pale ameenda kuhutubia baraza la iddi lakini pia kwa kutumia hadhira ile ilitaka taifa lipate ujumbe kwani mambo aliyoyazungumza pale ndio misingi ya amani tuliyonayo! Jaribu kusifia mtu akifanya vizuri hata kama humpendibinafsi nimeiona hotuba kuwa ya kawaida sana, labda inatokana na hotuba hiyo kutokidhi matarajio yangu kwani pamoja na kwamba jukwaa lilikuwa ni la kidini zaidi lakini mimi nili husisha na ule utaratibu wa rais kuhutubia taifa mwisho wa mwezi japo hatujamskia kwa miezi kadhaa. Despite of mambo mengi yaliyotokea katikati na ambayo bila shaka watz wenzangu wangependa kuskia rais wao anasemaje leo nilitega sikio kuona kama rais angeua ndege wawil kwa jiwe moja yaani kujibu risala ya walio mualika lakini pia kikidhi haja ya wale pia wasioweza kuandaa jukwaa na kumualika rais na hivyo kupaza sauti zao kupitia risala. Hapa raisi anapaswa kujua matatizo yanayoikabili sehemu kubwa ya raia wake kwa kipindi chote ambacho hajaweza kuwahutubia, japo hotuba yake isingekuwa dawa lakini yaweza kurudisha matumaini yaliyopotea. Labda basi kuna hotuba ya kitaifa itafuata baada ya hii, kama hakuna basi sikufurahishwa sana na hotuba ya leo