Barazani Kwa Ahmed Rajab: Muungano wa Mkataba utaleta Umoja wa Afrika

Tanganyika hawaogopi kuvunja muungano Barubaru, as a matter of fact, mjadala ya muungano haujageuzwa kuwa three course meal kama ilivyo kwa Zanzibar. Kinacholeta shida hapa ni hizi kelele za 'divorce' lakini hakuna mtu anajaza fomu za talaka - for years! Mtu unasema unataka talaka lakini wakati huo huo unamtayarishia maji ya kuoga na chakula mezani kawa kawaida - hivi hapo unadai talaka au unataka kujua kama una bei?
Taratibu za kuachana na ndoa zinajulikana, hizi geresha za nini? Au mnatishia ili bill ya umeme mlipiwe tena?
Hiyo three course meal imeniacha hoi, ha ha ha !
kuhusu Talaka Mkuu Mkandara alishawahi kuweka usemi wake kuwa 'Kadhi kaingia mjini wanandoa hawataki kudai talaka' ndicho kinachoonekana.

Ukisoma makala ya Ahmed, amesema inatakiwa kuwa na mkataba ambao nchi zote zitakuwa sawa bila mmoja kuwa mshiriki mkuu. Katika mambo wanayotaka yawe ya mkataba ni pamoja na Ulinzi na Usalama ambao bajeti yake ni Bilioni 900+. Bajeti ya ZNZ ni sh Bilioni 600. Sasa hapo tukigawana usawa ZNZ watabaki na nini?
Maana ya usawa si maneno ni ushiriki ati, vinginevyo Tanganyika itabeba sehemu kubwa na hapo suala la ushiriki mkuu halitaepukika

ZNZ kamwe hawataki kuomba Passport yao kwasababu kubwa moja, wakiwa nayao tayari ni wageni.
Maana rahisi ya mkataba ni kuwa 'tuwasaidie' ili waendeleze nchi yao kwa rasilimali zetu, ukisema zao haraka haraka wanapeleka mswada kama ule wa gasi na mafuta.
Sasa tunajiuliza ni mkataba wa kitu gani ambao Mtanganyika atasema naam ushikirikiano una manufaa.
Huwezi kuwasikia wanadai sarafu yao kwasababu wanajua kuwa vitu kama umeme vitakuwa kwa dola.

Kwa ufupi mkataba wanaotaka ni wa mambo haya:
1. Urahisi wa kuwekeza bara (halinatabu hili kama wanataka maana tunakaribisha wawekezaji kwa taratibu maalumu )
2. Ardhi (linawasumbua kichwa sana, Waitaliano taratibu wanawahamisha kwenda pembezoni)
3. Soko la Ajira ( WZNZ walioajiriwa bara ni wengi kuliko walioajiriwa na SMZ,nje ya muungano kitumbua kidogo)
4. Soko la Biashara (Kontena 800 walizolalmika TRA inawawekea kauzibe zilikuwa zinaingia bara, mfano mmoja tu)
5. Ruzuku (Bajeti yao haijitoshelezi, karafuu na utalii vina ushindani sana duniani)
6. Ulinzi na usalama (Hawana bajeti hata ya senti tano, wamestarehe mgongoni wanakula halua)
7. Elimu ya juu ( Hawana bajeti hata senti tano, watoto wanasoma kwa social welfare ya Tanganyika)
8. Wastaafu na Mishahara (Yote inatoka Hazina Dar, wanataka tuendelee kuwalea wastaafu wao na wafanyakazi)
9. Supplies (Wanajua nje ya muungano na sarafu tofauti, biashara itakuwa katika mizania ya 'world currency')
10. Bandari huru (wanajua access ya bidhaa zao EA ni kupitia Tanganyika, Tanganyika ikiwa na bandari huru kwishnehi)
11. Energy(wanajua hawana vyanzo mbadala vya nishati kama umeme, nje ya muungano no free ride)

Ninachosema hapa ni kuwa mkataba maana yake ni kuweka mambo yatakyowasaidia.
Hakuna jambo hata moja, narudia hakuna jambo hata moja Tanganyika itawahitaji ZNZ! None!
Sasa tunahitaji mkataba nao wa nini?
 
Tanganyika hawaogopi kuvunja muungano Barubaru, as a matter of fact, mjadala ya muungano haujageuzwa kuwa three course meal kama ilivyo kwa Zanzibar. Kinacholeta shida hapa ni hizi kelele za 'dovorce' lakini hakuna mtu anajaza fomu za talaka - for years! Mtu unasema unataka talaka lakini wakati huo huo unamtayarishia maji ya kuoga na chakula mezani kawa kawaida - hivi hapo unadai talaka au unataka kujua kama una bei?

Taratibu za kuachana na ndoa zinajulikana, hizi geresha za nini? Au mnatishia ili bill ya umeme mlipiwe tena?

"Ndugu" zetu hawa ni watu waliokuwa misguided hata wasijue nini wanataka tena..............hisia zao zimetawaliwa na jazba na hamaki tupu. Kusema kweli Watanganyika hatuna shaka sema tu hawa ni kama mbu wapigao kelele sikioni, inakera kweli kweli
 
Tatizo wana ma-guru wao wa kuongelea mambo yao. Hawa maguru wakisema tu kila mzanzibari anafuata. Ngoja siku si nyingi maguru watakuja na mfumo mpya walioubuni..........na kila Mzanzibari atauimba!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Nguruvi3 Muungano aka Mfumo kristo sisi tutaendelea kuupinga . Wewe endelea kuutetea kwasababu ndio unakuweka mjini. Miaka ya kuburuzana imekwisha, fanyeni Muungano na Kenya ,Uganda na wengine hulka na tamaduni zenu zinafanana.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo wana ma-guru wao wa kuongelea mambo yao. Hawa maguru wakisema tu kila mzanzibari anafuata. Ngoja siku si nyingi maguru watakuja na mfumo mpya walioubuni..........na kila Mzanzibari atauimba!

Guru mkubwa alikua dikteta Nyelele...Ajabu ,pamoja na kwamba amefariki lakini bado anaendelea kuabudiwa na watu kama wewe brain washed...Zidumu fikra za mwenyekiti !!! Hapana, hapa kila mtu ana fikra zake.
 
"Ndugu" zetu hawa ni watu waliokuwa misguided hata wasijue nini wanataka tena..............hisia zao zimetawaliwa na jazba na hamaki tupu. Kusema kweli Watanganyika hatuna shaka sema tu hawa ni kama mbu wapigao kelele sikioni, inakera kweli kweli

Na huyu nae, Hapa kila Mzanzibari anajua anachokitaka, tatizo nyinyi bado mnaendelea kutawaliwa na mawazo ya mfu aka dikteka Nyelele.
 
....ZNZ kamwe hawataki kuomba Passport yao kwasababu kubwa moja, wakiwa nayao tayari ni wageni.
Maana rahisi ya mkataba ni kuwa 'tuwasaidie' ili waendeleze nchi yao kwa rasilimali zetu, ukisema zao haraka haraka wanapeleka mswada kama ule wa gasi na mafuta. ....
Nyimbo zenu mkawaimbie watoto wa chekechea ...OH, TUNAWAPA UMEME , OH TUNAWALINDA , OH TUNAWAPA AJIRA, OH ,BLAH BLAH NYINGI ...HAMNA LOLOTE . sisi hatutaki msaada wenu , umeme ulikuwepo znz kabla ya Muungano.
 
Mkuu Nguruvi3, kwa kweli ni vigumu kwa mtu yeyote mwenye akili timamu kuwaelewa hawa Wazanzibari kuwa ni kitu gani hasa wanachokitaka kwa mfano huyu anayejiita takashi;
Umelewa pombe au umevuta unga au umechanganya? Sisi "tuachiwe tupumue" temekua tukidai kura ya maoni kuhusu Muungano. CCM na vibaraka wao hawataki suala la kura ya maoni kwasababu wanajua matokeo yake ni nini... CCM ndio imeshikilia mpini Tanganyka na ZNZ, nadhani unaona madhila yanayowakuta CHADEMA. Lakini tanasema mwanzo wa mwisho umeanza.

Kundi la vibaraka lililo vishwa vilemba vya ukoka bado wamo katika ndoto za mchana. Ukombozi unakuja kwa njia moja au nyengine. Tumechoka na Muungano aka mfumo kristo.
Katika hitimisho lake akitoa hotuba bungeni kwa niaba ya kambi ya Upinzani, Mh. Tundu Lisu alikuwa na haya ya kusema kuhusu Muungano;
Mheshimiwa Spika, Katiba ya sasa ya Zanzibar ambayo mashabiki wa Muungano wameileta kwa kupitia Sheria ya Mabadiliko ya Kumi ya Katiba tayari imewapa wananchi wa Zanzibar haki ya kuamua, kwa kura ya maoni, mambo mbali mbali yanayoihusu nchi hiyo na namna itakavyoongozwa. Mashabiki hawa wa Muungano wakubali kuvuna walichopanda, wasibeze wale wote wanaotaka kutumia haki ya kura ya maoni kuamua hatma ya Muungano na nafasi ya Zanzibar ndani au nje yake.

Mheshimiwa Spika, ni wazi, kwa kuzingatia ushahidi huu, kwamba madai ya kuwa na kura ya maoni ya wananchi ili kuamua masuala makubwa yanayohusu Muungano wetu ni ya siku nyingi na yametolewa na watu na taasisi mbali mbali. Madai haya hayajaanzishwa na wana-Uamsho wala CHADEMA. Ni wazi vile vile kwamba kura ya maoni inaruhusiwa kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya Zanzibar.

Kwa sababu hizi, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaungana na wale wote ambao wamedai, na wanaendelea kudai kuitishwa kura ya maoni ya wananchi ili waweze kuamua mustakbala wa nchi yetu. Kuendelea na kiini macho cha Muungano wakati Serikali zote mbili na chama tawala cha CCM wanauvunja kivitendo kutaipelekea nchi yetu kwenye njia ya Ethiopia na Eritrea, au Sudan na Sudan Kusini au Yugoslavia ya zamani.

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inataka Watanzania waamue, kwa kura ya maoni, kama bado wanataka kuendelea na Muungano na kama jibu lao ni ndio, ni muundo gani wa Muungano wanautaka. Kama, kwa busara zao, wataamua kwamba nusu karne ya Muungano inatosha basi itakuwa afadhali kwenda njia ya Czechoslovakia ya zamani kuliko kwenda njia ya Yugoslavia ya zamani, au Ethiopia na Eritrea au Sudan na Sudan Kusini.

Mwisho, Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali iwaeleze Watanzania juu ya hatua, kama zipo, ilizozichukua kuzuia ukiukwaji huu wa Makubaliano ya Muungano, Sheria ya Muungano na Katiba. Na mwisho, Serikali itoe kauli mbele ya Bunge hili tukufu kama - kwa ukiukwaji huu wa Makubaliano ya Muungano, Sheria ya Muungano na Katiba ya Muungano – Bunge hili tukufu litakuwa ndani ya mamlaka yake kuchukua hatua za kumshtaki Rais kwa mujibu wa ibara ya 46A ya Katiba kwa kushindwa kuihifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Muungano kama kiapo cha kazi yake kinavyomtaka.
Ajabu ni kwamba Wabunge wote kutoka Zanzibar bila kujali tofauti zao (CUF, CCM na UAMSHO) waliungana na wabunge wa CCM wa bara kumshambulia, kumkebehi na hata kumtukana Mh. Tundu Lisu kwa msimamo wake huo. Kwa kweli Nguruvi3, kuendelea kujadili mada za watu kama Ahmed Rajab ni kupoteza muda, hawajui wanataka ama wanapinga nini mradi tu wanapiga kelele wasikike. Amini usiamini wangekuwa kweli hawautaki Muungano, kwa kutumia katiba yao ya sasa, wangeishauvunjilia mbali kitambo ila kwa sababu ni wapenda vya bwerere, hawataacha kulialia. Kama mtu hawezi hata kujua kuwa huu tulio nao ni muungano wa kikataba halafu andai ni wabara ndio hawaelewi mkataba na kitu gani, huyo kweli ni wa kujadiliana naye? Shuhudia hayo aliyoyasema takashi ni ushahidi tosha wa ugonjwa walio nao hawa jamaa...
 
Katika hitimisho lake akitoa hotuba bungeni kwa niaba ya kambi ya Upinzani, Mh. Tundu Lisu alikuwa na haya ya kusema kuhusu Muungano;

Mag3

Mimi nilitegemea Mh. Lissu angelivalia njuga suala la kuirudisha Tanganyika na serikali ya Tanganyika kwa kupeleka bungeni mswada binafsi. Hapo sina shaka angepata wabunge wengi wa kumuunga mkono.

Hata hili la kura ya maoni nalo pia angelisimamia zaidi ya kutoa kauli tu bungeni.

Lakini hatupaswi kujifanya vipofu, Muungano ni mali ya CCM. CCM inayotawala (inang'ang'ania kutawala kwa ushindi wa kishindo) Tanganyika na pia Zanzibar. Mizengwe inayofanywa na CCM katika "kuulinda muungano" haihitaji darubini. Sote tunaijua.

Katika mchango wako unazungumza na Mkuu Nguruvi3, lakini Nguruvi3 hataki Tanganyika irudi wala serikali ya Tanganyaka irudi. Hata MJJ pia ni vivyo hivyo.

Hawa pia hujawahi kuwasikia wakimshauri Mh. Lissu au mbunge yeyote wa Tanganyika(Tz bara/bara) kuyasimamia hayo masuala mawili; kuirudisha srikali ya Tanganyika na kura ya maoni juu ya muungano.

Kwa bahati mbaya , MJJ na Nguruvi3 wanashajihisha tukubali nchi moja,serikali moja ,taifa moja....na hii ni sera ya CCM.

Nilishawahi kutoa rai kuwa kama Zanzibar haitaki kutoka katika muungano, kitu ambacho chini ya serikali za CCM hicho hakiwezekani, basi ifukuzwe kama Malaysia ilivyoifukuza(expulsion) kupitia kura ya bungeni, Singapore kutoka katika Muungano.

Na hapo umuhimu wa mbunge wa CHADEMA kuanzisha hii move unajitokeza.

Siasa za Tanzania zinaweza kumpa mtu maradhi ya moyo!!!! Ni usanii kwenda mbele.
 
Nyimbo zenu mkawaimbie watoto wa chekechea ...OH, TUNAWAPA UMEME , OH TUNAWALINDA , OH TUNAWAPA AJIRA, OH ,BLAH BLAH NYINGI ...HAMNA LOLOTE . sisi hatutaki msaada wenu , umeme ulikuwepo znz kabla ya Muungano.
Mkuu Takashi, nionyeshe Bajeti ya ulinzi na usalama ya SMZ YA MWAKA 2012-2013!
Ahmed Rajab makala ya wiki iliyokwisha alithibitisha kuwa wapo wazanzibar wanafanya kazi katika halmashauri na taasisi za bara na akahoji WZNZ hao wanaisaidiaje ZN. Sasa Ahmed akikiri hivyo wewe una ubavu wa kukataa kama nani maana msemaji wa WZNZ wengi keshasema ati.

Ninakuhakikishia kuwa muungano unaajiri waznz wengi kuliko SMZ, na si kuajiri tu hata mishahara ya wafanyakazi wa SMZ imekuwa inatoka hazina. Shahidi wa haya ni Salimin Amour, Aman Abeid Karume, Nahodha Shamsa Vuai, Basili pesambili Mramba, Zakia Hamdan Meghji, Mustafa Mkulo kwa uchache tu.

Kifaa cha umeme kilipoharibika Chumbe baada ya kushindwa kupata pesa, Nahodha akiwa waziri kiongozi aliomba Muungano usaidie na ndipo zikatolewa bilioni 5.

Ukweli kuwa ZNZ haijawahi kulipa hata senti tano ya umeme hauhitaji shahada ua Diploma. Lakini pia hata mgao hawaujui wenzetu hawa kwa jinsi walivyopakatwa kama cheke chea.

SMZ hailipi hata senti tano kwa Mwanafunzi wa ZNZ anyesoma elimu ya juu. Na sikuwa hailipi haina hata bodi ya mikopo.
Wametaka kuanzisha bodi ya mikopo cha kushangaza eti wanaomba fungu kutoka bara kana kwamba ni haki yao.

Viwango vya ufaulu kwa wanafunzi wa ZNZ na nafasi za upendeleo ni nafasi nyingine, ushahidi upo Vyuo vyote vya elimu ya juu. 2/3 ya viongozi wote wa ZNZ wamesomea bara na wengine kama akina Seif bureee, leo ndio wanachagiza wenzao kwasababu watoto wao tayari wanasoma majuu.

Umeme ulikuwepo ZNZ siku nyingi, lakini dunia imebadilika. Kama wanadhani hawautaki wa Tanganyika wasingekubali kupakatwa kirahisi kwa kuachiwa deni la bilioni 50+

Licha ya yote hayo ZNZ inapata mgao wa asilimia 7 ya pato la taifa kila mwezi kwasababu kodi yao haiwezi kuendesha serikali. ZNZ inakusanya bilioni 15 kwa mwezi na takribani bilioni 200 kama kodi kutoka vyanzo vyote kwa mwaka.
Pengo la bilioni 400 linafidiwa na kodi za Watanganyika.

Hayo yote Ahmed hawaambii anawaeleza neema wakati wa Sultani. Anawadanganya kuwa bidhaa nyingi zinatoka bara Asia kama sahani, viberiti n.k. Asichowaambia ni kuwa Vyakula vinatoka Tanganyika sio Mauritius, Kenya au Malaysia.

Usijae jazba wakati huu maana hapa JF ukweli utasemwa hata kama ni mchungu.
Hayo yote kama ni uongo basi jibu hoja kwa hoja.
Ukweli usio na kificho ni kuwa ZNZ inahaha na kutapa tapa, hizi kelele za mkataba n.k. ni sehemu ya mahangaiko.

Sisi tunasema tunawatakia heri majirani zetu, kwasasa LET ZNZ GO!
 
Nonda, kitu usichokubali ni madai ya WZN kuwa wanaonewa, wananyang'anywa rasilimali zao, wangekuwa kama Malaysia, walikuwa wa kwanza kuwa na TV ya rangi Afrika, walipata umeme wa meli siku nyingi n.k.

Wanadai muungano ndio umedhoofisha ile nchi, ni muungano ndio umepeleka kuwepo na ujambazi, umalaya, uvutaji madawa ya kulevya, uchangudoa, ulevi n.k.

Tanganyika haijawahi kulalamika kuwa umasikini wake ni kwasababu ya kuibeba ZNZ, haijawahi kulalamika kuwa uwepo wa matendo maovu ni matokeo ya nchi yoyote.

Muungano huu kama ilivyo mingine una matatizo lakini basi matatizo yazungumzike kwa njia za amani.
Tanganyika imebaguliwa sana bila kulalamika. Leo Mtanganyika anapewa kitambulisho cha ukazi kama Mgiriki au Mzimbabwe. Hayo yakiendelea Wazanzibar walioko bara hawabughudhiwi kwa lolote lile.

Mtanganyika anachomwa moto akiwa na kibanda cha biashara, haijatokea mpemba au mzanzibar mwingine kuchomewa moto biashara zake zaidi ya kupewa mahali pa kuishi kwa amani.

Mtanganyika hapewi ajira SMZ, lakini huku bara wamejaa na hakuna aliyenyimwa ajira kwa Uzanzibar wake.
Mlolongo wa mambo ni mengi kama nilivyoorodhesha hapo awali.

Kwa vile Maalimu Seif ameenda kuomba kiti UN, na Ahmed anataka kiti EU na EAC, hakuna shaka kuwa anayetaka kuondoka katika muungano ni MZN. Vinginevyo hakuna sababu ya ZNZ kuomba kiti.

Kilio kikubwa cha WZNZ ni kuwa na taifa huru na mamlaka kamili.
Huu ni ushahidi kuwa wao ndio wanapaswa kuamua hatima yao. Tena wanavyombo vyao kuanzia bendera, wimbo wa taifa BLW n.k. (Ingawa passport hawataki kusikia habari hiyo).
Kwa kutumia hivyo vyombo kama walivyovitumia kuwa na SUK n.k. wana haki na uwezo wa kuamua hatima ya muungano.

Kinyume chake wamebaki wakimsikiliza Ahmed Rajab anayewaacha njia panda kila mara akibanwa na kukosa hoja.

Nonda, Mkataba mnaoutaka ni wa kitu gani? mbona hamnijibu mnakimbia kimbia
Hivi unakubali kuwa kuna mkataba mzuri kama wa Senegambia?

Anayelalamika ndiye anatafuta haki, kama mnadhani Tanganyika inawaonea amueni hatima yenu si kuzunguka zunguka kwa maneno meengi, matusi na kashfa huku mkijua fika muungano ni kimbilio lenu katika nyakati hizi.
 
............


Inayumkinika kwamba hili zoezi la kukusanya na kuyaratibu maoni ya wananchi litahitimishwa katika muda wa miezi sita ijayo. Litapomalizika sitostaajabu nikiwaona baadhi ya watu wakitahayari na kujaribu kuziziba nyuso zao. Hawa ni wale wasioamini kwamba Tume itayawakilisha vilivyo maoni inayoyakusanya Zanzibar(2).


Uchambuzi wangu: Chanzo cha taarifa hii ni makala katika gazeti la Raia mwema wiki hii.

Namba (2) anasema tume itakusanya maoni ya wznz
kikamilifu hata kama tume hiyo inakusanya pia kutoka Tanganyika. Hapa anaonyesha kuwa wanaolilia hatima ya muungano ni ZNZ na siyo Tanganyika. Kwa mantiki hiyo wangeweza kufanya kura ya maoni wao kuamua hatima yao bila kusubiri tume.


Baada ya kukugaragaza hoja namba moja kuhusu "undugu" na "mali" na kama ulivyotaka kuchakachuwa na umeshindwa kutetea hiyo hoja, nakushauri kitafute kisa cha "Adili na Nduguze" au kitafute kisa cha Mtume Yusuf (AS) utapata kuuelewa undugu na mali...

Wacha niende kwenye hoja yako uliyoifanya ya pili (Namba 2). Hapo naona hujachambuwa bali umebadili maneno, aliyoandika Ahmed Rajab mengine, wewe umefanya hila kuyabadili kuwa mengine kabisa. Huoni haya wala hujui vibaya.

Hivi unaelewa Kiswahili au unakurupuka tu? Hayo yote niliyokuwekea nyekundu sikuyaona katika hiyo hoja ya Ahmed Rajab (nayo ni hiyo nimeiweka hapo), kwanini ubadili maneno na kusema ni yake? Nimeweka alivyoandika yeye na ulivyobadili wewe, bila kuongeza nukta wala koma, ni kama ardhi na mbingu, vitu tofauti.

Kwa nini unachakachuwa kiasi cha kuibadili maana kabisa?
Ili iweje? kwa faida ya nani? ya kujidanganya nafsi yako au kupotosha wanaosoma?
 
Hivi ni nini kinachowazuia Wazanzibar kujitoa kwenye Muungano?!! Tumechoshwa na kelele zenu. Khah!! Mshapewa hadi desa la jinsi ya kujitoa lakini bado tu mnaendelea kutupigia kelele na kutudhalilisha watu wa Tanzania bara. Kama mmeuchoka Muungano mshaambiwa pelekeni muswada BLW na mpitishe kujitoa. Hizi kelele za bata hazisaidii kitu hapa!

Takalani....,
Waliotoa desa walirudi tena na kutwambia tudai serikali moja, nchi moja na taifa moja. Au hukupata ujumbe huo?

Umeuliza nini kinawazuia wazanzibari kujitoa.
Hili halitaki uwe mchambuzi kama Nguruvi3 au MJJ.

CCM ndio inayozuia Zanzibar isitoke kwenye muungano. Sio kuzuia kutoka tu,lakini CCM wanakauli ya kuuimarisha muungano. Unaelewa maana yake?

CCM kwa kutumia mamlaka ya dola ya Muungano na vyombo vya ulinzi na usalama wanafanya yale wanayofanya pia kwa Tanganyika(Tz bara/ bara) kuzuia mabadiliko. Muungano ndio uhai wa CCM na kwa hilo unaweza kufahamu kwa nini CCM hawawezi au hawataki kujinyonga.

Kwa kuhofia mabadiliko juu ya Muungano na muundo wake, CCM hulazimika kushinda uchaguzi mkuu "kwa kishindo" ili kuhakikisha kinaendelea kuulinda muungano na kujihakikishia uhai wake.

Kwa upande wa Zanzibar, Serikali ya muungano ambayo inaongozwa na CCM inahakikisha inasimika serikali ya CCM hata pale inaposhindwa kupitia kisanduku cha kura. Kwani tume ya uchaguzi ya Taifa huku bara inatangaza mshindi wa kura za uraisi kwa kutegemea kura zilizopigwa?

Hapa tunazungumzia Chama cha Mapinduzi kinachoogopa mapinduzi/ kupinduliwa!!!(kuondoshwa madarakani hata kwa njia halali ya kisanduku cha kura)

Ndio sababu ya CCM kuwa na kauli yao ya Mapinduzi daima.

CCM inanyoa watu Tanganyika , pia inanyoa watu Zanzibar.

Kauli yako na kauli za wachangia wengi wa hii thread zitaleta maana kama ni wanaCCM tu.
 
Mpotezee tu huyo...nia yake ni utoke kwenye msingi wa hoja zako, uanze kujadili vitu trivial.
 
Hivi ndio vitu nilivyokuwa najaribu kuelezea, jazba, hamaki na shutuma zisizo hata na basis.Sasa na kuuliza ni nini unachokitaka? ni kipi kinachokuzuia kukipata? Tafadhali jaribu kuwa clear kwenye majibu yako na kuweka jazba pembeni.
 
Nguruvi3 Hii longo longo ya ukarimu wenu tumechoka nayo...Sisi tunataka nchi yetu, kuamua wenyewe mustakbali wetu, nawashauri muanze na kukata umeme...Zuwieni maharage , viazi visije ZNZ. Baadae mkae msubiri mzanzibari afe njaa... Kazi yenu kutuwekea kauzibe , hamna mbele wala nyuma baadae mnatulazimisha sisi kwenye mkumbo.
 
Last edited by a moderator:
Hivi ndio vitu nilivyokuwa najaribu kuelezea, jazba, hamaki na shutuma zisizo hata na basis.Sasa na kuuliza ni nini unachokitaka? ni kipi kinachokuzuia kukipata? Tafadhali jaribu kuwa clear kwenye majibu yako na kuweka jazba pembeni.

Elizabeth,

Kama hiyo picha ni yako kweli ,Mashaallah . Sisi tuanataka ZANZIBAR huru, yenye mamlaka kamili. Kinachotuzuwia ni mfumo mzima wa Muungano. Kwamba Tanganyika (Tanzania) inatudhulumu haki zetu. Nyinyi mnautumia Muungano kwa maslahi yenu (Tanganyika). Lakini Zanzibar inanyimwa fursa nyingi ikiwemo kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Taasisi au Mashirika ya kimataifa.

Zanzibar, imezuwiwa kujiunga na OIC, pamoja na kwamba 99% ni waislamu. Leo hii makafiri kwa kutumia Mfumo Kristo (Muungano) ndio wamekuwa waamuzi wa mustakbali wa Zanzibar.

Hamaki ni muhimu katika kuonesha kuchukia kitu...Hii ni hatua ya mwanzo ya kuonesha kutopendezwa na jambo . Ni tabia ya mwanaadamu, nothing strange here.
 
Nguruvi3 Bwana Mkubwa, Sisi tunasema hatutaki kubebwa...Nadhani hiki nikiswashili sahihi kabisa. Kwanini mjilazimishe kubeba mzigo? Tunasema hatutaki....Ukweli usiotaka kuusema kama yule Mtakatifu wenu (dikteta Nyelele) aliwadanganya kuwaambia kwamba Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika. Na hii ndio siri ya kulazimisha Muungano. Hakuna haja ya kuzungunka mbuyu.

Msijipe mamlaka ya kuisadia ZNZ wakati watanganyika wenyewe masikini wakutupwa.
 
Last edited by a moderator:
Takashi na Zomba naona bado munawapa darasa wadanganyika endeeleeni inshallah watafahamu tuu kwamba tunataka nini
 
Back
Top Bottom