kama mfungishaji hakusajiliwa na serikali. Kwa hiyo sheria uliyoitaja haiwezi kutengeneza adhabu kwa ndoa bali itatengeneza adhabu kwa yule aliyefungisha ndoa bila ya kusajiliwa. Maelezo yako kwamba: “…Ndoa anayoifungisha mtu huyo kisheria ni batili” yanatoa adhabu kwa ndoa na maharusi badala ya mfungishaji.

Kwa mujibu wa madhumuni ya sheria hiyo ulitakiwa utamke “wafungishaji batili wa ndoa wataadhibiwa”. Au “Ndoa iliyofungishwa na mfungishaji batili haitasajiliwa RITA”. Ni kinyume na sheria kutamka “ndoa hiyo ni batili”. Sheria uliyoitaja haina madhumuni wala mamlaka ya kuhalalisha na kubatilisha chochote katika Qur’an na Sunna.

Tumalizie kwa kukutakia kheri na utendaji mwema katika majukumu yako. Hata hivyo kuteleza ni jambo linalotokea kwa binadamu. Ni muhimu ukasimama tena kwenye vyombo vya habari kwaajili ya kusahihisha kasoro hiyo kubwa.

Tunatanguliza shukrani:
Wako katika utumishi wa Umma

* Sheikh PONDA ISSA PONDA
KATIBU MKUU*
Nakala:
• Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania (BARAZA KUU).
• Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
• Baraza la Sunna Tanzania (BASUTA).
• Shura ya Maimamu Tanzania.
• Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu (Hayatul-Ulamaa Tanzania).
• Tanzania Islamic Foundation (TIF).
• Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Tanzania.
• Chama cha Wanataaluma wa Kiislamu (TAMPRO).
• Alhikma Foundation.
• Jumuiya ya Wahadiri wa Kiislamu (ALMALID).
• Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
• Baraza la Wakristo Tanzania (CCT).
• Kanisa la Kilutheri Tanzania (KKKT).
• Uongozi wa Walokole (Tanzania).
• Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wakati mwingine kabla ya kutoa matamko haya ingefaa sana viongozi wakakutana na viongozi wa Dini kwa mashauriano zaidi
 
SIJAONA KOSA LA WAZIRI Yeye amesema "KISHERIA NI BATILI" na yeye yupo hapo kwa mujibu wa sheria za nchi HAJASEMA "KIDINI NI BATILI" wala bado HAJASEMA "KIJAMII NI BATILI"

Tukumbuke yapo mambo kadhaa IMANI ZETU ZINAPISHANA NA SHERIA ZA NCHI
Sheria imetoa muda maalum ukiishi na mwanamke huyo Ni mkeo hata Kama hamjafunga ndoa kisheria , mbona hajasema hii Sheria pia Ni batili?
 
Hapa ndugu zetu wataona wamenyimwa haki zao,wakati ni utaratibu wa Sheria
 
SIJAONA KOSA LA WAZIRI Yeye amesema "KISHERIA NI BATILI" na yeye yupo hapo kwa mujibu wa sheria za nchi HAJASEMA "KIDINI NI BATILI" wala bado HAJASEMA "KIJAMII NI BATILI"

Tukumbuke yapo mambo kadhaa IMANI ZETU ZINAPISHANA NA SHERIA ZA NCHI
Nawashangaa! Yeye kasema kwa mujibu wa sheria.
Walitaka avunje sheria ili kuridhisha kundi fulani lenye mtazamo kinzani?
 
Kwa hiyo sheria uliyoitaja haiwezi kutengeneza adhabu kwa ndoa bali itatengeneza adhabu kwa yule aliyefungisha ndoa bila ya kusajiliwa. Maelezo yako kwamba: “…Ndoa anayoifungisha mtu huyo kisheria ni batili” yanatoa adhabu kwa ndoa na maharusi badala ya mfungishaji.
 
Waziri anasimamia sheria ila wengi mnampiga mawe kama yeye ndiye katunga.

Alafu tutambue umuhinu wa sheria hauonekani kwa macho na ninavyofaham wanawake wa kiislamu wanaipenda hii japo hawawezi kusema mbele zenu, course zinawapa ulinzi wa ile tabia ya fukuza fukuza na kuachwa ovyo.
 
Hatutaki taifa letu liongozwe kidini. Tatizo mojawapo kubwa la nchi yetu ni watu wa serikali kujaribu kuleta mitazamo yao ya kidini kwenye uongozi wa nchi.
Matatizo makubwa katika Nchi iitwayo Tanzania ni watu wanaopewa mamlaka yauongozi kwa kisingizio cha elimu ya kisekula tu, hawana maono kwenye elimu ya dini hasa dini ya kiislamu Tanzania wamekuwa wakidharau kwenye nafasi kama hizi nyeti.,

Hawa kina Kabudi ndio mara huwapeleka watu Beijing waende wakadai haki zao huko mana ufinyu wao wakielimu hudhani hapa duniani tupo tupo tu kila kitu inabidi kipangwe na mwanadamu ambaye asili yake ameumbwa na Mungu, baadaE Mungu akampa miongozo kupitia kitabu chake.,

Ndoza za kiislamu iwe ni sahihi au imevunjia hakuna uhusiano wowote na sharia za kitwaghuti., Ndio mana kwenye bunge la katiba waislamu walitaka kuwe na Mahakama ya Kadhi kwa mambo kama haya leo mtu kama Kabudi anapata wapi mdogo kuwasemea waislamu kwenye ndoa zao.

Waislamu mambo yetu yapo katika kitabu kitakatifu (Quran).
 
Hayo mambo ya serikali kuongozwa na wenye dini yamepitwa na wakati
Wakati mwingine kabla ya kutoa matamko haya ingefaa sana viongozi wakakutana na viongozi wa Dini kwa mashauriano zaidi
 
Kama huyo mwanamke amekubali wewe ni nani umpangie?
Me mwenyewe nilishangaa sana et unasema huna uhalali wa kushika ugoni. Yaani niishi na mwanamke 5 years then atokee muhuni nimshuhudie anamtomba mie nimchekee tu et kisa sijafunga ndoa? Akiliza za mawaziri wengine ni upuuzi mtupu.
 
Hatutaki taifa letu liongozwe kidini. Tatizo mojawapo kubwa la nchi yetu ni watu wa serikali kujaribu kuleta mitazamo yao ya kidini kwenye uongozi wa nchi.
Ungejuwa definition ya dini wala usingeandika upuuzi huu.,

Dini ni mfumo wa maisha kwa mwanadamu., sasa unapojaribu kuiweka dini kama ni by the way issue lazima utakutana na hizo changamoto zisizokwisha., "mumelishwa na kuambiwa nchi yenu musiilete kwenye mitazamo ya kidini" lakini jiulize aliyesema na kuagiza maneno haya yeye ni kama nani? kwanini yeye aonekane kama ndio kioo cha maisha ya watu? taka kujua usikubali wazo la mtu wa kawaida likawa ndio sheria kwako na kuidumaza akili yako isiwe huru kuleta idea ambayo italeta mafanikio katika maisha yako lakini kwa nchi.
 
Matatizo makubwa katika Nchi iitwayo Tanzania ni watu wanaopewa mamlaka yauongozi kwa kisingizio cha elimu ya kisekula tu, hawana maono kwenye elimu ya dini hasa dini ya kiislamu Tanzania wamekuwa wakidharau kwenye nafasi kama hizi nyeti.,

Hawa kina Kabudi ndio mara huwapeleka watu Beijing waende wakadai haki zao huko mana ufinyu wao wakielimu hudhani hapa duniani tupo tupo tu kila kitu inabidi kipangwe na mwanadamu ambaye asili yake ameumbwa na Mungu, baadaE Mungu akampa miongozo kupitia kitabu chake.,

Ndoza za kiislamu iwe ni sahihi au imevunjia hakuna uhusiano wowote na sharia za kitwaghuti., Ndio mana kwenye bunge la katiba waislamu walitaka kuwe na Mahakama ya Kadhi kwa mambo kama haya leo mtu kama Kabudi anapata wapi mdogo kuwasemea waislamu kwenye ndoa zao.

Waislamu mambo yetu yapo katika kitabu kitakatifu (Quran).
Je, leo ikianzishwa dini inayoruhusu ndoa kati ya binadamu na mnyama, ndo hiyo ikubaliwe na serikali kisa tu serikali haiakiwi kuruka mipaka na kusimamia sheria zake?
 
Back
Top Bottom