Baraza la Wazee kujenga jamii inayoheshimu haki za binadamu

FikraPevu

JF-Expert Member
Jan 2, 2010
303
236
Serikali imeshauriwa kuharakisha upitishaji na utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kuzuia unyanyasaji na mauaji ya wazee nchini utakaosaidia kuundwa kwa Baraza la Wazee na kujenga jamii inayoheshimu haki za watu wachache.

Kwa mujibu wa Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wazee imefikia milioni 2.5 ambayo ni sawa na asilimia 5.6 ya wananchi wote. Lakini idadi hiyo inaongezeka kila mwaka na kutishia usalama wao ikiwa hatua mathubuti hazitachukuliwa.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wazee Morogoro (MOREPEO), Samson Msemembo amesema katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya haki za binadamu, jamii na serikali inapaswa kuwaangalia wazee na kuwatoa katika hali duni inayowakabili.

Amesema wazee wanakabiliwa na umaskini, unyanyasaji, mauaji na kukosa huduma muhimu za matibabu na usalama ambazo zinawaweka katika hatari ya kutothaminiwa na jamii inayowazunguka.

“Tunapoadhimisha kilele cha siku ya haki za binadamu kimataifa, wazee nchini bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kuendelea kuwepo kwa unyanyasaji na mauaji ya wazee kwa imani za kishirikina na uwakilishi hafifu wa wazee katika vyombo mbalimbali vya kutoa maamuzi”, amesema mzee Msemembo.

Ameshauri serikali kutunga na kuboresha sera na sheria zitakazo wahakikishia usalama na maslai yao katika jamii.

“Tunapaza sauti setu kuiomba serikali kuharakisha upitishaji na utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kuzuia unyanyasaji na mauaji ya wazee kwa imani za kishirikina”, amesema mzee Msemembo na kuongeza kuwa, “kukamilisha kutungwa kwa sheria ya wazee ili kuyapa uzito masuala ya wazee na kuanzisha mabaraza ya wazee nchi nzima, ili kujenga mfumo imara wa uwakilishi”.

Kulingana na Shirika la HelpAge International Tanzania linaeleza kuwa asilimia 96 ya wazee hawana uhakika wa kipato na kuwaweka katika hatari ya kuishi katika umaskini na kushambuliwa na magonjwa ya mara kwa mara.

Zaidi, soma hapa => Wapigania kuundwa kwa baraza la wazee, kujenga mfumo imara wa uwakilishi | FikraPevu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom