Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,201
- 236
Dear ,
Mwaaa
Habari zako , za moyo wako , za tabasamu lako , za kicheko chako , sauti yako na kila kitu kizuri chako ? Najua kila kitu kitakuwa safi sana kuanzia moyo wako mzuri na mtamu uliojaa upendo na mapenzi ya dhati kabisa ulio mkweli na mvumilivu .
Angalia ndani ya moyo wako , utakuta hakuna kitu cha kuficha , pengine unaweza kuficha kwa sababu ni wajibu wa kila mtu katika maisha yake , lakini linapokuja suala la kupendana basi mambo ya kuficha hakuna tena kama ukiwa na uhakika kuhusu uhusiano wako .
Nikifikiria kuhusu wewe , nafikiria kuhusu dunia ya mapenzi iliyo nyooka na iliyo katika njia sahihi kabisa , mpaka hapo jua tu mimi na wewe mpaka milele kwenye mabonde twende , baharini tuogelee hata hewani tutapaa .
Tabasamu lako ambalo ndio nalipenda zaidi , na kila mara huwa nalihisi liko mbeleni mwangu lakini kama unavyojua muda mwingi uko mbali najaribu kufikiri tu je kama tungekuwa tuko wote masaa 24 siku 7 usiku na mchana sijui ningesema maneno gani kusema za ukweli namisi tabasamu lako maridani .
Kicheko chako ambacho nikisikia moyo wangu huenda kasi kuliko wakati wowote ule , Dear labda nikuambie kitu Fulani , mimi napenda sana kusikia vicheko , unajua kuna wakati ukiwa sehemu Fulani Fulani jinsi unavyocheka ndio watu wale wanavyoweza kukuweka katika kundi gani , wewe kicheko chako nakuweka katika kundi la wanadamu maridani .
Hiyo sauti yako ni zaidi ya Coco Lee , honey kama hujui au hujawahi kusikia , Coco Lee ndio mwanamuziki wa kike mwenye sauti ya mvuto zaidi duniani mpaka sasa hivi , moja ya nyimbo nzuri kabisa aliimba na Julio Iglesius inaitwa WHEN U TELL ME THAT U LOVE ME kwahiyo wewe ni zaidi yake , pengine ungeamua kuimba leo ningekuwa naandika kuhusu kitu kingine cha zaidi .
Honey huwa napata furaha sana kila ninapopata wasaa wa kukuandikia email , kila ninapopata nafasi ya kukusalimia wewe , wengine hawapati nafasi hii kutokana na sababu zao mbali mbali , wengine hawana mikono ya kuandika , wengine wameachana na wapenzi wao , wengine wamegombana na wapenzi wao na kadhalika lakini mimi nafurahi nakuandikia email hii kwa furaha kuu kuliko zote .
Kikomo naishia hapa , naomba tuendelee kuwasiliana siku nyingine tena , mwisho wa barua moja ndio mwanzo wa barua nyingine nzuri na bora zaidi , kwahiyo usijali sana mrembo wangu .
Natamani ningekuwa kengele
Ningelia unisikie hapo ulipo
Mwaaa
Habari zako , za moyo wako , za tabasamu lako , za kicheko chako , sauti yako na kila kitu kizuri chako ? Najua kila kitu kitakuwa safi sana kuanzia moyo wako mzuri na mtamu uliojaa upendo na mapenzi ya dhati kabisa ulio mkweli na mvumilivu .
Angalia ndani ya moyo wako , utakuta hakuna kitu cha kuficha , pengine unaweza kuficha kwa sababu ni wajibu wa kila mtu katika maisha yake , lakini linapokuja suala la kupendana basi mambo ya kuficha hakuna tena kama ukiwa na uhakika kuhusu uhusiano wako .
Nikifikiria kuhusu wewe , nafikiria kuhusu dunia ya mapenzi iliyo nyooka na iliyo katika njia sahihi kabisa , mpaka hapo jua tu mimi na wewe mpaka milele kwenye mabonde twende , baharini tuogelee hata hewani tutapaa .
Tabasamu lako ambalo ndio nalipenda zaidi , na kila mara huwa nalihisi liko mbeleni mwangu lakini kama unavyojua muda mwingi uko mbali najaribu kufikiri tu je kama tungekuwa tuko wote masaa 24 siku 7 usiku na mchana sijui ningesema maneno gani kusema za ukweli namisi tabasamu lako maridani .
Kicheko chako ambacho nikisikia moyo wangu huenda kasi kuliko wakati wowote ule , Dear labda nikuambie kitu Fulani , mimi napenda sana kusikia vicheko , unajua kuna wakati ukiwa sehemu Fulani Fulani jinsi unavyocheka ndio watu wale wanavyoweza kukuweka katika kundi gani , wewe kicheko chako nakuweka katika kundi la wanadamu maridani .
Hiyo sauti yako ni zaidi ya Coco Lee , honey kama hujui au hujawahi kusikia , Coco Lee ndio mwanamuziki wa kike mwenye sauti ya mvuto zaidi duniani mpaka sasa hivi , moja ya nyimbo nzuri kabisa aliimba na Julio Iglesius inaitwa WHEN U TELL ME THAT U LOVE ME kwahiyo wewe ni zaidi yake , pengine ungeamua kuimba leo ningekuwa naandika kuhusu kitu kingine cha zaidi .
Honey huwa napata furaha sana kila ninapopata wasaa wa kukuandikia email , kila ninapopata nafasi ya kukusalimia wewe , wengine hawapati nafasi hii kutokana na sababu zao mbali mbali , wengine hawana mikono ya kuandika , wengine wameachana na wapenzi wao , wengine wamegombana na wapenzi wao na kadhalika lakini mimi nafurahi nakuandikia email hii kwa furaha kuu kuliko zote .
Kikomo naishia hapa , naomba tuendelee kuwasiliana siku nyingine tena , mwisho wa barua moja ndio mwanzo wa barua nyingine nzuri na bora zaidi , kwahiyo usijali sana mrembo wangu .
Natamani ningekuwa kengele
Ningelia unisikie hapo ulipo