Barrick Waingilia Michezo?!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Sina data nzuri na kuhusiana na wadhamini wa michezo hapa Tanzania, ila najua wimbi la udhamini limeongezeka kwa kasi katika nyanja mbalimbali za michezo hapa nchini. Kama habari ifuatayo inavyosema:

NATIONAL BASKETBALL TOURNEY: Barrick Gold injects 50m/-

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

BARRICK Gold Tanzania will sponsor this year’s national basketball championship to be held in the city later this month.

Tanzania Basketball Federation (TBF) president Richard Kasesela told reporters in the city yesterday the sponsorship amounts to 50m/-.

’’I hereby announce that Barrick Gold Tanzania are the main sponsors of the national basketball championship,’’ Kasesela said.

Kasesela said the sponsorship package includes production costs for team kits, headbands, wristbands, medals, trophies and branding.

’’In addition, Barrick will also cover costs for radio advertisements, flyers, posters, t-shirts and caps for fans,’’ he said.

He said part of the sponsorship package gives the main sponsor rights to brand the event and display its logo, which carries the tournament’s new name � Barrick Gold Cup.

Kasesela also unveiled a new TBF logo, which will feature in all events sanctioned by the federation and will be the key in promoting basketball across the country.

Speaking at the same occasion, Barrick public relations manager Teweli Teweli said Barrick felt it was essential to support a tournament that consistently brings together teams from all over the country.

’’We commend the organizations and individuals who have dedicated so much effort towards promoting basketball and we’re proud to be associated with them,’’ he said.

’’We look forward to joining forces in promoting the sport across Tanzania,’’ he added.

The Barrick Gold Cup will be held at the National Indoor Stadium from October 21-28. Games will start at 8.00am and run to 8.00pm.

Tanzania Breweries Limited (TBL) has also injected 15m/- in the championship.

Source link: ThisDay.

Maswali ninayojiuliza sasa hivi ni kuwa:
--Je, Barrick walikuwa wanadhamini michezo siku kitambo zilizopita?!

--Kama walishawahi, je ni michezo ipi au timu zipi hizo?
--Kama walishawahi, je walijitangaza kama hivi sasa?
--Kama hawajawahi, je ni kipi kimewapelekea kuanza kudhamini timu nyakati hizi?
--Kama hawajawahi/walishawahi, je hili ni jambo la maana wao kufanya kwenye nyakati kama hizi ambapo wanasakamwa kutokana na utata wa Buzwagi?
--Je, wadhaminiwa wanajisikiaje kuhusu kukumbatiwa na washutumiwa?

WanaJF, naomba msaada wenu kwenye maswali haya. Ahsanteni.

SteveD.
 
SteveD,

Hawa jamaa wanakwepa kulipa mabilioni wanayostahili kulipa kama kodi kwa Watanzania. Si ajabu wameshaambiwa wakimwaga vijisenti hivyo kwenye michezo basi wananchi wanaweza kupunguza hasira zao dhidi ya mikataba feki waliyosaini ambayo haina maslahi kwa Watanzania. Lakini wanasahau kwamba Watanzania hawawezi kununuliwa kwa vijisenti vichache vitakavyoelekezwa kwenye michezo. Tunachotaka ni kusaini mkataba mpya utaowekwa bayana ili Watanzania wote tuweze kuusoma na kisha kuukubali kwa kuwa una maslahi kwa nchi yetu.

Tunajua ni lazima wapate faida, lakini Watanzania pia tunataka kuona faida kutoka kwenye rasilimali zetu, sio ziwanufaishe wageni tu.
 
Barrick kudhamini michezo si mara ya kwanza. Iwewahi kuihost kambi ya Taifa stars mara mbili kule Bulyanhulu na kuwalipia gharama zooote na dola 60,000 juu. Pia imewahi kudhamini michezo ya timu za mgodi na wanavijiji wanaoizunguka migodi yake yoote (Tulawaka, North Mara na Bulyanhulu) kwa kutoa jezi na zawadi kwa washindi.

Kwa hili la michezo nadhani Barrick isidhaniwe kwamaba inajitangaza au kujisafisha. Ni utamaduni wao
 
Halali mtu hapa hizo peremende hazina faida yoyote, mali wanayoiba ambayo ni haki ya WTZ ni lazima irudi tena sasa hawawezi kuchukua rasilimali yetu bure na kutupatia peremende ili tusahau. Sisi sio watoto wadogo wa chekechea.
 
SteveD,

Hawa jamaa wanakwepa kulipa mabilioni wanayostahili kulipa kama kodi kwa Watanzania. Si ajabu wameshaambiwa wakimwaga vijisenti hivyo kwenye michezo basi wananchi wanaweza kupunguza hasira zao dhidi ya mikataba feki waliyosaini ambayo haina maslahi kwa Watanzania. Lakini wanasahau kwamba Watanzania hawawezi kununuliwa kwa vijisenti vichache vitakavyoelekezwa kwenye michezo. Tunachotaka ni kusaini mkataba mpya utaowekwa bayana ili Watanzania wote tuweze kuusoma na kisha kuukubali kwa kuwa una maslahi kwa nchi yetu.

Tunajua ni lazima wapate faida, lakini Watanzania pia tunataka kuona faida kutoka kwenye rasilimali zetu, sio ziwanufaishe wageni tu.
Good.
 
Back
Top Bottom