Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Wakati Spika wa Bunge Makinda akianza kazi aliliagiza bunge na kamati zake kwamba wanapokwenda nje kwa shughuli za bunge hupewa posho, hivyo si sahihi kupewa posho nyingine kwani ni dalili ya rushwa na inawezekana ikawafanya wasifanye kazi zao kwa haki. Sasa hii safari ya Barrick kuandaliwa ndege na kupewa sh. laki tatu kila mbunge inaashiria nini?
Barrick yamwaga noti kwa wabunge
KILA MMOJA APEWA 300,000/- KWA SIKU
UONGOZI wa mgodi wa North Mara unaomilikiwa na Kampuni ya Barrick uliopo Nyamongo, Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, juzi ulitoa sh 300,000 kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira waliokwenda mgodini hapo juzi. Tanzania Daima, limedokezwa na mmoja wa wabunge waliokuwamo kwenye safari hiyo alisema kuwa fedha hizo walilipwa kwa ajili ya safari ya siku moja na wala si kuwafumba mdomo. Mbunge huyo alisema kuwa msafara uliongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli, walibaini madudu mengi katika mgodi huo mojawapo ikiwepo ya kutokuwapo kwa visima saba vilivyodaiwa kujengwa na Barick kwa wakazi wanaozunguka mgodi huo.
kuwa walipofika mgodini hapo, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais (Mazingira) Dk. Terezya Luoga, alibanwa na Mbunge wa Longido, Mike Lekule Laizer aliyehoji viko wapi visima saba vinavyodaiwa kujengwa na Barick.
Kwa mujibu wa wabunge wengine waliokuwa kwenye msafara swali hilo aliulizwa kutokana na jibu lake alilolitoa Julai mwaka huu kwa Mbunge wa Viti Maalum, Esther Matiko, aliyetaka kujua mgodi huo umejenga visima vingapi kwa wanakijiji wanaozunguka mgodi husika ambao walikuwa wakiutegemea mto Tigite. Mto Tigite unadaiwa kuchafuliwa na maji ya sumu yanayotoka katika mgodi huo na kamati ya Bunge iliwahi kuchunguza jambo hilo na ziara ya juzi ilikuwa kwenda kuangalia shughuli zinavyoendelea katika mgodi huo.
Tanzania Daima limedokezwa kuwa baada ya kubanwa Waziri Luoga alisema inawezekana alipewa taarifa zisizo sahihi kuhusu ujenzi huo, kwani juzi alishuhudia kutojengwa kwa visimaa hivyo. Hata hivyo, wajumbe wa kamati hiyo walimbana waziri kwa madai kuwa alilidanganya Bunge kuwa naye alifanya ziara katika mgodi huo na kuona visima hivyo. Ilikuwa aibu kwa waziri maana Barickk walikiri kuwa hawakujenga visima hivyo bali wapo kwenye mchakato wa kuvijenga, serikali yetu iliaibika, alisema.
Inadaiwa kuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kewanja kinachopakana na mgodi huo, Omtanzania Mpima, aliwaeleza wajumbe wa kamati hiyo kuwa Barick haijajenga visima hivyo kama inavyodaiwa. Uongozi wa Barick ulidai kuwa bado hawajajenga visima hivyo na wapo kwenye mchakato wa kuvijenga, lakini kwa hivi sasa wamekuwa wakiwapa maji wananchi kwa kutumia magari.
Tanzania Daima, liliwasiliana na Waziri Kivuli wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mazingira) Mchungaji Peter Msingwa, ambaye alisema utaratibu wa safari ile ulipitia ofisi ya Bunge, hivyo wajumbe wengi hawakujua iligharimia na Barick. Alisema wajumbe hawakuwa na wasiwasi na safari hiyo kwa kuwa ni jambo la kawaida ofisi ya bunge kugharimia safari za kamati husika. Aliongeza kuwa walibaini kuwa Barick ndiyo waliogharimia hiyo safari, lakini jambo hilo haliwezi kubadili mawazo yao na kile walichokiona kwenye mgodi huo.
Mimi siwezi kununuliwa na Barick au yoyote yule, ziara ile tuliifanya bila kujua nani mfadhili, lakini kimsingi tumeona kila kitu kwakuwa tulikwenda na mitambo yote ya kurekodiwa 'Hansard' na video Kamera, alisema. Msingwa alisema katika utaratibu wa kawaida mtuhumiwa hawezi kumfadhili mpelelezi na matokeo yakawa mazuri, lakini ni vema wananchi wakawa na imani na wabunge waliokwenda kwenye mgodi huo. Siwezi kusema wabunge tulihongwa na Barick kwa sababu ziara ile ilifanywa kwa maelekezo ya Spika kwa hiyo kama unasema tumehongwa basi ofisi ya Spika ndiyo ilikuwa ya kwanza, alisema.
Juzi Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilifanya ziara ya siku moja mgodini Nyamongo ikitokea mjini Dodoma, ziara ambayo kwa mujibu wa Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel ililenga kukagua utekelezaji wa maelekezo yake iliyoyatoa mwaka jana kuhusu athari za mazingira zilizosababisha baadhi ya wakazi wanaouzunguka kupata athari za kiafya. Mbunge wa Tarime (CCM), Nyambari Nyangwine alialikwa kuambatana na kamati hiyo, lakini safari yake iliishia Uwanja wa Ndege Dodoma baada ya kubaini kwamba ndege husika zilikuwa zimekodiwa na kampuni ya Barrick.
Inasadikiwa zaidi ya wabunge 20 waliokuwamo kwenye msafara huo ambao ni Susan Lyimo (CHADEMA) Esther Matiko, (CHADEMA) Mary Mwanjelwa (CCM), Mbunge wa Buchosa (CCM), Dk. Charles Tizeba, Mbunge wa Kikwajuni (CCM), Hamad Yusuff Masauni na Mbunge wa Longido (CCM), Mike Lekule Laizer. Wengine ni James Lembeli (CCM), Abdulkader Shah na Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa na msafara huo unadaiwa kuongozwa na Ofisa wa Barick Deo Mwanyika.
Tanzania Daima
Barrick yamwaga noti kwa wabunge
KILA MMOJA APEWA 300,000/- KWA SIKU
UONGOZI wa mgodi wa North Mara unaomilikiwa na Kampuni ya Barrick uliopo Nyamongo, Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, juzi ulitoa sh 300,000 kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira waliokwenda mgodini hapo juzi. Tanzania Daima, limedokezwa na mmoja wa wabunge waliokuwamo kwenye safari hiyo alisema kuwa fedha hizo walilipwa kwa ajili ya safari ya siku moja na wala si kuwafumba mdomo. Mbunge huyo alisema kuwa msafara uliongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli, walibaini madudu mengi katika mgodi huo mojawapo ikiwepo ya kutokuwapo kwa visima saba vilivyodaiwa kujengwa na Barick kwa wakazi wanaozunguka mgodi huo.
kuwa walipofika mgodini hapo, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais (Mazingira) Dk. Terezya Luoga, alibanwa na Mbunge wa Longido, Mike Lekule Laizer aliyehoji viko wapi visima saba vinavyodaiwa kujengwa na Barick.
Kwa mujibu wa wabunge wengine waliokuwa kwenye msafara swali hilo aliulizwa kutokana na jibu lake alilolitoa Julai mwaka huu kwa Mbunge wa Viti Maalum, Esther Matiko, aliyetaka kujua mgodi huo umejenga visima vingapi kwa wanakijiji wanaozunguka mgodi husika ambao walikuwa wakiutegemea mto Tigite. Mto Tigite unadaiwa kuchafuliwa na maji ya sumu yanayotoka katika mgodi huo na kamati ya Bunge iliwahi kuchunguza jambo hilo na ziara ya juzi ilikuwa kwenda kuangalia shughuli zinavyoendelea katika mgodi huo.
Tanzania Daima limedokezwa kuwa baada ya kubanwa Waziri Luoga alisema inawezekana alipewa taarifa zisizo sahihi kuhusu ujenzi huo, kwani juzi alishuhudia kutojengwa kwa visimaa hivyo. Hata hivyo, wajumbe wa kamati hiyo walimbana waziri kwa madai kuwa alilidanganya Bunge kuwa naye alifanya ziara katika mgodi huo na kuona visima hivyo. Ilikuwa aibu kwa waziri maana Barickk walikiri kuwa hawakujenga visima hivyo bali wapo kwenye mchakato wa kuvijenga, serikali yetu iliaibika, alisema.
Inadaiwa kuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kewanja kinachopakana na mgodi huo, Omtanzania Mpima, aliwaeleza wajumbe wa kamati hiyo kuwa Barick haijajenga visima hivyo kama inavyodaiwa. Uongozi wa Barick ulidai kuwa bado hawajajenga visima hivyo na wapo kwenye mchakato wa kuvijenga, lakini kwa hivi sasa wamekuwa wakiwapa maji wananchi kwa kutumia magari.
Tanzania Daima, liliwasiliana na Waziri Kivuli wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mazingira) Mchungaji Peter Msingwa, ambaye alisema utaratibu wa safari ile ulipitia ofisi ya Bunge, hivyo wajumbe wengi hawakujua iligharimia na Barick. Alisema wajumbe hawakuwa na wasiwasi na safari hiyo kwa kuwa ni jambo la kawaida ofisi ya bunge kugharimia safari za kamati husika. Aliongeza kuwa walibaini kuwa Barick ndiyo waliogharimia hiyo safari, lakini jambo hilo haliwezi kubadili mawazo yao na kile walichokiona kwenye mgodi huo.
Mimi siwezi kununuliwa na Barick au yoyote yule, ziara ile tuliifanya bila kujua nani mfadhili, lakini kimsingi tumeona kila kitu kwakuwa tulikwenda na mitambo yote ya kurekodiwa 'Hansard' na video Kamera, alisema. Msingwa alisema katika utaratibu wa kawaida mtuhumiwa hawezi kumfadhili mpelelezi na matokeo yakawa mazuri, lakini ni vema wananchi wakawa na imani na wabunge waliokwenda kwenye mgodi huo. Siwezi kusema wabunge tulihongwa na Barick kwa sababu ziara ile ilifanywa kwa maelekezo ya Spika kwa hiyo kama unasema tumehongwa basi ofisi ya Spika ndiyo ilikuwa ya kwanza, alisema.
Juzi Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilifanya ziara ya siku moja mgodini Nyamongo ikitokea mjini Dodoma, ziara ambayo kwa mujibu wa Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel ililenga kukagua utekelezaji wa maelekezo yake iliyoyatoa mwaka jana kuhusu athari za mazingira zilizosababisha baadhi ya wakazi wanaouzunguka kupata athari za kiafya. Mbunge wa Tarime (CCM), Nyambari Nyangwine alialikwa kuambatana na kamati hiyo, lakini safari yake iliishia Uwanja wa Ndege Dodoma baada ya kubaini kwamba ndege husika zilikuwa zimekodiwa na kampuni ya Barrick.
Inasadikiwa zaidi ya wabunge 20 waliokuwamo kwenye msafara huo ambao ni Susan Lyimo (CHADEMA) Esther Matiko, (CHADEMA) Mary Mwanjelwa (CCM), Mbunge wa Buchosa (CCM), Dk. Charles Tizeba, Mbunge wa Kikwajuni (CCM), Hamad Yusuff Masauni na Mbunge wa Longido (CCM), Mike Lekule Laizer. Wengine ni James Lembeli (CCM), Abdulkader Shah na Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa na msafara huo unadaiwa kuongozwa na Ofisa wa Barick Deo Mwanyika.
Tanzania Daima