Zakumi
JF-Expert Member
- Sep 24, 2008
- 5,063
- 2,471
- Thread starter
- #41
Bwana CJ suala la watu wanaozunguka rasilimali fulani kunufaika na mapato ya rasilimali hiyo kwa mtizamo wangu halihitaji serikali za majimbo. Chini ya mfumo tulionao sasa, mbali ya serikali kuu tuna local goverments ambazo sipo katika mtindo wa majiji, manispaa, miji, mitaa na vijiji. Chini ya utaratibu huu inaweekana sheria ikawekwa kwamba asilimia fulani ya mapato yanayopatikana kwa mfano katika madini itumike kuboresha huduma za kijamii katika jamii inayozunguka rasilimali husika.
GJ:
Kwa Tanzania serikali za majimbo kwa namna fulani zipo. Tatizo ni kuwa wananchi hawana madaraka nazo. Wananchi hawana madaraka ya kumchagua Mkuu wa mkoa au wilaya.
Local authorities zipo. Lakini technocraties wa local authories hizi bado wanateuliwa na rais au ofisi ya waziri mkuu. Mkuu wa mkoa anasikiliza amri kutoka kwa rais kwa sababu ndie aliyempa nafasi hiyo. Lakini akichaguliwa na wananchi, basi ni lazima ajiandae kufanya vile wananchi wanavyotaka.