Baraza la Mawaziri, sura mpya, uchakachuaji unaendelea

FarLeftist

JF-Expert Member
Oct 20, 2010
363
20
Wadau jana kwenye hotuba Bungeni nilimsikia akisema kwamba ataunda baraza bila kujali vyama, je kuna dalili yoyote akachagua mawaziri kutoka vyama vingine? hii itakuaje na msimamo wetu CHADEMA uko wazi tayari..
 
CCM wana Muafaka na CUF, mbona Zanzibar ni wamoja?, atatengeneza baraza na vyama vyake matawi ya CCM
 
CCM wana Muafaka na CUF, mbona Zanzibar ni wamoja?, atatengeneza baraza na vyama vyake matawi ya CCM

Akifanya hivyo atakuwa ameimarisha CHADEMA kwani vyama vilivyo serikali ni nadra kupinga maamuzi ya serikali hata kama hana maslahi kwa Taifa
 
Aunde tu, ila CHADEMA no.....tena itapendeza zaidi ili wananchi wote wajue kuwa nao it is CHADEMA Vs CCM & Co. kuliko kudhani uko na akina Mrema, Mbatia na wajinga wengine wakina Mohamed
 
Nafikiri anaweza kuunda serikali ya mseto kwa kuvishirikisha vyama vya CUF,NCCR-MAGEUZI,TLP na UDP.
 
JK hana tatizo kwa nia ya kuteua wenye sifa hizo alizotaja!!!!!!!! Tatizo ni uwezo wake wa kukatalia mawshiba ndiyo tatizo! Huoni tayari amemsogeza mama mkwe karibu kupewa wizara ya wanyamapori ili waarabu waendelee kufaidi mbuga zetu!!!!!!!!!! Je atawaacha ghasia na sophia simba??????????????????????????? This time vicky kamata is another test!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!, Ateue CDM thubutu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hiyo ndo tunayoitaka ili 2015 iwe CHADEMA VS CCM & Co, hatuhitaji vyama 18 vya siasa hapa ni vyama vingine ni uchuro mtupu kama vya akina DOVUTWA ni Njaaa tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.
 
Nakumbuka kusikia hiyo point kwenye hotuba yake ila sidhani kama ataweza kweli kuwajumuisha wapinzani, labda hakuwa anamaanisha kile alichosema
 
JK anakazi kubwa sana mbele yake kwa maana ya kulipa fadhila. Fadhila CCM ni mtaji wa kuendeleza utawala. Hivyo Ghasia na Sofia hawataachwa na wengine wapya na wa zamani watarudi. Uwezo wa kuwakatalia hana kilichobaki ni kuwapa fursa na kuondoa lawama.

Angekuwa mtu wa kujifunza angekuwa amejifunza ktk baraza lililopita ambapo aliweka asilimia zaidi ya 98 maswaiba wake. Sina uhakika kama JK amejifunza jinsi Baraza la mawaziri lililopita (kwa kiasi kikubwa) walivyomharibia kazi. Ilifika kipindi ikasemwa kuwa JK yuko vizuri lakini baraza lake halijatulia/halimsaidii kufanya kazi vizuri.
 
Wadau jana kwenye hotuba Bungeni nilimsikia akisema kwamba ataunda baraza bila kujali vyama, je kuna dalili yoyote akachagua mawaziri kutoka vyama vingine? hii itakuaje na msimamo wetu CHADEMA uko wazi tayari..

Hakusema hivyo ulim quote vibaya
 
Kuna taarifa kwamba JK amejifungia kuchakachua mapendekezo ya watu wa usalama na washauri wake (sio Sheikh Yahya na Maji Marefu).

Wizara zinazoumiza vichwa ni Mambo ya Nje, Mambo ya Ndani, Fedha na Uchumi, Maliasili na Utalii, Elimu, Afya na Ardhi.

Prof Anna Tibaijuka alitaka kumpa Mambo ya Nje,watu wakasema anafaa ardhi na makazi maana kuwa UN haina mana ni mwanadiplomasia. Hoja hiyo inatokana na Membe kuzidiwa na mizengwe ya kutaka kumtoa, kwa kigezo kile kile cha kumtoa Sitta kwamba eti makundi na wakose yote Membe na Lowassa!!!

Jina la January Makamba nalo liko juu, huku majina mapya ya vijana kibao yakijitokeza, baadhi wakiwa ni kutoka visiwani na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Bado tatizo la ukubwa wa baraza haliepukiki kwa sasa. Ila kwa kweli kundi la mafisadi lina nguvu kubwa kwa CCM na JK anapata shida sana kujitenga na nguvu hizo na sasa zinamtesa sana.

Wizara ya Miundombinu nayo inatakiwa na mafisadi kwa nguvu zote.

More to come from Msoga.
 
JK atafanya kosa kubwa sana kuwapa vijana wanaoingia Bungeni kwa mara ya kwanza uwaziri au Unaibu Waziri kama alivyofanya kwa Masha. Mimi binafsi ninaamini ni muhimu kuwaacha vijana hawa wajijenge kama wabunge kwanza kwa karibu miaka miwili hivi kitu ambacho Masha alinyimwa kwa kweli. Lakini hatari zaidi naamini kuwa madaraka makubwa kama uwaziri yanakuja na kile kinachoitwa "trappings of power".. na ina hatari sana ya kuwaharibu.. tumeona ya Ngeleja. Waacheni wajijenge kama viongozi wa kisiasa, waacheni waweze kuconnect na wananchi, kujifunza vurugu za Bungeni n.k

Ninaamini, kinyume na wengine wanavyoaamini binafsi ninaamini tatizo la serikali iliyopita halikuwa kwenye umri (wazee vs vijana). Ninaamini ni tatizo la uwezo. Hivyo, licha ya hilo nililolisema hapo juu ni muhimu kupima viongozi wanaokuja kwa kuangalia uwezo. Uwezo hauji kwa sababu ya elimu tu bali unakuja kutokana na uzoefu wa muda mrefu, uthabiti wa kushughulikia maatizo, ubunifu na maono yaliyo nje ya sanduku la yale yaliyozoelekea. Hivyo, hana budi kurudi nyuma na kuangalia uwezo kuliko majina na umri.

Sasa hivi hana udhuru tena "wa sikufahamu" na hatakuwa na udhuru wa kuwa "tunajaribu". Ni lazima apange kikosi kinachoenda kufanya kazi na siyo kitakachoonesha malipo ya kisiasa. Na hapa ninaamini ni bora arudishe baraza la wakongwe walioonesha uwezo kuliko kuingiza baraza la vijana ambalo halijawahi kujaribiwa hasa ukizingatia changamoto za taifa letu.

Pamoja na hilo, safari hii tunakokwenda Watanzania hawatawalalamikia tena "wasaidizi wake" kama walivyofanya miaka hii mitano; huko mbeleni wateule wake wakianza kuboronga guess nani atabebeshwa lawama squarely?
 
kuna kijana mmoja ana kashfa hadi za UN/WHO/UNAIDS lakini hukawii kusikia kapewa ulaji
 
mwanakijiji
tatizo halikuwa umri/experience ya masha na ngeleja bali ni intentions zao. walikuwa kwa ajili ya kujinufaisha na sio kuwatumikia wananchi
 
Back
Top Bottom