Nashauri Prof Baregu aanzishe Baregu Foundation for Peace and Development (BFPD)

TANURU

Senior Member
Jan 13, 2010
162
6
Wakuu,

Kutokana na ujuzi alionao na umuhimu wake katika taifa letu, tumshauri Profesa Baregu aanzishe taasisi ya BAREGU FOUNDATION FOR PEACE AND DEVELOPMENT (BFPD). Naamini wengi tutamuunga mkono na hasa vyombo vya habari na wanafunzi wa elimu ya juu. Moja ya shughuli kuu za taasisi hii iwe ni kutoa elimu ya uraia kwa Watanzania kila wiki kupitia televisheni na redio.

Naomba kuwasilisha.

==

1701858197831.jpeg
Prof. Mwesiga Baregu alikuwa mwanazuoni na mwanasiasa mahiri nchini Tanzania. Prof. Baregu, alikuwa mhadhiri katika chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Idara ya Sayansi ya Siasa. Aliwahi kuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mwaka 1995 hadi 1997, Prof. Baregu alikuwa mwanachama na mshauri wa Augustino Lyatonga Mrema, wakati mwanasiasa huyo alipokuwa mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi na mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano.
Prof. Baregu alijiondoa kwenye kazi ya kumshauri Mrema, baada ya kujiridhisha kuwa aliyepewa kazi ya kumshauri, “ana washauri wengine, wanaofanya kazi ileile.”

Pia Soma TANZIA - Prof. Mwesiga Baregu afariki dunia
 
Zipo nyingine nyingi tu kama hizo. Ajiunge nazo kuziongezea nguvu. Aende MNF kwa kuanzia ambako kunafanywa SIASA zaidi.
 
Wakuu,

Kutokana na ujuzi alionao na umuhimu wake katika taifa letu, tumshauri Profesa Baregu aanzishe taasisi ya BAREGU FOUNDATION FOR PEACE AND DEVELOPMENT (BFPD). Naamini wengi tutamuunga mkono na hasa vyombo vya habari na wanafunzi wa elimu ya juu. Moja ya shughuli kuu za taasisi hii iwe ni kutoa elimu ya uraia kwa Watanzania kila wiki kupitia televisheni na redio.

Naomba kuwasilisha.

Iam strongly propose the motion. Hii ndio inatakuwa komesha jeuri ya serikali kwa kumtimua chuoni.Atengeneze ya kwake hana haja ya kuungana na wengine kama ndau mmoja alivyadai.
 
Iam strongly propose the motion. Hii ndio inatakuwa komesha jeuri ya serikali kwa kumtimua chuoni.Atengeneze ya kwake hana haja ya kuungana na wengine kama ndau mmoja alivyadai.
Kama ni hivyo, isiwe NGO kiwe chama cha siasa kabisa! Aachane na CHADEMA ambacho sio chake! NGO haitampa makali anayoyataka/mnayomtakia.
 
Kama ni hivyo, isiwe NGO kiwe chama cha siasa kabisa! Aachane na CHADEMA ambacho sio chake! NGO haitampa makali anayoyataka/mnayomtakia.

Kwani chadema ni cha nani tutoe mawazo kuwa chama ni mali ya mtu ina maana akianzisha kingine kitakuwa mali yake, chama chochote kile cha siasa ni mali ya wananchi hivi CCM ni mali ya nani, hana haja ya kuanzisha chama kingine cha siasa Chadema kinamtosha si vibaya kuwa na NGO sambamba na chama cha siasa.
 
Wana JF na waTZ kwa ujumla msipate taabu sana. Huu ushauri uliotolewa hapa tayari Baregu amekwisha kwenda nao hatua 10 mbele. For your tip, something like this is coming under the name Great Lakes Inst. for Peace
 
Huyu Professor amekwenda kinyume na contract aliyo saini kwenye kazi yake, nimzembe na hawajibiki. Hawa ndio wale wasomi wetu wasiofuata kanuni na maadili ya kazi wanaoendeshwa na maslai bila kujali professiopnal na responsibilty zake.

Tunachosubiri atutajie ma-professor wengine walifanya ujinga kama wake (hata kama ni CCM) tuwawajibishe

Kama yeye kavunja sheria ya kazi yake basi hafai na haaminki tena na jamii na hakuna excuse ya kuwa kuna watu wengine wanavunjasheria namimi acha nivunje. Huyu hafai
 
Wana JF na waTZ kwa ujumla msipate taabu sana. Huu ushauri uliotolewa hapa tayari Baregu amekwisha kwenda nao hatua 10 mbele. For your tip, something like this is coming under the name Great Lakes Inst. for Peace

Hongera zake sana. Tunaisubiri kwa hamu.
 
Zipo nyingine nyingi tu kama hizo. Ajiunge nazo kuziongezea nguvu. Aende MNF kwa kuanzia ambako kunafanywa SIASA zaidi.

Sentensi hii haiitendei haki Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) iliyoanzishwa na kubarikiwa na Mwalimu mwenyewe kwa ajili ya kuendeleza yale mema ambayo alikuwa akiyasimamia kwa manufaa ya nchi yetu, Afrika na duniani kwa ujumla.

Kumwambia Baregu aende MNF ambako kunafanywa "siasa zaidi" ni kumpotosha Baregu, kupotosha watu na kuidhalilisha Taasisi. Zogo lililotokea baada ya MNF kufanya Kongamano la Kumbukumbu ya Miaka 10 ya Kifo cha Baba wa Taifa la Tanzania na baadhi wa watu kutoa madukuduku yao ya kisiasa kusiwe sababu ya kuipaka matope Taasisi ambayo lengo lake kuu ni kusaidiana na wananchi kujenga na kuimarisha Amani, Umoja na Maendeleo ya wote.

Baregu si 'haini' ni Mtanzania kama Watanzania wengine mwenye uchungu na nchi yake. Naamini MNF itaweza kumpokea Baregu kwa mikono miwili endapo atataka kujiunga na Taasisi hiyo kwa madhumuni ya kusaidia Taasisi itekeleze/ifanikishe malengo yake kwa kufuata misingi ya ujenzi wa amani, umoja na maendeleo ya wote kama Mwalimu Nyerere alivyoagiza.
 
Huyu Professor amekwenda kinyume na contract aliyo saini kwenye kazi yake, nimzembe na hawajibiki. Hawa ndio wale wasomi wetu wasiofuata kanuni na maadili ya kazi wanaoendeshwa na maslai bila kujali professiopnal na responsibilty zake.

Tunachosubiri atutajie ma-professor wengine walifanya ujinga kama wake (hata kama ni CCM) tuwawajibishe

Kama yeye kavunja sheria ya kazi yake basi hafai na haaminki tena na jamii na hakuna excuse ya kuwa kuna watu wengine wanavunjasheria namimi acha nivunje. Huyu hafai
Bull,
Je sheria iliyovunjwa ni ipi na sheria inaapply kwa Baregu tu?
Dr. Mvungi ni nani?
Late Prof. Shayo alikuwa nani?
Nawe akili zako ni za kukurupuka kama za huyo Ghasia.
Naomba muangalie vitu kwa undani, marefu na mapana yake na practice inayoendelea nchini bila kuwa subjective. Lets be objective in our urguments, yes we learn how to disagree but we must give reasons to support our urguments!!!!!!!!
 
Bull,
Je sheria iliyovunjwa ni ipi na sheria inaapply kwa Baregu tu?
Dr. Mvungi ni nani?
Late Prof. Shayo alikuwa nani?
Nawe akili zako ni za kukurupuka kama za huyo Ghasia.
Naomba muangalie vitu kwa undani, marefu na mapana yake na practice inayoendelea nchini bila kuwa subjective. Lets be objective in our urguments, yes we learn how to disagree but we must give reasons to support our urguments!!!!!!!!



Huwezi kuwa na cheo kwenye chama cha siasa na wakati huohuo ni mfanyakazi kwenye public corprtion kama alivyo saini agrement.

Kama kunawatu walivunja sheria huyu kama Professor anatakiwa kulaani uvunjaji sheria sio kujiunga kwenye mkumbo, kwakizingizio eti fulani pia kafanya

wasomi kama hawa wanapoona mwenzake kafanya ufisadi nae anajiunga!! wasomi namna hii hatunashida nao hapa Tanzania.
 
Huyu Professor amekwenda kinyume na contract aliyo saini kwenye kazi yake, nimzembe na hawajibiki. Hawa ndio wale wasomi wetu wasiofuata kanuni na maadili ya kazi wanaoendeshwa na maslai bila kujali professiopnal na responsibilty zake.

Tunachosubiri atutajie ma-professor wengine walifanya ujinga kama wake (hata kama ni CCM) tuwawajibishe

Kama yeye kavunja sheria ya kazi yake basi hafai na haaminki tena na jamii na hakuna excuse ya kuwa kuna watu wengine wanavunjasheria namimi acha nivunje. Huyu hafai

Uko off topic hapa tunazungumzia Baregu Foundation na si ajira ya Baregu, kwa taarifa yako tu Baregu alishasema hana haja ya ajira hiyo.
 
Wana JF na waTZ kwa ujumla msipate taabu sana. Huu ushauri uliotolewa hapa tayari Baregu amekwisha kwenda nao hatua 10 mbele. For your tip, something like this is coming under the name Great Lakes Inst. for Peace


tunashukuru kwa taarifa hiyo sasa imefikia wapi tujulishane mkuu
 
Uko off topic hapa tunazungumzia Baregu Foundation na si ajira ya Baregu, kwa taarifa yako tu Baregu alishasema hana haja ya ajira hiyo.



Tutamuamini vipi kuendesha foundation wakati anazembea katika mambo ya terms na agrements?

Huoni wasomi kama hawa ni hatari kumpa dhamana nzito yoyote? naaliniacha ho alipo jitetea wakati wa kunyimwa ku-extend contract.
 
hapa umesema ukweli kabisa ila ni kwa sababu tu ya mambo ya siasa na vile kama akitoa yupo ndani ya CHADEMA basi anaonekana ni mtu wa ajabu sana
 
Tutamuamini vipi kuendesha foundation wakati anazembea katika mambo ya terms na agrements?

Huoni wasomi kama hawa ni hatari kumpa dhamana nzito yoyote? naaliniacha ho alipo jitetea wakati wa kunyimwa ku-extend contract.

Ndugu Bull
Usichanganye mambo kuongoza NGO ni tofauti na kuongoza Chama cha Siasa, hata wewe unaweza kuanzisha NGO yako kutegemea na malengo yako na uwezo wako hakuna atakaye kuuliza kwa nini wewe umejiweka Chairman mke wako treasurer binamu katibu etc. tofauti na chama cha siasa ambacho malengo yake ni kushika dora kiongozi anakuwa answerable kwa wananchi.

Kuhusu ajira ya Baregu nimesema hii thread haihusu hilo kuna thread nyingine inasema 'kwa nini Baregu amenyimwa kazi UDSM' nafikiri bado ipo tukutane huko bye.
 
Back
Top Bottom