Barua kwa Dr. Slaa: Mageuzi/Mapinduzi ni kubwa kuliko agenda ya Ufisadi

System inaundwa na watu, ndugu. Hakuna kitu System.
Na hiyo System kwa kiwango kikubwa ndo imehamia upande wa pili. Sasa ni system gani mnayotaka kuungusha?
unakubali kwamba CHADEMA nao wana mfumo wao? kwanini unaamini lowassa ataibadili CHADEMA na si CHADEMA kumbadili lowassa (japo hana cha kubadilishwa) ukizingatia kubadili mfumo ni kazi kuliko kumbadili mtu.
 
unakubali kwamba CHADEMA nao wana mfumo wao? kwanini unaamini lowassa ataibadili CHADEMA na si CHADEMA kumbadili lowassa (japo hana cha kubadilishwa) ukizingatia kubadili mfumo ni kazi kuliko kumbadili mtu.

Taasisi ya urais ni System tofauti na System ya chama. Ningependa ukaelewa hilo kwanza. System ni watu, ama kwa lugha rahisi ni mtandao wa watu (ktk siasa za tz) ndo system. Na huo mtandano wa watu umeshahamia upande wa pili. Sasa ni mtandao wa watu wapi mnaotaka kuungusha? Maana neno system linaweza kuwa msamiati kwa baadhi yetu.

NB: System ya chama inaongozwa na katiba ya chama na System ya urais inaongozwa na katiba ya Jumhuri wa Muungano wa Tanzania.
 
Dr Slaa u kimya wake kwa maslahi ya nani? Mi binafsi simwelewi kama mtu msomi kuumiza washabiki na Wana Chama na Chama chake kwa maslahi ya nani? Wote tulifikiri kama yeye but tumewasikia watu wengi wenye mapenzi mema na nchi yetu tumebadilika na tumekubaliana na uamzi wa viongozi wetu. Sasa yeye kukaa kimya na kuruhusu uongo huu uendelee nao ni ufisadi tu mi najisikia kuanza kumchukia Dr Slaa. Ni muhimu akatumia akili hata kidogo tu anachokifanya ni kwa maslahi ya nani? Najua hawezi kurudi CCM Atakua amaufuata mtambo wa kuzalisha mafisadi. Hawezi kwenda Act Sasa unashindwaje kuliona hili wote tulitamani kuhama akili ya kawaida tu Imetuzuia. Nakusihi uwe na roho ya utu na huruma mzaha wako ni angamizo la ukombozi wa kweli wa watanzania.
 
Taasisi ya urais ni System tofauti na System ya chama. Ningependa ukaelewa hilo kwanza. System ni watu, ama kwa lugha rahisi ni mtandao wa watu (ktk siasa za tz) ndo system. Na huo mtandano wa watu umeshahamia upande wa pili. Sasa ni mtandao wa watu wapi mnaotaka kuungusha? Maana neno system linaweza kuwa msamiati kwa baadhi yetu.

NB: System ya chama inaongozwa na katiba ya chama na System ya urais inaongozwa na katiba ya Jumhuri wa Muungano wa Tanzania.
harafu unajichanganya, uumesema mfumo ni mtandao wa watu. hii inamaana Lowassa akisimama peke yake anakuwa hana mfumo anaowakilisha. iweje sasa aende CHADEMA na kubadisha mfumo?. hata kama wanahama wengi wanatakiwa kuwa kuwa na power huko waendako ili kuinfluence mambo.

pia unavyosema mfumo umehamia upande wa pili unazua maswali. inamaana huo mfumo unaenda kureplace waliokuwa nao CHADEMA au CHADEMA hawakuwa na wao na huo ndiyo watauchukua? pia unavyosema umehama, huko ulikotoka wamebaki na mfumo gani?


Magufuli alipochaguliwa alisema "wazee msiogope nitawalinda". tunataka kutoa huo mfumo wa kulindana.naona unaunderestimate nguvu ya chama kuendesha urais? mtu kama magufuli hata iweje hawezi kwenda tofauti na matakwa ya chama.
 
harafu unajichanganya, uumesema mfumo ni mtandao wa watu. hii inamaana Lowassa akisimama peke yake anakuwa hana mfumo anaowakilisha. iweje sasa aende CHADEMA na kubadisha mfumo?. hata kama wanahama wengi wanatakiwa kuwa kuwa na power huko waendako ili kuinfluence mambo.

pia unavyosema mfumo umehamia upande wa pili unazua maswali. inamaana huo mfumo unaenda kureplace waliokuwa nao CHADEMA au CHADEMA hawakuwa na wao na huo ndiyo watauchukua? pia unavyosema umehama, huko ulikotoka wamebaki na mfumo gani?


Magufuli alipochaguliwa alisema "wazee msiogope nitawalinda". tunataka kutoa huo mfumo wa kulindana.naona unaunderestimate nguvu ya chama kuendesha urais? mtu kama magufuli hata iweje hawezi kwenda tofauti na matakwa ya chama.

Unachochanganya wewe ni naamini ni muundo na mfumo. Yani structure na system.
Uzuri mfano upo wazi tu.
yule marehemu Mbigu wa Malawi naye alikaribishwa hivi hivi kwa style hiii hii ya Lowasa, alipokuwa rais akawapiga chini na chama chao na akaanzisha na chama chake akiwa rais. Na mpaka leo hicho chama mdogo wake anakiongoza malawi.

Taasisi ya urais ni tofauti na ya chama mnaongea theory mno.
 
Barua kwa Kipenzi Chetu Dr. Slaa

Ninaomba upate dakika chache upitie hiki kibarua kifupi ili upate mioyo ya wapenzi wako chini ya Chadema inavyopiga kutokana na sintofahamu iliyopo kuhusu shughuli zako katika chama chako cha CHADEMA.

Dr. Slaa, mimi pamoja na maelfu ya Watanzania waliopo ndani ya nchi na nje ya nchi tunafuatilia kinachoendelea kuhusu kutopatikana kwako katika kusukuma hili vuguvugu la mabadiliko.

Dr Slaa ninaomba upokee ujumbe mfupi kama ifuatavyo:

1. Hakuna siri wewe ni shujaa na mtenda haki ya kweli ktk siasa za hapa nchini.

2. Hakuna siri wewe ni mtetea haki ya kweli kwa watanzania walio sahauliwa.

3. Hakuna siri kuwa katika historia itakayo andikwa kuhusu kupigania mabadiliko ya watanzania jina lako litakuwa na nafasi ya pekee.

4. Hakuna siri kuwa kwa mtu yeyote awe kiongozi wako mkuu au wa chini yako hatatenda haki kama hatakuwa tayari kufahamu mchango wako katika mafanikio ya chama chenu.

5. Dr. Slaa yapo mengi MAZURI ya kuandika kuhusu WEWE.

Hitimisho:

Dr. Slaa kilio changu na cha wengi ni kuwa tunakuhitaji haraka sana katika team ya kampeni itakayo anza hivi karibuni. Wengi wetu tunajua kuwa hata pale historia itakapokuja kukujudge wewe na viongozi wenzanko, ikiwa ni hasi (negative) wewe hautakuwepo na ikiwa chanya (postive) basi wewe utakuwepo. Wengi wetu tunajua kinacho endelea na ndiyo maana uamzi wako wa kurudi kwenye meza moja na viongozi wenzako tutauchukulia kama ushindi kwako pamaoja na sisi. Tunakuomba ujitokeze na kuwapa matumaini watanzania ambao sasa hivi mioyo yao haina utulivu.

Mhs Mbowe angalia kuwa kwa gharama yoyote ile inabidi Dr Slaa awe katika team ya USHINDI.

Kwa wale waliozoea kutukana na wafanye hivyo lakini ujumbe ndio huo.

Wabuyaga.
 
Ndugu!

Nakusalimu katika jina la MAGEUZI.

Ni takribani wiki sasa kukiwa na hali ya sintofahamu juu ya kiongozi wetu mpendwa wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndg. Dr. Wilbroad Peter Slaa. Ni dhahiri kuwa kwa watanzania tulio wengi hasa wapenda mageuzi ambao haturidhiki na kasi ya uongozi wa watawala (CCM) na serikali yote kwa ujumla katika suala zima la kutuletea maendeleo na kupambana na changamoto kama Umasikini ulio kithiri (extreme poverty), ujinga(illiteracy) na maradhi (diseases). Lengo/malengo ya bandiko hili lenye maadhi ya barua, ni mambo mawili;-

Kwanza kabisa kumsihi baba yangu Dr. Slaa aelewe agenda ya mabadiriko(changes) kwenye mkitadha wa utawala/uongozi(system) katika nchi yetu (Tanzania). Staki kuhukumu kuwa hajui anachokifanya ila naomba nieleweke kuwa yanayosemwa kwenye mitandao ya jamii na baadhi ya vyombo vya habari juu ya maisha yake ya kisiasa hasa kuhusishwa na kuachana na siasa za vuguvugu la mageuzi (movement politics) kama yasemwayo yatakuwa ni kweli au yakaja kutimia kuwa kweli binafsi nitakuona baba yangu Dr.Slaa kama MSALITI wa wanamageuzi/wanamapinduzi wa Tanzania na pia msaliti wa wanyonge wote waliishio katika dimbwi zito la umasikini, mardahi na ujinga usio na ndoto za kusita katika taifa hili isipokuwa kwa kufanya mapinduzi/mageuzi ya mfumo wa uongozi (the leadership system).

Niliyosema hapo juu yamejengwa juu ya msingi mmoja tu, nao ni MAGEUZI YA KWELI pasipo kujua yatakujaje ila kwa kuangalia kila fursa iliyopo mbele yetu na kuitumia kikamilifu ili kufanikisha dhana nzima ya UKOMBOZI wa wanyonge kwa kuleta mageuzi katika nyanja za uchumi(economic reform), uongozi bora (leadership reform) na fikra (mind set) za watu(watanzania).

Ni ukweli usiyo na chembe ya shaka kuwa sasa hivi (kipindi cha uchaguzi) ni muda wa sisi wanamapinduzi/wanamageuzi (changes championes) tukiongozwa na viongozi wa vyama vya wanamaguzi watu kama Dr. slaa, Limpumba, Mbowe, Mnyika, Mbatia, Lissu, Mdee, S.Lyimo, kwa kutaja tu wachache ila na wengine kwa uchache wao ambao ni wanazuoni wetu wanaotuongoza katika kuendesha mapambano haya, nikishawishika kumtaja Prof. Baregu, Prof. Safari, Wakili msomi Mabere Marando. Wengine sikwamba sitambui mchango wenu na mimi pia nikiwa mstari wa mbele ingawa sionekani ila labda kwasababu ya ufupi wangu( umhimu mdogo) kwa jinsi waonavyo walio warefu( wenye nyazifa) hii haiwezi kuwa sababu ya kujipuuza na kujitisha tamaa katika safari hii ya kutafuta mageuzi ya kweli (real changes) kwangu mimi lililo la msingi ni kuyatia mkononi magauzi ya sekta/nyanja nilizotaja hapo juu.

Kidogo nitoe historia yangu kusupport mageuzi iliko anzia, ni mwaka 2007 nikiwa nimemaliza kidato cha sita, nilipata daraja la tatu kwangu ulikuwa ufaulu mkubwa sana nikilinganisha mazingira niliyosomea(shule za serikali) nilinyimwa mkopo na Bodi ya mikopo ya elimu ya juu. Mwaka 2008 nilifanya mtihani tena kam amtahiniwa binafsi, nikapata point 10(dvsn3) sababu ya kutorudia somo la GS, niliomba vyuo nikachaguliwa chuo pendwa (UDOM) katika masomo humanities, shida ikalrudi ileile nikinyimwa mkopo sababu ya penalty a GS, hii haikuwa sababu ya msingi ila tu mfumo dhaifu wa usimamizi wa elimu ulipelekea watu tulikuwa na matatizo kama haya kuhangaika sana.

Nilipambana mpaka kwa mkurugenzi wa elimu ya juu, wengi wa wanafunzi wenzangu walifukuzwa chuo, kiukweli nilivumilia matatizo kwa mwaka na nusu nikisoma bila mkopo hatimaye ule msemo wa HAKI HAIPOTEI ILA INAWEZA CHELEWESHWA TU, ulitimia ingwa pia wanasema HAKI ILIYOCHELEWESHWA NI SAWA NA HAKI ILIYOPOTEA. Sikukata tama mwisho nilipata hati yangu ya kulipiwa na serikali kama watanzania wengine. Kwangu ilikuwa ni funzo kubwa sana, na kuanzia hapo niliamua kujiunga na wanamapinduzi na ilikuwa mwanzo wa kujua kuwa kuna haja kufanya mageuzi. Nisiwachoshe sana.

Nikirudi kuelezea msimamo wangu juu ya ujio wa Lowasa katika siasa za Mageuzi, ni kweli usiopingika kuwa kilichombele yetu kama kizuizi cha mabadiriko ya uchumi, siasa(uongozi), kijamii na mambo ya maendeleo kwa ujumla ni mfumo(CCM) na bila chenga ya aibu naomba niwaeleweshw watanzania wapi tumekwama kwenye kujikomboa kwenye umasikini na ujinga vitu ambavyo ni kikwanzo kwa kila binadamu duniani katika kujieletea maendeleo.

Moja, Siasa za kuandaana katika kubadirishana madaraka; hii kati ya changamoto kubwa inayotupelekea kuishi jinsi tunavyoishi leo, si vibaya kiongozi yeyote kuwaandaa watu wake ili katika kutokuwepo kwake awepo mtu mwingine atakayechukua nafasi ya kuwaongoza au kuwatawala. Shida inayojitokeza ni kuwa hapa nchini hawaandaliwi watu badala yake anaandaliwa mtu( kibaraka) katika haya kumekuwa na juhudu nyingi za watu wenye nyazifa wamekuwa wakitumia nafasi zao katika kutafuta ridhaa ya kuwaongoza watnazania. Haya ni kati ya makosa makubwa katika mstabari mzima wa uongozi wa Tanzania.

Nimalize tena na tena kwa kumuumba Dr. slaa. Chondechonde hakikisha unatambua kuwa agenda ya MAGEUZI/MAPINDUZI ni kubwa kuliko agenda ya UFISADI twajua umetukuka kwa kupinga ufisadi ila katika hili la ujio wa LOWASA kukufanya uonekane kupoteza uelekeo katika agenda ya kutafuta mabadiriko(changes) haitakuwa sawa. Umma wa watanzania wanatambua mchango wako katika kuleta na kupigania mabadiriko tadhali na unaombwa kwa niaba ya WAPENDA MABADILIKO tunakusihi sana tubaki kitu kimoja huku agenda ya ujio wa Lowasa ikituongoza kama sime ya kuchinjia mfumo mfu wa SSM katika nchi yetu. MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKA TANZANIA. Mageuzi yabaki agenda kubwa kuliko zote!

Nimeandika makala haya kwa niaba nzuri ya Taifa letu.
KATASAN'KAZA...
Kijana Mdogo wangu Pole kwa hayo Mahangaiko ya HELSB....
HONGERA Kwa kusoma pia...
naomba nikuulize...kumbe unamjua Dr.Slaa...je ni yeye ndo aliesababisha hali hii itokee?
Kwanini TUsimsihi aliesababisha hali hii ajirudi,abadili Uamuzi wake?,KWANI NDIE AMETUFIKISHA HAPA TULIPO LEO KWA HII SINTOFAHAMU,
Dr.Wilbroad Peter Slaa ni mwana Philosophy na Mwana Theolojia pia,anaenda na Reasoning ya Tukio,sio kukimbia mbele tuu kama unavyotaka kumshawishi
Mwisho namalizia wewe ukijikwaa unaangalia ulipojikwaa au ulipoangukia???
Ni hoja tuuu.."MAGEUZI" Mbele...
CC:wabuyaga
 
ujumbe kwa mwenyekiti taifa nauunga mkono.

kila linalowezekana lifanyike kumaliza tofauti zote. Dr arudi haraka kwenye mapambano.
 
dr slaa ni key engine katika ushindi ni mpumbavu tu ndiye atayempuuza
 
Yaani wewe kushindwa kwako kufaulu mitihani kama wenzako inahusianaje na mfumo wa uongozi wa nchi kama unavyouita. Nenda shule kasome wewe Acha ubabaishaji hapa ndorobo wee
 
To you the younger generation and leaders of tomorrow, I must tell you, that, Pioneers never live to see or enjoy fruits of their labor, they establish new trails so you can all safely pass through.

We are living in a new era. Era of “New World Economic Order” an era whereby where only the strong survive!

Even though my days have numbered, my struggle for equality between stronger and weaker nations will never stop. My struggle for fairness between nations will never stop. My Struggle for comparative Economic Advantage, and social justice will live on. My fight against corruption will never stop. I will never compromise these principles as long as I live.

I may never live to see my beautiful country enjoy its comparative economic advantage, but my children, my grandchildren and millions of young people in my country, fed-up with lifelong corruption, mismanagement and social injustice will. This is what, I m living for. I am living for Economic and social liberation

Well, this is what pioneers do!


Dr. Wilbrod Peter Slaa,
Keynote Adress: Purdue University,
April, 2015
 
Barua yangu fupi kwa Dr. Slaa.

Kamwe usichangamane na mafisadi wanataka wakutumie tu kwenye uchaguzi, uchaguzi ukipita hakuna atakaekukumbuka.

Mijitu imetawaliwa na tamaa ya fedha na madaraka hawana uzalendo wowote ule.

Sharti la Kurudi Slaa, Lowassa atemwe hakuna namna nyingine. La sivyo endeleeni na safari ya matumaini na ufisadi lukuki.

Mnataka mmuchafue kila mtu kwa fedha zenu chafu, Lazima kama Taifa tubaki na Wazalendo hata kama ni mmoja lakini historia itamlinda kuliko kuja kuonekana kizazi chote kilikuwa cha laana.
 
Dr Slaa na usomi wake alitakiwa kujua siasa ni mchezo wa kucompromise. you can't have it all.
Mimi naona upofu tu na ubinafsi unamsumbua; hivi Lowassa angebakia sisiem na akawa mgombea halafu katiba ikaruhusu Raisi kuteua hata mawaziri toka upinzani akaamua kuchukua UKAWA watupu atawale nao si ingekuwa ujinga kukataa fursa ya kuingia uwanjani kufunga goli? Hata Wamarekani wanashirikiana na Iran kumpiga ISIS. Penye common enemy watu huunganisha nguvu kumtoa baada ya hapo ndio waanze kujichambua ipi pumba ipi mchele lakini si kabla ya hapo
 
Mimi naona upofu tu na ubinafsi unamsumbua; hivi Lowassa angebakia sisiem na akawa mgombea halafu katiba ikaruhusu Raisi kuteua hata mawaziri toka upinzani akaamua kuchukua UKAWA watupu atawale nao si ingekuwa ujinga kukataa fursa ya kuingia uwanjani kufunga goli? Hata Wamarekani wanashirikiana na Iran kumpiga ISIS. Penye common enemy watu huunganisha nguvu kumtoa baada ya hapo ndio waanze kujichambua ipi pumba ipi mchele lakini si kabla ya hapo
sure mkuu. first thing first. huwezi pata mambo yote kwa wakati mmoja.
 
Dr. Slaa inabidi atulie na kutafakari kwa kina na apime vema athari za maamuzi yake kwake yeye mwenyewe binafsi, kwa chama chake, kwa UKAWA (ambao lengo kubwa ni kutetea katiba ya wananchi), na kwa taifa kwa ujumla wake.

Maana kuna faida na hasara katika kila uamuzi atakaouchukua. Mwanzo kwa akili ya kawaida yaani common sense nilifikiria kuwa ili kulinda hadhi yake mbele ya umma wa watanzania uamuzi bora zaidi kwake ni kujiuzulu.

Lakini baada ya kutafakari kwa kina nikaona uamuzi huo japo unaweza kuwa na faida binafsi kwake kwa njia moja au nyingine lakini utaleta hasara kubwa kwa kuudhohofisha upinzani nchini, na kudhoofisha azma ya UKAWA.

Hivyo kwa kuzingatia maslahi mapana ya taifa na maandiko matakatifu ambayo sina shaka Dr. Slaa anayafahamu fika, ni vema akatambua kuwa hapa anahitaji kujitwika zigo la mabaya yote ( ikiwemo chuki, hasira, huzuni, fedheha, kuzushiwa, kutukanwa, nk) kwa ajili ya kuepuka kuudhohofisha upinzani hapa nchini.

Kama anahisi ndani ya upinzani kwa sasa ana maadui basi akumbuke maandiko yanasemaje juu ya kuwapenda maadui zetu.

Lakini pia atambue kuwa taifa imara linajengwa kwa jitihada za pamoja (collective efforts), hamasa na wakati mwingine kujitoa muanga kwa kuyavumilia na hata kuyakubali yale tusiyoyapenda as long as yanania njema ya kutuongezea nguvu ya kusonga mbele na pengine kuimarika zaidi.

Kwa hiyo nahitimisha kwa kumuomba na kumsihi Dr. Slaa asing'oke CHADEMA na UKAWA kwa sasa. Kama hilo wazo lipo basi pengine aliahirishe hadi baada ya tarehe 25 Octoba, 2015 baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu.

Akumbuke kuwa:"Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari, haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na wakweli; huyavumilia yote, huamini yote; hutumaini yote, hustahimili yote." (1Wakorintho 13:4-7).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom