Baraza la Mitihani latangaza Matokeo ya Kidato Cha Sita 2016

SniperBoi

JF-Expert Member
Feb 3, 2016
1,103
1,125
Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza matokeo ya kidato cha Sita mwaka huu wa 2016 na wanaume wameongoza kwa wingi katika kumi bora, katibu mtendaji wa NECTA bado anaendelea kuongea mnaweza ona matokeo kwa website yao na ya TAMISEMI,

Ufaulu umeshuka kwa asilimia 0.93 ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo ufaulu ulikuwa 98.87.

Shule 10 zilizofanya vizuri:
1.Kisimiri,-Arusha
2.Feza Boys,-Dar es Salaam
3.Alliance Girls,-Mwanza
4. Feza Girls,-Dar es Salaam
5. Marian Boys,-Pwani
6.Tabora Boys,-Tabora
7.Kibaha,-Pwani
8.Mzumbe-Morogoro
9.Ilboru,-Arusha
10. Tandahimba-Mtwara

Shule 10 zilizofanya vibaya:
1.Mpendae-Unguja
2.Ben Bella-Unguja
3.Tumekuja-Unguja
4.Green Bird Boys-Kilimanjaro
5.Jang'ombe-Unguja
6.Kiembe Samaki-Unguja
7.Tanzania Adventist-Arusha
8.Al- Ishan Girls-Unguja
9.Azania-Dar es Salaam
10.Lumumba-Unguja



KWA MATOKEO: BOFYA HAPA
 
Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza matokeo ya kidato cha Sita mwaka huu wa 2016 na wanaume wameongoza kwa wingi katika kumi bora, katibu mtendaji wa NECTA bado anaendelea kuongea mnaweza ona matokeo kwa website yao na ya TAMISEMI,

Ufaulu umeshuka kwa asilimia 0.93 ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo ufaulu ulikuwa 98.87.

Shule 10 zilizofanya vizuri: Kisimiri, Feza Boys, Alliance Girls, Feza Girls, Marian Boys, Tabora Boys, Kibaha, Mzumbe, Ilboru, na Tandahimba

KWA MATOKEO: BOFYA HAPA
 
Naona wakongwe wameanza kurudi katika chart Tabora boys Kibaha mzumbe Ilboru ndani ya kumi bora tulishawasahau shule ınayoongoza ya Kisimiri pia ni ya serikali. Tabora girls wapo namba 13, kilakala -20, msalato 21. Imekuaje shule za serikali zimeibuka ghafla baada ya kuingia Magufuli? Zilishapotezwa kabisa ladha yake
 
Habari Wana JF,

Haya watahiniwa mlitihaniwa 2016 jitazameni kama ni Elimu ya juu au diploma, matokeo yenu yapo hewani. Ila three nyingi hazitoenda chuo kikuu. Kwa maana mtu kapata DE, BE na kadhalika.
 
Back
Top Bottom