Barabara ya kibaha mlandizi imekua ndogo magari mengi, usafiri umekua tabu sana kwa sasa

sanalii

JF-Expert Member
Oct 1, 2018
1,432
5,081
Kuna hitaji ujenzi wa dharura wa barabara ya zamani ya kibaha mlandizi then mpango wa barabara nne ulioishia kibaha mailimoja ufike japo mlandizi, kwa sasa ikifika jioni ni shida, kwa mfano leo gari moja tu lime break down basi tangu saa kumi hadi saa nne hii ni foleni, TANROADS naomba mulione hili
 
Nimepata hapo kama masaa 2 yaliyopita .
Hali ni mbaya kwa kweli.
Watu wanaweza Kesha kwenye foleni leo.
 
Makame ameingia kwa ofisi atatenda, lile jibu lililotumbuliwa juzi lilikua linaangalia maslahi yake tu.
 
Kwa kweli hicho kipande huwa ni shida sana especially jioni, hata kama hakuna breakdown hali huwa ni tete. Yaani kuanzia mlandizi, misugusugu,Kongowe, kwa mfipa, kwa Mathius, picha ya ndege mpk Kibaha stand ya zamani ni msongamano tu wa magari unaweza kutembea hata masaa 2 usipocheza cheza rough. Cha kushangaza ukishafika kwenye njia sita pale Kibaha gari zinaanza kutembea, unakuta askari na mitochi yao hapo karibu na St. Joseph University, sasa kwa njia zile wanataka watu watembee kama wanasindikiza harusi tena, nchi ya ajabu sana hii.
 
Wangekuwa wanajali maslahi ya wananchi, wangejitahidi mpaka Morogoro watanue njia tu, wananchi wanataka kuwahi na kupiga mishe zao.

Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom