Baraza Jipya la Mawaziri hili hapa...

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,437
113,445

Wanabodi,

Hatimaye Baraza jipya la Mawaziri ndio lianza kutangazwa sasa live kupitia TBC!
Endelea kufuatilia...

UPDATES:

  • Wizara ya maji imeunganishwa na Kilimo - Itakuwa Wizara ya Kilimo na umwagiliaji!
  • Kazi ajira na vijana - kitengo cha vijana kimehamishiwa michezo na utamaduni
  • Uwezeshaji wa wananchi (Baraza la uwezeshaji) - Ilikuwa wizara ya fedha, imebidi kuipunguzia Hazina mzigo huu na kulielekeza Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Waziri wa TAMISEMI atakuwa na manaibu wawili
  • Wizara ya Miundo Mbinu imepunguzwa, imegawanyika kuwa na Wizara ya Ujenzi (barabara na viwanja vya ndege) & Wizara ya Uchukuzi - Reli, bandari na usafiri wa majini
  • Magufuli atachukua wizara ya Ujenzi na msaidizi wake ni Mwakyembe
  • Sitta atakuwa waziri wa Wizara ya ushirikiano wa Afrika Mashariki
  • Membe ataendelea kuwa waziri wa mambo ya nchi za nje
  • Ngeleja ataendelea kubaki wizara ya Nishati na Madini
  • Wizara ya Mambo ya Ndani atakuwepo Nahodha akishirikiana na Kagasheki
  • Anna Tibaijuka atakuwa waziri wa Wizara ya Ardhi na Makazi
  • Hakuna jina la Januari Makamba wala Lowassa kama wengi walivyokuwa wakishuku
WIZARA NA MAWAZIRI WAKE:

baraza_Page_1.jpg

baraza_Page_2.jpg

baraza_Page_3.jpg
 
Last edited by a moderator:
Jamaa ameamua kutangaza saa 6 kamili juu ya alama, mtangazaji Shabani Kissu ndio yuko jikoni viwanja vya Ikulu, nilitamani sana, niwepo viwanjani hapo, bahati mbaya leo ma reporters ni ma editors wenyewe!
 
Ah watangaze au wasitangaze, kwa mfumo huu wa CCM na katiba hii hakuna faida ýoyote ya kuwa na Baraza la Mawaziri kwani kila mtu yupo kwa maslahi yake tu!
 
Nawaona ma editors wa vyombo mbalimbali vya habari hadi clouds radio ndani ya nyumba, nadhani pia itakuwa live kwenye redio yao.
 
namuona kibonde yuko busy na mshana sijui wanadiscuss nini, jamaa kakaa mbele kabisa, kiherehere huyu
 
ya man thanks,jamani hakuna radio ktk mtandao inayo tangazaaaa? kwani bongo radio naona hakuna kitu
mapinduziiii daimaaaa
 
itakuwa ni saa sita kamili kwa saa za Dar Es Salaam. Rais kuzungumza na waandish wa habari.
 
wanahabari wengi wapo wanamsubiri mkwere, mtangazaji kobonde wa clounds naye yumo
 
Back
Top Bottom