Kingu Victor EL
Member
- Aug 21, 2011
- 26
- 0
Nilisoma gazeti la Mwana halisi la 31August kuhusu malalamiko ya wahusika dhidi ya Mwajiri au aliyekuwa Mwajiri wao. Nionavyo mimi. Lawama hazistahili kwenda kwa Kampuni ya Barrick kabla ya kuangalia mapungufu yameanzia wapi? Watu wanaangalia na kulaumu walipoangukia bila kuangalia wamejikwaa wapi? 1.Sheria zetu za kazi hazimlindi ipasavyo mfanyakazi kutokana na athari anazoweza kuzipata kutokana na kazi anayofanya. 2. Sheria zetu hazitoi fidia ya kuridhisha kwa mfanyakazi anayeathirika na magonjwa yatokanayo na kazi. 3. Wasimamizi wa sheria hawana MENO MAKALI ya kuweza kusimamia ipasavyo hata hizo sheria dhaifu zilizopo. Angalia sheria ya hii. Mfanyakazi akiumwa na akashindwa kufanya kazi, Mwajiri kwa uthibitisho wa Daktari atampa likizo ya ugonjwa yenye malipo kwa siku 62 endapo hajapona ataongezewa siku zingine 62 zenye nusu malipo. Baada ya hapo Mwajiri anamwachisha kazi mhusika. Hatutakiwi kulalamikia huruma za Waajiri. Ati Barrick hawana utu. Ninawauliza Wana JF. Nani ameshawahi kukutana na Mwajiri binafsi mwenye Utu. Nani asiyejua kuwa endapo atatatanguliza utu maana yake ni kujipunguzia faida yeye mwenyewe. Ukiona Mwajiri binafsi anatoa msaada ujue ANAWEKEZA AU ANATAKA UMAARUFU FULANI ambao baadaye utamsaidia kupata unafuu fulani katika uendeshaji wa biashara zake, kwa maana ya faida zaidi. Walinzi wa sheria wanapewa lift kwenye ndege za Barrick unategemea sheria dhaifu itekelezwe kweli? Sijui wana JF manasemaje?