Baraza jipya la Mawaziri kujulikana Feb 12

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
Taarifa kutoka Dodoma zinasema Baraza jipya la mawaziri litatangazwa muda wowote KESHO na si leo kama ilivyotarajiwa.

Ni hayo tu... Just for your information.

Invisible
 
Mkuu Invi..... Asante kwa taarifa manake tunalingojea kwa uchu mkubwa sana.... Lets wait and see!!
 
Mkuu Invi..... Asante kwa taarifa manake tunalingojea kwa uchu mkubwa sana.... Lets wait and see!!

Inaelekea kazi ya panga pangua imekuwa ngumu kutokana na kuwa rais anatakiwa kuhakikisha hawapi nafasi tena wanao-hisiwa (ama kutambulika kwake) kuhusika na ufisadi wa aina yoyote. Kumbuka ripoti ya BoT anayo na anawajua wahusika kadhaa wanaoguswa nayo.

Ni mawazo tu
 
Taarifa kutoka Dodoma zinasema Baraza jipya la mawaziri litatangazwa muda wowote KESHO na si leo kama ilivyotarajiwa.

Ni hayo tu... Just for your information.

Invisible


Kazi ipo...

Hili baraza tumelisubiria kwa hamu sana leo, anway Subira yavuta kheri... tutaendelea kusubiri.

thanx for info mkuu
 
inahisi sasa hapa ndo kuna kukata majina na kuingiza majina mapya
,mana why ipelekwe kesho?kuna siri kubwa imefichika behind,ambayo wakubwa wenyewe ndo wanaijua siri hiyo.
 
Inaelekea kazi ya panga pangua imekuwa ngumu kutokana na kuwa rais anatakiwa kuhakikisha hawapi nafasi tena wanao-hisiwa (ama kutambulika kwake) kuhusika na ufisadi wa aina yoyote. Kumbuka ripoti ya BoT anayo na anawajua wahusika kadhaa wanaoguswa nayo.

Ni mawazo tu

Possibly,
Unajua Wadanganyika wamekuwa wakilalamika na kuonya kwamba hawawataki barazani wale wote ambao wametajwa na tume. Hopefully hatutasikia jina la yoyote ambaye kaguswa katika tume zote zilizo kazini muda huu. Huenda hii ndio inayompa maumivu ya kichwa mkuu wa kaya, kwani wengine ni watendaji wazuri lakini tume zimewataja!
Tusubiri tuone.
 
Waliweka captions to that effect on TVT.

Mara zote watu makini wanapofanya kazi, ukiulizwa ETA lazima utoe muda utakaokupa the high end of the estimated timeframe.

Sasa kama administration hii tulivyozoea, wamesema watatoa baraza Jumatatu, creating false expectations kwa watu only to dissapoint.Kulikuwa na ulazima wa kuahidi baraza Jumatatu? Hii kazi ya kupanga timu siyo ndogo, ningeweza kuwapa a few days wamalize hilo.

Next time wawe makini kuto create false expectations.I don't care much if it takes a day or three, lakini najua kuna mijitu presha inapanda by the hour huko.
 
Baraza la Mawaziri limekuwa gumzo hasa; nasikia JK anafanya mawasiliano na Wapinzani kuwa ndani ya Baraza, sijui ni za kweli soma Tanzania Daima ya leo.
 
Baraza la Mawaziri limekuwa gumzo hasa; nasikia JK anafanya mawasiliano na Wapinzani kuwa ndani ya Baraza, sijui ni za kweli soma Tanzania Daima ya leo.

Sidhani kama atawaingiza wapinzani barazani, huo utakuwa mseto sasa! Kama kuna mawasiliano anafanya na wapinzani, nadhani itakuwa ni kuomba ushauri wa "Watu gani wasio na mawaa mnaona wanafaa kuwa barazani?" Sidhani kama ni vinginevyo!
 
Hii kweli Invisible?
au umeamua tu kuturusha roho ndugu yangu?
Kama itakuwa kweli mbona sasa kazi hiyo?

Ndo taarifa nilizopewa na 'mwandishi wetu' aliye Dodoma. Inashangaza RTD nasikia wao wanadai 'taarifa za baraza jipya la mawaziri zitawajia pindi tukipata mawasiliano na Dodoma'.

Ingependeza mheshimiwa Rais angeweka pembeni tofauti na akaangalia ndani ya wapinzani wale wanaotufaa kuwa mawaziri na akawapa fursa ya kuwatumikia watanzania. Huo ndio uzalendo! Siamini kama wapinzani hawawezi...

Ni fursa nzuri sana kwa JK kurekebisha makosa
 
Ndo taarifa nilizopewa na 'mwandishi wetu' aliye Dodoma. Inashangaza RTD nasikia wao wanadai 'taarifa za baraza jipya la mawaziri zitawajia pindi tukipata mawasiliano na Dodoma'.

Ingependeza mheshimiwa Rais angeweka pembeni tofauti na akaangalia ndani ya wapinzani wale wanaotufaa kuwa mawaziri na akawapa fursa ya kuwatumikia watanzania. Huo ndio uzalendo! Siamini kama wapinzani hawawezi...

Ni fursa nzuri sana kwa JK kurekebisha makosa

Hapana invisible, sidhani kama chama tawala kimeishiwa watu hadi kufikia kuhitaji kukopa kutoka kwa wapinzani! Naamini CCM inao watu wa kutosha na waadilifu wa kupewa hizo nafasi za uwaziri. Wapinzani waendelee kufanya bidii, na siku moja inshaallah watashinda nao wataunda serikali yao. Mazingira ya sasa hivi hayatoi sababu yoyote ya kuunda serikali ya mseto, CCM ni chama tawala na kina asilimia kubwa sana ya wabunge. Upinzani ndio minority Bungeni. Sasa kama Rais atachukua tena hao minority awape uwaziri, atakuwa amezidi kufifisha upinzani. Awaache wapinzani waendelee kuisahihisha na kuikosoa serikali bungeni.
 
Invisible na wengine...JK hana muda kushauriana na Wapinzani...hii ni kutokana na Jeuri ya CCM. kushauriana na Upinzani as if CC ya CCM haipo. Pia hio itahitaji baadhi ya vitu vya kikatiba..sina hakika kama katiba ya sasa inaruhusu au La..pengine CCM watakuja na kusema MSETO haukuwa ktk SERA zao.

Pia Kama JK angekuwa na dhamira ya Kweli ya MSETO angeeza na ZNZ ambapo kuna sababu LUKUKI za kufanya mseto kule, lkn JEURI, UFISADI na mengineyo mnayoyajua ndio yamefanya tufike hapa tulipo. Baadhi ya wana CCM wao wanaona ushindi kuwashinda UPINZANI na si ROHO ZA WANANCHI wa Tanzania.
 
Inaweza kuwa tactics za kuwaziba mdomo wabunge machachari.

Inaweza pia kutoa access zaidi kwa wapinzani katika machinery ya serikali.

Inaweza kuwa speculations za magazeti, but isn't Tanzania Daima supposed to be a reputable source?
 
Inaweza kuwa tactics za kuwaziba mdomo wabunge machachari.

Inaweza pia kutoa access zaidi kwa wapinzani katika machinery ya serikali.

Inaweza kuwa speculations za magazeti, but isn't Tanzania Daima supposed to be a reputable source?

Namna bora ya wapinzani kuwa katika serikali ni kushinda uchaguzi, si kusubiri "kuzawadiwa" mseto, maana hiyo haitakuwa tofauti na ufisadi. Wakishazawadiwa huo mseto wapinzani wote watageuka "midebwedo"!
 
Hapana invisible, sidhani kama chama tawala kimeishiwa watu hadi kufikia kuhitaji kukopa kutoka kwa wapinzani! Naamini CCM inao watu wa kutosha na waadilifu wa kupewa hizo nafasi za uwaziri. Wapinzani waendelee kufanya bidii, na siku moja inshaallah watashinda nao wataunda serikali yao. Mazingira ya sasa hivi hayatoi sababu yoyote ya kuunda serikali ya mseto, CCM ni chama tawala na kina asilimia kubwa sana ya wabunge. Upinzani ndio minority Bungeni. Sasa kama Rais atachukua tena hao minority awape uwaziri, atakuwa amezidi kufifisha upinzani. Awaache wapinzani waendelee kuisahihisha na kuikosoa serikali bungeni.


Mheshimiwa hii sentensi yako inanishangaza sana. Ina maana JK alivyoteua Kabwe kwenye kamati ya madini ina maana CCM ilikuwa imeishiwa watu? Sidhani kama ni busara kuona kuwa watu kutoka CCM peke yao ndio wanaweza kufanya kazi kwenye serikali. Kwa maana nyingine unataka kama opposition wakishinda CCM wote waondolewe kwenye nyadhifa zao, hizi sio siasa njema, hizo ndio siasa za kale. Kama kweli JK akiingiza wawili au watatu opposition itakuwa precedence moja nzuri sana, na strategically ni hatua nzuri!
 
RTD ndo wamepata taarifa sasa na wame-confirm kuwa Baraza jipya litatangazwa KESHO na SAA YOYOTE na si leo kama ilivyotarajiwa.

Hivi kukiwa na waziri toka Upinzani itakuwa ni kuufifisha upinzani mkuu Kithuku? Hilo sikujua, ila 'kwa fikra zangu' nilionelea kwakuwa hawa nao ni watanzania na wapo tunaokiri wenyewe kuwa wanafaa basi haina budi wapewe majukumu ambayo ni wazi wanaweza kuyabeba katika kulipeleka Taifa tunakotaka.

Aidha binafsi naona ni fursa nzuri kwa JK kuwaweka kando wale aliokuwa akitanabaisha waziwazi kuwa wanamwangusha (japo bila kuwataja) na awaadhibu kwa kuwanyima u-waziri. Akifanya kweli basi watanzania watarejesha imani yao iliyoanza kupotea tokana na ugumu wa maisha ulosababishwa na mafisadi wachache (kama alivyosema Mama Malecela hawazidi 20 hivi).

Tanzania yenye neema bado inawezekana! Ufanisi ama kuanguka kwa Tanzania kwa sasa kuko mikononi mwa JK na wasaidizi wake atakaotuletea kesho.

Mungu ibariki Tanzania
 
Baraza la Mawaziri limekuwa gumzo hasa; nasikia JK anafanya mawasiliano na Wapinzani kuwa ndani ya Baraza, sijui ni za kweli soma Tanzania Daima ya leo.

So itakuwa kama serikali ya Kibaki. But, hata kama akiwaingiza wapinzani sitegemi wakapewa wizara nyeti sana sana watapewa wizara ya Afrika mashariki au utamaduni,michezo na vichekesho
 
Kazi hiyo sio ndogo kutokana na CV za baadhi ya wanaotarajiwa kuchafuka, hivyo umakini mkubwa unahitajika. Ole wao watakaokimbilia Bagamoyo!!!!! Na kwa sera za CCM wapinzani kuwepo kwenye baraza si rahisi.
 
Mheshimiwa hii sentensi yako inanishangaza sana. Ina maana JK alivyoteua Kabwe kwenye kamati ya madini ina maana CCM ilikuwa imeishiwa watu? Sidhani kama ni busara kuona kuwa watu kutoka CCM peke yao ndio wanaweza kufanya kazi kwenye serikali. Kwa maana nyingine unataka kama opposition wakishinda CCM wote waondolewe kwenye nyadhifa zao, hizi sio siasa njema, hizo ndio siasa za kale. Kama kweli JK akiingiza wawili au watatu opposition itakuwa precedence moja nzuri sana, na strategically ni hatua nzuri!

Tofautisha kamati na serikali. Hata kamati za bunge zote zina wapinzani ndani. Lakini serikali ni ya CCM inatekeleza ilani iliyowafanya kuchaguliwa. Kamati za bunge ni sauti ya wananchi, lakini serikali ni chombo cha kutekeleza ilani ya chama tawala, hakuna mantiki ya kuweka wapinzani humo. Wapinzani wanaweza kushirikishwa iwapo chama tawala hakina majority bungeni au ushindi ni karibu nusu kwa nusu(maana yake walioikata ilani hiyo kwa idadi ni karibu sawa na walioikubali, kwa hiyo inabidi kuchangia madaraka ili matakwa ya pande zote yazingatiwe katika serikali). Mantiki hiyo ingeweza kutumika Zanzibar lakini mazingira hayo hayapo katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Back
Top Bottom