Baraza la Mawaziri: Nani atoke, Nani abaki, Nani aingie?

Kuna kila dalili kwamba mabadiliko makubwa ya baraza la mawaziri yapo njiani. Hii ni kwasababu sio tu kwamba upinzani na umma umekuwa ukilalamika kwa muda mrefu juu ya ubabaishaji wa mawaziri kadhaa kiutendaji, bali sasa kilio hiki kimeingia hadi ndani ya chama Tawala ambapo watendaji wake wakuu (kinana na nape) wametamka waziwazi juu ya umuhimu wa kufanyika kwa mabadiliko.

Iwapo Rais Kikwete atafanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri, hii baraza husika litakuwa ni kama la tano tangia aingie Ikulu. Kwa maana hii, na kwa kuzingatia kwamba mabadiliko haya yatakuwa ni ya mwisho kabla ya uchaguzi mkuu 2015, ni dhahiri kwamba selection ya mawaziri itafanywa kwa ustadi mkubwa ili kurudisha imani ya wananchi kwa serikali ya ccm, lakini hasa ili kutekeleza kauli za Kinana mikoani kwamba sasa ni wakati wa serikali ya ccm kurudi katika mstari na kuanza kutekeleza sera zake kwa vitendo.

Ingekuwa wewe ni Rais au mshauri wa Rais, je ungependekeza:

*Nani abaki, Nani atoke, na nani aingie?
*Je, kwa hoja zipi ambazo ni nje ya ushabiki wa kisiasa?
*Je, nje ya mabadiliko ya baraza la mawaziri, nini kingine inatakiwa kifanyike ili kuwezesha mawaziri watakaoteuliwa wawewe deliver katika kipindi kilichobakia kuelekea 2015? Je, sera na mikakati iliyopo ni mizuri, kinachokosekana ni usimamizi na utekelezaji? Je, kuna haja ya kubadili sera, mfumo na mikakati? Kama ipo haja, ni mfumo, sera na mikakati ipi ina mapungufu na ambayo haitasaidia sana mawaziri wapya kuboresha performance ya serikali katika kuhudumia wananchi?

Matarajio ya uzi huu ni mchango wa hoja zinazolenga kujenga, sio kubomoa kwa mujibu wa muktadha uliowasilishwa hapo juu, na mchango wa aina hiyo utathaminiwa sana. Isitoshe, hauwezi jua, pengine consistency ya hoja zenye kujenga zita influence mamlaka ya uteuzi baada ya sauti zetu wananchi kusikika ngazi husika. Mawaziri hawa wataenda kuendesha serikali kupitia kodi tunazolipa sasa na kwenda mbele, hivyo hata kama tumechoshwa na ubabaishaji wa viongozi, basi angalau tufanikishe kodi zetu zifanye kazi kwa ufanisi kwa kipindi kilichobakia, kabla ya kutumia haki zetu za kikatiba kwa ukamilifu kwa kuchagua viongozi wanao ona wanafaa, na kwa wale watakaoamua kwenda mbali zaidi, kuchagua chama cha siasa wanacho ona kinafaa, 2015.

Pengine kwa nia ya kuchokoza mada, nitaje watu watano ambao ningeshauri Rais Kikwete awape wizara zifuatazo:

1. John Magufuli - Waziri Mkuu. Kama alivyobainisha david kafulila bungeni, wa sasa hatoshi kwani ni mpole mno, hivyo mawaziri wanampuuza na kumdharau. Kafulila anasema kwamba anahitajika waziri mkuu mwenye uwezo na mwenye ushawishi au atakayeogopwa na mawaziri pamoja na watendaji serikalini. Kuogopwa sio sifa ya uongozi lakini kama itasaidia kunyoosha utendaji serikalini, kama anavyosema Kafulila, ni bora kuwa basi na waziri mkuu anayeogopwa iwapo hatopatikana waziri mkuu mwenye ushawishi na mwenye uwezo wa kutekeleza sera, maazimio ya bunge, ahadi za serikali bungeni, na kusimamia sheria. Magufuli anatosha kote - katika kusimamia sera, maamuzi ya bunge, sheria, lakini pia utendaji wake utawajaza woga viongozi legelege.

2.Mark Mwandosya - Nishati Na Madini kwa sababu ana uzoefu na hili akianzia kama kamishna wa nishati, katibu mkuu wizara ya nishati, mwanzilishi wa taasisi ya utafiti wa masuala ya nishati na mazingira inayotambulika kinataifa (CEEST), na ame publish tafiti nyingi sana zinazotumiwa ndani na nje ya nchi.

3. Samuel Sitta - Waziri wa Sheria na Katiba. Huyu ni mtaalamu wa sheria, amewahi kuwa waziri hapa awamu ya pili, na ameonyesha uwezo na nia ya kusimamia haki na sheria kupitia uspika na katika jamii kwa ujumla. Mtu wa aina hii atatusaidia kutupatia katiba bora na sio bora katiba.

4. Edward Lowassa - hapa, Rais aiondoe TAMISEMI kutoka ofisi ya waziri mkuu na badala yake ijitegemee kama wizara. Lowassa anaweza rekebisha mapungufu yaliyopo katika wizara hii nyeti inayogusa wananchi wengi kuliko wizara yoyote. Alionyesha uwezo mkubwa akiwa ardhi, na baadae maji, na kujizolea sifa nyingi za uchapa kazi pamoja na mrema awamu ya pili.

5. Anna Tibaijuka - Wizara ya fedha. Huyu ni professor wa uchumi mwenye uzoefu na uwezo unaotambulika, hivyo sina haja ya kumjadili kwa kirefu.

6. Professor Hassa Mlawa - mkuu wa kitengo cha IDS UDSM, amteue ubunge na kumpa wizara ya sayansi, mawasiliano na tekinolojia. Mlawa ni msomi na mtaalamu katika masuala ya innovation, science and technology, hasa roles za haya katika industrialization, na anaheshimika kimataifa katika utafiti wa maeneo haya. Moja ya vikwazo vikubwa vya kuendelea kiuchumi nchini ni nchi yetu kukosa msingi ya kutuwezesha kuwa na uwezo wa ushindani katika uchumi wa sasa wa dunia ambao upo more knowledge driven.

Hawa ni wachache ambao naamini watabadili sana sura ya serikali, hasa katika maeneo hayo. Nje ya kuteua watu wenye uwezo na sifa za kutosha, kuna haja ya kuangalia tena sera, mfumo na mikakati iliyopo ili kuongeza ufanisi katika utendaji serikalini. Tutayaangalia haya baadae.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

kaka.wanatangaza saaa ngapi baraza
 
Mh. Ndungulile, unaweza kufafanua kidogo juu ya suala hili muhimu la 'mfumo", hasa kuliweka vyema katika muktadha wake? Mfumo wa chama tawala au mfumo wa utawala wa nchi?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mchambuzi swali lako hili kwa DK,, binafsi naungana nae kwa kilio cha mfumo [tumezoe SYSTEM].Nitajibu kwa upande wangu mimi kama ifuatavyo.
1: Je unaamini katika MFUMO kama ndio engine halisi ya kujenga ama kubomoa Nchi?
2: Nchi yetu Watanzania Tunaiendesha katika aina ipi ya MFUMO.Je ni mfumo wa KITAIFA kwanza ndio unaoendesha Taifa au MFUMO wa CHAMA tawala Kwanza ndio unaoendesha Nchi.Kati ya aina hizo mbili mfumo upi ndio mfumo mama wa jamii yetu watanzania.

Naamini kwa uwezo wako siitaji kufafanua mfumo ni nini kwako?

Madhara ya mfumo wa uendeshaji Taifa ulipoguswa na kada ya wafanyabishara ndipo itilafu ilipoingia ndani ya engine.
Mfano unazungumzia uteuzi.Ni kweli ni jambo jema tu,lakini wateule ni aina gani ya watu kwenye society yetu.Historia ya wateule wetu ni POSITIVE au NEGATIVE kwenye jamii anayotoka mteule, manake Charity Begins At Home.Je viongozi wetu ni aina hiyo ya watu?

3: Je vetting zinafanyika na kufuata historia za kizazi cha mteule kwa maana uongozi na maadili uanzia nyumbani.

4: Je mwenendo mzima wa wajibu na kanuni za utendaji wa mteule zinapimwa kwa vigezo kubalika na hasa jamii, inapotokea mteule kushindwa matarajio ya WANANCHI ambao ndio waajili wakuu. mteule je awajibike kwa kwa nani
(a) Awajibike kwa WANANCHI waliowaajili wakuu kikatiba wasio na uwezo wa kumtoa au kumwajili kiutendaji wa mfumo?
(b) Ama awajibike kwa Mteuzi aliyemteua ambae kapewa dhamana na Wananchi kupitia sanduku la kura au ajira ya Serikali?

Mfano tumeshuhudia mawaziri wanne[4] wakitimuliwa.Lakini ndani ya hao mawaziri wanne,ni mmoja tu Kagasheki aliyeonyesha kutambua MWAJILI wake mkuu ni nani!!Na akamuomba Mwajili mwenye dhamana ya KIKATIBA yani mteuzi wake kuachia ngazi kwa kuwa WANANCHI wameongea.Je ndio mfumo wetu unaanda Viongozi walioko madarakani au watalajiwa kuwa na mindset za Kagasheki au Rais Mstaafu Ally H Mwinyi?
5: Mfumo wetu huko tayari kupokea na kufanya kazi na watu wasio na ITIKADI ZA VYAMA VYA SIASA.Je engine watendaji wetu wakuu ambao kwa ujumla wao tunaita mfumo wanaitikadi ipi ndani ya mioyo yao, yani wana mlengo upi kimawazo, kimtizamo, kifikra, kimausiano, kiuwajibikaji, kiutekelezaji.nk,?
(a) Je Ni Taifa Kwanza ?
(b) Ama ni Chama Cha Kisiasa Kwanza na Taifa Baadae linakuja baada ya msambaratiko?

Ebu nakuja Mkuu
 
Katika yote unasoma upepo wa LOWASSA tu wewe, yaaani na akili zetu watu sie LOWASSA arejee? mnadhani watanzania wanasahau haraka kiasi hicho au?
 
Kuna kijana amemaliza UDOM anaitwa Saul Mwaisenye nasikia anatajwa tajwa kushika nafasi ya Amosi Makalla hadi hivi sasa inasemekana ameisha itwa Dsm kwenda kumalizia Logistics za mwisho za ubunge wa kuteuliwa. All the best kijana wa kitanzania
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Kuna kila dalili kwamba mabadiliko makubwa ya baraza la mawaziri yapo njiani. Hii ni kwasababu sio tu kwamba upinzani na umma umekuwa ukilalamika kwa muda mrefu juu ya ubabaishaji wa mawaziri kadhaa kiutendaji, bali sasa kilio hiki kimeingia hadi ndani ya chama Tawala ambapo watendaji wake wakuu (kinana na nape) wametamka waziwazi juu ya umuhimu wa kufanyika kwa mabadiliko.

Iwapo Rais Kikwete atafanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri, hii baraza husika litakuwa ni kama la tano tangia aingie Ikulu. Kwa maana hii, na kwa kuzingatia kwamba mabadiliko haya yatakuwa ni ya mwisho kabla ya uchaguzi mkuu 2015, ni dhahiri kwamba selection ya mawaziri itafanywa kwa ustadi mkubwa ili kurudisha imani ya wananchi kwa serikali ya ccm, lakini hasa ili kutekeleza kauli za Kinana mikoani kwamba sasa ni wakati wa serikali ya ccm kurudi katika mstari na kuanza kutekeleza sera zake kwa vitendo.

Ingekuwa wewe ni Rais au mshauri wa Rais, je ungependekeza:

*Nani abaki, Nani atoke, na nani aingie?
*Je, kwa hoja zipi ambazo ni nje ya ushabiki wa kisiasa?
*Je, nje ya mabadiliko ya baraza la mawaziri, nini kingine inatakiwa kifanyike ili kuwezesha mawaziri watakaoteuliwa wawewe deliver katika kipindi kilichobakia kuelekea 2015? Je, sera na mikakati iliyopo ni mizuri, kinachokosekana ni usimamizi na utekelezaji? Je, kuna haja ya kubadili sera, mfumo na mikakati? Kama ipo haja, ni mfumo, sera na mikakati ipi ina mapungufu na ambayo haitasaidia sana mawaziri wapya kuboresha performance ya serikali katika kuhudumia wananchi?

Matarajio ya uzi huu ni mchango wa hoja zinazolenga kujenga, sio kubomoa kwa mujibu wa muktadha uliowasilishwa hapo juu, na mchango wa aina hiyo utathaminiwa sana. Isitoshe, hauwezi jua, pengine consistency ya hoja zenye kujenga zita influence mamlaka ya uteuzi baada ya sauti zetu wananchi kusikika ngazi husika. Mawaziri hawa wataenda kuendesha serikali kupitia kodi tunazolipa sasa na kwenda mbele, hivyo hata kama tumechoshwa na ubabaishaji wa viongozi, basi angalau tufanikishe kodi zetu zifanye kazi kwa ufanisi kwa kipindi kilichobakia, kabla ya kutumia haki zetu za kikatiba kwa ukamilifu kwa kuchagua viongozi wanao ona wanafaa, na kwa wale watakaoamua kwenda mbali zaidi, kuchagua chama cha siasa wanacho ona kinafaa, 2015.

Pengine kwa nia ya kuchokoza mada, nitaje watu watano ambao ningeshauri Rais Kikwete awape wizara zifuatazo:

1. John Magufuli - Waziri Mkuu. Kama alivyobainisha david kafulila bungeni, wa sasa hatoshi kwani ni mpole mno, hivyo mawaziri wanampuuza na kumdharau. Kafulila anasema kwamba anahitajika waziri mkuu mwenye uwezo na mwenye ushawishi au atakayeogopwa na mawaziri pamoja na watendaji serikalini. Kuogopwa sio sifa ya uongozi lakini kama itasaidia kunyoosha utendaji serikalini, kama anavyosema Kafulila, ni bora kuwa basi na waziri mkuu anayeogopwa iwapo hatopatikana waziri mkuu mwenye ushawishi na mwenye uwezo wa kutekeleza sera, maazimio ya bunge, ahadi za serikali bungeni, na kusimamia sheria. Magufuli anatosha kote - katika kusimamia sera, maamuzi ya bunge, sheria, lakini pia utendaji wake utawajaza woga viongozi legelege.

2.Mark Mwandosya - Nishati Na Madini kwa sababu ana uzoefu na hili akianzia kama kamishna wa nishati, katibu mkuu wizara ya nishati, mwanzilishi wa taasisi ya utafiti wa masuala ya nishati na mazingira inayotambulika kinataifa (CEEST), na ame publish tafiti nyingi sana zinazotumiwa ndani na nje ya nchi.

3. Samuel Sitta - Waziri wa Sheria na Katiba. Huyu ni mtaalamu wa sheria, amewahi kuwa waziri hapa awamu ya pili, na ameonyesha uwezo na nia ya kusimamia haki na sheria kupitia uspika na katika jamii kwa ujumla. Mtu wa aina hii atatusaidia kutupatia katiba bora na sio bora katiba.

4. Edward Lowassa - hapa, Rais aiondoe TAMISEMI kutoka ofisi ya waziri mkuu na badala yake ijitegemee kama wizara. Lowassa anaweza rekebisha mapungufu yaliyopo katika wizara hii nyeti inayogusa wananchi wengi kuliko wizara yoyote. Alionyesha uwezo mkubwa akiwa ardhi, na baadae maji, na kujizolea sifa nyingi za uchapa kazi pamoja na mrema awamu ya pili.

5. Anna Tibaijuka - Wizara ya fedha. Huyu ni professor wa uchumi mwenye uzoefu na uwezo unaotambulika, hivyo sina haja ya kumjadili kwa kirefu.

6. Professor Hassa Mlawa - mkuu wa kitengo cha IDS UDSM, amteue ubunge na kumpa wizara ya sayansi, mawasiliano na tekinolojia. Mlawa ni msomi na mtaalamu katika masuala ya innovation, science and technology, hasa roles za haya katika industrialization, na anaheshimika kimataifa katika utafiti wa maeneo haya. Moja ya vikwazo vikubwa vya kuendelea kiuchumi nchini ni nchi yetu kukosa msingi ya kutuwezesha kuwa na uwezo wa ushindani katika uchumi wa sasa wa dunia ambao upo more knowledge driven.

Hawa ni wachache ambao naamini watabadili sana sura ya serikali, hasa katika maeneo hayo. Nje ya kuteua watu wenye uwezo na sifa za kutosha, kuna haja ya kuangalia tena sera, mfumo na mikakati iliyopo ili kuongeza ufanisi katika utendaji serikalini. Tutayaangalia haya baadae.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mimi kwa upande wangu namuona BALOZI KHAMISI KAGASHEKI anafaa kuwa WAZIRI MKUU!
Nimependezwa na utendaji kasi wake, ni mchapakazi mwenye kujiamini.
 
Natokea mkoa wa Kagera na kwa sababu hiyo Prof Tibaijuka ni home girl wangu kwa ufupi dada yangu. Na kiukweli nilikuwa na imani naye kweli kabla hajateuliwa katika nafasi aliyonayo. Lakini ni dhahiri dada yangu huyu ameniangusha kweli. Hizi hapa ni sababu zangu:-

- Kupanda kwa gharama za kulipia viwanja

- Migogoro ya ardhi imeongezeka hadi kusababisha mauaji (Kilombero Kiteto na Mwanza)

- Mipanagilio ya miji yetu inaendelea kuwa hovyo na haonyeshi hata matumaini ya kuwa na majibu

- Uchafu wa miji yetu, hili linamgusa maana wizara yake inahusika na makazi

Dada yangu huyu ni member wa Jf labda anaweza kuja kujitetea, lakini najiuliza kama David Mathayo alitimuliwa kwa sababu ng'ombe wanazurura, kwanini Prof Tibaijuka aendelee kuwa waziri wakati wananchi wanakufa kwa magonvi ya ardhi? Na mbaya zaidi hawezi hata kwenda eneo la tukio?
 
Nimekutana na kitu cha aina hii Mchambuzi nisaidie kujua kupitia taarifa hii hapa mfumo wa Watendaji na Viongozi wetu ni upi kupitia MINDSET ZAO. Je NI TAIFA KWANZA vyama baadae au ni VYAMA KWANZA TAIFA NNTONDO AU IGOLO.!!!Samaahani kwa kutumia msamiati nimeutumia kuweka msisitizo.

Haya chini kwangu binafsi ndio majanga!!Kinaconiuma hatuna organ ya kumonitor viongoz na watendaji wetu mind set zao na matendo yao ni yepi na kuwalekebisha tena ikibid kwa kutmia ukali pale inapobidi tukizingatia MASLAHI YA TAIFA NA WANANCHI WAKE KWANZA NA SIO MASLAHI YA VYAMA NA BINAFSI.

MKURUGENZI wa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Moshi,MUWSA
mhandisi Cyprian Luhemeja amejikuta akiingizwa katika masuala ya
kisiasa bila ya kujua baada ya viongozi wa chama cha Mapinduzi (CCM)
kudaiwa kuugeuza uzinduzi wa mradi wa maji wa Kiboriloni kama kete ya
kisiasa kuelekea uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata hiyo.

Kata ya Kiboriloni iliachwa wazi mwishoni mwa mwaka jana baada ya
Diwani wake, Vincent Rimoy (Chadema) ambaye pia alikuwa Naibu Meya wa
Manispaa ya Moshi kufariki dunia.Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
ilitangaza chaguzi ndogo zitafanyika mwezi Februari mwaka huu.

Kutokana na hali hiyo viongozi wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro
walishtukia mchezo huo na kulazimika kwenda eneo la Mnazi mmoja ambako
kulifanyika uzinduzi licha ya kwamba hawakuwa miongoni mwa waalikwa.

Viongozi walifika katika eneo hilo ni pamoja na mbunge wa jimbo la
Moshi mjini ,Philmon Ndesamburo,wabunge wa viti maalumu Chadema,Lucy
Owenya na Suzan Lymo pamoja na madiwani wa kata za manispaa
wakiongozwa na mstahiki meya wa manispaa ya Moshi Jafary Michael.

Mipango ya CCM ilionekana kugonga mwamba baada ya kuwepo kwa muitikio
hafifu wa wakazi wa eneo la Kiboriloni ambalo linatajwa ni kuwa ni
ngome ya Chama cha demokrasia kwa kipindi kirefu huku watendaji kwa
kushirikiana na baadhi ya viongozi wa CCM wakijaribu kuokoa jahazi kwa
kubadili ratiba ya shughuli hiyo.

Awali ratiba ilikuwa inaonesha baada ya msafara wa Waziri Maghembe
kufika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Ofisi za mamlaka ya maji
safi na maji taka mjini Moshi na kupita katika mitaa mitatu ya kata
hiyo inaonesha mwenyekiti wa mtaa wa Mnazi Frank Kagoma ndiye alikuwa
afanye ukaribisho pamoja na utambulisho.

Hata hivyo hali hiyo ilibadilirishwa ghafla kufuatia maelekezo
yanayodaiwa kutoka kwa viongozi wa CCM kumuondoa katika ratiba
mwenyekiti huyo ambaye anatajwa kugombea nafasi ya udiwani katika kata
hiyo licha ya kwamba alikuwa eneo la tukio hakupata hata nafasi ya
kutambulishwa.

Akizungumza baada ya kupatiwa nafasi mbunge wa Moshi mjini Ndesamburo
alianza kwa kurusha vijembe huku akimsihi Waziri Maghembe kuwaonya
watendaji wasisababishe wanasiasa kugombana kwa sababu ya shughuli za
maendeleo.

"Ndesamburo kama mbunge wa Moshi Mjini na mkazi wa eneo hili la
Kiboriloni nimekuja hapa lakini sikualikwa, mradi huu unazinduliwa kwa
sababu tuna uchaguzi mdogo wa udiwani kwenye kata hii mwezi
ujao…Mheshimiwa Waziri (Maghembe) watendaji wasitugombanishe wanasiasa
kwa ajili ya shughuli za maendeleo,Nitaomba uchukue hatua na
nitakukumbusha hata tukiwa kwenye vikao vyetu kule Dodoma,"alisema
Ndesamburo.

Baada ya Ndesamburo kumaliza kuzungumza,Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya
Moshi Mjini,Elizabeth Minde, alisimama na yeye katika jukwaa hilo
akiwaambia wakazi wa Kiboriloni kwamba kinachofanyika Kiboriloni ni
utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwa kiliahidi maji
safi na salama wananchi wake.

"Kwanza hiki alichokisema mbunge wetu (Ndesamburo) wala hatujui huo
uchaguzi utafanyika lini maana hata tarehe
haijatangazwa.Kinachofanyika ni utekelezaji wa ilani ya CCM kwa sababu
tulipeleka kwa wananchi mwaka 2010 na wao Chadema walipeleka ya kwao
sisi tukashinda kuunda serikali kwa hiyo ndo mana tunatekeleza
tulichoahidi,"alisema Minde.

Akizungumza na Tz daima kuhusu hatua yake ya kugomea kwenda kuotesha
mti katika eneo hilo la mradi Meya wa Manispaa ya Moshi,Japhari
Michael,alisema kilichotokea ni kitu kibaya katika siasa kwa sababu
miradi ya maendeleo inataka kuwagawa wananchi badala ya kuwapa faraja
ya kufikia malengo yao katika mipango ya kichumi na hasa huduma za
jamii.

"Nilichokuwa namwambia mkurugenzi wa maji, nchi hii inaongozwa kwa
mujibu wa katiba,na wananchi ndio wanatakiwa wasimamie miradi
hii,walinde mabomba ,mali na vitu vingine na hao hao ndio wanatakiwa
wachangia huduma hii ya maji,ukiingiza siasa kwenye vitu kama hivi
mana yake unaanza kugawanya wananchi"alisema Michael.

Alisema mkurugenzi huyo asipokuwa makini atashindwa kuendesha miradi
ya maji katika manispaa kutokana na ukweli kwamba jukumu la kulinda
miundo mbinu ya maji liko kwa wananchi na wao wamekuwa wakiwatumia
madiwani kusimamia suala la ulinzi ya miuondo mbinu hiyo.

"Sisi hatujazoea haya mambo ya kugawanya watu katika maswala ya
maji,leo mradi wa maji mmeingiza watu wa CCM ,kama CCM wanataka kura
za udiwani wafanye kwa utaratibu wao sio kwa kutumia mamlaka ya
maji,"alisema Michael.

"Halmashauri manispaa ya Moshi tuna miradi ya maji ya kuchimba visima
ya kusapoti maji ya Moshi, kwa hiyo na sisi tuzuie hii miradi ya maji
isije kwa MUWSA maana tumekuwa tunashirikiana na mamlaka kwa sababu ya
Maji….yeye anawaatamia CCM waonekane kwamba ndio wanafanya hii
kazi,wasubiri wakati wa Uchaguzi."aliongeza Michael.

Hata hivyo,Waziri Maghembe alisema hakuna ubishi kwamba mradi huo
unatokana na utelelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi na kwamba
kikubwa wananchi wamepata huduma ya maji safi na salama na kwamba
suala la uchaguzi mdogo ni suala jingine.

Mradi huo wa maji Kiboriloni ulipangwa kutekelezwa kwa awamu
tatu,ambapo awamu ya kwanza ilihusisha ujenzi wa bomba kubwa umbali wa
kilomita moja kutoka mto Rau hadi KDC wakati awamu ya pili ilihusisha
ujenzi wa umbali wa kilimota 1.2 kutoka KDC hadi Kiboriloni mnazi na
awamu ya tatu ni uchimbaji wa kisima kikubwa eneo la KDC.

Mwisho.
 
Cabinet ijayo ni timu ushindi. Pindi Chana hawezi kabisa kuletwa, anajifanya tuu strictly mguu upande haweki!. Alipaswa awe waziri zamani tatizo sio mnyenyekevu!.
Pasco
Hapa I was dam wrong!, kumbe kupata uwaziri siku hizi, mtu sio lazima mpaka ukae mguu upande!. Uteuzi wa Mhe. Pindi Chana ni uthibitisho wa hili.
Hongera zake!.
Pasco.
 
Mkuu Salary Slip, angalau ulituandaa tusijeshangaa!, huvyo hatushangai!.
Pasco.

Mkuu Pasco ,hapa ninachokiona kwa siku za usoni ni kuwa endapo baraza hili litavurunda,basi wabunge na wananchi kwa ujumla wata-demand raisi mwenyewe ajiuzulu.

Kwa maneno mengine,Kikwete kawabeba hawa mawaziri akiwemo waziri mkuu kwa gharama za uraisi wake kwa siku zijazo.

Mkuu,usitarajie tena watu watalia na Pinda au mawaziri bali Kikwete himself will be the next target for resignation.

Tusubiri,time will tell.
 
Last edited by a moderator:
summon
Atakayeingizwa ni Deo Filikunjombe ili kumcontain, Dr. Mwaki pia atahamishwa to save his face na madudu ya Bandari na ATCL
Pasco
ni Deo Filikunjombe ili kumcontain....
at last...contained!....
RIP Deo Filikunjombe!.
Pasco
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom