Baraka Shamte aliyemkosoa Rais wa Zanzibar, ajeruhiwa, akufukuzwa uanachama CCM

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,624
218,047
Hii ndio Taarifa mpya iliyotufikia usiku huu, inadaiwa kwamba mtu huyu mzalendo, aliyetekwa na kunusurika kuuawa na Janjawidi pamoja na Mazombie, ambao ni watekaji maalum wa Zanzibar (Tanganyika wanaitwa wasiojulikana), hata baada ya kuokotwa na Majeraha makubwa bado ametimuliwa ndani ya CCM.

Bado haijajulikana ni vikao gani vya ccm vya ngazi ipi vilivyokubaliana kumfuta uanachama.

Pia soma: Shamte: Katiba ya nchi haijasema 'Head of State' atawale miaka 10, miaka mitano ikiisha tutafute Rais mwingine lakini siyo huyu

======
Baraka Mohamed Shamte.jpg
CCM Mkoa wa Mjini Zanzibar imemfukuza Uanachama Mwanasiasa Baraka Shamte ikisema ni sababu amekashifu madaraka ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi hadharani.

Uamuzi huu umekuja baada ya Shamte kuzungumza mambo mbalimbali na video yake kusambaa huku moja ya kauli zake ikisema: “Ukitaka utajiri acha uongozi ukafanye biashara, miiko ya uongozi haifuatwi”.

Imeelezwa kwamba Mzee Baraka Shamte amelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja Zanzibar kutokana na kupigwa na Watu wasiojulikana ambapo Polisi Zanzibar, leo wamekiri kupokea taarifa za kujeruhiwa kwa Mzee huyu mwenye umri wa miaka 83 akiwa eneo la Unguja Ukuu.

==================

Baraka Shamte akizunguma kuhusu utawala wa Zanzibar​

SERIKALI YALAANI SHAMTE KUJERUHIWA

FVKTrN2XsAADdHO.jpg


TAMKO LA JESHI LA POLISI ZANZIBAR
1.jpg

2.jpg

 
CCM Mkoa wa Mjini Znz imemfukuza Uanachama Mwanasiasa Baraka Shamte ikisema ni sababu amekashifu madaraka ya Rais Dr. Hussein Mwinyi hadharani.

Uamuzi huu umekuja baada ya Shamte kuzungumza mambo mbalimbali na video yake kusambaa huku moja ya kauli zake ikisema “ukitaka utajiri acha uongozi ukafanye biashara, miiko ya uongozi haifuatwi”

Imeelezwa kwamba Mzee Baraka Shamte amelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja Zanzibar kutokana na kupigwa na Watu wasiojulikana ambapo Polisi Znz leo wamekiri kupokea taarifa za kujeruhiwa kwa Mzee huyu mwenye umri wa miaka 83 akiwa eneo la Unguja Ukuu.
 
Mwache ayaone c ndo yeye aliyekuwa akishangilia akina Maalim seif na Wafuasi wake walivyokuwa wakteswa na hivyo vikosi vyao vya majanjawiri hata bado sisi tunataka wamuuwe hasa wajuwe kwamba ccm ndo ile ile hakuna muafaka wala umoja wa kitaifa wanaoutaka.
CCM kuua ni jambo la kawaida sana
 
Mwache ayaone c ndo yeye aliyekuwa akishangilia akina Maalim seif na Wafuasi wake walivyokuwa wakteswa na hivyo vikosi vyao vya majanjawiri hata bado sisi tunataka wamuuwe hasa wajuwe kwamba ccm ndo ile ile hakuna muafaka wala umoja wa kitaifa wanaoutaka.
Alisema Mh Lema, wakitumaliza sisi watawageukia na nyie, sasa ccm uwaneni kabisa ili mtoane kafara,
....hicho kibabu cha 83 years nadhan wangekiua tu, kiliwazodoa sana akina Maalim.
 
Mzee busara hakuna kabisa alikurupuka hata vijana wadogo kwenye chama hawawezi kuongea utumbo kama ule,amuulize mwenzake huku bara saizi anajuta.
 
Back
Top Bottom