Baraza Dogo la Mawaziri na Muundo wa Wizara

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Wakati macho na masikio ya watanzania wengi ni kusubiri kwa hamu kuhusu “Nani na Nani’ watakuwepo kwenye baraza na watakuwa ‘wapi’; mjadala wa MUUNDO umetawaliwa zaidi na kutazama “sura”. Mjadala wa “watu’, MODS napendekeza uendelee katika ile thread ya “uchambuzi kuhusu baraza la mawaziri”; hii iachwe pekee kwa lengo la kujadili ‘masuala’ ya ukubwa wa baraza lenyewe na mpangilio wa wizara. Wakati “sura” ni suala la muhimu sana la kwanza kabisa kabla ya ‘mfumo’ mzima, ni muhimu pia tujadili muundo wa baraza kwa maana ya mpangilio wa wizara na idadi ya wizara. Sauti ya umma kupitia kwa wapinzani, asasi za kiraia, wasomi nk wakati wote zimekuwa ni ‘tunataka baraza dogo la mawaziri lakini lenye ufanisi’. Swali la kujiuliza- ni baraza dogo kiasi gani? Mwaka 2005 ‘war room’ ya CHADEMA tuliwahi kukaa chini na kuanza kutafakari- kama tungeshinda nchi na kuongoza dola- tungetekeleza vipi sera yetu ya kuwa na “mfumo mpya wa utawala” ambao pamoja na mambo mengine ungekuwa na ‘small but yet accountable and effective government’? Wakati huo tulitengeneza Muundo wa Baraza Dogo ambalo mawaziri walikuwa takribani 15 tu. Huku nilipo, nimeshindwa kuipata ile nyaraka ya ndani ya mapendekezo ya wakati huo. Lakini nimeona bado ni vyema nikachokoza mjadala huu kwa mawazo yangu binafsi.

Naanzia na dhana kwamba sikubaliani na muundo wetu wa sasa wa Baraza lenye Mawaziri takribani 29- hili ni kubwa sana. Hata Uingereza ambao wana idadi kubwa ya watu na fedha nyingi na ndio ambao wanachangia bajeti yetu kwa kiasi kikubwa ikiwemo bajeti ya mishahara tunayowalipa mawaziri wetu- wamejipangia kabisa wizara zisizidi 20. Kama Waziri mkuu anataka kuongeza ya 21 inabidi aombe kibali maalumu. Na wizara yoyote zaidi ya hapo basi waziri mkuu anaigharamia mwenyewe kwa fedha zake. Sisi sasa tunazo 29 na Jeshi la manaibu kibao. Kwa kauli ya Waziri Mkuu Pinda inaelekea JK atakubaliana na wazo la wapinzani na wananchi kwa ujumla la kupunguza baraza la mawaziri. Je, apunguze kwa kiasi gani? Huu ndio mjadala wa hapa-

Kwa maoni yangu- atoke toka Wizara 29 mpaka Wizara zisizozidi 10; kwa maneno mengine apunguze wizara takribani 10 katika hatua ya sasa. Afanye namna gani?

Kwanza aamue kabisa kwamba Yeye asiwe Waziri wa Wizara yoyote- huu muundo wa baadhi ya Wizara kuwa Ofisi ya Rais unamfanya Rais ajiingize katika kazi za Uwaziri bila sababu yoyote ya msingi. Rais yeye awe Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri tu na mwongozaji mkuu wa Wizara zote. Nakumbuka wakati wa Rais Mkapa alikuwa pia Waziri wa TAMISEMI, matokeo yake ilikuwa ni aibu ya moja kwa moja kwa Rais kwa kuwa alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2004! Sasa TAMISEMI ilikuwa kwa waziri mkuu lakini bado, kuna mawaziri waliokuwa katika ofisi ya Rais.

Pili, nashauri baadhi ya wizara ziunganishwe kama nitakavyopendekeza na baadhi ya Wizara kwa kweli zilikuwa hazistahili kuwa Wizara kabisa; labda ziwe idara tu katika wizara Fulani Fulani. Kwa ujumla sitapendekeza wizara ziitwejwe, lakini nitaunganisha zaidi yale majukumu ili kujua ni yapi waziri anayependekezwa atahusika nayo. Baada ya kukubaliana MAJUKUMU- ndio suala la JINA LA WIZARA linafuata halafu ndio JINA LA WAZIRI:

Mapendekezo yangu ya Wizara 19:

1. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano
2. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Afrika Mashariki( ingekuwa vyema masuala ya Afrika ya Mashariki yakawa kwenye mahusiano ya Kimataifa- hata hivyo, kuna azimio nakumbuka liliwahi kupitishwa na EAC kwamba kila nchi inapaswa kuwa na Wizara mahususi ya Afrika Mashariki).
3. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma
4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)- chini ya D&D, wizara hii ni kiungo muhimu katika ya serikali kuu na serikali za mitaa.
5. Wizara ya Mambo ya Nje(na Mahusiano ya Kimataifa)
6. Wizara ya Ulinzi( Na jeshi la Kujenga Taifa)
7. Wizara ya Uchumi na Fedha(na mipango)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
8. Wizara ya Mambo ya Ndani( Na usalama wa Raia)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
9. Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika( na Chakula)- Hapa napendekeza Wizara mbili ziunganishwe.
10. Wizara ya Maliasili na Utalii( pamoja na kuwa ni rahisi kushawishika kuunganisha mazingira hapa, lakini kwa unyeti wa sekta ya utalii katika uchumi wa taifa siku za usoni ni vyema majukumu yakaishia hapo tu).
11. Wizara ya Miundo Mbinu- hii itajumuisha pia masuala yote ya ujenzi wa barabara na mawasiliano, unaweza kushawishika kuingiza hapa pia nyumba na makazi lakini mzigo utakuwa mkubwa sana.
12. Wizara ya Maji, Nishati na Madini- hapa wizara mbili zimeunganishwa. Maji ni sekta ambayo ingeweza kuingia katika wizara kadhaa nyingine mathalani kilimo, maliasili ama ardhi lakini hapa inaweza kukaa vizuri zaidi.
13. Elimu na Teknolojia- hapa imeunganisha wizara mbili, ya elimu na ufundi stadi na ile ya elimu ya juu; ni vyema masuala yote ya elimu yakakaa mahali pamoja.
14. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Vijana na Watoto- hapa nimeunganisha Wizara moja pamoja na sekta ya vijana ambayo awali ilikuwa Wizara ya Kazi na ajira.
15. Wizara ya Afya(na ustawi wa jamii)- ni vyema kutakakari kuurudisha ustawi wa jamii kwenye wizara ya maendeleo ya jamii.
16. Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko
17. Wizara ya Ardhi, Makazi(Nyumba) na Mazingira- hapa nimeunganisha Wizara na Waziri mwingine ambaye alikuwa ofisi ya Makamu wa Rais.
18. Habari, Utamaduni na Michezo- Kuna hoja kwamba utamaduni ukae kwenye elimu; na habari iwe kitengo tu kama MAELEZO au IKULU na michezo iwekwe karibu na wizara yenye Vijana. Hata hivyo, kwa umuhimu wa Utamaduni kwa Taifa; na fursa ya Michezo kuwa sekta ya muhimu katika uchumi- haya mambo ni vyema yakapewa uzito unaostahili. Na ukishakuwa na wizara hiyo, ni rahisi kuunganisha na habari hapo hapo.
19. Kazi, (Ajira na Uwezeshaji)- ni rahisi kuiacha hii wizara ikawa ya masuala ya Kazi(Labour pekee) na masuala ya ajira(employment) ukayepeleka kwenye uchumi au ukayaacha kuwa mtambuka(cross cutting katika kila wizara). Lakini kwa hali ya uchumi wetu wa sasa wa kutegemea wageni na kuwaweka mstari wa mbele wageni- tunahaja ya kuwa na wizara ambao inalinga maslahi na kuendeleza maslahi. Kama Afrika Kusini walivyokuwa na sera/sheria ya ‘black empowerment”, hapa napo tunahitaji kwa muda kulipa kipaumbele suala la UWEZESHAJI. Wizara hii inaweza kuondolewa masuala ya uwezeshaji baadaye ikabaki na KAZI pekee.

Kwa mapendekezo haya:

Wizara ya Sheria na Katiba inafutwa badala yake majukumu yake ya kiutendaji yanapelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni sehemu ya Baraza la Mawaziri. Na majukumu ya Usimamizi wa Sheria yanabaki kwa Mahakama. Majukumu ya kusimamia HAKI, yanabaki chini ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi-Utawala Bora anafutwa- Majukumu ya kusimamia utawala bora kwa maana ya uongozi yanabaki wa Rais Mwenyewe. Kwa maana ya Kulinda utawala bora, yabaki kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Sekretariati ya Maadili ya Watumishi wa Umma; Masuala ya Usalama wa Taifa yanabaki kwa Rais Mwenyewe. Masuala ya TAKUKURU inabidi kubadili sheria kukifanya kuwa chombo huru zaidi baada ya kusimamiwa na Waziri kwa maelekezo ya Rais.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Bunge, anafutwa; masuala ya Bunge ashughulikie Waziri Mkuu mwenyewe ili kuongeza uwajibikaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Siasa na Uhusiano wa Jamii anafutwa- Wizara hii haikuwa na sababu yoyoye ya kuwepo, ilianzishwa kisiasa kwa lengo la kumpa nafasi Kingunge kuwa karibu na Rais, kuuingiza kwenye Baraza la Mawaziri na kupata fursa ya kuropoka hadharani masuala ya kisiasa na uhusiano wa kijamii. Kazi ambayo hata yenyewe ameshindwa kuifanya! Hivyo, anapaswa kuondoka yeye na wizara iliyoazishwa kwa ajili yake. Majukumu haya ya siasa na uhusiano na jamii ni mambo ya kawaida ya ofisi ya Rais hayahitaji kuundiwa Wizara.

Huu ndio muundo wa Baraza Jipya la Mawaziri 19 tu ninalopendekeza lijadiliwe. Katika hali hii, manaibu nao wanapaswa kupungua kabisa, na ikiwezekana baadhi ya Wizara zisiewe kabisa na manaibu. Kama Manaibu sio wajumbe wenye kura wa Baraza la Mawaziri, wanafanya nini? Kwa nini wasiwe under secretaries tu?

Haya ni maoni yangu binafsi, tujadili- tunataka Baraza la Mawaziri dogo na lenye ufanisi kiasi gani?
 
Wakati macho na masikio ya watanzania wengi ni kusubiri kwa hamu kuhusu “Nani na Nani’ watakuwepo kwenye baraza na watakuwa ‘wapi’; mjadala wa MUUNDO umetawaliwa zaidi na kutazama “sura”. Mjadala wa “watu’, MODS napendekeza uendelee katika ile thread ya “uchambuzi kuhusu baraza la mawaziri”; hii iachwe pekee kwa lengo la kujadili ‘masuala’ ya ukubwa wa baraza lenyewe na mpangilio wa wizara. Wakati “sura” ni suala la muhimu sana la kwanza kabisa kabla ya ‘mfumo’ mzima, ni muhimu pia tujadili muundo wa baraza kwa maana ya mpangilio wa wizara na idadi ya wizara. Sauti ya umma kupitia kwa wapinzani, asasi za kiraia, wasomi nk wakati wote zimekuwa ni ‘tunataka baraza dogo la mawaziri lakini lenye ufanisi’. Swali la kujiuliza- ni baraza dogo kiasi gani? Mwaka 2005 ‘war room’ ya CHADEMA tuliwahi kukaa chini na kuanza kutafakari- kama tungeshinda nchi na kuongoza dola- tungetekeleza vipi sera yetu ya kuwa na “mfumo mpya wa utawala” ambao pamoja na mambo mengine ungekuwa na ‘small but yet accountable and effective government’? Wakati huo tulitengeneza Muundo wa Baraza Dogo ambalo mawaziri walikuwa takribani 15 tu. Huku nilipo, nimeshindwa kuipata ile nyaraka ya ndani ya mapendekezo ya wakati huo. Lakini nimeona bado ni vyema nikachokoza mjadala huu kwa mawazo yangu binafsi.

Naanzia na dhana kwamba sikubaliani na muundo wetu wa sasa wa Baraza lenye Mawaziri takribani 29- hili ni kubwa sana. Hata Uingereza ambao wana idadi kubwa ya watu na fedha nyingi na ndio ambao wanachangia bajeti yetu kwa kiasi kikubwa ikiwemo bajeti ya mishahara tunayowalipa mawaziri wetu- wamejipangia kabisa wizara zisizidi 20. Kama Waziri mkuu anataka kuongeza ya 21 inabidi aombe kibali maalumu. Na wizara yoyote zaidi ya hapo basi waziri mkuu anaigharamia mwenyewe kwa fedha zake. Sisi sasa tunazo 29 na Jeshi la manaibu kibao. Kwa kauli ya Waziri Mkuu Pinda inaelekea JK atakubaliana na wazo la wapinzani na wananchi kwa ujumla la kupunguza baraza la mawaziri. Je, apunguze kwa kiasi gani? Huu ndio mjadala wa hapa-

Kwa maoni yangu- atoke toka Wizara 29 mpaka Wizara zisizozidi 10; kwa maneno mengine apunguze wizara takribani 10 katika hatua ya sasa. Afanye namna gani?

Kwanza aamue kabisa kwamba Yeye asiwe Waziri wa Wizara yoyote- huu muundo wa baadhi ya Wizara kuwa Ofisi ya Rais unamfanya Rais ajiingize katika kazi za Uwaziri bila sababu yoyote ya msingi. Rais yeye awe Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri tu na mwongozaji mkuu wa Wizara zote. Nakumbuka wakati wa Rais Mkapa alikuwa pia Waziri wa TAMISEMI, matokeo yake ilikuwa ni aibu ya moja kwa moja kwa Rais kwa kuwa alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2004! Sasa TAMISEMI ilikuwa kwa waziri mkuu lakini bado, kuna mawaziri waliokuwa katika ofisi ya Rais.

Pili, nashauri baadhi ya wizara ziunganishwe kama nitakavyopendekeza na baadhi ya Wizara kwa kweli zilikuwa hazistahili kuwa Wizara kabisa; labda ziwe idara tu katika wizara Fulani Fulani. Kwa ujumla sitapendekeza wizara ziitwejwe, lakini nitaunganisha zaidi yale majukumu ili kujua ni yapi waziri anayependekezwa atahusika nayo. Baada ya kukubaliana MAJUKUMU- ndio suala la JINA LA WIZARA linafuata halafu ndio JINA LA WAZIRI:

Mapendekezo yangu ya Wizara 19:

1. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano
2. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Afrika Mashariki( ingekuwa vyema masuala ya Afrika ya Mashariki yakawa kwenye mahusiano ya Kimataifa- hata hivyo, kuna azimio nakumbuka liliwahi kupitishwa na EAC kwamba kila nchi inapaswa kuwa na Wizara mahususi ya Afrika Mashariki).
3. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma
4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)- chini ya D&D, wizara hii ni kiungo muhimu katika ya serikali kuu na serikali za mitaa.
5. Wizara ya Mambo ya Nje(na Mahusiano ya Kimataifa)
6. Wizara ya Ulinzi( Na jeshi la Kujenga Taifa)
7. Wizara ya Uchumi na Fedha(na mipango)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
8. Wizara ya Mambo ya Ndani( Na usalama wa Raia)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
9. Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika( na Chakula)- Hapa napendekeza Wizara mbili ziunganishwe.
10. Wizara ya Maliasili na Utalii( pamoja na kuwa ni rahisi kushawishika kuunganisha mazingira hapa, lakini kwa unyeti wa sekta ya utalii katika uchumi wa taifa siku za usoni ni vyema majukumu yakaishia hapo tu).
11. Wizara ya Miundo Mbinu- hii itajumuisha pia masuala yote ya ujenzi wa barabara na mawasiliano, unaweza kushawishika kuingiza hapa pia nyumba na makazi lakini mzigo utakuwa mkubwa sana.
12. Wizara ya Maji, Nishati na Madini- hapa wizara mbili zimeunganishwa. Maji ni sekta ambayo ingeweza kuingia katika wizara kadhaa nyingine mathalani kilimo, maliasili ama ardhi lakini hapa inaweza kukaa vizuri zaidi.
13. Elimu na Teknolojia- hapa imeunganisha wizara mbili, ya elimu na ufundi stadi na ile ya elimu ya juu; ni vyema masuala yote ya elimu yakakaa mahali pamoja.
14. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Vijana na Watoto- hapa nimeunganisha Wizara moja pamoja na sekta ya vijana ambayo awali ilikuwa Wizara ya Kazi na ajira.
15. Wizara ya Afya(na ustawi wa jamii)- ni vyema kutakakari kuurudisha ustawi wa jamii kwenye wizara ya maendeleo ya jamii.
16. Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko
17. Wizara ya Ardhi, Makazi(Nyumba) na Mazingira- hapa nimeunganisha Wizara na Waziri mwingine ambaye alikuwa ofisi ya Makamu wa Rais.
18. Habari, Utamaduni na Michezo- Kuna hoja kwamba utamaduni ukae kwenye elimu; na habari iwe kitengo tu kama MAELEZO au IKULU na michezo iwekwe karibu na wizara yenye Vijana. Hata hivyo, kwa umuhimu wa Utamaduni kwa Taifa; na fursa ya Michezo kuwa sekta ya muhimu katika uchumi- haya mambo ni vyema yakapewa uzito unaostahili. Na ukishakuwa na wizara hiyo, ni rahisi kuunganisha na habari hapo hapo.
19. Kazi, (Ajira na Uwezeshaji)- ni rahisi kuiacha hii wizara ikawa ya masuala ya Kazi(Labour pekee) na masuala ya ajira(employment) ukayepeleka kwenye uchumi au ukayaacha kuwa mtambuka(cross cutting katika kila wizara). Lakini kwa hali ya uchumi wetu wa sasa wa kutegemea wageni na kuwaweka mstari wa mbele wageni- tunahaja ya kuwa na wizara ambao inalinga maslahi na kuendeleza maslahi. Kama Afrika Kusini walivyokuwa na sera/sheria ya ‘black empowerment”, hapa napo tunahitaji kwa muda kulipa kipaumbele suala la UWEZESHAJI. Wizara hii inaweza kuondolewa masuala ya uwezeshaji baadaye ikabaki na KAZI pekee.

Kwa mapendekezo haya:

Wizara ya Sheria na Katiba inafutwa badala yake majukumu yake ya kiutendaji yanapelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni sehemu ya Baraza la Mawaziri. Na majukumu ya Usimamizi wa Sheria yanabaki kwa Mahakama. Majukumu ya kusimamia HAKI, yanabaki chini ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi-Utawala Bora anafutwa- Majukumu ya kusimamia utawala bora kwa maana ya uongozi yanabaki wa Rais Mwenyewe. Kwa maana ya Kulinda utawala bora, yabaki kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Sekretariati ya Maadili ya Watumishi wa Umma; Masuala ya Usalama wa Taifa yanabaki kwa Rais Mwenyewe. Masuala ya TAKUKURU inabidi kubadili sheria kukifanya kuwa chombo huru zaidi baada ya kusimamiwa na Waziri kwa maelekezo ya Rais.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Bunge, anafutwa; masuala ya Bunge ashughulikie Waziri Mkuu mwenyewe ili kuongeza uwajibikaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Siasa na Uhusiano wa Jamii anafutwa- Wizara hii haikuwa na sababu yoyoye ya kuwepo, ilianzishwa kisiasa kwa lengo la kumpa nafasi Kingunge kuwa karibu na Rais, kuuingiza kwenye Baraza la Mawaziri na kupata fursa ya kuropoka hadharani masuala ya kisiasa na uhusiano wa kijamii. Kazi ambayo hata yenyewe ameshindwa kuifanya! Hivyo, anapaswa kuondoka yeye na wizara iliyoazishwa kwa ajili yake. Majukumu haya ya siasa na uhusiano na jamii ni mambo ya kawaida ya ofisi ya Rais hayahitaji kuundiwa Wizara.

Huu ndio muundo wa Baraza Jipya la Mawaziri 19 tu ninalopendekeza lijadiliwe. Katika hali hii, manaibu nao wanapaswa kupungua kabisa, na ikiwezekana baadhi ya Wizara zisiewe kabisa na manaibu. Kama Manaibu sio wajumbe wenye kura wa Baraza la Mawaziri, wanafanya nini? Kwa nini wasiwe under secretaries tu?

Haya ni maoni yangu binafsi, tujadili- tunataka Baraza la Mawaziri dogo na lenye ufanisi kiasi gani?

Kumradhi kwa kosa la uchapaji. Nilimaanisha toka 29 mpaka 19 sio 10

JJ
 
John Mnyika,

Mulifanya kazi nzuri, nakubaliana na wewe kwa asilimia kama 70%, lakini asilimia 30% hapa...nitaijibu kwa kuweka mbadala wake....

Mapendekezo yangu ni Haya

ORGANIZATION OF THE GOVERNMENT OF THE REPUBLIC OF TANZANIA

-Ofisi ya Rais
-Ofisi ya Makamu wa Rais
-Ofisi ya Waziri Mkuu


-Wizara ya TAMISEMI ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu
-Wizara ya Fedha
-Wizara ya Mipango na Uwezeshaji [Planning and National Development]
-Wizara ya Afya
-Wizara ya Uchukuzi, barabara na Ujenzi
-Wizara ya Elimu na Ufundi
-Wizara ya Elimu ya Juu, Science na Technologia
-Wizara ya Kilimo
-Wizara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi (Livestock and fisheries development)
-Wizara ya Mambo ya Nje
-Wizara ya Regional Affairs (East Africa and SADC)
-Wizara ya Justice and Constitutional Affairs (ikumbukwe uendeshaji wa mahakama administratively uko hapa)
-Wizara ya Jinsia, Michezo, Utamaduni na Ustawi wa Jamii
-Wizara ya Habari na Mawasiliano (Information anc Communications)
-Wizara ya Nishati na Madini
-Wizara ya Utalii na Wanyama Pori
-Wizara ya Maji na Umwagiliaji (Water and Irigation)
-Wizara ya Ushirika, Biashara na Masoko (co-operatives, industry and trade)
-Wizara ya Mali asili na Mazingira (Natural resource and Environment)
-Wizara ya Ardhi na Nyumba
-Wizara ya Kazi na Ajira (Labour and Human Resources Development)​
-Mwanasheria Mkuu [State Law Office)
-Mahakama (Judiciary)
-Tume ya Uchaguzi [National Electrol Commission]
-Tume ya Haki za Binadamu
-Tume ya maadili ya viongozi na utawala bora [commission for national ethics and good governance]
-Tume ya Utumishi [comming soon to Tanzania]
-Mdhibiti mkuu wa Hesabu za Serikali [National Audit General Office]
-Bunge la Jamhuri [National Assembly]
-Taasisi ya PCCB


Maelezo ya Ziada
-Ustawi wa Jamii umepelekwa kwenye gender, sports, cultural and social affairs
-Mawasiliano imeondolewa kwenye miundo mbinu kwa kuwa kwa mfumo wa sasa haitendewi haki, information [maelezo] imeunganishwa na mawasiliano kuunda wizara.
-Hakuna waziri utawala bora, bali kuna tume ya maadili na utawala bora
-Hakuna waziri anayehusika na Utumishi, kwani kutaundwa tume ya utumishi wa umma.
-Wizara ya Maji, imewekewe na Umwagiliaji
-Wizara ya Kilimo ni wizara likubwa mno limebaki lenyewe
-Mifugo imeongezewa Uvuvi kwa ajili ya ku-take advantage ya mali asili hii tunayoichezea.
-Utalii na Wanyama Pori [Tourism and Wildlife Development], Mali asili sio mahali pake.. Utalii ili upate msukumo... ukiangalia vizuri uvuvi umeondolewa hapa.
-Mali asili sasa iko na Mazingira... in short... unatakiwa kumtoa Mh. Mark Mwandosya kutoka kwenye makamu wa raisi umpe mazingira na mali asili.

Niko tayari sasa kuchukua maswali yenu.
 
Wakati macho na masikio ya watanzania wengi ni kusubiri kwa hamu kuhusu “Nani na Nani’ watakuwepo kwenye baraza na watakuwa ‘wapi’; mjadala wa MUUNDO umetawaliwa zaidi na kutazama “sura”. Mjadala wa “watu’, MODS napendekeza uendelee katika ile thread ya “uchambuzi kuhusu baraza la mawaziri”; hii iachwe pekee kwa lengo la kujadili ‘masuala’ ya ukubwa wa baraza lenyewe na mpangilio wa wizara. Wakati “sura” ni suala la muhimu sana la kwanza kabisa kabla ya ‘mfumo’ mzima, ni muhimu pia tujadili muundo wa baraza kwa maana ya mpangilio wa wizara na idadi ya wizara. Sauti ya umma kupitia kwa wapinzani, asasi za kiraia, wasomi nk wakati wote zimekuwa ni ‘tunataka baraza dogo la mawaziri lakini lenye ufanisi’. Swali la kujiuliza- ni baraza dogo kiasi gani? Mwaka 2005 ‘war room’ ya CHADEMA tuliwahi kukaa chini na kuanza kutafakari- kama tungeshinda nchi na kuongoza dola- tungetekeleza vipi sera yetu ya kuwa na “mfumo mpya wa utawala” ambao pamoja na mambo mengine ungekuwa na ‘small but yet accountable and effective government’? Wakati huo tulitengeneza Muundo wa Baraza Dogo ambalo mawaziri walikuwa takribani 15 tu. Huku nilipo, nimeshindwa kuipata ile nyaraka ya ndani ya mapendekezo ya wakati huo. Lakini nimeona bado ni vyema nikachokoza mjadala huu kwa mawazo yangu binafsi.

Naanzia na dhana kwamba sikubaliani na muundo wetu wa sasa wa Baraza lenye Mawaziri takribani 29- hili ni kubwa sana. Hata Uingereza ambao wana idadi kubwa ya watu na fedha nyingi na ndio ambao wanachangia bajeti yetu kwa kiasi kikubwa ikiwemo bajeti ya mishahara tunayowalipa mawaziri wetu- wamejipangia kabisa wizara zisizidi 20. Kama Waziri mkuu anataka kuongeza ya 21 inabidi aombe kibali maalumu. Na wizara yoyote zaidi ya hapo basi waziri mkuu anaigharamia mwenyewe kwa fedha zake. Sisi sasa tunazo 29 na Jeshi la manaibu kibao. Kwa kauli ya Waziri Mkuu Pinda inaelekea JK atakubaliana na wazo la wapinzani na wananchi kwa ujumla la kupunguza baraza la mawaziri. Je, apunguze kwa kiasi gani? Huu ndio mjadala wa hapa-

Kwa maoni yangu- atoke toka Wizara 29 mpaka Wizara zisizozidi 10; kwa maneno mengine apunguze wizara takribani 10 katika hatua ya sasa. Afanye namna gani?

Kwanza aamue kabisa kwamba Yeye asiwe Waziri wa Wizara yoyote- huu muundo wa baadhi ya Wizara kuwa Ofisi ya Rais unamfanya Rais ajiingize katika kazi za Uwaziri bila sababu yoyote ya msingi. Rais yeye awe Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri tu na mwongozaji mkuu wa Wizara zote. Nakumbuka wakati wa Rais Mkapa alikuwa pia Waziri wa TAMISEMI, matokeo yake ilikuwa ni aibu ya moja kwa moja kwa Rais kwa kuwa alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2004! Sasa TAMISEMI ilikuwa kwa waziri mkuu lakini bado, kuna mawaziri waliokuwa katika ofisi ya Rais.

Pili, nashauri baadhi ya wizara ziunganishwe kama nitakavyopendekeza na baadhi ya Wizara kwa kweli zilikuwa hazistahili kuwa Wizara kabisa; labda ziwe idara tu katika wizara Fulani Fulani. Kwa ujumla sitapendekeza wizara ziitwejwe, lakini nitaunganisha zaidi yale majukumu ili kujua ni yapi waziri anayependekezwa atahusika nayo. Baada ya kukubaliana MAJUKUMU- ndio suala la JINA LA WIZARA linafuata halafu ndio JINA LA WAZIRI:

Mapendekezo yangu ya Wizara 19:

1. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano
2. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Afrika Mashariki( ingekuwa vyema masuala ya Afrika ya Mashariki yakawa kwenye mahusiano ya Kimataifa- hata hivyo, kuna azimio nakumbuka liliwahi kupitishwa na EAC kwamba kila nchi inapaswa kuwa na Wizara mahususi ya Afrika Mashariki).
3. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma
4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)- chini ya D&D, wizara hii ni kiungo muhimu katika ya serikali kuu na serikali za mitaa.
5. Wizara ya Mambo ya Nje(na Mahusiano ya Kimataifa)
6. Wizara ya Ulinzi( Na jeshi la Kujenga Taifa)
7. Wizara ya Uchumi na Fedha(na mipango)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
8. Wizara ya Mambo ya Ndani( Na usalama wa Raia)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
9. Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika( na Chakula)- Hapa napendekeza Wizara mbili ziunganishwe.
10. Wizara ya Maliasili na Utalii( pamoja na kuwa ni rahisi kushawishika kuunganisha mazingira hapa, lakini kwa unyeti wa sekta ya utalii katika uchumi wa taifa siku za usoni ni vyema majukumu yakaishia hapo tu).
11. Wizara ya Miundo Mbinu- hii itajumuisha pia masuala yote ya ujenzi wa barabara na mawasiliano, unaweza kushawishika kuingiza hapa pia nyumba na makazi lakini mzigo utakuwa mkubwa sana.
12. Wizara ya Maji, Nishati na Madini- hapa wizara mbili zimeunganishwa. Maji ni sekta ambayo ingeweza kuingia katika wizara kadhaa nyingine mathalani kilimo, maliasili ama ardhi lakini hapa inaweza kukaa vizuri zaidi.
13. Elimu na Teknolojia- hapa imeunganisha wizara mbili, ya elimu na ufundi stadi na ile ya elimu ya juu; ni vyema masuala yote ya elimu yakakaa mahali pamoja.
14. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Vijana na Watoto- hapa nimeunganisha Wizara moja pamoja na sekta ya vijana ambayo awali ilikuwa Wizara ya Kazi na ajira.
15. Wizara ya Afya(na ustawi wa jamii)- ni vyema kutakakari kuurudisha ustawi wa jamii kwenye wizara ya maendeleo ya jamii.
16. Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko
17. Wizara ya Ardhi, Makazi(Nyumba) na Mazingira- hapa nimeunganisha Wizara na Waziri mwingine ambaye alikuwa ofisi ya Makamu wa Rais.
18. Habari, Utamaduni na Michezo- Kuna hoja kwamba utamaduni ukae kwenye elimu; na habari iwe kitengo tu kama MAELEZO au IKULU na michezo iwekwe karibu na wizara yenye Vijana. Hata hivyo, kwa umuhimu wa Utamaduni kwa Taifa; na fursa ya Michezo kuwa sekta ya muhimu katika uchumi- haya mambo ni vyema yakapewa uzito unaostahili. Na ukishakuwa na wizara hiyo, ni rahisi kuunganisha na habari hapo hapo.
19. Kazi, (Ajira na Uwezeshaji)- ni rahisi kuiacha hii wizara ikawa ya masuala ya Kazi(Labour pekee) na masuala ya ajira(employment) ukayepeleka kwenye uchumi au ukayaacha kuwa mtambuka(cross cutting katika kila wizara). Lakini kwa hali ya uchumi wetu wa sasa wa kutegemea wageni na kuwaweka mstari wa mbele wageni- tunahaja ya kuwa na wizara ambao inalinga maslahi na kuendeleza maslahi. Kama Afrika Kusini walivyokuwa na sera/sheria ya ‘black empowerment”, hapa napo tunahitaji kwa muda kulipa kipaumbele suala la UWEZESHAJI. Wizara hii inaweza kuondolewa masuala ya uwezeshaji baadaye ikabaki na KAZI pekee.

Kwa mapendekezo haya:

Wizara ya Sheria na Katiba inafutwa badala yake majukumu yake ya kiutendaji yanapelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni sehemu ya Baraza la Mawaziri. Na majukumu ya Usimamizi wa Sheria yanabaki kwa Mahakama. Majukumu ya kusimamia HAKI, yanabaki chini ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi-Utawala Bora anafutwa- Majukumu ya kusimamia utawala bora kwa maana ya uongozi yanabaki wa Rais Mwenyewe. Kwa maana ya Kulinda utawala bora, yabaki kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Sekretariati ya Maadili ya Watumishi wa Umma; Masuala ya Usalama wa Taifa yanabaki kwa Rais Mwenyewe. Masuala ya TAKUKURU inabidi kubadili sheria kukifanya kuwa chombo huru zaidi baada ya kusimamiwa na Waziri kwa maelekezo ya Rais.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Bunge, anafutwa; masuala ya Bunge ashughulikie Waziri Mkuu mwenyewe ili kuongeza uwajibikaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Siasa na Uhusiano wa Jamii anafutwa- Wizara hii haikuwa na sababu yoyoye ya kuwepo, ilianzishwa kisiasa kwa lengo la kumpa nafasi Kingunge kuwa karibu na Rais, kuuingiza kwenye Baraza la Mawaziri na kupata fursa ya kuropoka hadharani masuala ya kisiasa na uhusiano wa kijamii. Kazi ambayo hata yenyewe ameshindwa kuifanya! Hivyo, anapaswa kuondoka yeye na wizara iliyoazishwa kwa ajili yake. Majukumu haya ya siasa na uhusiano na jamii ni mambo ya kawaida ya ofisi ya Rais hayahitaji kuundiwa Wizara.

Huu ndio muundo wa Baraza Jipya la Mawaziri 19 tu ninalopendekeza lijadiliwe. Katika hali hii, manaibu nao wanapaswa kupungua kabisa, na ikiwezekana baadhi ya Wizara zisiewe kabisa na manaibu. Kama Manaibu sio wajumbe wenye kura wa Baraza la Mawaziri, wanafanya nini? Kwa nini wasiwe under secretaries tu?

Haya ni maoni yangu binafsi, tujadili- tunataka Baraza la Mawaziri dogo na lenye ufanisi kiasi gani?

John,
Hivi unataka kusema Rais aunde wizara kwa kufuata manifesto ya CHADEMA na wala siyo yale ambayo anataka kuyatelekeza kwa mujibu ya manifesto ya Chama chake?
Tafadhali naomba ufafanuzi.
 
Wakati macho na masikio ya watanzania wengi ni kusubiri kwa hamu kuhusu “Nani na Nani’ watakuwepo kwenye baraza na watakuwa ‘wapi’; mjadala wa MUUNDO umetawaliwa zaidi na kutazama “sura”. Mjadala wa “watu’, MODS napendekeza uendelee katika ile thread ya “uchambuzi kuhusu baraza la mawaziri”; hii iachwe pekee kwa lengo la kujadili ‘masuala’ ya ukubwa wa baraza lenyewe na mpangilio wa wizara. Wakati “sura” ni suala la muhimu sana la kwanza kabisa kabla ya ‘mfumo’ mzima, ni muhimu pia tujadili muundo wa baraza kwa maana ya mpangilio wa wizara na idadi ya wizara. Sauti ya umma kupitia kwa wapinzani, asasi za kiraia, wasomi nk wakati wote zimekuwa ni ‘tunataka baraza dogo la mawaziri lakini lenye ufanisi’. Swali la kujiuliza- ni baraza dogo kiasi gani? Mwaka 2005 ‘war room’ ya CHADEMA tuliwahi kukaa chini na kuanza kutafakari- kama tungeshinda nchi na kuongoza dola- tungetekeleza vipi sera yetu ya kuwa na “mfumo mpya wa utawala” ambao pamoja na mambo mengine ungekuwa na ‘small but yet accountable and effective government’? Wakati huo tulitengeneza Muundo wa Baraza Dogo ambalo mawaziri walikuwa takribani 15 tu. Huku nilipo, nimeshindwa kuipata ile nyaraka ya ndani ya mapendekezo ya wakati huo. Lakini nimeona bado ni vyema nikachokoza mjadala huu kwa mawazo yangu binafsi.

Naanzia na dhana kwamba sikubaliani na muundo wetu wa sasa wa Baraza lenye Mawaziri takribani 29- hili ni kubwa sana. Hata Uingereza ambao wana idadi kubwa ya watu na fedha nyingi na ndio ambao wanachangia bajeti yetu kwa kiasi kikubwa ikiwemo bajeti ya mishahara tunayowalipa mawaziri wetu- wamejipangia kabisa wizara zisizidi 20. Kama Waziri mkuu anataka kuongeza ya 21 inabidi aombe kibali maalumu. Na wizara yoyote zaidi ya hapo basi waziri mkuu anaigharamia mwenyewe kwa fedha zake. Sisi sasa tunazo 29 na Jeshi la manaibu kibao. Kwa kauli ya Waziri Mkuu Pinda inaelekea JK atakubaliana na wazo la wapinzani na wananchi kwa ujumla la kupunguza baraza la mawaziri. Je, apunguze kwa kiasi gani? Huu ndio mjadala wa hapa-

Kwa maoni yangu- atoke toka Wizara 29 mpaka Wizara zisizozidi 10; kwa maneno mengine apunguze wizara takribani 10 katika hatua ya sasa. Afanye namna gani?

Kwanza aamue kabisa kwamba Yeye asiwe Waziri wa Wizara yoyote- huu muundo wa baadhi ya Wizara kuwa Ofisi ya Rais unamfanya Rais ajiingize katika kazi za Uwaziri bila sababu yoyote ya msingi. Rais yeye awe Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri tu na mwongozaji mkuu wa Wizara zote. Nakumbuka wakati wa Rais Mkapa alikuwa pia Waziri wa TAMISEMI, matokeo yake ilikuwa ni aibu ya moja kwa moja kwa Rais kwa kuwa alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2004! Sasa TAMISEMI ilikuwa kwa waziri mkuu lakini bado, kuna mawaziri waliokuwa katika ofisi ya Rais.

Pili, nashauri baadhi ya wizara ziunganishwe kama nitakavyopendekeza na baadhi ya Wizara kwa kweli zilikuwa hazistahili kuwa Wizara kabisa; labda ziwe idara tu katika wizara Fulani Fulani. Kwa ujumla sitapendekeza wizara ziitwejwe, lakini nitaunganisha zaidi yale majukumu ili kujua ni yapi waziri anayependekezwa atahusika nayo. Baada ya kukubaliana MAJUKUMU- ndio suala la JINA LA WIZARA linafuata halafu ndio JINA LA WAZIRI:

Mapendekezo yangu ya Wizara 19:

1. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano
2. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Afrika Mashariki( ingekuwa vyema masuala ya Afrika ya Mashariki yakawa kwenye mahusiano ya Kimataifa- hata hivyo, kuna azimio nakumbuka liliwahi kupitishwa na EAC kwamba kila nchi inapaswa kuwa na Wizara mahususi ya Afrika Mashariki).
3. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma
4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)- chini ya D&D, wizara hii ni kiungo muhimu katika ya serikali kuu na serikali za mitaa.
5. Wizara ya Mambo ya Nje(na Mahusiano ya Kimataifa)
6. Wizara ya Ulinzi( Na jeshi la Kujenga Taifa)
7. Wizara ya Uchumi na Fedha(na mipango)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
8. Wizara ya Mambo ya Ndani( Na usalama wa Raia)- hapa napendekeza wizara mbili ziunganishwe
9. Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika( na Chakula)- Hapa napendekeza Wizara mbili ziunganishwe.
10. Wizara ya Maliasili na Utalii( pamoja na kuwa ni rahisi kushawishika kuunganisha mazingira hapa, lakini kwa unyeti wa sekta ya utalii katika uchumi wa taifa siku za usoni ni vyema majukumu yakaishia hapo tu).
11. Wizara ya Miundo Mbinu- hii itajumuisha pia masuala yote ya ujenzi wa barabara na mawasiliano, unaweza kushawishika kuingiza hapa pia nyumba na makazi lakini mzigo utakuwa mkubwa sana.
12. Wizara ya Maji, Nishati na Madini- hapa wizara mbili zimeunganishwa. Maji ni sekta ambayo ingeweza kuingia katika wizara kadhaa nyingine mathalani kilimo, maliasili ama ardhi lakini hapa inaweza kukaa vizuri zaidi.
13. Elimu na Teknolojia- hapa imeunganisha wizara mbili, ya elimu na ufundi stadi na ile ya elimu ya juu; ni vyema masuala yote ya elimu yakakaa mahali pamoja.
14. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Vijana na Watoto- hapa nimeunganisha Wizara moja pamoja na sekta ya vijana ambayo awali ilikuwa Wizara ya Kazi na ajira.
15. Wizara ya Afya(na ustawi wa jamii)- ni vyema kutakakari kuurudisha ustawi wa jamii kwenye wizara ya maendeleo ya jamii.
16. Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko
17. Wizara ya Ardhi, Makazi(Nyumba) na Mazingira- hapa nimeunganisha Wizara na Waziri mwingine ambaye alikuwa ofisi ya Makamu wa Rais.
18. Habari, Utamaduni na Michezo- Kuna hoja kwamba utamaduni ukae kwenye elimu; na habari iwe kitengo tu kama MAELEZO au IKULU na michezo iwekwe karibu na wizara yenye Vijana. Hata hivyo, kwa umuhimu wa Utamaduni kwa Taifa; na fursa ya Michezo kuwa sekta ya muhimu katika uchumi- haya mambo ni vyema yakapewa uzito unaostahili. Na ukishakuwa na wizara hiyo, ni rahisi kuunganisha na habari hapo hapo.
19. Kazi, (Ajira na Uwezeshaji)- ni rahisi kuiacha hii wizara ikawa ya masuala ya Kazi(Labour pekee) na masuala ya ajira(employment) ukayepeleka kwenye uchumi au ukayaacha kuwa mtambuka(cross cutting katika kila wizara). Lakini kwa hali ya uchumi wetu wa sasa wa kutegemea wageni na kuwaweka mstari wa mbele wageni- tunahaja ya kuwa na wizara ambao inalinga maslahi na kuendeleza maslahi. Kama Afrika Kusini walivyokuwa na sera/sheria ya ‘black empowerment”, hapa napo tunahitaji kwa muda kulipa kipaumbele suala la UWEZESHAJI. Wizara hii inaweza kuondolewa masuala ya uwezeshaji baadaye ikabaki na KAZI pekee.

Kwa mapendekezo haya:

Wizara ya Sheria na Katiba inafutwa badala yake majukumu yake ya kiutendaji yanapelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni sehemu ya Baraza la Mawaziri. Na majukumu ya Usimamizi wa Sheria yanabaki kwa Mahakama. Majukumu ya kusimamia HAKI, yanabaki chini ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi-Utawala Bora anafutwa- Majukumu ya kusimamia utawala bora kwa maana ya uongozi yanabaki wa Rais Mwenyewe. Kwa maana ya Kulinda utawala bora, yabaki kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Sekretariati ya Maadili ya Watumishi wa Umma; Masuala ya Usalama wa Taifa yanabaki kwa Rais Mwenyewe. Masuala ya TAKUKURU inabidi kubadili sheria kukifanya kuwa chombo huru zaidi baada ya kusimamiwa na Waziri kwa maelekezo ya Rais.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Bunge, anafutwa; masuala ya Bunge ashughulikie Waziri Mkuu mwenyewe ili kuongeza uwajibikaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Siasa na Uhusiano wa Jamii anafutwa- Wizara hii haikuwa na sababu yoyoye ya kuwepo, ilianzishwa kisiasa kwa lengo la kumpa nafasi Kingunge kuwa karibu na Rais, kuuingiza kwenye Baraza la Mawaziri na kupata fursa ya kuropoka hadharani masuala ya kisiasa na uhusiano wa kijamii. Kazi ambayo hata yenyewe ameshindwa kuifanya! Hivyo, anapaswa kuondoka yeye na wizara iliyoazishwa kwa ajili yake. Majukumu haya ya siasa na uhusiano na jamii ni mambo ya kawaida ya ofisi ya Rais hayahitaji kuundiwa Wizara.

Huu ndio muundo wa Baraza Jipya la Mawaziri 19 tu ninalopendekeza lijadiliwe. Katika hali hii, manaibu nao wanapaswa kupungua kabisa, na ikiwezekana baadhi ya Wizara zisiewe kabisa na manaibu. Kama Manaibu sio wajumbe wenye kura wa Baraza la Mawaziri, wanafanya nini? Kwa nini wasiwe under secretaries tu?

Haya ni maoni yangu binafsi, tujadili- tunataka Baraza la Mawaziri dogo na lenye ufanisi kiasi gani?


John I think hii imetulia sana...
 
John I think hii imetulia sana...

Mzee angalia version yangu kwanza mkuu!!! then utaona imeenda shule zaidi!!! kwi kwi kwi...

tatizo la baraza la JK lililopita ni mrundikano wa Manaibu... well kitu kizuri lakini wengi walikuwa vijana, yaani waliwekwa kwa ajili ya kusoma mazingira... sasa hivi wengi wata-be-promoted na wazee wataenda home...
 
Mimi napendekeza kusiwe na wizara hata moja, mbadala kuwe na Raisi na makatibu wa kila idara itayoona panabidi pashughulukiwe, mfano,

Katibu wa fedha, katibu wa mambo ya nje, katibu wa.....

Hii itaondoa matatizo ya uwajibikaji, na raisi ndie muwajibikaji mkuu kwa makatibu wake na itakuwa hakuna kulindana na itakuwa kila katibu anateuliwa na kuajiriwa kutokana na elimu na uzoefu wa fani yake, mfano katibu wa afya, lazima awe kweli mtu wa afya na aonyeshe kisha fanya nini kwa uzoefu wake.

Na kila katibu lazima apitishwe na kuchambuliwa bungeni kabla hajaaapishwa.

Tuondokanae na mfumo wa kifalme, wa kuwa na mawaziri.
 
Baraza dogo kabisa la mawaziri ninaloliona hapa halipungui mawaziri 40, kama sio 50, nusu wakiwa wakristo na nusu wakiwa waislamu. Mkumbuke kuwa karibu kila mko "lazima" upate mawaziri 2, na walau mmoja au wawili kutoka Zanzibar. Ni wazi kuwa baraza dogo tunalotegemea halina udogo wowote, na sijui baraza dogo analosema Pinda litakuwa na udogo kiasi gani. Lingekuwa dogo kwa kuwa na mawaziri 20 ningeliita dogo, but i do not see that coming, au nae Mheshimiwa Pinda ameanza porojo!!
 
mimi ninapendekeza wizara kumi na tano za msingi na majina yake.
wizara zenyewe ziwe kama hivi ifuatavyo:

1-wizara ya uchumi na mapato ya taifa
2-wizara ya rasilimali na maliasili
3-wizara ya demokrasia na muungano
4-wizara ya sheria na haki

5-wizara ya ulinzi
6-wizara ya miundo mbinu
7-wizara ya uwezeshaji na uwekezaji
8-wizara ya chakula na afya
9-wizara ya mambo ya kimataifa
10-wizara ya mafuta na umeme
11-wizara ya elimu na tekinolojia
12-wizara ya utamaduni na michezo
13-wizara ya kazi na maendeleo ya vijana
14-wizara ya jamii na watoto
15-wizara ya mambo ya ndani
 
mimi ninapendekeza wizara kumi na tano za msingi na majina yake.
wizara zenyewe ziwe kama hivi ifuatavyo:

1-wizara ya uchumi na mapato ya taifa
2-wizara ya rasilimali na maliasili
3-wizara ya demokrasia na muungano
4-wizara ya sheria na haki

5-wizara ya ulinzi
6-wizara ya miundo mbinu
7-wizara ya uwezeshaji na uwekezaji
8-wizara ya chakula na afya
9-wizara ya mambo ya kimataifa
10-wizara ya mafuta na umeme
11-wizara ya elimu na tekinolojia
12-wizara ya utamaduni na michezo
13-wizara ya kazi na maendeleo ya vijana
14-wizara ya jamii na watoto
15-wizara ya mambo ya ndani

Gamba la Nyoka,

tunaomba ufafanuzi zaidi,,, maana isijekuwa na strategy ya kuondoa shughuli zingine za serikali.
1. Ardhi inaingia wapi?
2. Utalii [Toursim] unaingia wapi ?
3. Kilimo kinaingia wapi?
4. Je madini yanaingia kwenye mali asili?
5. Kama mafuta, je Gas?
6. Usalama wa Raia inaingia wapi,
7. Uhamiaji inaingia wapi?

Haya maswali lazima ya kukomaze kwamba hiyo kazi sio rahisi sana...
 
Gamba la Nyoka,

tunaomba ufafanuzi zaidi,,, maana isijekuwa na strategy ya kuondoa shughuli zingine za serikali.
1. Ardhi inaingia wapi?
2. Utalii [Toursim] unaingia wapi ?
3. Kilimo kinaingia wapi?
4. Je madini yanaingia kwenye mali asili?
5. Kama mafuta, je Gas?
6. Usalama wa Raia inaingia wapi,
7. Uhamiaji inaingia wapi?

Haya maswali lazima ya kukomaze kwamba hiyo kazi sio rahisi sana...

Kasheshe
Ardhi inaingia katika- wizara ya Rasilimali na maliasili

utalii utaingia katika -wizara ya uchumi na mapato ya Taifa
Madini yataingia katika-wizara ya rasilimali na maliasili
mafuta yataingia katika-wizara ya Mafuta na umeme
Usalama wa raia utaingia katika -wizara ya mambo ya ndani
Uhamiaji utaingia katika wizara ya mambo ya ndani.

Kilimo kitaingia katika wizara mbili
Wizara ya uchumi na mapato ya Taifa ,kwa yale mazao yote yasiyo ya chakula.
na kwa mazao yote ya chakula yataingia katika-Wizara ya Chakula na afya.
 
Kasheshe
Ardhi inaingia katika- wizara ya Rasilimali na maliasili

utalii utaingia katika -wizara ya uchumi na mapato ya Taifa
Madini yataingia katika-wizara ya rasilimali na maliasili
mafuta yataingia katika-wizara ya Mafuta na umeme
Usalama wa raia utaingia katika -wizara ya mambo ya ndani
Uhamiaji utaingia katika wizara ya mambo ya ndani.

Kilimo kitaingia katika wizara mbili
Wizara ya uchumi na mapato ya Taifa ,kwa yale mazao yote yasiyo ya chakula.
na kwa mazao yote ya chakula yataingia katika-Wizara ya Chakula na afya.

Ahsante mkuu lakini; nishitushwa na watanzania wanavyotaka kuendesha nchi kina-dharia...I assure you huu mpangilio wako,,, serikali yako isingedumu hata kwa miezi mitatu!!!

Tuna tofauti ya mazinginra yanayolazimisha tushindwe ku-consolidate wizara.

-Elimu ya Watendaji na Wananchi wetu.
-Miundombinu . Barabara, Viwanja vya ndege, Reli n.k.
-Communications systems - Internet, (conferencing video.audio)

Haya ndiyo yanayosabisha uhitaji mawaziri wengi kwa uangalizi wa karibu wa shughuli za serikali maana kuwafikia stakeholders ni ngumu...

Kwa mfano... unless waziri asisafiri hata siku moja hizo wizara zako... waziri anaweza kudanganywa tu na wataalamu wake... hali ya kuwa kwenye vijijini labda mambo ni ya ajabu sana....au aende vijiji vichache ndani ya mwaka alafu akirudi wizarani mambo yamelala.

Please compare apple to apple... and not orange to apple.
 
Ahsante mkuu lakini; nishitushwa na watanzania wanavyotaka kuendesha nchi kina-dharia...I assure you huu mpangilio wako,,, serikali yako isingedumu hata kwa miezi mitatu!!!

Tuna tofauti ya mazinginra yanayolazimisha tushindwe ku-consolidate wizara.

-Elimu ya Watendaji na Wananchi wetu.
-Miundombinu . Barabara, Viwanja vya ndege, Reli n.k.
-Communications systems - Internet, (conferencing video.audio)

Haya ndiyo yanayosabisha uhitaji mawaziri wengi kwa uangalizi wa karibu wa shughuli za serikali maana kuwafikia stakeholders ni ngumu...



Kwa mfano... unless waziri asisafiri hata siku moja hizo wizara zako... waziri anaweza kudanganywa tu na wataalamu wake... hali ya kuwa kwenye vijijini labda mambo ni ya ajabu sana....au aende vijiji vichache ndani ya mwaka alafu akirudi wizarani mambo yamelala.

Please compare apple to apple... and not orange to apple.

Yaani kwa mpangilio wangu huo maana yake kutakuwa na mawaziri 15 na manaibu waziri 15, kwa maoni yangu ni kwamba litakuwa baraza la mawaziri la watu 32 bimaana plus waziri mkuu na raisi, kwa nchi kama ya kwetu tunayotakiwa "kuprioritize" mambo nadhani hilo linatosha.tukilifanya kubwa, gharama za uendeshaji zitakuwa kubwa na itafikia mahali waziri mmoja anafanya kazi ambayo ingeweza kufanywa na waziri mwingine.
 
Yohana,

Tuangalie Wamarekani, mfumo wao ukoje wa Cabinet? Je udogo wao ni tija au tutadai wao matajiri? je ni lazima kila kitu kiundiwe wizara? hatuwezi kuwa na idara zinazoongozwa na makamishna ambao si wanasiasa?

Nafikiri tatizo letu limekuwa ni huku kudai tunataka kuleta uwiano wa Wateule kufuatilia misingi ya kidini, jinsia, umri na kimikoa (kikabila). Sisi kama Taifa tumepevuka sana na hakuna sababu yeyote kuunda baraza la mawaziri kufuatia hisia kama hizo. Kuendelea kutumia hivo vigezo, ni kukomaza mgawanyiko huo.

Kinachohitajika ni kuunda Baraza dogo ambalo litakuwa makini, fanisi, wajibikaji na adilifu. Unapokuwa na safu kubwa kama iliyokuwepo, kunatoa mwanya wa ubangaizaji na hata kulea mawazo ya hujuma.

Kila wizara iwe na naibu mmoja na ikiwezekana, cheo hiki kisiwe cha kisiasa tena. Nafikiri jambo hili litafanikiwa pindi mabadiliko ya katiba yakifanyika na kuondoa Uwaziri kutoka kwenye Ubunge. Manaibu wasipewe marupurupu sawa na Mawaziri. Manaibu pamoja na makatibu wakuu wawe ni wataalamu wa wizara wanazowekwa na si wababaishaji wa kupiga domo kama Nchimbi (samahani nimeleta jina kama mfano.)

Tukiangalia Wamarekani, baraza lao la Mawaziri huundwa kwa wizara zifuatazo ambazo ni:
The Cabinet includes the Vice President and the heads of 15 executive departments-the Secretaries of Agriculture, Commerce, Defense, Education, Energy, Health and Human Services, Homeland Security, Housing and Urban Development, Interior, Labor, State, Transportation, Treasury, and Veterans Affairs, and the Attorney General. Under President George W. Bush, Cabinet-level rank also has been accorded to the Administrator, Environmental Protection Agency; Director, Office of Management and Budget; the Director, National Drug Control Policy; and the U.S. Trade Representative.
source:-http://www.whitehouse.gov/government/cabinet.html
 
Wizara kwa kweli ni sita tu ambazo zitakuwa na mawizara na maidara.
Hebu angalia:-
1-wizara ya uchumi rasilimali na mali ya asili (Idara- Ardhi ,mafuta umeme na yanayohusiana zinaingia hapwa)
2-wizara ya Ulinzi,(Idara -Sheria ,Mahakama ,Jeshi(bara,majini anga na polisi) na vyombo vyengine vya usalama )

3-wizara ya mambo ya ndani jamii na tekinolojia (Idara-Jamii,Usafiri anga bara maji, utamaduni,watoto ,vijana,wazee ,Michezo na zinazohusiana)
4-wizara ya kazi ( Idara -miundo mbinu uwezeshaji na uwekezaji na zinazohusiana)
5-wizara ya elimu na tekinolojia (Idara -mafuzo ya Msingi,Mafunzo ya Sekondari ,Vyuo na elimu ya nje scholarship)
6-wizara ya Chakula na mambo ya Kimataifa.(Idara- mambo nje ,misaada na mikopo)
Naona hii topiki imechelewa mwisho leo usiku ,kama watonyaji watawahi.
 
Wizara kwa kweli ni sita tu ambazo zitakuwa na mawizara na maidara.
Hebu angalia:-
1-wizara ya uchumi rasilimali na mali ya asili (Idara- Ardhi ,mafuta umeme na yanayohusiana zinaingia hapwa)
2-wizara ya sheria ,haki na ulinzi (Idara -Mahakama ,Jeshi ,Polisi na vyombo vyengine vya usalama )

3-wizara ya mambo ya ndani jamii na tekinolojia (Idara-Jamii utamaduni,watoto ,vijana,wazee ,Michezo na zinazohusiana)
4-wizara ya kazi ( Idara -miundo mbinu uwezeshaji na uwekezaji na zinazohusiana)
5-wizara ya elimu na tekinolojia (Idara -mafuzo ya Msingi,Mafunzo ya Sekondari ,Vyuo na elimu ya nje scholarship)
6-wizara ya Chakula na mambo ya Kimataifa.(Idara- mambo nje ,misaada na mikopo)
Naona hii topiki imechelewa mwisho leo usiku ,kama watonyaji watawahi.


HAYA WAKUU TUENDELEENI KUTUUNDIA BARAZA


SASA MNAUNDA KUTOKEA NA BASIS ZIPI?

JEE MMEPITIA ELIMU YA MAMBO HAYA? AU JUST UTASHI TU?


AU NDOTO ZA ALINACHA?


AU KUBWABWAJA TU?

JEE MSHAWAHI KUPITIA CAUSE HIZI ?

WATANZANIA BWANA KILA MTU MTAALUMA SAWA TUSONGENI BWANA KIWETE NA MIZENGWE NJOONI MCHAGUE SAMPLE MNAYOIONA ITAKUWA SAFI
 
HAYA WAKUU TUENDELEENI KUTUUNDIA BARAZA


SASA MNAUNDA KUTOKEA NA BASIS ZIPI?

JEE MMEPITIA ELIMU YA MAMBO HAYA? AU JUST UTASHI TU?


AU NDOTO ZA ALINACHA?


AU KUBWABWAJA TU?

JEE MSHAWAHI KUPITIA CAUSE HIZI ?

WATANZANIA BWANA KILA MTU MTAALUMA SAWA TUSONGENI BWANA KIWETE NA MIZENGWE NJOONI MCHAGUE SAMPLE MNAYOIONA ITAKUWA SAFI
Nilishiriki katika somo la uongozi na katika project moja niliwakilisha hivyo hivyo na tulipeleka kwenye visiwa vya Canary hiyo ilipasi ila waliongeza mambo mengine ambayo yalikuwa ya kibinafsi waliwekaa walinzi wa Jamhuri ambao waliundiwa Waziri wao hili ni kundi ambalo linahusiana na ulizi kwa viongozi na serikali yake na hupewa mafunzo maalum na mbinu zao zinakuwa kubwa sana,na zaidi hutumika katika nchi za kifalme au mtu kama Saddam serikali inakuwa na jeshi maalum na mambo yao maalum na amri zao maalum.Mbali ya lile Jeshi la umma pata mpatae.
 
Mapendekezo yangu ni kuwa na Serikali yenye Wizara zifuatazo na Idara kuu/Tume:

Ofisi ya Rais; Kurugenzi ya Usalama wa Taifa(TISS)
Ofisi ya Makamu wa Rais: Waziri wa Masuala ya Muungano, Waziri wa Jumuiya Afrika Mashariki
Ofisi ya Waziri Mkuu; Waziri Utumishi na Maadili, Waziri Maendeleo ya Mijini na Vijijini, Idara ya masuala ya Bunge

Wizara hizi zifuatazo zitaongozwa na Waziri akiwa na naibu mmoja na Makatibu Wakuu wa kutosha ambao watahakikisha utendaji wa kila kitengo.

  • Wizara ya Fedha na Mipango ya Uchumi;
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko; Brela, TIC, BIT, BET
  • Wizara ya Kilimo: Mifugo, Washirika, Chakula, Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Elimu: Elimu ya Juu na teknolojia, ufundi, baraza la mitiani, mitaala
  • Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama wa Taifa; Uhamiaji, magereza, polisi, mgambo, zimamoto, Masuala ya Dharura (emergency)
  • Wizara ya Maji, nishati na madini
  • Wizara ya Miundombinu; ujenzi, mawasiliano na uchukuzi
  • Wizara ya Mambo ya nje na masuala ya Kimataifa
  • Wizara ya Kazi
  • Wizara ya Mambo ya Jamii: Kinamama, wazee, wastaafu, walemavu, vijana, utamaduni na michezo
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Mazingira;
  • Wizara ya Tawala za mikoa, serikali za mitaa
  • Mwanasheria Mkuu; Sheria na Katiba
Kuwe na Idara Kuu zinazoongozwa na Makamishna ambao watawajibika kwa Cabinet
  • Mamlaka ya Kodi na Ushuru
  • Mamlaka ya Utalii Maliasili
  • Idara ya Habari
  • Mkemia Mkuu
  • Mamlaka ya Viwango na Ubora
  • DCI (Directorate of Criminal Investigations)Hii iwe independent kutoka Polisi
  • DAC(Directorate of Anti-Corruption)
  • DDEA(Directorate of Drugs Enforcement and Arms)
 
REv. Kishoka,
Tuangalie Wamarekani, mfumo wao ukoje wa Cabinet? Je udogo wao ni tija au tutadai wao matajiri? je ni lazima kila kitu kiundiwe wizara? hatuwezi kuwa na idara zinazoongozwa na makamishna ambao si wanasiasa?
Nafikiri tatizo letu limekuwa ni huku kudai tunataka kuleta uwiano wa Wateule kufuatilia misingi ya kidini, jinsia, umri na kimikoa (kikabila). Sisi kama Taifa tumepevuka sana na hakuna sababu yeyote kuunda baraza la mawaziri kufuatia hisia kama hizo. Kuendelea kutumia hivo vigezo, ni kukomaza mgawanyiko huo.
Kinachohitajika ni kuunda Baraza dogo ambalo litakuwa makini, fanisi, wajibikaji na adilifu. Unapokuwa na safu kubwa kama iliyokuwepo, kunatoa mwanya wa ubangaizaji na hata kulea mawazo ya hujuma

Nakubaliana nawe mia kwa mia hapa mkuu wangu.
Kwanza kabisa pamoja na kutazama mifano ya nchi kama Marekani ni muhimu tujiulize sisi kuwa hivi Tanzania kweli bado ni nchi ya Kijamaa ama tumebadilisha mfumo mzima na kuwa nchi yenye kufuata mfumo wa nchi hizo.
Sasa basi Kama serikali kazi yake ni utunzi wa sheria na kuhakikisha ipo nje ya biashara kama hizi inabidi tutazame ni wizara gani zinazotakiwa kufanya usimamizi badala ya wizara kujihusisha moja kwa moja na Taasisi zinazoendesha biashara nchini kama vile sioni sababu ya kuwa na Wizara ya Utalii ambayo ni biashara badala yake tungekuwa na wizara ya Maliasili na Mazingira. Utalii iwe chini ya Taasisi inayohusiana na masoko na sio Masoko ama Biashara kupewa wizara kamili kwani hapa tutakuwa tunaleta mvutano kati ya wafanya biashara na wizara.
 
Back
Top Bottom