RAIS WANGU KIKWETE BILA UMAKINI UTAIACHA NCHI KATIKA VISASI!
Rais wangu niliyasikiliza kwa makini sana mawaidha yaliyotolewa katika
swala ya Ijumaa iliyopita kama yalivyorushwa na kituo cha televisheni
cha TBC. Sheikhe alielekeza mawaidha yake katika maisha ya kiongozi wa
uma mtume Mohamad (SAW) na mafundisho yake.
Alisema mtume aliwafundisha waumini wake kuwapenda wengine hata kama
wale wengine siyo waislamu. Akahubiri amani na kuwataka waumini wake
kuwa watu wenye subira. Akasema hata ilipokuwa lazima kuingia katika
vita aliwaasa kutowadhuru akina mama, watoto, miti na mimea mingine.
Mawaidha yale yanamfanya mtu yeyote makini kujua na kuelewa kuwa
vurugu kama zile za Mbagala na zile za ijumaa iliyopita Kariakoo
haziko kwa mujibu wa dini ya kiislamu. Siyo uislamu ule! Ni vurugu na
fujo za wahuni fulani wanaotaka kuitumia dini vibaya.
Rais wangu ugaidi hauna dini. Ugaidi hauna kabila. Isipokuwa magaidi
wanapotaka kutekeleza matakwa yao ya kigaidi hutafuta mwavuli kwa
lengo la kutaka kuungwa mkono na maamuma na magaidi wenzao wengine.
Ndiyo maana utakuta magaidi wanaotumia ukabila kama wasomali au dini
kama ukristu au uislamu. Watu wa namna hii ni magaidi tu popote
wanapopatikana duniani, hata kama ni hapa kwetu Tanzania!
Unateteaje uislamu kwa kuvunja vioo vya gari la mwislamu mwenzako?
Tena ni muislamu tunayemjua kuwa ni swala tano! Hiki si kitendo cha
kiislamu, hiki ni kitendo cha kigaidi.
Ndugu Rais ni nani ameleta ugaidi nchini mwetu? Ugaidi nchini mwetu
umeletwa na wanasiasa uchwara, wachovu, waliofirisika kisiasa.
Wanasiasa dhaifu walipoona kampeni za chaguzi mbalimbali zinawaelemea
na hasa uchaguzi mkuu 2010, ndipo wakaanza kupandikiza sumu ya udini
ambayo sasa namshukuru Mungu imeanza kuwatafuna wenyewe. Nayo
itawamaliza vibaya muda si mrefu kwasababu sheria za magaidi ziko
wazi.
Siku zote Watanzania wamekuwa hawana udini lakini viongozi dhaifu
wakawa wanalazimisha wananchi waone kama kuna udini miongoni mwetu.
Watanzania kwa jadi yao siyo wadini. Tumekuwa na umoja, upendo na
mshikamano kwa muda mrefu sana. Na hata sasa Watanzania hawana udini.
Lakini tunao baadhi ya viongozi wanaolazimisha udini kwa maslahi yao
binafsi. Maamuma hawakosekani, wanawapata baadhi wanawaunga mkono.
Hali hii ya sasa inaweza kutazamwa kama ifuatavyo; Malofa hawa wa
kisiasa na hawa ambao wao walidhani ni maamuma wa kila kitu wakaunda
timu ya ushindi huku wanasiasa hawa wachovu wakiwaahidi karibu kila
kitu. Makundi haya mawili ambayo sasa yakawa kundi moja kila kundi
likiwa na lengo la kutaka kutawala nchi. Wakati kundi la wanasiasa
likianika wazi lengo lake, wenzao walifanya siri. Ili kufanikisha
lengo kila kundi liliona ni muhimu kupanda kwenye mgongo wa kundi
mwenza.
Wanasiasa ndio walioanza kuwapanda wenzao, wakafanikisha. Ushindi
ulipopatikana utekelezaji wa ahadi ukawa mgumu. Kuwaachia wenzao nao
wawapande mgongoni ili watimize lengo lao ni sawa na kuwaachia nchi.
Ikawa haiwezekani.
Rais wangu vurugu zote hizi ni kundi mwenza kulazimisha kundi la
wanasiasa kutimiza ahadi zao kama walivyokubaliana. Hapa hakuna dini.
Hapa kuna dili! Watu wamegeukana wenyewe kwa wenyewe. Ndiyo maana
hata kuwakamata imekuwa ngumu kwao. Watu wanasimama hadharani na
kukashfu dini za wengine serikali inachekelea tu. Magazeti yanatukana
huku radio na TV fitinishi vikitumika kukashfu dini zingine, serikali
inachekelea tu! Mungu mkubwa sasa yamewafika!
Ndugu Rais waliosema mkuki kwa nguruwe mtamu, kwa binadamu mchungu,
hawakuwa wajinga! Yanapochomwa makanisa serikali inacheeka huku ikitoa
machozi ya Mamba! Sasa mkuki umegeuka, serikali inashangaa, Ala,
kumbe! Jambo la hatari, tunachekelea? Lakini wamechelewa!
Katikati ya kadhia hii anatokeza waziri na kupiga marufuku mihadhara
ya kashfa kwa siku thelathini pekee. Yaani baada ya siku thelathini
kashfa ruksa ziendelee! Kupiga marufuku moja kwa moja kashfa
zinazotolewa dhidi ya dini nyingine kupitia mihadhara, magazeti, radio
na televisheni haiwezekani kwasababu ukifanya hivyo utakuwa unavunja
makubaliano. Na bado kidogo wanajua watawahitaji hawa; uchaguzi si
umesogea? Ni kweli kabisa, tutapata wapi waziri kama huyu! Hawa
ndiyo viongozi wetu! Sijui ni mikosi gani awamu hii ilizaliwa nayo!
Rais wangu katika hali kama hii wananchi watamsahau vipi Waziri wa
Mambo ya Ndani wa ukweli, Augustine Lyatonga Mrema? Nikikumbusha
utendaji wa mtu mahiri mjinga anadhani anabebwa mtu. Ni mbebe Mrema,
nimpeleke wapi? Umahiri wake katika utendaji kazi ndiyo unaombeba.
Naandika kuililia nchi yangu na amani kwa watu wake. Siandiki
kumfurahisha mtu. Ninaandika ninachokiamini kuwa ni sahihi. Kudhani
naweza kuandika anavyotaka mtu fulani au kwa upambe na kushabikia, ni
udhalilishaji. Badala ya kukumbatia vinavyowaunganisha wapuuzi
wamevingangania vinavyowatofautisha!
Rais wangu sitasita hata siku moja kuhoji ukimya wa waziri mkuu wangu
katika wakati huu ambao taifa linapita katika majaribu magumu hata
kama kwa kuhoji huko kutaifanya milima itikisike! Amani imetoweka.
Hofu katika mioyo ya wananchi imetamalaki. Wananchi wanaishi katika
wasiwasi mkubwa huku kanisa likilia machozi! Kwa tishio kubwa kwa
amani ya nchi kama hili waziri mkuu kuwa kimya na kuonekana kama
hayupo haliwezi kunyamaziwa hata kidogo!
Mwanamwema Kija kutoka Njiro, Arusha akaniandikia, Umesema kweli
mwalimu mkuu wa watu, Pinda siyo kama hayupo ni hayupo kabisaa! Mimi
naona serikali yote haipo. Nchi imewashinda sasa wanyonge hatumwoni
wakumshika mkono! Pamoja na yote Edward Lowassa ndo waziri mkuu pekee
angalau alifanya kazi! Yaani haingii akilini mpaka sasa Pinda hajasema
chochote, ama ni mgonjwa wametuficha?
Rais wangu, Pinda lazima aliliwe hata kama mbingu zitaanguka kwasababu
alipoteuliwa kuwa waziri mkuu aliwapa matumaini makubwa wananchi
ingawa yeye mwenyewe hakujua! Wananchi walijawa na matumaini makubwa
kwasababu Mizengo Pinda wakati hila za kutafuta madaraka zilipokuwa
zikifanywa na baadhi ya viongozi waliopo madarakani hivi sasa yeye
hakuwa mmoja wao! Hivyo wananchi walidhani angekuwa na nafasi nzuri ya
kuwa upande wao kwa maana wametelekezwa! Yeye hakuwa katika
majadiliano na wafanya vurugu wa sasa! Hawamdai kitu chochote.
Kama vile haitoshi, serikali imetangaza balaa la njaa! Ukimya huu wa
mtendaji mkuu ukiendelea unadhani nini kitatokea? Siyo kwakutaka kwetu
bali tunalazimishwa kukumbuka balaa la njaa lililopita. Tulishuhudia
Waziri mkuu Edward Lowassa alivyokuwa wakihaha nchi nzima kuhakikisha
maisha ya Watanzania hayapotei kwa sababu ya njaa. Nani asiyekumbuka
ziara ya Waziri mkuu Edward Lowassa kule Same? Njaa imeshika kasi,
wananchi wanataabika kwa njaa, mkurugenzi kakaa na mahindi ya njaa
ofisini! Eti Same yote hakukuwa na mtu mwenye uwezo wa kuyasafirisha.
Mtu huyu hakuwa na kile wadhaifu wanaita maamuzi magumu. Aliamua
mahindi yagawiwe kwa wananchi akiwepo! Wakati wakuondoka kurudi Dar es
salaam akaondoka na mkurugenzi; kazi ya mkurugenzi ikawa imeisha.
Mwangwi wake ukaenea katika masikio ya wakurugenzi wote nchi nzima!
Nani ataichezea serikali kwa kuwatesa wananchi? Kungekuwa na ukimya
kama huu kule Same wangekufa wananchi wangapi?
Lazima Waziri mkuu atokeze aseme na wananchi wanaoishi kwa wasiwasi
katika nchi yao. Atokeze awajibu Maaskofu wanaolia! Asimame akemee
ugaidi huu!
Maaskofu wanahoji, Watu hawa wavamie nini ndipo hatua zichukuliwe?
Wachome nini ndipo viongozi wenye dhamana ya kulinda mali na uhai
washtuke? Wamue nani ndipo iaminike kuwa watu hawa ni tishio kwa
usalama wa Taifa letu?
Ni nini hiki wanachosema Maaskofu kuwa, Katika mateso haya kanisa
litaimarika zaidi; na katika majivu haya ya Mbagala Tanzania mpya
itazaliwa na ukombozi wa kweli utapatikana?
Kabla yakusema hayo walisema, Kilichotokea Mbagala katika wiki ya
kuadhimisha siku ya Baba wa Taifa, ni kebehi si kwa baba wa Taifa tu,
bali kwetu sisi wenyewe tunaokalia kiti alichokalia Baba wa Taifa.
Kebehi kwetu sisi wenyewe tuliokalia kiti alichokalia Baba wa Taifa.
Ni nani huyu aliyekalia kiti cha Baba wa Taifa anayefanyiwa kebehi hii
halafu hajiwezi hata kujibu? Ninachokiona hapa ni kuchokwa na kutengwa
kwa waliokalia kiti alichokalia Baba wa Taifa. Kwasababu mbegu
waliyoipanda na kuaicha ikomae imeamua kupeleka machungu yake Ikulu,
basi matumaini ya Tanzania mpya itakayojali upendo, uvumilivu, umoja,
mshikamano, uhuru wa kuabudu na dola isiyo na dini kuzaliwa,
yatatimia! Ukombozi wa kweli utapatikana!
Tumeona katika kundi la watu waliofikishwa mahakamani ni mchanganyiko
wa makabila mbalimbali. Ni mchanganyiko wa dini tofautitofauti. Ni
mchanganyiko wa kada mbalimbali, vibaka, waporaji na wakora wote pia
wamo.
Hivyo siyo sahihi hata kidogo kuwatambulisha waliokamatwa wakifanya
uhalifu kwa kutumia kigezo kimoja tu cha dini. Kuwaita hawa wafanya
vurugu waislamu ni kutaka kuidhalilisha dini ya Mwenyezi Mungu kwa
kuihusisha na ugaidi. Uislam ni amani, upendo na uvumilivu! Kuchoma
makanisa ni ugaidi bila kujali kama waliochoma makanisa hayo ni
Wanyamwezi kwa kabila lao au Waislamu kwa dini yao!
Ni vema jamii na hasa viongozi wetu wa serikali na vyombo vya habari
kuacha kupotosha kwa kuwatambulisha waliotenda ugaidi huu kuwa ni
wanaharakati wa dini ya kiislamu. Waumini wema tuwakatae watu hawa na
hasa wakati huu ambao baadhi ya viongozi wetu wamekuwa kama samaki
waliomeza chambo chenye ndoani. Imebaki kuvuliwa tu!
Rai yangu kwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba
na wanatume wenzake wote watambue kuwa nao pia ni wananchi, hivyo
wasisahau kutoa maoni yao. Kati ya maoni yao wahakikishe katiba
itakayopatikana inaelekeza kwa uwazi njia halali ambazo wananchi
watazitumia kuitoa madarakani kabla ya muda wa uchaguzi, serikali
itakayothibitika kuwa imeshindwa kuongoza.
Moja ya sababu kubwa ambayo itoshe kuiondoa serikali iliyoko
madarakani ni pale itakapofikia uamuzi wa kuligeuza Jeshi la Ulinzi
wa wananchi JWTZ kuwa jeshi la kupambana na wananchi. Matumizi ya
Jeshi bila idhini ya Bunge ndivyo walivyokuwa wanafanya akina Iddi
Amin, Bokassa, Hittler na wenzake! Katika utawala uliostaarabika
kidemokrasia hii ni dhambi kubwa haikubaliki.
Nyingine iwe ni serikali kutuhumiwa kwa unyama na mauaji ya raia wasio
na hatia na hivyo kuwafanya wananchi waishi maisha ya hofu! Nchi kujaa
migomo na vurugu zinazowafanya wananchi kukosa amani nchini mwao.
Rais wangu hapa mlipowafikisha wananchi, nchi inatengeneza visasi
vingi! Bila kuwa makini kitakachofuata baada ya wewe kuondoka itakuwa
ni kulipizana visasi tu! Tutawaficha wapi watoto wetu na wana wa nchi
hii?
Robert Manumba mkurugenzi wa upelelezi nchini, akimlilia kamanda wa
Polisi wa mkoa wa Mwanza aliyeuawa na majambazi amewaamrisha Polisi
walipe kisasi dhidi ya raia. Ni tamko la bahati mbaya kwa wadhifa
alionao!
Wanawema wakaniambia mwalimu mkuu tushitakie huyu mtu kwa baba yako!
Kumbe baba ulikuwa Oman. Iweje uahirishe safari ya kwenda nje kutokana
na kifo cha mwigizaji wa michezo huku ukitoa ubani wa milioni kumi
halafu uende Oman wakati mauti yamemfika Kamanda wa Polisi wa mkoa wa
Mwanza, Liberatus Barlow?
Madhali baba Mwenyezi Mungu amekujalia umerudi salama wajibu watu
wako! Watu wa Mungu wanauliza je, na raia nao watumie amri hiyohiyo ya
Manumba kulipiza kisasi kwa Polisi majambazi waliowapora mali zao na
kisha kuwaua kinyama wanawema wafanyabiashara wa madini wa Ulanga na
dereva Taxi katika msitu wa Pande? Baba bila kuwa makini utaiacha nchi
katika visasi vya maangamizo!
PASCHALLY MAYEGA: MAKALA GAZETI LA TANZANIA DAIMA 10-24-2012
TEL 0713334239
Rais wangu niliyasikiliza kwa makini sana mawaidha yaliyotolewa katika
swala ya Ijumaa iliyopita kama yalivyorushwa na kituo cha televisheni
cha TBC. Sheikhe alielekeza mawaidha yake katika maisha ya kiongozi wa
uma mtume Mohamad (SAW) na mafundisho yake.
Alisema mtume aliwafundisha waumini wake kuwapenda wengine hata kama
wale wengine siyo waislamu. Akahubiri amani na kuwataka waumini wake
kuwa watu wenye subira. Akasema hata ilipokuwa lazima kuingia katika
vita aliwaasa kutowadhuru akina mama, watoto, miti na mimea mingine.
Mawaidha yale yanamfanya mtu yeyote makini kujua na kuelewa kuwa
vurugu kama zile za Mbagala na zile za ijumaa iliyopita Kariakoo
haziko kwa mujibu wa dini ya kiislamu. Siyo uislamu ule! Ni vurugu na
fujo za wahuni fulani wanaotaka kuitumia dini vibaya.
Rais wangu ugaidi hauna dini. Ugaidi hauna kabila. Isipokuwa magaidi
wanapotaka kutekeleza matakwa yao ya kigaidi hutafuta mwavuli kwa
lengo la kutaka kuungwa mkono na maamuma na magaidi wenzao wengine.
Ndiyo maana utakuta magaidi wanaotumia ukabila kama wasomali au dini
kama ukristu au uislamu. Watu wa namna hii ni magaidi tu popote
wanapopatikana duniani, hata kama ni hapa kwetu Tanzania!
Unateteaje uislamu kwa kuvunja vioo vya gari la mwislamu mwenzako?
Tena ni muislamu tunayemjua kuwa ni swala tano! Hiki si kitendo cha
kiislamu, hiki ni kitendo cha kigaidi.
Ndugu Rais ni nani ameleta ugaidi nchini mwetu? Ugaidi nchini mwetu
umeletwa na wanasiasa uchwara, wachovu, waliofirisika kisiasa.
Wanasiasa dhaifu walipoona kampeni za chaguzi mbalimbali zinawaelemea
na hasa uchaguzi mkuu 2010, ndipo wakaanza kupandikiza sumu ya udini
ambayo sasa namshukuru Mungu imeanza kuwatafuna wenyewe. Nayo
itawamaliza vibaya muda si mrefu kwasababu sheria za magaidi ziko
wazi.
Siku zote Watanzania wamekuwa hawana udini lakini viongozi dhaifu
wakawa wanalazimisha wananchi waone kama kuna udini miongoni mwetu.
Watanzania kwa jadi yao siyo wadini. Tumekuwa na umoja, upendo na
mshikamano kwa muda mrefu sana. Na hata sasa Watanzania hawana udini.
Lakini tunao baadhi ya viongozi wanaolazimisha udini kwa maslahi yao
binafsi. Maamuma hawakosekani, wanawapata baadhi wanawaunga mkono.
Hali hii ya sasa inaweza kutazamwa kama ifuatavyo; Malofa hawa wa
kisiasa na hawa ambao wao walidhani ni maamuma wa kila kitu wakaunda
timu ya ushindi huku wanasiasa hawa wachovu wakiwaahidi karibu kila
kitu. Makundi haya mawili ambayo sasa yakawa kundi moja kila kundi
likiwa na lengo la kutaka kutawala nchi. Wakati kundi la wanasiasa
likianika wazi lengo lake, wenzao walifanya siri. Ili kufanikisha
lengo kila kundi liliona ni muhimu kupanda kwenye mgongo wa kundi
mwenza.
Wanasiasa ndio walioanza kuwapanda wenzao, wakafanikisha. Ushindi
ulipopatikana utekelezaji wa ahadi ukawa mgumu. Kuwaachia wenzao nao
wawapande mgongoni ili watimize lengo lao ni sawa na kuwaachia nchi.
Ikawa haiwezekani.
Rais wangu vurugu zote hizi ni kundi mwenza kulazimisha kundi la
wanasiasa kutimiza ahadi zao kama walivyokubaliana. Hapa hakuna dini.
Hapa kuna dili! Watu wamegeukana wenyewe kwa wenyewe. Ndiyo maana
hata kuwakamata imekuwa ngumu kwao. Watu wanasimama hadharani na
kukashfu dini za wengine serikali inachekelea tu. Magazeti yanatukana
huku radio na TV fitinishi vikitumika kukashfu dini zingine, serikali
inachekelea tu! Mungu mkubwa sasa yamewafika!
Ndugu Rais waliosema mkuki kwa nguruwe mtamu, kwa binadamu mchungu,
hawakuwa wajinga! Yanapochomwa makanisa serikali inacheeka huku ikitoa
machozi ya Mamba! Sasa mkuki umegeuka, serikali inashangaa, Ala,
kumbe! Jambo la hatari, tunachekelea? Lakini wamechelewa!
Katikati ya kadhia hii anatokeza waziri na kupiga marufuku mihadhara
ya kashfa kwa siku thelathini pekee. Yaani baada ya siku thelathini
kashfa ruksa ziendelee! Kupiga marufuku moja kwa moja kashfa
zinazotolewa dhidi ya dini nyingine kupitia mihadhara, magazeti, radio
na televisheni haiwezekani kwasababu ukifanya hivyo utakuwa unavunja
makubaliano. Na bado kidogo wanajua watawahitaji hawa; uchaguzi si
umesogea? Ni kweli kabisa, tutapata wapi waziri kama huyu! Hawa
ndiyo viongozi wetu! Sijui ni mikosi gani awamu hii ilizaliwa nayo!
Rais wangu katika hali kama hii wananchi watamsahau vipi Waziri wa
Mambo ya Ndani wa ukweli, Augustine Lyatonga Mrema? Nikikumbusha
utendaji wa mtu mahiri mjinga anadhani anabebwa mtu. Ni mbebe Mrema,
nimpeleke wapi? Umahiri wake katika utendaji kazi ndiyo unaombeba.
Naandika kuililia nchi yangu na amani kwa watu wake. Siandiki
kumfurahisha mtu. Ninaandika ninachokiamini kuwa ni sahihi. Kudhani
naweza kuandika anavyotaka mtu fulani au kwa upambe na kushabikia, ni
udhalilishaji. Badala ya kukumbatia vinavyowaunganisha wapuuzi
wamevingangania vinavyowatofautisha!
Rais wangu sitasita hata siku moja kuhoji ukimya wa waziri mkuu wangu
katika wakati huu ambao taifa linapita katika majaribu magumu hata
kama kwa kuhoji huko kutaifanya milima itikisike! Amani imetoweka.
Hofu katika mioyo ya wananchi imetamalaki. Wananchi wanaishi katika
wasiwasi mkubwa huku kanisa likilia machozi! Kwa tishio kubwa kwa
amani ya nchi kama hili waziri mkuu kuwa kimya na kuonekana kama
hayupo haliwezi kunyamaziwa hata kidogo!
Mwanamwema Kija kutoka Njiro, Arusha akaniandikia, Umesema kweli
mwalimu mkuu wa watu, Pinda siyo kama hayupo ni hayupo kabisaa! Mimi
naona serikali yote haipo. Nchi imewashinda sasa wanyonge hatumwoni
wakumshika mkono! Pamoja na yote Edward Lowassa ndo waziri mkuu pekee
angalau alifanya kazi! Yaani haingii akilini mpaka sasa Pinda hajasema
chochote, ama ni mgonjwa wametuficha?
Rais wangu, Pinda lazima aliliwe hata kama mbingu zitaanguka kwasababu
alipoteuliwa kuwa waziri mkuu aliwapa matumaini makubwa wananchi
ingawa yeye mwenyewe hakujua! Wananchi walijawa na matumaini makubwa
kwasababu Mizengo Pinda wakati hila za kutafuta madaraka zilipokuwa
zikifanywa na baadhi ya viongozi waliopo madarakani hivi sasa yeye
hakuwa mmoja wao! Hivyo wananchi walidhani angekuwa na nafasi nzuri ya
kuwa upande wao kwa maana wametelekezwa! Yeye hakuwa katika
majadiliano na wafanya vurugu wa sasa! Hawamdai kitu chochote.
Kama vile haitoshi, serikali imetangaza balaa la njaa! Ukimya huu wa
mtendaji mkuu ukiendelea unadhani nini kitatokea? Siyo kwakutaka kwetu
bali tunalazimishwa kukumbuka balaa la njaa lililopita. Tulishuhudia
Waziri mkuu Edward Lowassa alivyokuwa wakihaha nchi nzima kuhakikisha
maisha ya Watanzania hayapotei kwa sababu ya njaa. Nani asiyekumbuka
ziara ya Waziri mkuu Edward Lowassa kule Same? Njaa imeshika kasi,
wananchi wanataabika kwa njaa, mkurugenzi kakaa na mahindi ya njaa
ofisini! Eti Same yote hakukuwa na mtu mwenye uwezo wa kuyasafirisha.
Mtu huyu hakuwa na kile wadhaifu wanaita maamuzi magumu. Aliamua
mahindi yagawiwe kwa wananchi akiwepo! Wakati wakuondoka kurudi Dar es
salaam akaondoka na mkurugenzi; kazi ya mkurugenzi ikawa imeisha.
Mwangwi wake ukaenea katika masikio ya wakurugenzi wote nchi nzima!
Nani ataichezea serikali kwa kuwatesa wananchi? Kungekuwa na ukimya
kama huu kule Same wangekufa wananchi wangapi?
Lazima Waziri mkuu atokeze aseme na wananchi wanaoishi kwa wasiwasi
katika nchi yao. Atokeze awajibu Maaskofu wanaolia! Asimame akemee
ugaidi huu!
Maaskofu wanahoji, Watu hawa wavamie nini ndipo hatua zichukuliwe?
Wachome nini ndipo viongozi wenye dhamana ya kulinda mali na uhai
washtuke? Wamue nani ndipo iaminike kuwa watu hawa ni tishio kwa
usalama wa Taifa letu?
Ni nini hiki wanachosema Maaskofu kuwa, Katika mateso haya kanisa
litaimarika zaidi; na katika majivu haya ya Mbagala Tanzania mpya
itazaliwa na ukombozi wa kweli utapatikana?
Kabla yakusema hayo walisema, Kilichotokea Mbagala katika wiki ya
kuadhimisha siku ya Baba wa Taifa, ni kebehi si kwa baba wa Taifa tu,
bali kwetu sisi wenyewe tunaokalia kiti alichokalia Baba wa Taifa.
Kebehi kwetu sisi wenyewe tuliokalia kiti alichokalia Baba wa Taifa.
Ni nani huyu aliyekalia kiti cha Baba wa Taifa anayefanyiwa kebehi hii
halafu hajiwezi hata kujibu? Ninachokiona hapa ni kuchokwa na kutengwa
kwa waliokalia kiti alichokalia Baba wa Taifa. Kwasababu mbegu
waliyoipanda na kuaicha ikomae imeamua kupeleka machungu yake Ikulu,
basi matumaini ya Tanzania mpya itakayojali upendo, uvumilivu, umoja,
mshikamano, uhuru wa kuabudu na dola isiyo na dini kuzaliwa,
yatatimia! Ukombozi wa kweli utapatikana!
Tumeona katika kundi la watu waliofikishwa mahakamani ni mchanganyiko
wa makabila mbalimbali. Ni mchanganyiko wa dini tofautitofauti. Ni
mchanganyiko wa kada mbalimbali, vibaka, waporaji na wakora wote pia
wamo.
Hivyo siyo sahihi hata kidogo kuwatambulisha waliokamatwa wakifanya
uhalifu kwa kutumia kigezo kimoja tu cha dini. Kuwaita hawa wafanya
vurugu waislamu ni kutaka kuidhalilisha dini ya Mwenyezi Mungu kwa
kuihusisha na ugaidi. Uislam ni amani, upendo na uvumilivu! Kuchoma
makanisa ni ugaidi bila kujali kama waliochoma makanisa hayo ni
Wanyamwezi kwa kabila lao au Waislamu kwa dini yao!
Ni vema jamii na hasa viongozi wetu wa serikali na vyombo vya habari
kuacha kupotosha kwa kuwatambulisha waliotenda ugaidi huu kuwa ni
wanaharakati wa dini ya kiislamu. Waumini wema tuwakatae watu hawa na
hasa wakati huu ambao baadhi ya viongozi wetu wamekuwa kama samaki
waliomeza chambo chenye ndoani. Imebaki kuvuliwa tu!
Rai yangu kwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba
na wanatume wenzake wote watambue kuwa nao pia ni wananchi, hivyo
wasisahau kutoa maoni yao. Kati ya maoni yao wahakikishe katiba
itakayopatikana inaelekeza kwa uwazi njia halali ambazo wananchi
watazitumia kuitoa madarakani kabla ya muda wa uchaguzi, serikali
itakayothibitika kuwa imeshindwa kuongoza.
Moja ya sababu kubwa ambayo itoshe kuiondoa serikali iliyoko
madarakani ni pale itakapofikia uamuzi wa kuligeuza Jeshi la Ulinzi
wa wananchi JWTZ kuwa jeshi la kupambana na wananchi. Matumizi ya
Jeshi bila idhini ya Bunge ndivyo walivyokuwa wanafanya akina Iddi
Amin, Bokassa, Hittler na wenzake! Katika utawala uliostaarabika
kidemokrasia hii ni dhambi kubwa haikubaliki.
Nyingine iwe ni serikali kutuhumiwa kwa unyama na mauaji ya raia wasio
na hatia na hivyo kuwafanya wananchi waishi maisha ya hofu! Nchi kujaa
migomo na vurugu zinazowafanya wananchi kukosa amani nchini mwao.
Rais wangu hapa mlipowafikisha wananchi, nchi inatengeneza visasi
vingi! Bila kuwa makini kitakachofuata baada ya wewe kuondoka itakuwa
ni kulipizana visasi tu! Tutawaficha wapi watoto wetu na wana wa nchi
hii?
Robert Manumba mkurugenzi wa upelelezi nchini, akimlilia kamanda wa
Polisi wa mkoa wa Mwanza aliyeuawa na majambazi amewaamrisha Polisi
walipe kisasi dhidi ya raia. Ni tamko la bahati mbaya kwa wadhifa
alionao!
Wanawema wakaniambia mwalimu mkuu tushitakie huyu mtu kwa baba yako!
Kumbe baba ulikuwa Oman. Iweje uahirishe safari ya kwenda nje kutokana
na kifo cha mwigizaji wa michezo huku ukitoa ubani wa milioni kumi
halafu uende Oman wakati mauti yamemfika Kamanda wa Polisi wa mkoa wa
Mwanza, Liberatus Barlow?
Madhali baba Mwenyezi Mungu amekujalia umerudi salama wajibu watu
wako! Watu wa Mungu wanauliza je, na raia nao watumie amri hiyohiyo ya
Manumba kulipiza kisasi kwa Polisi majambazi waliowapora mali zao na
kisha kuwaua kinyama wanawema wafanyabiashara wa madini wa Ulanga na
dereva Taxi katika msitu wa Pande? Baba bila kuwa makini utaiacha nchi
katika visasi vya maangamizo!
PASCHALLY MAYEGA: MAKALA GAZETI LA TANZANIA DAIMA 10-24-2012
TEL 0713334239