Tango73
JF-Expert Member
- Dec 14, 2008
- 2,128
- 1,225
Ndugu watanzania!
Mumegundua kuwa baraza la mawaziri la tanzania halina uzalendo? Yaani hawajali kabisaa kuipeleka nchi na watu wake katika malisho mema. Hii ni hatari sana maana kila waziri kageuza wizara yake ni chimbo la nguvu la madini. Ukianzia wizara ya nishati na madini, huko kuna sikititisha kuona kuwa waziri na katibu wake hawajui hata kuokoa wananchi ili wapate umeme wa kutosha.
Kashfa ya kuwahonga wabunge ili wasiohoji bajeti ya wizara ya madini, ni kitendo kisicho cha kizarendo kabisaa. Ukija wizara ya utalii, ndiko utazania inamilikiwa na waarabu. Maana kitendo cha taifa la kiarabu kuingia hapa nchini na kubeba twiga 133 si cha kizalendo kabisaa. Ukija wizara ya mambo ya nje, utaona wanamkemea balozi wa Libya, eti kapandisha bendera ya NTC badala ile ya utawala wa Gadafi!
Jamani Gadafi huyu aliyeshirikiana na Iddi amini kuwauwa Watanznaia haswa ndugu zetu wa kihaya, leo waziri wa mambo ya nje , kakataa kabisaa kuitambua serikali ya wananchi wa libya waliompindua gadafi! tena kamkemea balozi wa Libya kwa kupandisha bendera ya NTC!
hiki si kitendo cha kizarendo kabisaa! Ukija wizara ya elimu, huko ndiko kunanuka uozo wa mawaziri wasiojali kabisaa kushuka kwa elimu ya vijana wetu. Division VI na O zikizidi 40% lazima waziri wa elimu awajibishwe, lakini hawa mawaziri ndio walaa, . hiki nacho si kitendo cha kizarendo! Jamani nisaidieni na vingine , haswaa huko Sheria walikowachiwa wauza unga kutoka pakistani! Wizara ya mabo ya ndani kuruhusu raia wengi wa kigeni kupata vibali vya kazi za wazawa!
Hii ni hatari kubwa sana , maana tunaonekana kama vile tupo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, wakati nchi ni ya amani na utulivu. Uganda na Kenya , ndio haooo, wanatuacha kwa kasi ya duma! Jamani ni lini nyie mawaziri mutachukua moyo wa sokoine? Jamani nayo hiyo inataka elimu ya juu kiasi gani?
Mumegundua kuwa baraza la mawaziri la tanzania halina uzalendo? Yaani hawajali kabisaa kuipeleka nchi na watu wake katika malisho mema. Hii ni hatari sana maana kila waziri kageuza wizara yake ni chimbo la nguvu la madini. Ukianzia wizara ya nishati na madini, huko kuna sikititisha kuona kuwa waziri na katibu wake hawajui hata kuokoa wananchi ili wapate umeme wa kutosha.
Kashfa ya kuwahonga wabunge ili wasiohoji bajeti ya wizara ya madini, ni kitendo kisicho cha kizarendo kabisaa. Ukija wizara ya utalii, ndiko utazania inamilikiwa na waarabu. Maana kitendo cha taifa la kiarabu kuingia hapa nchini na kubeba twiga 133 si cha kizalendo kabisaa. Ukija wizara ya mambo ya nje, utaona wanamkemea balozi wa Libya, eti kapandisha bendera ya NTC badala ile ya utawala wa Gadafi!
Jamani Gadafi huyu aliyeshirikiana na Iddi amini kuwauwa Watanznaia haswa ndugu zetu wa kihaya, leo waziri wa mambo ya nje , kakataa kabisaa kuitambua serikali ya wananchi wa libya waliompindua gadafi! tena kamkemea balozi wa Libya kwa kupandisha bendera ya NTC!
hiki si kitendo cha kizarendo kabisaa! Ukija wizara ya elimu, huko ndiko kunanuka uozo wa mawaziri wasiojali kabisaa kushuka kwa elimu ya vijana wetu. Division VI na O zikizidi 40% lazima waziri wa elimu awajibishwe, lakini hawa mawaziri ndio walaa, . hiki nacho si kitendo cha kizarendo! Jamani nisaidieni na vingine , haswaa huko Sheria walikowachiwa wauza unga kutoka pakistani! Wizara ya mabo ya ndani kuruhusu raia wengi wa kigeni kupata vibali vya kazi za wazawa!
Hii ni hatari kubwa sana , maana tunaonekana kama vile tupo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, wakati nchi ni ya amani na utulivu. Uganda na Kenya , ndio haooo, wanatuacha kwa kasi ya duma! Jamani ni lini nyie mawaziri mutachukua moyo wa sokoine? Jamani nayo hiyo inataka elimu ya juu kiasi gani?