Baraza la Mitihani acheni kuua wawekezaji binafsi kwenye elimu kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani

comte

JF-Expert Member
Dec 11, 2011
8,171
5,905
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.
 
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.
Sasa hayo maelezo kamilli unataka hilo Baraza la Mitihani likuwekee humu jukwaani? Unatakiwa uende kwenye ofisi zao ili ukaelimishwe namna hao wadanganyifu wanavyo kamatwa kirahisi.

Ila kwa ufupi kabisa unatakiwa kutambua kwamba NECTA ni moja ya Taasisi za Serikali zinazojitahidi sana kusimama kwenye haki, ukilinganisha na taasisi nyingine.

Na unatakiwa ujiulize, kwa ulalamike wewe ambaye hukuwepo eneo la tukio! Badala ya hao waliofutiwa matokeo kwa udanganyifu? Na umeshajiuliza kwa nini wamefutiwa hao, badala ya shule zote? Tuungane kukataa udanganyifu, ili tuwe na Taifa la watu wanajiamini.


NB:- NECTA huwa inatoa adhabu kwa wale wote wanaoshiriki kwenye udanganyifu! Na siyo shule binafsi tu!

Kuna mwaka waliwahi kufuta matokeo ya shule za Msingi za Serikali Wilaya ya Bahi kule Dodoma, baada ya Afisa Elimu na Walimu Wakuu wake kujihusisha na udanganyifu kupitia group lao la whatasapp.
 
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.
Vipi ndg yako shule yake imefutiwa?

Shule binafsi ni waongo.
Kuna shule wanafunzi walipata maswli yote kasoro moja tu.
Na wote wakalikosa wanafunzi 120 inaingia akilini?
 
Sasa hayo maelezo kamilli unataka hilo Baraza la Mitihani likuwekee humu jukwaani? Unatakiwa uende kwenye ofisi zao ili ukaelimishwe namna hao wadanganyifu wanavyo kamatwa kirahisi.

Ila kwa ufupi kabisa unatakiwa kutambua kwamba NECTA ni moja ya Taasisi za Serikali zinazojitahidi sana kusimama kwenye haki, ukilinganisha na taasisi nyingine.

Na unatakiwa ujiulize, kwa ulalamike wewe ambaye hukuwepo eneo la tukio! Badala ya hao waliofutiwa matokeo kwa udanganyifu? Na umeshajiuliza kwa nini wamefutiwa hao, badala ya shule zote? Tuungane kukataa udanganyifu, ili tuwe na Taifa la watu wanajiamini.


NB:- NECTA huwa inatoa adhabu kwa wale wote wanaoshiriki kwenye udanganyifu! Na siyo shule binafsi tu!

Kuna mwaka waliwahi kufuta matokeo ya shule za Msingi za Serikali Wilaya ya Bahi kule Dodoma, baada ya Afisa Elimu na Walimu Wakuu wake kujihusisha na udanganyifu kupitia group lao la whatasapp.
Wanakatazwa kuweka? Unamukumu vipi mtu halafu unamnyima ushahidi uliomtia hatiani? Kama ni siri wanatutangazia sisi tusio husika ili iweje? Si wangepeana barua za maamuzi yao kimya kimya.
 
Ndugu muwekezaji, sio shule bimafsi tu zipo mpaka za serkali na mfano wake ni Olympio yenye watahiniwa zaidi ya 600...
Haijalishi, watoe ushahidi sambamba na hukumu yao. Mkuu kwenye vyuo ukikamatwa kwa udanyanyifu unasaini kwenye fomu kukubali uliyofanya na ushahidi inaambatanishwa. Unapokuja kuitwa kujieleza unajua kosa lako na adhabu. Hawa jamaa wanajifungia chumbani wanaamua wanavyotaka. WANASHANGAA watoto kujibu swali kwa namna inavofanana. Kwa nini hii kufanana kwa majibu iwe ni jambo la kushangaza wakati watoto hao wamefundishwa na mwalimu mmoja?
 
Haijalishi, watoe ushahidi sambamba na hukumu yao. Mkuu kwenye vyuo ukikamatwa kwa udanyanyifu unasaini kwenye fomu kukubali uliyofanya na ushahidi inaambatanishwa. Unapokuja kuitwa kujieleza unajua kosa lako na adhabu. Hawa jamaa wanajifungia chumbani wanaamua wanavyotaka. WANASHANGAA watoto kujibu swali kwa namna inavofanana. Kwa nini hii kufanana kwa majibu iwe ni jambo la kushangaza wakati watoto hao wamefundishwa na mwalimu mmoja?
Unq fahamu wana ongozwa na sheria ipi?

Una fahamu hizo ni mamlaka mbili tofauti chini ya sheria tofauti??

Vipi wale ma-CO walio futiwa mitihani na kufanya upya???

Una fahamu kwa mamlaka waliyo pewa chini ya sheria gani walifanya vile kuwa futia na kuanza upya???

Necta sio mara ya kwanza kufuta au kubadili mitihani, wahenga waliopo humu wana elewa miaka ya nyuma nini kilitokea kidato cha nne...!?

Ndg. Pambana shule yako ifate utaratibu... usitake kufaulisha wanafunzi kwa janja janja, hauto weza na mwisho wake sio mzuri
 
Unq fahamu wana ongozwa na sheria ipi?

Una fahamu hizo ni mamlaka mbili tofauti chini ya sheria tofauti??

Vipi wale ma-CO walio futiwa mitihani na kufanya upya???

Una fahamu kwa mamlaka waliyo pewa chini ya sheria gani walifanya vile kuwa futia na kuanza upya???

Necta sio mara ya kwanza kufuta au kubadili mitihani, wahenga waliopo humu wana elewa miaka ya nyuma nini kilitokea kidato cha nne...!?

Ndg. Pambana shule yako ifate utaratibu... usitake kufaulisha wanafunzi kwa janja janja, hauto weza na mwisho wake sio mzuri
Sheria inayokandamiza haki ya asili haiwezi kuwa sheria nzuri na wala hiyo sheria unayoisema haiweki utaratibu huo. Mimi kwa maoni yangu nasema wanachofanya baraza la mitihani siyo sawa kwa sababu hakuna uwazi. Hakana popote waliposema waliwakamata watu wakifanya udanganyifu badala yake wanatwambia kuna viashiria vya udanganyifu tena bila kuvitaja viashiria hivyo- hii ni dhuluma.
Mimi sina shule wala ndugu anayemiliki shule isipokuwa mashaka yangu ni kukosekana kwa uwazi kwa hatua zinazochukuliwa na baraza la mitihani.
 
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.

Wacha kelele kwenye mambo ya msingi! Baraza liweke hadharani nyaraka za serikali? Au wawaache wadanganyifu kwasababu ni wawekezaji? Hatutaki wawekezaji wezi! Kama huna akili unakuja kuwekeza wizi wa mitihani, hufai
 
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.

Mpaka wanafunga au kufuta wanaushahidi isio na shaka kuwa umewekwza kwenye wizi wa mitihani! Nenda mahakamani ukapinge!
 
NB:- NECTA huwa inatoa adhabu kwa wale wote wanaoshiriki kwenye udanganyifu! Na siyo shule binafsi tu!

Kuna mwaka waliwahi kufuta matokeo ya shule za Msingi za Serikali Wilaya ya Bahi kule Dodoma, baada ya Afisa Elimu na Walimu Wakuu wake kujihusisha na udanganyifu kupitia group lao la whatasapp.
Ilikuwa ni wilaya ya Chemba sio Bahi.
 
Sheria inayokandamiza haki ya asili haiwezi kuwa sheria nzuri na wala hiyo sheria unayoisema haiweki utaratibu huo. Mimi kwa maoni yangu nasema wanachofanya baraza la mitihani siyo sawa kwa sababu hakuna uwazi. Hakana popote waliposema waliwakamata watu wakifanya udanganyifu badala yake wanatwambia kuna viashiria vya udanganyifu tena bila kuvitaja viashiria hivyo- hii ni dhuluma.
Mimi sina shule wala ndugu anayemiliki shule isipokuwa mashaka yangu ni kukosekana kwa uwazi kwa hatua zinazochukuliwa na baraza la mitihani.
Nimekushauri kutembelea NECTa ili ukaelimishwe namna huo udanganyifu unavyofanyika, hutaki! Badala yake umechagua njia ya kulalamika! Huku ukiwa hujui chochote.
 
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.
Nimesoma uzi wako pamoja na comments zako.

Kuna mambo ambayo husemi kweli kwa makusudi au hujui au huna taarifa sahihi.

Taarifa ya shule kufutiwa matokeo kutokana na sababu za ku cheat huwa haiji ghafla bila wahusika kujua ikiwa ni pamoja na uongozi wa shule kupitia mwalimu mkuu ambaye ni sehemu ya wasimamizi.

Kunapokuwa na tukio la ku cheat au viashiria vyake kuna chain ndefu ya watu huwa wanahusika katika katika jambo hilo.

Ukiona shule imefutiwa matokeo jua kwamba kuna blunders kubwa sana zinakuwa zimeafanyika na mwalimu mkuu lazima anakuwa anajua matokeo ya mtihani wa kituo chake yatafutwa.

USIWADANGANYE WATU HAPA JUKWAANI KUWA TAARIFA YA NECTA KUFUTA MATOKEO YA MITIHANI HUWA INAKUJA KAMA SURPRISE, Kwa sababu kabla ya kufikia hatua hiyo kuna hatua zinachukuliwa ili kuokoa jahazi, ila kama issue ni kubwa basi wanafuta. NA USHAHIDI HUWA UPO.

Kama NECTA wakiwa hawana ushahidi wa kutosha lakini wanaona kuna viashiria hasa kabla na wakati wa marking huwa wanayakamata matokeo kwa muda ili wafanye uchunguzi, wakiona hakuna issue wanaachia matokeo ila wakithibitisha udanganyifu wanafuta.
 
Sasa hayo maelezo kamilli unataka hilo Baraza la Mitihani likuwekee humu jukwaani? Unatakiwa uende kwenye ofisi zao ili ukaelimishwe namna hao wadanganyifu wanavyo kamatwa kirahisi.

Ila kwa ufupi kabisa unatakiwa kutambua kwamba NECTA ni moja ya Taasisi za Serikali zinazojitahidi sana kusimama kwenye haki, ukilinganisha na taasisi nyingine.

Na unatakiwa ujiulize, kwa ulalamike wewe ambaye hukuwepo eneo la tukio! Badala ya hao waliofutiwa matokeo kwa udanganyifu? Na umeshajiuliza kwa nini wamefutiwa hao, badala ya shule zote? Tuungane kukataa udanganyifu, ili tuwe na Taifa la watu wanajiamini.


NB:- NECTA huwa inatoa adhabu kwa wale wote wanaoshiriki kwenye udanganyifu! Na siyo shule binafsi tu!

Kuna mwaka waliwahi kufuta matokeo ya shule za Msingi za Serikali Wilaya ya Bahi kule Dodoma, baada ya Afisa Elimu na Walimu Wakuu wake kujihusisha na udanganyifu kupitia group lao la whatasapp.
Umemuelimisha vema.
 
Baraza la mitihani limekubuhu kwa tabia ya kufuta na kufungia shule kwa kisingizio cha udanganyifu katika mitihani. Hii inafanyika kwa namna ya kuonyesha kuwa udanganyifu huo unafanyika kwenye shule binafsi tu. Bahati mbaya hakuna uwazi wa namna wanavyofikia maamuzi yao.

Kwa kawaida udangayifu unatakiwa uonekane wakati mitihani inapokuwa inafanyika. Kama ni hivyo kweli basi malalamiko yasingekuwepo mengi na wahusika wangekuwa wanajua kabisa kuwa kwa ushahidi waliokamatwa nao watakuwa wanakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo au kituo.

Kwa namna inavyotokea na kwa kuhusisha shule za watu binafsi, tunahitaji maelezo kamili kutoka kwa baraza la mitihani ili tuelewe kinachotokea. Vinginevyo itaonekana kuwa ni njama za baraza kuua uwekezaji kwenye elimu kutoka kwa sekta binafsi.
Hauna taarifa sahihi bahati mbaya. Ila NECTA mpaka kufutiwa matokeo kunahatua kadhaa huwa zinachukuliwa, ikiwemo kuhojiwa kwa wasimamizi wa mtihani husika, mkuu wa shule husika na wengine wote wanaotuhumiwa kuhusika na udanganyifu , wakijiridhisha matokeo yanafutwa kwahiyo inakuwa inajulikana hata kabla ya ku release matokeo ya jumla hasa kwa wahusika, ila wengine tunakuja kujua baadae baada ya matokeo ya jumla kutoka.
 
Hauna taarifa sahihi bahati mbaya. Ila NECTA mpaka kufutiwa matokeo kunahatua kadhaa huwa zinachukuliwa, ikiwemo kuhojiwa kwa wasimamizi wa mtihani husika, mkuu wa shule husika na wengine wote wanaotuhumiwa kuhusika na udanganyifu , wakijiridhisha matokeo yanafutwa kwahiyo inakuwa inajulikana hata kabla ya ku release matokeo ya jumla hasa kwa wahusika, ila wengine tunakuja kujua baadae baada ya matokeo ya jumla kutoka.
Hatujaambiwa hayo unayodhani unayajua wewe pekee yako. Kwa maelezo yako inaelekea msingi wa uchunguzi na namna wanafunzi walivyojibu maswali. hii inamaanisha kuwa hakuna ushahidi wa moja kwa moja kutoka kwenye eneo la tukio na wakati wa tukio yaani wasimamizi hawakuona udanganyifu wowote kwenye kituo wakati mitihani inafanyika. Hapa ndipo ninataka baraza la mitihani litusaidie.
 
Nimesoma uzi wako pamoja na comments zako.

Kuna mambo ambayo husemi kweli kwa makusudi au hujui au huna taarifa sahihi.

Taarifa ya shule kufutiwa matokeo kutokana na sababu za ku cheat huwa haiji ghafla bila wahusika kujua ikiwa ni pamoja na uongozi wa shule kupitia mwalimu mkuu ambaye ni sehemu ya wasimamizi.

Kunapokuwa na tukio la ku cheat au viashiria vyake kuna chain ndefu ya watu huwa wanahusika katika katika jambo hilo.

Ukiona shule imefutiwa matokeo jua kwamba kuna blunders kubwa sana zinakuwa zimeafanyika na mwalimu mkuu lazima anakuwa anajua matokeo ya mtihani wa kituo chake yatafutwa.

USIWADANGANYE WATU HAPA JUKWAANI KUWA TAARIFA YA NECTA KUFUTA MATOKEO YA MITIHANI HUWA INAKUJA KAMA SURPRISE, Kwa sababu kabla ya kufikia hatua hiyo kuna hatua zinachukuliwa ili kuokoa jahazi, ila kama issue ni kubwa basi wanafuta. NA USHAHIDI HUWA UPO.

Kama NECTA wakiwa hawana ushahidi wa kutosha lakini wanaona kuna viashiria hasa kabla na wakati wa marking huwa wanayakamata matokeo kwa muda ili wafanye uchunguzi, wakiona hakuna issue wanaachia matokeo ila wakithibitisha udanganyifu wanafuta.
Umeandika maelezo mengi ila hakuna jipya ndani yake. Naomba unisaidie maelezo kama:-
1. Kuna ushahidi wa moja kwa moja uliokamatwa kwenye kituo wakati mitihani ikifanyika?
2. Kuna maelezo ya wahusika kwa maana ya i) wanafunzi waliokamatwa wakidanganya ii) wasimamizi waliogundua na kukamata wanafunnzi wakifanya udanganyifu iii) ushahidi uliokamatwa
Hii habari ya kuwa kuna sijui viashiria au sijui darasa zima majibu yanafanana ni ujinga mtupu ambao unaweza kutumia ama unatumika kwa nia ovu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom