Barabara inayopandisha Mbezi Juu (kushoto juu, pale kituo cha Tangi Bovu) ipigwe lami mpaka inapokutana na Barabara ya Goba

cvb-1

Member
Dec 14, 2018
43
46
Barabara inayopandisha Mbezi Juu (inayopandisha kushoto juu, pale kituo cha tangi bovu) ipigwe lami mpaka inapokutana na Goba Road.

Hii itasaidia usafiri, itapunguza foleni, na itachochea kukua kwa uchumi kwenye eneo hilo zuri la kilimani lenye hewa nzuri. Vilevile barabara hii itapitika vizuri zaidi kipindi cha mvua.

Eneo hilo litakuwa mtaa mzuri wenye kupendeza, kama mitaa ya Masaki/Oysterbay.

Kama unatoka mjini, barabara hii iko kushoto (ina panda juu) opposite na kanisa la KKKT la Tangi Bovu. Inapita Enocksville, inapita mpaka kituo cha mafuta cha Matala Empire (ukicheki kwenye google map).

Vilevile nashauri barabara hii iitwe Tangi Bovu Road au Masaki Road au Rombo Road.

Barabara hii itaunganisha Bagamoyo Road na Goba Road, kupitia maeneo hayo ya ndani ndani.

Je, TANROADS au TARURA au TAMISEMI au Wizara ya Ujenzi au Serikali ya mkoa au Halmashauri ya Jiji au serikali za mitaa au Development Partners (wafadhili kama World Bank, JICA, DFID, EU delegation etc.) wanaweza kuijenga hii bara bara?

Hivi, hii barabara imeshawekwa kwenye ramani za mipango miji?
 
Je, TANROADS au TARURA au TAMISEMI au Wizara ya Ujenzi au Serikali ya mkoa au Halmashauri ya Jiji au serikali za mitaa au Development Partners (wafadhili kama World Bank, JICA, DFID, EU delegation etc.) wanaweza kuijenga hii bara bara?
 
Halafu inashangaza kuona katika manispaa ya Kinondoni barabara za mitaa zenye lami ni chache sana ukikinganisha na manispaa nyingine kama vile temeke na ilala.
 
Yani barabara za mtaa za manispaa ya Kinondoni zimesahaulika sana ikiwemo hiyo ya tank bovu kupitia Gold Star hadi Goba
 
Inabidi wananchi wajitokeze kudai hiyo barabara ijengwe hususa kipindi huki tunapoelekea kipindi cha Campaign na Uchaguzi wa Mtaa na ule mkuu wa mwakani
 
Halafu napitaga ile njia kwa wakati fulani nyakati fulani lakini sijawahi kuona ikichongwa japo na vijiko vya Manispaa
 
Yani zinachongwa barabara za mbali nje ya mji kama vile mabwepande, mbopo , Madala n.k lakini hiyo ya karibu kabisa na barabara kuu ya bagamoyo haichongwi

Sijui kuna nini?

Nazani wananchi wanatakiwa kuanza kujitambua na kuanza kufatilia na kudai haki zao
 
Picha tafadhari, ukamatwe vizuri kwa kuhujumu uchumi. Nani amekuruhusu kuongerea humu kwenye mitandao mabeberu waache kuja huku kutuletea dora za kununulia ndege.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mayalla maana yake ni NJAA, sio mimi nimekuita hivyo bali nimenukuu mahala na ushahidi ninao.

Bahati kwako ni kuwa hukuthubutu kuipiga picha hiyo barabara unayoitetea iwekwe lami maana ungeswekwa lupango kwa kuhujumu uchumi.
Wewe barabara inakusaidia nini ikiwekwa lami?
Kuna mambo ya msingi ya kujadili ndugu achana na lami,
Na ukiona mvua inakutesa hama au upande ndege.

Mayalla ndege huzioni au

Kupanga ni kuchagua na badala ya kuwawekea lami pesa tumezielekeza kwa akina (mashinji) na wengineo tuendelee mbeRe.

MATAGA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilio chenu kimesikilizwa ?

Afadhali sana, naona pale mwanzoni wameipiga grader vizuri (kipande kirefu), na wamejenga mfereji pembeni (kwa kutumia tofali na cement).

Inabidi waendelee mbele zaidi wapande kile kilima, na mbele zaidi.

Halafu waipige lami.

Hakuna shida kama yatakuwepo maeneo ambayo barabara inaweza ikawa nyembamba.
 
Naona sasa imeboreshwa. I hope wata iboresha zaidi.

Waiboreshe zaidi tu, lakini wasi ipanue.
 
Back
Top Bottom