Barrick Gold wants tax refund from Tanzania Government!

Toka lini tumesajiliwa kuwa charity ya MAKAMPUNI ya kigeni?
Hawa wanatudai au tunawadai?
Hayo mafuta ni kwa manufaa ya kampuni yao, ni mikataba mibovu baada ya wao kuwanunua viongozi wetu.
 
Yaani, we are paying them more than they put in the treasury.
Huu ni ujinga wa kupindukia sasa, tumekuwa wendawazimu wa kugeuzwa kila wawekezaji wanavyotaka. Hapa sasa kilichobaki ni kutumia nguvu ya umma kuiadabisha serikali ya vichaa hii. Haiwezekani makambuni yanayolipa mrahaba wa aslimia tatu halafu mwisho wa siku mnakuja kukaa kwenye meza kujadili kurejesha fedha tena kwa makampuni hayo. Hapa hasira imenipanda na uvumivu umeniishia. Tuamke watanzania kwani hata kipofu mwisho hutambua pale hujuma inapozidi kiasi.
 
Unbelievable! ama kweli wajinga ndio waliwao, inavyoonekana aliyesaini hii mikataba hakuisoma kabisa. Hawa jamaa wanachukua dhahabu kwa bei chee na bado wanataka walipiwa mafuta ya uendeshaji. Hii haingii akilini kabisa. This government must go before signing any more mikataba mibovu.
 
Tungewapatia umeme wa kutosha wakailipa Tanesco ingekuwa faida kwetu, badala yake umeme wakawa wanazalisha wenyewe na serikali ilikubali kutowatoza VAT kwenye fuel lakini ili kuzuia matumizi mabaya ya hizi exemptions, VAT hukusanywa kwa kila kitu kisha wahusika wanadai refund from treasury.
Kumbuka haya ni malimbikizo ya miaka 10.
 
Ni kweli hakuna haja ya kuwa na jazba. Tulisaini mikataba, lets keep our promises maana kama mjuavyo mambo ya the race to the bottom haya. Wa kutandikwa viboko ni hao waliosaini mikataba kwa niaba ya Watanzania. Unajua nchi za Africa zinashindana kuwa the cheapest place for investors. Na nachoona hapa ni mambo ya prisoner's dilema. Nikiwawekea ngumu wawekezaje basi watahamia Ghana, na Ghana nae ana feel the same. Anayefaidika ni Investor. We need to solve that in future contracts.
point...lakini mh, kumbuka kuwa resources sio kitu kinachoisha. In the longrun, you hold the bargaining power! Hicho ndicho kitu ambacho hatujajifunza! Tatizo ni hawa viongozi wetu WAJINGA wasiokuwa na upeo. Wao wanawaza leo, leo, leo, na tumbo langu, tumbo langu, tumbo langu. Ingali ningepata nafasi ya uongozi...bongo mngelia! Sipendi ujinga kabisa!!!
 
Si ajabu hata huo mrahaba wa 3% wanaolipa kila mwaka tangu waanze kuchimba dhahabu, jumla yake tangu mwaka 2000 hadi sasa haijafikia $273 million.

ukiulizwa utaambiwa ni siri! Zitto yupo wapi aje kutupa data. Mapato yetu vs Mapato yao. Hicho ndio tunataka kujua! Nimechoka kudanganywa!
 
Tungewapatia umeme wa kutosha wakailipa Tanesco ingekuwa faida kwetu, badala yake umeme wakawa wanazalisha wenyewe na serikali ilikubali kutowatoza VAT kwenye fuel lakini ili kuzuia matumizi mabaya ya hizi exemptions, VAT hukusanywa kwa kila kitu kisha wahusika wanadai refund from treasury.
Kumbuka haya ni malimbikizo ya miaka 10.

Kwa nini kulimbikiza miaka yote 10?
 
Kwa nini kulimbikiza miaka yote 10?

si ili upate nyingi kwa mpigo!!
Lakini kumbuka pia hii kampuni inapoteza hapa! Maana kama ingechukua pesa yake toka mwanzo (yani ikusanye kila mwaka), ingeweza kuwekeza hiyo pesa ipate riba. Lakini kwa kuiacha na TRA kwa miaka 10, ina maana haipati riba yeyote hapo! Lakini pia unaweza kukuta huo mkataba una sehemu ya riba. Huwezi kujua ujinga hawa viongozi wanaoweza ku-sign. Hata mimi naidai serikali huku tax refund ya miaka 3. Lakini sipati riba ya hiyo pesa!! Ningechukua kila mwaka, ningeweza kuweka benki na kupata riba yangu! But its a cost-benefit analysis!
 
Lakini tukumbuke hii migodi zi ya wazungu 100% kuna watanzania wenzetu, ndio wenye share humo, Kama ..........., ndio waliojua weakness za watendaji wa serikali yetu, na hao watendaji AKA........... wana mgao wao hapa. Nahisi Wazungu wanawashangaa sana, manake ni Watanzania ndio wanaotoa hizo tricks,
Waziri gani ahusike wakati gani,
Katibu gani apewe nini, watanzania wenzetu, na wala si wazungu, wanaojua hongo kiasi gani apewe nani,

Mie nina hasira sana na kizazi fulani hapa nyuma,
kizazi cha viongozi wa umma, waliofilisi mashirika walioongoza, walioiba kwenye mabenki walioongoza

kwa sasa wameingia ubia na makampuni ya nje makamuni haya makubwa kama ya simu, sementi, migodi nk, kwa kweli inabidi kufuatilia mali za viongozi iwe kazi kubwa sana!!
Hopefull watoto wetu watatusamehe kwa kuwa tunajitahidi kurekebisha hii hali.

MIMI SIWEZI KUWASAMEHE HAWA WATU WALIOIBA WAKAFILISI MASHIRIKA YETU, NA SASA WANAENDELEA KUHONGA SERIKALI KUPATA MIKATABA YA AJABU AJABU KUMULIKI MAKAMPUNI MAKUBWA YANAYOENDELEA KUTUNYONYA.
Kama anavyosema Kingunge Ubinafsi kila kona.
 
Hiki ndicho kipindi cha kujivua magamba, ccm walianza, sasa ni barick, sumu zao sasa ni dhahiri zitaumiza wengi, kumbe ngozi ikiwa ngumu uwezo wa kung'ata unakuwa wa matatizo.
 
AAAAAUGH hili balaa. Nahisi shinikizo la damu, Hivi kuna sababu yoyote kwa yeyote kutetea hiki? Sina maneno mengi ila nasema ile Timu ya madini iliyoongozwa na Zito ilitambua haya lakini kwa vile na yeye alishaingizwa ndani ya kundi ameyachunia.ZITO NAKUTUHUMU RASMI KWENYE HILI UNALIJUA NA UMEWAFICHA WANANCHI.
 
Jazba ni muhimu kuwa nayo kwa issue kama hii ya madini, siku tukija kustuka tutakuwa tumebaki na mashimo, na madini si kama mahindi au maharagwe yakichimbwa yanaisha hatuwezi kuyapanda, Naamini MUNGU yupo, MKAPA na KIKWETE watasulubiwa kwa makosa walioyafanya na wanayoendelea kuyafanya.
 
Nadhani CDM watautaarifu umma--katika operation itakayoanza nyanda za juu kusini hivi karibuni--kuhusu haya madudu yanayofanywa na serikali ya chama cha mafisadi
 
Kama hatutamuondoa Kikwete na mafisadi wenzake tutaendelea kulia na kusaga meno khe khe kheeeeeeeeeee huko ndiko alikojaza share zake na familia yake then mnauliza Riz anapata wapi mpunga? Hiyo ni mbinu yake lazima mmlipe hadi chozi la damu liwatoke!
Hivyo ndivyo anavyowashughulikia mafisadi khe khe kheeeeeeeeeeeeeee.


Nashindwa kuelewa ni jinsi gani Kikwete anahusika moja kwa moja hapa. Katika mambo haya kuna sera na sheria husika.
Ile sera ya madini ya mwaka 1997 (na marekebisho yake 2009) ndiyo iliyowaleta hawa wanyonyaji.

Sheria zinazolinda udhalimu huu ni sheria ya madini ya mwaka 1998 (ambayo ilirekebishwa mwaka 2010 ila bado ina mapungufu kedekede), Sheria ya kuhamasisha na kulinda uwekezaji ya taifa ya mwaka 1990, sheria ya uwekezaji ya mwaka 1997, sheria ya kodi ya mwaka 1973 na marekebisho yake ya (sheria ya fedha) ya mwaka 1992.

Ni sera na sheria hizi ndizo zinazoainisha mgawanyo wa mapato kwa kiwango cha mrahaba na kodi (pamoja na merejesho yake). Ukweli ni kwamba sheria mama hizi zliandikwa na kupitishwa kabla Kikwete hajawa kiongozi mkuu wa nchi hii.

Ukitaka kumnanga Kikwete basi sharti pia ulinange na mabunge, mabaraza ya mawaziri na marais wa vipindi vile maana wote ndio wanahusika hapa.

Nchi hii ilishauzwa kabla ya milenia na hapa tulipo watu tunafunika mashimo tu. Marekebisho ya sera na sheria ya Madini yaliyofanyika 2009 na 2010 yaligubikwa na mkono mkubwa wa makampuni haya dhalimu na nilishangaa hata kuona kuna mabadiliko finyu.

Ukweli ni kwamba Barrick na wenzao walishatupiga bao toka mwaka 1998, sasa katafuteni wachawi kule.
Anza na wataalam waliohusika

Lakini tukumbuke hii migodi zi ya wazungu 100% kuna watanzania wenzetu, ndio wenye share humo, Kama ..........., ndio waliojua weakness za watendaji wa serikali yetu, na hao watendaji AKA........... wana mgao wao hapa. Nahisi Wazungu wanawashangaa sana, manake ni Watanzania ndio wanaotoa hizo tricks,
Waziri gani ahusike wakati gani,
Katibu gani apewe nini, watanzania wenzetu, na wala si wazungu, wanaojua hongo kiasi gani apewe nani,

Mie nina hasira sana na kizazi fulani hapa nyuma,
kizazi cha viongozi wa umma, waliofilisi mashirika walioongoza, walioiba kwenye mabenki walioongoza

kwa sasa wameingia ubia na makampuni ya nje makamuni haya makubwa kama ya simu, sementi, migodi nk, kwa kweli inabidi kufuatilia mali za viongozi iwe kazi kubwa sana!!
Hopefull watoto wetu watatusamehe kwa kuwa tunajitahidi kurekebisha hii hali.

MIMI SIWEZI KUWASAMEHE HAWA WATU WALIOIBA WAKAFILISI MASHIRIKA YETU, NA SASA WANAENDELEA KUHONGA SERIKALI KUPATA MIKATABA YA AJABU AJABU KUMULIKI MAKAMPUNI MAKUBWA YANAYOENDELEA KUTUNYONYA.
Kama anavyosema Kingunge Ubinafsi kila kona.

Huyo mzee naye pia ni mnafiki. Unajua hawa watu wanafikiri watanzania tunasahau sahau hovyo? Vipi zile tenda za Smart Holdings na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam?
Nauelewa uchungu wako Haika, mikataba hii ni sawa na ile minyororo ya utumwa waliyofungwa mababu zetu, ambao tusisahau kwamba waliuzwa na weusi wenzao. Hii ni kasumba ya sisi weusi, siku zote sisi tunajiuza utumwani wenyewe.
 
Tusiwe na jazba, tusipinge kwanza. Naomba watu wafanye utafiti kwanza wajue katika kipindi wanachodai fidia, nchi tumefaidika kwa kupata tsh ngapi kutokana na mrahaba na kodi kutoka kwao. Then tuambiwe wao wamepata faida kiasi gani katika kipindi hicho. Halafu kwa kuwa wao ndio waliofanya upembuzi wa viability ya mradi, watuambie kuwa kwenye project plan yao walitarajia kupata revenue kiasi gani kwa unit fuel inayotumika, na je hiyo fuel iliyotumika, inalingana na kiasi cha revenue walichopata kwa mujibu wa makadirio yao ya awali? Kama hailingani, watuambie kuwa ni kwa nini watumie mafuta mengi kupata revenue kidogo? Je tuna uhakika gani kuwa mafuta hayo yalitumika sawasawa?

Wakiweza kutujibu vyema hayo, then serikali iwalipe
 
Nadhani CDM watautaarifu umma--katika operation itakayoanza nyanda za juu kusini hivi karibuni--kuhusu haya madudu yanayofanywa na serikali ya chama cha mafisadi
Sasa Chadema inahusika vipi hapa? tatizo la wadanganyika kila kitu wanadhani kinahitaji kusuluhishwa kisiasa.
 
Hii mikataba ya madini humu nchini inasadikika iko juu ya serikali. Ndio sababu ya haya. Inasainiwa hotelini London usiku.
 
Pascaldaudi,
Yule aliyesaini mkataba nina hakika anazo shares kwenye migodi ya Barrick, ndiyo maana hasumbuliwi na ripoti kama hizi. Ni kweli kisheria hakuna jinsi, unless tuwe na regime change, regime mpya ibatilishe mikataba yote kwa justification ya kwamba ilisainiwa kifisadi. Otherwise tutabaki historia tu kuwa once upon a time Tanzania was the 3rd world producer of gold, and we have nothing to show for it. Have you ever wondered why a person like Riz1 anaitwa new billionaire? Are there shortcuts for getting rich in Tanzania these days?

ndomana mzee wa kaya anasema fikra za kijamaa ndo zinaturudisha nyuma kupata wawekezaji, sababu anajua wanachokipata kwenye uwekezaji na nazani alikua anamaanisha familia yake ndo inarudishwa nyuma na hizo fikra za ujamaa sababu Tanzania kama taifa alinufaiki na chochote na uwekezaji.
 
Back
Top Bottom