Eng. Zezudu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2012
- 7,811
- 10,819
Eng. Zezudu,
S.L.P. .......,
Mbyct,
11/11/2020.
Rais wa JMT,
Dr. John P Magufuli,
S.l.p.. .....
Ikulu, Chamwino,
Dodoma.
Mpendwa Mheshiwa rais,
YAH. MAOMBI YA KAZI NDOGO AMBAYO ULIMUAHIDI TUNDU A LISSU KIPINDI CHA KAMPENI KAMA AGEACHANA NA KUPAMBANIA NAFASI HIYO AMBAYO ALIJUA KABISA HATA SHINDA
Husika na kichwa cha habari hapo juu , Kama kinavyojieleza, pia napenda kukupongeza kwa moyo wangu wote kwa ushindi wa kishindo ulioupata katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 28/10/2020, hongera sana.
Mimi ni kijana wa miaka 28+, Mtanzania, mwenye elimu ya shahada ya uhandisi umeme, kijana mwenye mtazamo mzuri kwa maendeleo ya nchi yetu, naweza sema I have bright future and prolific man.
Katika kipindi cha kampeni uliahidi kumpatia mwanasheria mzoefu na mwanaharakati mbobezi ndugu Tundu A Lissu kazi ndogo kama angeachana na kupambania nafasi ya urais ambayo asingeweza kushinda.
Nimechukua maamuzi haya ya kuomba hii nafasi baada ya Ndugu ,Tundu A Lissu kuondoka nchini na kwenda ughaibuni huko kwa mabeberu na kuikataa ofa ya kazi uliyompatia.
Hakika Mbinu, uwezo na akili ninazo za kuweza kufiti hiyo nafasi uliyomuhaidi ndugu yetu na Mtanzania mwenzetu, Tundu Lissu na najua Watanzania wengi wanaitolea macho hii nafasi na nimeona niwe wa kwanza kuandika barua ya wazi ya kuomba hii nafasi ambayo kama nitaipata nitaitumikia kwa moyo wote na kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.
Wako mtiifu
Eng. Zezudu
Nakala:
Kwa wale wote wanao pambania nafasi hii ,
S.L.P. .......,
Mbyct,
11/11/2020.
Rais wa JMT,
Dr. John P Magufuli,
S.l.p.. .....
Ikulu, Chamwino,
Dodoma.
Mpendwa Mheshiwa rais,
YAH. MAOMBI YA KAZI NDOGO AMBAYO ULIMUAHIDI TUNDU A LISSU KIPINDI CHA KAMPENI KAMA AGEACHANA NA KUPAMBANIA NAFASI HIYO AMBAYO ALIJUA KABISA HATA SHINDA
Husika na kichwa cha habari hapo juu , Kama kinavyojieleza, pia napenda kukupongeza kwa moyo wangu wote kwa ushindi wa kishindo ulioupata katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 28/10/2020, hongera sana.
Mimi ni kijana wa miaka 28+, Mtanzania, mwenye elimu ya shahada ya uhandisi umeme, kijana mwenye mtazamo mzuri kwa maendeleo ya nchi yetu, naweza sema I have bright future and prolific man.
Katika kipindi cha kampeni uliahidi kumpatia mwanasheria mzoefu na mwanaharakati mbobezi ndugu Tundu A Lissu kazi ndogo kama angeachana na kupambania nafasi ya urais ambayo asingeweza kushinda.
Nimechukua maamuzi haya ya kuomba hii nafasi baada ya Ndugu ,Tundu A Lissu kuondoka nchini na kwenda ughaibuni huko kwa mabeberu na kuikataa ofa ya kazi uliyompatia.
Hakika Mbinu, uwezo na akili ninazo za kuweza kufiti hiyo nafasi uliyomuhaidi ndugu yetu na Mtanzania mwenzetu, Tundu Lissu na najua Watanzania wengi wanaitolea macho hii nafasi na nimeona niwe wa kwanza kuandika barua ya wazi ya kuomba hii nafasi ambayo kama nitaipata nitaitumikia kwa moyo wote na kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.
Wako mtiifu
Eng. Zezudu
Nakala:
Kwa wale wote wanao pambania nafasi hii ,
- Pascal Mayalla,
- USSR,
- Wengine wote ambao mnapamba kuipata hii nafasi .