Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, inatarajia kuunda baraza la mawaziri lenye wizara 14 ambazo zitagawanywa baina ya CCM na CUF kwa uwiano wa asilimia ya idadi wa wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi.
Kwa mujibu wa taarifa tulizopata kutoka ndani ya serikali hiyo CCM itapewa wizara nane na CUF wizara sita.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa mchakato wa uundaji wa baraza hilo la mawaziri, umekamilika na kwamba rais Dk Ali Mohamed Shein, atalitangaza wakati wowote juma lijalo.
Muundo huo unatokana na Katiba ya Zanzibar inayotoa mwongozo kuwa serikali hiyo itaundwa kulingana na uwiano wa asilimia za uwakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi baina ya vyama hivyo viwili.
My take: Kipi kitakuwa chama kikuu cha upinzani au tunarudi miaka ileee yenye ukiritimba wa chama kimoja?
Kwa mujibu wa taarifa tulizopata kutoka ndani ya serikali hiyo CCM itapewa wizara nane na CUF wizara sita.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa mchakato wa uundaji wa baraza hilo la mawaziri, umekamilika na kwamba rais Dk Ali Mohamed Shein, atalitangaza wakati wowote juma lijalo.
Muundo huo unatokana na Katiba ya Zanzibar inayotoa mwongozo kuwa serikali hiyo itaundwa kulingana na uwiano wa asilimia za uwakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi baina ya vyama hivyo viwili.
My take: Kipi kitakuwa chama kikuu cha upinzani au tunarudi miaka ileee yenye ukiritimba wa chama kimoja?