Barrick: Wanavyochezea akili zetu

Nguruvi3

Platinum Member
Jun 21, 2010
15,389
31,335
By DAILY NEWS Reporter, 7th September 2011 @ 12:37, Total Comments: 0, Hits: 139

AFRICAN Barrick Gold (ABG) has launched US$10 million (about 16bn/-) to govern community investment programmes in Tanzania, that will focus on several areas including health, education, environment, water, skills development and training.

"As part of ABG's corporate social responsibility, the Fund will also finance various philanthropic initiatives, donations, scholarships and partnerships," Ambassador Juma Mwapachu, ABG Director, said during the launch in Dar es Salaam yesterday.

He said ABG would be committing US$10 million to corporate social responsibility activities through Maendeleo Fund annually.

ABG Vice-President for Corporate Affairs, Mr Deo Mwanyika, said the mining firm has contributed heftly to the Tanzanian economy over the last 13 years, in terms of taxation, jobs and poverty reduction. He said it currently employs over 8,800 workers, where 90 per cent of them are Tanzanians.

Mr Mwanyika further said the firm has made available US$548 million to the country's economy, through proceeds from taxation, procurement, salaries and training of personnel as well as investment in community programmes.

Ambassador Mwapachu said provision of direct employment to over 8,800 people means a lot due to its multiplier effect. "People will spend their salaries on food, goods and many other services," he said.

Meanwhile, Mr Mwanyika told the news conference that ABG would complete the cross-listing process on the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) before the end of this year.

He said it was still negotiating with the Bank of Tanzania (BoT) and the Capital and Security Markets Authority (CMSA) on various requirements before listing on Tanzania's bourse.

"The move will enable Tanzanians to have ownership in one of the world's leading gold mining houses," he said.

ABG, which is listed on the London Stock Exchange is the subsidiary of Barrick Gold, a Canadian miner, listed on the Toronto Stock Exchange

My take:
Regia Mtema(MB) aliweka thread iliyomkariri waziri mkuu na kampuni zilizoongoza kulipa kodi. Katika makampuni yaliyotajwa hakuna kampuni ya madini hata moja na moto uliwaka sana kwa hawa Barrick.
Tuhuma zimefikia mahali pa kusema Chibuku wanalipa kodi zaidi ya Barrick.

Juzi kulikuwa na taarifa ya mtafiti iliyoelezea mambo kadha yaliyoigusa Barrick. Kama kawaida moto uliwaka na kuwaweka mahali pagumu.

Ikumbukwe ni hawa ndio walioleta kizaazaa bungeni kutokana na kusaini makataba hotelini London na watu kuachia ngazi.

Ukisoma habari hiyo hapo juu kuna mambo yanajitokeza:
1. CRS ni mpango wa ndani wa kampuni au shirika na hukana ulazima kuutangaza lakini wamefanya hilo makusudi. Wanasema watatoa kiasi cha dollar 10 katika mipango ya CSR ambazo si mwananchi au serikali inaweza kuzidai.

2. Wanadai wamechangia uchumi kwa miaka 13, hawatuelezi mwaka huu wamechangia kiasi gani. Wameweka idadi ya waajairiwa ili kuonyesha ni kiasi gani wanatoa ajira. Walichosahau ni kuwa idadi tu ya wafanyakazi inaeleza mapato.
Barrick wanataka kutudanganya ya kuwa, uwepo wa wafanyakazi wengi basi kila mfanyakazi analipa kodi.
Hawakutueleza wao wamelipa kodi kiasi gani mwaka huu.

3. Barrick wanasema wamelipa kiasi cha dollar 548 million kwa mambo kama procurement, mafunzo n.k.katika kuchangia uchumi.
Wame weka kiasi hicho ili ionekane kwa mwananchi kuwa wanalipa kodi sana. Tena hawakutueleza ni kipindi gani. Ni kwa miaka 13 au ni mwaka huu. Udanganyifu wa kucheza na namba tu. Unapomfunza mfanyakazi wako anayezalisha unachangia vipi uchumi moja kwa moja kama shirika la madini.

4. Wanasema wameajiri watu 8,800 na hiyo inajizidisha kutokana na huduma, kwahiyo watu wanalipa kodi kutoka mishahara yao na ununuzi wa chakula na huduma nyingine. Wanachosisitiza hapa ni kuwa japo wao hawalipi kodi lakini wafanyakazi wao wanalipa kodi. Kutupumbaza!!!

Mwisho: Kutokana na kutajwa tajwa kwa mabaya wanaona kuna uharibifu 'damage' wa jina lao. Njia rahisi ni kutoa takwimu za kuchanganya umma ili kuundoa katika mada muhimu ya wao wamechangia kodi kiasi gani.
Nia yao ni habari hii iishe ili isije zua mengine makubwa kama ilivyokaribia kuzua siku chache zilziopita.
Hapo wanafanya 'damage control' kwa bahati mbaya hilo halijafanikiwa.

Tunaomba mtu mwenye data za kiasi gani wamelipa kodi ziwekwe hapa, kwasababu kama CRS ni billion 16, kodi ambayo ni lazima ilipwe na kwa kiwango maalumu itakuwa zaidi.

wasicheze na akili zetu, na hapa ndipo nakubaliana na MM kuwa hawa ni 'wahalifu' wanaojulikana duniani kote.
 
Hawa Barrick wanatuona watz wajinga, wenyewe cha msingi walipe kodi kulingana na mapato wanayopata. Kuhusu hizo huduma za jamii ni lazima watoe maana ndo mkataba wenyewe. Na huyo Mwapachu hata siyo mzalendo kabisa anadiriki kusimama kidete kuwatetea wezi wa nchi yetu. Haya wanasema wameajiri watu 8,800 eti ndo wanatoa kodi, upuuzi mtupu, watu hao,si wanafanya kazi na wanazalisha? Ama kweli wanatuona majuha, Barrick wezi tu hao. WATOE KODI WAACHE WIZI.
 
Si walisema kuwa hawapati faida bado? sasa hizo billions watazitoa wapi tena jamani? mbona kizungumkuti hivi? halafu hayo mabilioni watayatoa kwa utaratibu gani? mmmhh haya
 
Barrick ni wezi wakubwa washukuru wanalindwa na serikali sijui nao wametoa zawadi za situ kwa wahusika fulani lakni time will come hawa watu wao wanaowanunulia suti hatakuwepo na ndio watalipa madini yetu ya kodi na mali wanazotuibia kila siku usiku na mchana kwa kujimba na kusafirisha madini yetu bure hawa wangekuwa wanalipa kodi za halali wangekuwa namba moja katika ulipaji wa kodi wala tusingeongelea kibuku kuwazidi
 
Hawa wakina Juma Mwapachu ndio makuwadi wa uchumi wanaonunuliwa suruali na shati halafu wanakubali kutumiwa kama wasemaji wa kampuni za madini kuhalalisha wizi wa madini yetu. Hebu tuambieni hiyo Mwapachu anayosema ni multiplier effect kutokana na ajira ya watu 8,800 ni fraction ngapi ya faida ya mapato ambayo Barrick wanapata kwa mwaka toka dhahabu yetu? Kumbuka gold now is selling at the highest price ever at U.S.$ 1900 a troy ounce!! Wenzetu Venezuela Chavez anawatoza windfall tax haya makampuni ya dhahabu kutokana na bei ya dhahabu kupanda kwenye soko la dunia. Sisi hatufanyi hivyo kwasababu genge la aina ya wakina Juma Mwapachu wanapewa crumbs na barrick!! Shame on you and you be cursed!.
 
Mi sijawahi kuelewa kwa nini sisi watz na serikali yetu hudhania CRS (corporate social responssibility) ni legal bind kisheria wakato kampuni huweza kujiamulia kiwango na hakuna legal action inayoweza kutolewa kama kampuni ime-default CRS
 
Mi sijawahi kuelewa kwa nini sisi watz na serikali yetu hudhania CRS (corporate social responssibility) ni legal bind kisheria wakato kampuni huweza kujiamulia kiwango na hakuna legal action inayoweza kutolewa kama kampuni ime-default CRS
Hiyo ni internal affair ya company, wanahiari ya kutoa au kutotoa.
 
Si walisema kuwa hawapati faida bado? sasa hizo billions watazitoa wapi tena jamani? mbona kizungumkuti hivi? halafu hayo mabilioni watayatoa kwa utaratibu gani? mmmhh haya
Ndipo unapoona vituko. Yani hawapati faida lakini wanatoa bilion 16 kwa miradi tu.
Wanatufanya wajinga na wamewanunua akina mwapachu kwa mishahara na wengine kwa misaada ya pipi.
 
CRS ni aina fulani ya usanii kwa nchi zetu za kiafrika. barrick watuambie katika migodi yao ukitoa DSM Office pale oysterbay watanzania walioko kwenye management level ni wangapi? makaburu ndio yamejazana na hayana hata elimu kwa sababu kwao RSA hakuna ajira yanaletwa barrick na kulipwa mpaka $ 35000 kwa mwezi huu si wizi wakati watanzania mnawalipa laki 6. Akina Mwanyika, na mwapachu nyinyi kazi yenu kunenepesha matumbo yenu tuu wazungu wanawaletea ripoti mnazisoma na kutanganza. wafanyakazi waafrika barrick wanaonewa sana. Succession Plan ya kupunguza wazungu mbona Buzwagi,North mara,Bulyanhulu hiajasaidia kuondoa wazungu kwenye kazi amabzo watanzania wanaweza kuzifanya, Hii nchi inakwenda wapi? Na sasa mmeingia mzimu wa wakenya angalieni patakuwa hapakaliki hapa na hayo ma V8 mtashindwa ku enjoy nayo jama, weusi tunataabika nchini kwetu. Uhamiaji inabidi mfanye audit na wizara ya kazi sio mkifika mgodini mkipewa burger na chips na bahasha mnaondoka billa ukweli. Hatuwataki wazungu wasio na elimu.
 
Back
Top Bottom