Baraza jipya la Mawaziri kujulikana Feb 12

In all fairness to Mama Kilango, nilivyofuatilia mjadala wa Zitto kuzibwa mdomo Mama Kilango aliprotest kwa kutoka nje ya bunge naamini baada ya machinery ya CCM kum-silence, mpaka magazeti yaliandika.

Sio kila mbunge wa CCM ana partisan politics.Tunahitaji kila mbunge atakayetusaidia katika vita dhidi ya ufisadi.Bila huyu mama taarifa za Hansard zingekuwa zina rekodi ya mwisho kwamba Lowassa kaonewa according to his resignation speech (albeit with no point by point rebuttal).Mama Kilango ali set the record straight kwa kusoma vimemo bungeni.It takes courage in CCM to do that at a time when some CCM MPs were clearly defending Lowassa.

Pundit
Huyu Mama mimi nilisha sema hapa kabla kwamba hakuanza leo .Wakati wa Zitto walked out kuonyesha kukerwa kwake na CCM wanajua .Si yeye pekee.Akina Meghji , Nagu na wengine wengi walikuwa wanampa Zitto kudo maana wanajua na walikuwa wanaona Nchi inavyo liwa . Spika hana maana kabisa . Huyu mama juzi alisema kitu kikubwa sana nadhani anakifanya sasa .Kwamba akifa bado awe anaishi kama Mwalimu .This is very enough kuliko Mwakenyembe kupata uwaziri. It is absurd watu kufikiri kwamba kila shujaa awe rewarded cheo . Hakuna kitu kama hiki mapambano ndiyo yalivyo .Mama Melecela nasema endelea una mapungufu yako nayajua sana lakini hafikii unayo simamia .
 
Kitio...mmmhhh!...bonge la jina.Heshima yako bro.

Kama JK hana watu wasafi wenye maadili ya kueleweka then dissolve the damn Bunge na itisha kura upya.The campaign theme should be "viongozi safi wasio na skendo". Nakwambia asilimia kubwa ya hawa mabwana hawatorudi.Asante.


Yaani tunaongea hivi kama vile JK mwenyewe ni safi na ana high moral standard kufanya hivyo.


Hiki kitu hakiwezi kutokea kwa sababu JK mwenyewe si safi na wala hategemei kuwa safi.Kampeni zote za CCM, zimeendeshwa kwa pesa chafu, na hii itakuwa hivyo hivyo hata 2010.

Sasa JK hawezi kuleta mageuzi yoyote serious, mageuzi lazima yalazimishwe.
 
In all fairness to Mama Kilango, nilivyofuatilia mjadala wa Zitto kuzibwa mdomo Mama Kilango aliprotest kwa kutoka nje ya bunge naamini baada ya machinery ya CCM kum-silence, mpaka magazeti yaliandika.

Sio kila mbunge wa CCM ana partisan politics.Tunahitaji kila mbunge atakayetusaidia katika vita dhidi ya ufisadi.Bila huyu mama taarifa za Hansard zingekuwa zina rekodi ya mwisho kwamba Lowassa kaonewa according to his resignation speech (albeit with no point by point rebuttal).Mama Kilango ali set the record straight kwa kusoma vimemo bungeni.It takes courage in CCM to do that at a time when some CCM MPs were clearly defending Lowassa.

Asante Pundit, umenielimisha.Swali linakuja hivi nani aliyemziba mdomo Mama Kilango hapo awali?We have a system of patronage politics taking root in Tz na nd'o hapo sasa wenye chama wanaleta za kuleta.
 
Yaani tunaongea hivi kama vile JK mwenyewe ni safi na ana high moral standard kufanya hivyo.


Hiki kitu hakiwezi kutokea kwa sababu JK mwenyewe si safi na wala hategemei kuwa safi.Kampeni zote za CCM, zimeendeshwa kwa pesa chafu, na hii itakuwa hivyo hivyo hata 2010.

Sasa JK hawezi kuleta mageuzi yoyote serious, mageuzi lazima yalazimishwe.

Asante Pundit na heshima yako upewe,
I have always thought that JK lazima awe answerable for these skendos.Japo najua wabongo watalalama, naamini Rais pia has to hold some responsibility.Hizi skendo kidogo ni too much for the president to keep reappointing hawa jamaa yet nchi is still bleeding.Mchango wangu huo.
 
Asante Pundit, umenielimisha.Swali linakuja hivi nani aliyemziba mdomo Mama Kilango hapo awali?We have a system of patronage politics taking root in Tz na nd'o hapo sasa wenye chama wanaleta za kuleta.

Bwana AB ....! Ungeangalia TVT Jumamosi,kulikuwa na mdahalo na mmoja wa washiriki alikuwa Mama Malicela!

Kwa mdomo wake alisema; ''wakati tumcheguliwa mwaka 2005 tuliambiwa kwenye vikao vya CCM tusiulize maswala muhimu bungeni kukisaidia chama na zaidi haya, mimi niliwahi kuuliza swali Bungeni kuhusu Richmond, nikaandikiwa barua na kiongozi mmoja na nikaitwa na kuonywa nisirudie tena kufanya hivyo, nikiwa na maswali kama hayo niyapeleke kwenye vikao vya CCM'' Hivyo bwana AB utaona kwamba huyu mama pamoja na wabunge wengine wa CCM wenye nia njema na nchi hii, walikuwa wanazibwa midomo na wakubwa wao!! This mama ana mapungufu yake, lakini hayazidi uzalendo anao uonyesha hivi sasa!!

festog
 
Mama Kilango atapewa tu uwaziri- ili anyamaze- na pia kama shukrani kwa Mzee Malecela!

Sijui kama ni wiraza ipi atapewa!
 
Mama Kilango atapewa tu uwaziri- ili anyamaze- na pia kama shukrani kwa Mzee Malecela!

Sijui kama ni wiraza ipi atapewa!

Hahaha watu mna hisia kali. Itabidi JK asimpe sasa! Ila she seems to develop politically nowadays. She deserves something na si kunyamazishwa!
 
Bwana AB ....! Ungeangalia TVT Jumamosi,kulikuwa na mdahalo na mmoja wa washiriki alikuwa Mama Malicela!

Kwa mdomo wake alisema; ''wakati tumcheguliwa mwaka 2005 tuliambiwa kwenye vikao vya CCM tusiulize maswala muhimu bungeni kukisaidia chama na zaidi haya, mimi niliwahi kuuliza swali Bungeni kuhusu Richmond, nikaandikiwa barua na kiongozi mmoja na nikaitwa na kuonywa nisirudie tena kufanya hivyo, nikiwa na maswali kama hayo niyapeleke kwenye vikao vya CCM'' Hivyo bwana AB utaona kwamba huyu mama pamoja na wabunge wengine wa CCM wenye nia njema na nchi hii, walikuwa wanazibwa midomo na wakubwa wao!! This mama ana mapungufu yake, lakini hayazidi uzalendo anao uonyesha hivi sasa!!

festog

Asante sana mufti Festog,heshima yako upewe,
A'fu naongeza,Mama Malecela is a darling to all lakini kama ulivyoainisha hapo juu...CCM inawenyewe,vigunge vya longtime! Mie nasikitika sana na nchi yetu kulingana na siasa kama hizi.Huu wote ni ubinafsi na wananchi hatuna haki iwapo mbunge wetu atazibwa mdomo asitetee haki zetu.Bongo jamani!!!Hii CCM should be reconstituted! Yes,I've said it.
 
Hahaha watu mna hisia kali. Itabidi JK asimpe sasa! Ila she seems to develop politically nowadays. She deserves something na si kunyamazishwa!

Kweli kabisa Invii, lakini je, do we need her silenced or do we need her vocal?
 
Kuna taarifa kule Rock City eti watu wameandaa party Diallo akimwagwa wafanye sherehe ng'ombe zimeandaliwa watu wale nyama. Hawa naona wana matatizo na wivu binafsi Huyu EL kaiba hela hatuoni kaziivest wapi? na yule mtoto wake akitanua tu lakini Diallo kaleta ndege hadi nauli zimekuwa nafuu bora!!! WIVU TU


Una maana "Matokea yanahalalisha Mbinu" mbona tuna safari ndefu...
 
Kweli kabisa Invii, lakini je, do we need her silenced or do we need her vocal?
Wait a minute,

Niulize swali dogo kwanza: Hivi ni kweli mtu akipewa u-waziri anakuwa kanyamazishwa? Kuna mtu anaweza kunithibitishia hili? Nimekuwa nikiona wengi wanadai "Flani atanyamazishwa kwa kupewa u-waziri"... I do not get it. Wote tunaamini mtu ananyamazishwa kwa kupewa u-waziri? Zitto kama upo, assume wewe umeteuliwa waziri mteule wa Wizara ya Fedha, ndo utakuwa mwisho wako kutoa hoja zenye tija kwa taifa lako kwakuwa umekuwa waziri? Frankly speaking hainiingii akilini.

Kama ni hivyo basi siasa zetu zina matatizo!

BTW: Anna Kilango Malecela hastahili kunyamazishwa kwa namna yoyote. Ni ishara ya wana-CCM wanaopenda mabadiliko. Ni ishara ya kukomaa kwa demokrasia ndani ya CCM. Lakini... Siwezi kujua siri nyuma ya pazia!
 
Wait a minute,

Niulize swali dogo kwanza: Hivi ni kweli mtu akipewa u-waziri anakuwa kanyamazishwa? Kuna mtu anaweza kunithibitishia hili? Nimekuwa nikiona wengi wanadai "Flani atanyamazishwa kwa kupewa u-waziri"... I do not get it. Wote tunaamini mtu ananyamazishwa kwa kupewa u-waziri? Zitto kama upo, assume wewe umeteuliwa waziri mteule wa Wizara ya Fedha, ndo utakuwa mwisho wako kutoa hoja zenye tija kwa taifa lako kwakuwa umekuwa waziri? Frankly speaking hainiingii akilini.

Jibu la haraka ni ndiyo. Anapokula kiapo cha Uwaziri sehemu ya pili baada ya kile cha kuilinda na kuitunza Katiba ni kiapo cha "na kwa vyovyote vile, sitatoa siri za baraza la Mawaziri" Ndio maana kwenye sakata la Richmond hujasikia Waziri hata mmoja akisema walichozungumza huko ni nini na kama kuna mtu alipinga lolote na ni nani.

Mtu unapokuwa Waziri unakuwa ndio mshauri wa karibu wa Rais na msaidizi wake, hivyo lazima uaminiwe kuwa utakuwa mkweli na mwadilifu. Kuwa, wanapokaa kufanya majadiliano huwa wanazungumza na kupiga kura kwenye Baraza la Mawaziri sasa hatujui nani alipigia kura "ndiyo" kampuni ya RDC na nani alipigia "hapana" kwa sababu ni siri lakini wakimaliza wanasema ni "uamuzi wa Baraza la Mawaziri".
Kama ni hivyo basi siasa zetu zina matatizo!

Hii ina maana kama mpinzani ataingia kwenye baraza hilo as full minister akiona mambo yanazungumzwa kwenye kabineti ambayo hakubaliani nayo hawezi kutoka nje na kuyasema, atafukuzwa kazi ni lazima akubali ile inayoitwa kuwa ni "collective responsibility"

Kwa sababu hii binafsi siamini kama Zitto au Slaa waingizwe kwenye baraza hili wanaweza kumpa ka Unaibu mtu fulani hivi.

BTW: Anna Kilango Malecela hastahili kunyamazishwa kwa namna yoyote. Ni ishara ya wana-CCM wanaopenda mabadiliko. Ni ishara ya kukomaa kwa demokrasia ndani ya CCM. Lakini... Siwezi kujua siri nyuma ya pazia!

Mama Kilango Malecela ni hivyo hivyo, kama anataka kuwa mtetezi wa kuisimamia kweli serikali asiingizwe kwenye hiyo Cabinet hata hivyo, somebody has to do it, so mapungufu ya kulazimika kuchagua wabunge kuwa mawaziri ndipo hapo yanapoonekana.
 
Invi... Hilo swali lako nimelifananisha na kile kipindi kwenye TV jamaa anasema ngoja aulize "Swali la kizushi"......

Lakini ni swali zuri sana mkuu... Ukumbuke zile semi "Mwana umelavyo ndivyo akuavyo" na "lisemwalo lipo"..... Zamani posti tuliamini kuwa:
1. Low level ukibishana na mkuu then unapelekwa mikoani (tena you are lucky kama hautapelekwa Kigoma, Sumbawanga, Lindi au something like that)
2. Ukiwa kibosi kidogo then unapelekwa ubalozini
3. Ukiwa rafiki sana basi lazima ukurugenzi wa parastatal unao
4. Ukiwa mshirika then unaingizwa serikalini kaka

So Mkuu Invi... mimi niliposoma swali lako nikakusoma kabisaaa kwa mapana kwamba kuna issue ya "Change in our Midsets".... Mkuu hii ni sawa na swala zima la mindsets za "Chama kimeshika hatamu"

Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.....
 
Wait a minute,

Niulize swali dogo kwanza: Hivi ni kweli mtu akipewa u-waziri anakuwa kanyamazishwa? Kuna mtu anaweza kunithibitishia hili? Nimekuwa nikiona wengi wanadai "Flani atanyamazishwa kwa kupewa u-waziri"... I do not get it. Wote tunaamini mtu ananyamazishwa kwa kupewa u-waziri? Zitto kama upo, assume wewe umeteuliwa waziri mteule wa Wizara ya Fedha, ndo utakuwa mwisho wako kutoa hoja zenye tija kwa taifa lako kwakuwa umekuwa waziri? Frankly speaking hainiingii akilini.

Kama ni hivyo basi siasa zetu zina matatizo!

BTW: Anna Kilango Malecela hastahili kunyamazishwa kwa namna yoyote. Ni ishara ya wana-CCM wanaopenda mabadiliko. Ni ishara ya kukomaa kwa demokrasia ndani ya CCM. Lakini... Siwezi kujua siri nyuma ya pazia!

Invii kakangu,
acha nikupe darasa la kishakji. Among the principles of parliamentary democracy kuna kitu kinaitwa "Collective Responsibility" ambapo kama upo kwenye baraza la mawaziri(Cabinet) inabidi uunge mkono all that comes from the govt side.You simply do this believing your leaders are democratically mature to be fair in all policies.Swali sasa ni je, sisi tumekomaa enuff kufikia kiwango hiki?Jaza mwenyewe mbongo mwenzangu!
 
Mtu unapokuwa Waziri unakuwa ndio mshauri wa karibu wa Rais na msaidizi wake, hivyo lazima uaminiwe kuwa utakuwa mkweli na mwadilifu. Kuwa, wanapokaa kufanya majadiliano huwa wanazungumza na kupiga kura kwenye Baraza la Mawaziri sasa hatujui nani alipigia kura "ndiyo" kampuni ya RDC na nani alipigia "hapana" kwa sababu ni siri lakini wakimaliza wanasema ni "uamuzi wa Baraza la Mawaziri".

So educative, basi Mwanakijiji unatakiwa upewe Wizara ya Elimu ya Juu Sayansi na Teknolojia.

:)
 
Hii ni kwa Mwananakijiji,
Hio kitu umesema hapo juu inaitwa "The Principle Of Collective Responsibility".Na kama nilivyomwaambia Inviiit all depends on the maturity of our politics.
 
Wait a minute,

Niulize swali dogo kwanza: Hivi ni kweli mtu akipewa u-waziri anakuwa kanyamazishwa? Kuna mtu anaweza kunithibitishia hili? Nimekuwa nikiona wengi wanadai "Flani atanyamazishwa kwa kupewa u-waziri"... I do not get it. Wote tunaamini mtu ananyamazishwa kwa kupewa u-waziri? Zitto kama upo, assume wewe umeteuliwa waziri mteule wa Wizara ya Fedha, ndo utakuwa mwisho wako kutoa hoja zenye tija kwa taifa lako kwakuwa umekuwa waziri? Frankly speaking hainiingii akilini.

Kama ni hivyo basi siasa zetu zina matatizo!

BTW: Anna Kilango Malecela hastahili kunyamazishwa kwa namna yoyote. Ni ishara ya wana-CCM wanaopenda mabadiliko. Ni ishara ya kukomaa kwa demokrasia ndani ya CCM. Lakini... Siwezi kujua siri nyuma ya pazia!

Invisible,
Kwanza nimpongeze Mwanakiji kwa ufafanuzi wake murua. Kwa kujazia kwa Mwanakijiji na wenzake ni kwamba, waziri yoyote kimsingi ni mbunge. Anapokuwa bungeni kabla ya kuteuliwa kuwa waziri, mbunge anakuwa anawakilisha wananchi wake katika chombo cha kutunga sheria (bunge)ambao ni mhimili mmojawapo kati ya ile mitatu ya dola na huwa anawauliza maswali mawaziri wahusika kwa kadri ya kero alizotumwa kuzipeleka bungeni kutoka kwa wananchi wa jimbo lake. Sasa basi, mbunge huyu anapopewa uwaziri, anahama kabisa kutoka chombo hiki (bunge) na kwenda kwenye chombo kingine (serikali) ambao ni watekelezaji wa maamuzi ya bunge. Kwa hiyo mpaka hapa waziri huyu badala ya kupeleka kero bungeni kama mbunge, anabadilika na kuanza kuzijibu hoja za wabunge akiwa kama mwakilishi wa serikali! Hii ndio maana halisi ya kuzibwa mdomo ambako umeuliza.
Nadhani nimegusa panapo ufafanuzi.
JF hapaharibiki kitu.
 
Mie naona watu hawakunielewa post yangu ina maana gani.
Hawa mafisadi waliiba hela zetu hawajainvest kwenye hela walizoiba zaidi ya kutanulia eg EL na huyu mwenzetu Diallo kainvest na kutupa unafuu wa nauli na usafiri wa uhakika, bora hata wangejenga viwanda wananchi wangepata ajira. WIVU??
 
Jibu la haraka ni ndiyo. Anapokula kiapo cha Uwaziri sehemu ya pili baada ya kile cha kuilinda na kuitunza Katiba ni kiapo cha "na kwa vyovyote vile, sitatoa siri za baraza la Mawaziri" Ndio maana kwenye sakata la Richmond hujasikia Waziri hata mmoja akisema walichozungumza huko ni nini na kama kuna mtu alipinga lolote na ni nani.

Mtu unapokuwa Waziri unakuwa ndio mshauri wa karibu wa Rais na msaidizi wake, hivyo lazima uaminiwe kuwa utakuwa mkweli na mwadilifu. Kuwa, wanapokaa kufanya majadiliano huwa wanazungumza na kupiga kura kwenye Baraza la Mawaziri sasa hatujui nani alipigia kura "ndiyo" kampuni ya RDC na nani alipigia "hapana" kwa sababu ni siri lakini wakimaliza wanasema ni "uamuzi wa Baraza la Mawaziri".
Kama ni hivyo basi siasa zetu zina matatizo!

Hii ina maana kama mpinzani ataingia kwenye baraza hilo as full minister akiona mambo yanazungumzwa kwenye kabineti ambayo hakubaliani nayo hawezi kutoka nje na kuyasema, atafukuzwa kazi ni lazima akubali ile inayoitwa kuwa ni "collective responsibility"

Kwa sababu hii binafsi siamini kama Zitto au Slaa waingizwe kwenye baraza hili wanaweza kumpa ka Unaibu mtu fulani hivi.


Mkulu Mwanakijiji,
Mimi nami sikubaliani kama kupewa Uwaziri kunaweza kukunyamazisha ila tu kama muhusika mwenyewe atakuwa tayari kukubali kufanya hivyo na kwenda kinyume na Katiba ambayo aliapa kuilinda na kuitumikia.Wengi wanaonyamazishwa ni kwa matakwa binafsi,kwamba wanakaa kimya ili kuneemeka.Kama mtu unatabia ya uadilifu na iko ndani ya damu,hata ukiwa Waziri hutakubali kupitisha vitu vya kipuuzi kama RICHMOND,IPTL,RADAR,etc. Hutaweza kuja hadharani na kusema ila utaweza kuwaeleza na kumshauri Rais kuwa hauko tayari kufanya hiki au kile kwa kuwa ni kinyume na Katiba,Taratibu na zaidi Maslahi ya nchi.

Kuwa Mkweli na Mwadilifu haina maana kumkubalia mkuu wako kila atakacho hata kama unajua ni wrong.Kuwa Mkweli ina maana kusimamia ukweli wakati wote bila kujali nani yuko mbele yako.Mwadilifu ni kuwa "Clean" na kuwa tayari kumwambia Rais ukweli bila woga pale unapoona uelekeo unakuwa mbaya.
Kwenye vingi viapo kuna neno "Niko tayari kupokea amri halali"Hii ina maana kuna amri zisizo halali ambazo unatakiwa kuzikataaa.
Tunahitaji watendaji walio wakweli na Waadilifu ambao watakuwa tayari kuchukua maamuzi mazito kabla hayaja-mature na kuleta hasara kwa Tanzania. Mambo ya kukaa tunasubiriana mpaka kitu kimeshaaribika pia inabidi tuondokane nacho,although kimsingi sipendi Dr.Slaa na Zitto waingie kwenye Baraza ila Mama Malecela naona ni bora kama upo uwezekano aukwae tu.
 
Back
Top Bottom