Baraza la Mawaziri nchini Burundi limesema kwamba linaongoza nchi hadi Rais mpya atakapoapishwa

RAKI BIG

JF-Expert Member
Apr 26, 2020
394
456
Uamuzi huo ulifikiwa kufuatia mkutano uliyofanywa siku ya Alhamisi chini ya uongozi wa Makamu wa Rais wa kwanza Gaston Sindimwo.

Kufikia sasa bado haijabainika ni lini kiongozi mpya ataapishwa, japo katiba iko wazi kuwa Spika wa bunge la kitaifa Pascal Nyabenda alitakiwa kuapishwa kushikilia wadhifa wa Rais kwa kipindi cha mpito hadi Rais Mteule atakapoapishwa rasmi kuchukua hatamu ya uongozi.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema Rais Mteule, JeneralI Évariste Ndayishimiye, pia ni mgonjwa Mke wake alipigwa picha akitia saini kitabu cha maombolezo japo Ndayishimiye hajaonekana hadharani.

Chama cha Mawakili nchini Burundi kimetoa wito wa kuapishwa mara moja kwa Rais mteule.

Tovuti ya Kibinafsi pamoja na vyombo vingine vya habari vimesema kuwa mawaziri waliifahamisha mahakama hiyo kuhusu nafasi iliyo wazi katika ofisi ya rais.

Mahakama ya Katiba sasa inasubiriwa kutoa uamuzi ni nani anastahili kuapishwa kuwa rais, ilisema taarifa iliyochapishwa na tovuti ya Iwacu.

Kwa mujibu wa katiba Spika wa Bunge, Pascal Nyabenda, anatakiwa kuapishwa kama kiongozi wa mpito. Hata hivyo, Evariste Ndayishimiye wa chama tawala cha CNDD-FDD aliyechaguliwa Mei 20 anatakiwa kuapishwa mwezi Agosti.

Rais wa zamani, Sylvestre Ntibantunganya, ametoa wito Ndayishimiye aapishwe mara moja kama rais wa Burundi.
Huku hayo yakijiri kundi la upinzani linataka uchaguzi ufanywe upya.

BBC Swahili
 
Baraza la Mawaziri nchini Burundi limesema kwamba linaongoza nchi hadi Rais mpya atakapoapishwa.

Uamuzi huo ulifikiwa kufuatia mkutano uliyofanywa siku ya Alhamisi chini ya uongozi wa Makamu wa Rais wa kwanza Gaston Sindimwo.

Kufikia sasa bado haijabainika ni lini kiongozi mpya ataapishwa, japo katiba iko wazi kuwa Spika wa bunge la kitaifa Pascal Nyabenda alitakiwa kuapishwa kushikilia wadhifa wa Rais kwa kipindi cha mpito hadi Rais Mteule atakapoapishwa rasmi kuchukua hatamu ya uongozi.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema Rais Mteule, JeneralI Évariste Ndayishimiye, pia ni mgonjwa.

Mke wake alipigwa picha akitia saini kitabu cha maombolezo japo Ndayishimiye hajaonekana hadharani.

Chama cha mawakili nchini Burundi kimetoa wito wa kuapishwa mara moja kwa rais mteule.

Tovuti ya kibinafsi pamoja na vyombo vingine vya habari vimesema kuwa mawaziri waliifahamisha mahakama hiyo kuhusu nafasi iliyo wazi katika ofisi ya rais.

Perezida Pierre Nkurunziza

Haki miliki ya pichaREUTERS

Mahakama ya Katiba sasa inasubiriwa kutoa uamuzi ni nani anastahili kuapishwa kuwa rais, ilisema taarifa iliyochapishwa na tovuti ya Iwacu.

Kwa mujibu wa katiba Spika wa Bunge, Pascal Nyabenda, anatakiwa kuapishwa kama kiongozi wa mpito.

Hata hivyo, Evariste Ndayishimiye wa chama tawala cha CNDD-FDD aliyechaguliwa Mei 20 anatakiwa kuapishwa mwezi Agosti.

Rais wa zamani, Sylvestre Ntibantunganya, ametoa wito Ndayishimiye aapishwe mara moja kama rais wa Burundi.

Huku hayo yakijiri kundi la upinzani linataka uchaguzi ufanywe upya.

Nkurunziza ni nani?
Pierre Nkurunziza amekuwa mwanasiasa wa Burundi na kuwa madarakani tangu mwaka 2005.

Bwana Nkurunziza, kijana wa aliyekuwa mbunge, alinusurika mauaji 1993 ya wanafunzi wa Kihutu katika chuo kiuu cha Burundi ambapo alikuwa mhadhiri na kujiunga na waasi wa FDD kundi ambalo baadae lilibadilika na kuwa chama tawala cha CNDD-FDD ambacho alikuja akawa kiongozi.

Alikuwa mwenyekiti wa chama tawala cha CNDD-FDD, hadi alipochaguliwa kama rais wa Burundi.

p08gk82g.jpg



Safari ya kisiasa ya Pierre Nkurunziza nchini Burundi
Baada ya makubaliano ya Amani ya Arusha kati ya serikali na waasi, Nkurunziza alitajwa kuwa waziri wa mambo ya ndani kabla ya bunge kumchagua kama rais Agosti 2005.

2015, Nkurunziza alichaguliwa katika uchaguzi uliokuwa na utata na chama chake kwa muhula wa tatu madarakani.

Wafuasi wake na wanaompinga Nkurunziza walikosa kukubaliana katika suala la ikiwa ilikuwa halali kwake kugombea tena na maandamano yakafuata.
 
Huu mvutano ni mkubwa ingawa hali bado si mbaya sana.

Ushauri alioutoa rais wa zamani si mbaya ingawa kuufuata ushauri huo kwa sasa ni mgogoro mkubwa.

Kiutaratibu, Spika anatakiwa kuchukua nafasi.
 
Huu mvutano ni mkubwa ingawa hali bado si mbaya sana.

Ushauri alioutoa rais wa zamani si mbaya ingawa kuufuata ushauri huo kwa sasa ni mgogoro mkubwa.

Kiutaratibu, Spika anatakiwa kuchukua nafasi.
Warundi wanaamini kuna mkono wa kagame kwenye kifo cha nkurunziza na kuumwa ndayishimiye,huyo spika awamuamini kabisa wanahisi yuko na kagame,akipewa urais ndio imetoka hiyo
 
Warundi wanaamini kuna mkono wa kagame kwenye kifo cha nkurunziza na kuumwa ndayishimiye,huyo spika awamuamini kabisa wanahisi yuko na kagame,akipewa urais ndio imetoka hiyo
Hata mm nilihisi kagame lazima ana mkono wake hapa. Rwanda na burundi ni kama vile undugu hivi napenda kufahamu historia ya kuanzishwa kwa taifa la burundi na rwanda. Ni nani aliyeemerge kutoka kwa mwenzake
 
Nilivyoishi Burundi na kuona hali ilivyo, sijui kama wataelewana, tuwaaombee haya jamaa
 
Hata mm nilihisi kagame lazima ana mkono wake hapa. Rwanda na burundi ni kama vile undugu hivi napenda kufahamu historia ya kuanzishwa kwa taifa la burundi na rwanda. Ni nani aliyeemerge kutoka kwa mwenzake

Mkuu, mimi ninavyo elewa nikiwa mdogo miaka hio.... kulikua na nchi ikiitwa RwandaUrundi, kama nchi moja, sasa hawa mabeberu wa kibeljiji ndio walikuja igawanya vipande viwili kwa sababu ya makabila hayo mawili...Hutu na Tustsi, hizi nchi mbili zina historia ndefu , wacha wanahistoria watujuze!!!
 
Back
Top Bottom