Uchaguzi 2020 Baraza la Mawaziri lijalo Rais aingize Wazungu, Wachina na Wahindi na wakumbukwe teuzi za Serikalini na Taasisi za Umma

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,911
51,889
Wakati wa Nyerere tulikuwa na mawaziri Wazungu na Wahindi. Naona ni wakati muafaka kuwaingiza wale ambao wamejitambulisha na kushikamana na jamii ya Watanzania kama sehemu ya Watanzania. Rais asisite kuwapa ubunge wa kuteuliwa wale anaoona wanafaa a kuwapa hata uwaziri ili tushirikiane nao kujenga nchi ni sehemu ya jamii yetu hao pia

Tanzania tunao watanzania Wazungu, Wahindi na Wachina kibao wanaotoa mchango mkubwa sana kwa taifa mfano yuko huyu Mholanzi Mtanzania Mheshimiwa Jonas Van Zeeland huyu alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mvomero na amekuwa diwani wa kata ya Diongoya amewatumikia wananchi wa wilaya ya Mvomero kwa awamu mbili mfululizo, tangu mwaka 2010 hadi 2020.

Raisi asisite pia kuwapa nafasi mbalimbali za uteuzi kwenye capacity anazoona wanafaa kuwepo kwa uwezo walionao katika serikali na taasisi za umma.
 
Rais Magufuli bora aingize machifu kwenye baraza la mawaziri kuliko hao Mabeberu.

Tumeikata Chadema Kwasababu Inatumika na Mabeberu mnataka kuleta Mabeberu kupitia mlango wa nyuma?

Nyie Chadema mwogopeni Mungu.
 
Rais Magufuli bora aingize machifu kwenye baraza la mawaziri kuliko hao Mabeberu.

Tumeikata Chadema Kwasababu Inatumika na Mabeberu mnataka kuleta Mabeberu kupitia mlango wa nyuma?

Nyie Chadema mwogopeni Mungu.
Una ushahidi kuwa wanatumika na hao unaodai? Kama unao.. uweke na evidence hapa.
 
Rais Magufuli bora aingize machifu kwenye baraza la mawaziri kuliko hao Mabeberu.

Tumeikata Chadema Kwasababu Inatumika na Mabeberu mnataka kuleta Mabeberu kupitia mlango wa nyuma?

Nyie Chadema mwogopeni Mungu.

Ni kwamba Mataga hamjuani, au ww ni kichwa nazi?
 
Mpaka wao wenyewe waombe mkuu kuwa bila idhini yao mwishowe watafanya Madudu na watasema nyinyi wenyewe mlitupa hatukuwaomba.
 
Una ushahidi kuwa wanatumika na hao unaodai? Kama unao.. uweke na evidence hapa.
Mgombea urais wa Chadema alisema mabeberu wanatulisha. Na alisema mabeberu wako nyuma yake na alisema mbele ya wanahabari pale ufipa street kinondoni.
Wapo alisema and how? Clarify na uweke ushahidi hapa with evidence.
Kwani wewe hukumsikia wakati anaongea na waandishi wa habari?
 
Mgombea urais wa Chadema alisema mabeberu wanatulisha. Na alisema mabeberu wako nyuma yake na alisema mbele ya wanahabari pale ufipa street kinondoni.
Kwani wewe hukumsikia wakati anaongea na waandishi wa habari?
Nadhani una miss my point. I want evidence.. sio maswali. Una evidence kuwa alisema hivyo. Weka hapa
 
Ukiangalie serikali ya Nyerere waliteuliwa watu kutoka makundi yote nafasi za uteuzi yaanayochangia sana kwenye nchi kijamii na kiuchumi yalipewa nafasi kwenye baraza la mawaziri.Baraza lisijae tu ma ex government officers
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom