Bara wabebe mzigo umeme Visiwani hadi lini?

MzalendoHalisi

JF-Expert Member
Jun 24, 2007
4,517
1,367
Kuhusu kupanda kwa bei ya umeme Zanzibar kwa asilimia 168, kutoka Sh 28 hadi Sh 75 kwa kilowati moja, Masebu alisema hiyo inatokana na wateja wa Zanzibar ambao ni Shirika la Umeme na Mafuta la visiwani humo kulipa bei ndogo ikilinganishwa na hali halisi ya gharama za uendeshaji.

"Pamoja na Zanzibar kuongezewa gharama kubwa, lakini bado bei hiyo ipo chini ukilinganisha na zinazolipwa na watumiaji wa umeme wa bara,"
http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=2279

Je ni sahihi Visiwani walipie Umeme bei ndogo kuliko bara? Umeme wote unatoka Kidatu! Ni kigezo gani kinatumika Visiwani walipie kiasi kidogo kuliko bara na kwa kwa nini? Je ni faida ya nani?

Au ndo faida za Muungano Visiwani?

Je ni nani anabeba huu mzigo? Sii mtumiaji mlalahoi wa umeme Bara?

Is this fair?

Could this be ndo maana inabidi bei ya umeme ipande kwa sasa -kwa vile Visiwani wanalipa kidogo kuliko bara?????
 
Tunasubiri waje wajibu wenyewe maana kila siku ni malalamiko tu.
 
Wanatakiwa watupatie Jibu Tanesco hizi tofauti za gharama, WaTZ wa bara ndo tunatakiwa kuchangia ili kuimarisha Muungano au ndo faida za Muungano kwa Zanzibar?

Mlalahoi ataweza kuweka umeme kwenye kajumba kake ka mbavu za mbwa ambako kana thamani ndogo sana ukilinganisha na geti la nyumba za waheshimiwa wa masaki?

Hawa mafisadi wataendelea kutubebesha mizigo hadi lini?
 
Wanatakiwa watupatie Jibu Tanesco hizi tofauti za gharama, WaTZ wa bara ndo tunatakiwa kuchangia ili kuimarisha Muungano au ndo faida za Muungano kwa Zanzibar?

Mlalahoi ataweza kuweka umeme kwenye kajumba kake ka mbavu za mbwa ambako kana thamani ndogo sana ukilinganisha na geti la nyumba za waheshimiwa wa masaki?

Hawa mafisadi wataendelea kutubebesha mizigo hadi lini?

Hili swali naona Karamagi mwenyewe ndie wa kulijibu na sio TANESCO.
Mimi sijasikia Tanganyika (Serikali)kuchangia Muungano lakini Zanzibar kama nchi inachangia katika Muungano, coz Bara hawana Serikali. Naelewa wananchi wa Bara wanachangia kama wananchi wa Zanzibar katika Muungano, maana hiyo ni kila Mtanzania.
Zanzibar kuuziwa (sio kupewa bure) umeme kwa bei ya chini imekuwa soo! Mmesahau ya kuwa Bara imechukuwa Serikali yoote ya Muungano na kila kilichomo ndani, chao chao chetu chao. Bara inapata na inafanya mangapi kwa jina la Tanzania na wakati hata Zanzibar hawajui kinachoendelea, yanaishia hukohuko.
Hata Zanzibar ikitaka bure huo umeme amini watapewa tu, coz BARA inaelewa haitaathiri chochote kutokana na wanachoingiza kwa Zanzibar kuwepo kwenye Muungano huo.
Wakati umefika wa kudai Tanganyika yenu, ili tu Zanzibar ipumue.
Na kwa nini hamdai?
Serikali tatu na kero kwisha.
 
Hata Zanzibar ikitaka bure huo umeme amini watapewa tu, coz BARA inaelewa haitaathiri chochote kutokana na wanachoingiza kwa Zanzibar kuwepo kwenye Muungano huo.
Wakati umefika wa kudai Tanganyika yenu, ili tu Zanzibar ipumue.
Na kwa nini hamdai?

Mimi nadhani inabidi tuuangalie huu muungano wetu kwa macho makavu. Tuainishe wazi gharama zake na mchango wa kila upande halafu mjadala uanze kuhusu namna ya muungano tunaouhitaji au hata kama Muungano wenyewe unahitajika. Wazanzibari waseme wazi kama wana nia na muungano na wale wa bara vilevile. Ni heri tukiwaiga iliyokuwa Czechoslovakia kuliko Yugoslavia. Canada walifanya referendum kuhusu Quebec na watu wa Quebec "blinked". Kama kweli ndugu zetu waZNZ hawafaidiki kwa namna yeyote na huu Muungano ni bora tuurekebishe au tukubali kuachana bila shari. Ni vizuri Muungano wetu uwe wa hiari kuliko huu wa kutupiana madongo kila kukicha. Leo wote ni maskini wa kutupwa, itakuwaje hapo mmoja wetu atakapogundua mafuta?
 
Wakati umefika wa kudai Tanganyika yenu, ili tu Zanzibar ipumue.
Na kwa nini hamdai?
Serikali tatu na kero kwisha.

Wako waliodai serikali ya Tanganyika na wote tunajua yaliyowasibu. Hizi mbili zinatusumbua tatu tutaweza kweli? Tutachangia vipi hiyo ya tatu? Mgawanyo wa madaraka utakuwaje? 50,50? Kama ni hivyo basi na uchangiaji uwe hivyo hivyo bila kuangalia ikubwa wa nchi. Au tufuate wenzetu, anayechangia zaidi ndiye anayenufaika zaidi. Tukifika hapo ya nini hii serikali ya tatu, si wote tu wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki? Kwa nini tuongeze gharama ya serikali ya tatu? Kama walivyosema wachina," be careful what you pray for, for you might get it!"
 
Hili swali naona Karamagi mwenyewe ndie wa kulijibu na sio TANESCO.
Mimi sijasikia Tanganyika (Serikali)kuchangia Muungano lakini Zanzibar kama nchi inachangia katika Muungano, coz Bara hawana Serikali. Naelewa wananchi wa Bara wanachangia kama wananchi wa Zanzibar katika Muungano, maana hiyo ni kila Mtanzania.
Zanzibar kuuziwa (sio kupewa bure) umeme kwa bei ya chini imekuwa soo! Mmesahau ya kuwa Bara imechukuwa Serikali yoote ya Muungano na kila kilichomo ndani, chao chao chetu chao. Bara inapata na inafanya mangapi kwa jina la Tanzania na wakati hata Zanzibar hawajui kinachoendelea, yanaishia hukohuko.
Hata Zanzibar ikitaka bure huo umeme amini watapewa tu, coz BARA inaelewa haitaathiri chochote kutokana na wanachoingiza kwa Zanzibar kuwepo kwenye Muungano huo.
Wakati umefika wa kudai Tanganyika yenu, ili tu Zanzibar ipumue.
Na kwa nini hamdai?
Serikali tatu na kero kwisha.

kula 5 mkuu manake hiyo ndio solution hamna zaidi.
 
hii mikataba ingekuwa imeingiwa na wazanzibari nina huakika mto wake kule akuna wa kuuzima,wazanzibari wanaumoja pole maslahi yao yanapochezewa.kwa sababu standerd ya maisha yao hayapishani sana kati ya mtu na mtu.lakini wa bara wanajifanya wajuaji ndio maana gharama za maisha ni tofauti na wazenji.siku zote na wapongeza wazenji kwa mshikamano wao ktk kutetea maslahi yao hapo huwa hakuna cuf wa ccm.
 
Wako waliodai serikali ya Tanganyika na wote tunajua yaliyowasibu. Hizi mbili zinatusumbua tatu tutaweza kweli? Tutachangia vipi hiyo ya tatu? Mgawanyo wa madaraka utakuwaje? 50,50? Kama ni hivyo basi na uchangiaji uwe hivyo hivyo bila kuangalia ikubwa wa nchi. Au tufuate wenzetu, anayechangia zaidi ndiye anayenufaika zaidi. Tukifika hapo ya nini hii serikali ya tatu, si wote tu wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki? Kwa nini tuongeze gharama ya serikali ya tatu? Kama walivyosema wachina," be careful what you pray for, for you might get it!"

Mchundo vipi?

Kwa ukubwa wa Tanzania bara, idadi yake ya watu na rasimali zake sioni uzito wa madai ya bei za umeme na muungano. Tanganyika ina watu zaidi ya millioni 35 na Zanzibar millioni 1. Kwa hesabu za haraka wazanzibar wakilipa sawa na bara, bado hesabu zitakuwa zile zile.
 
Mchundo vipi?

Kwa ukubwa wa Tanzania bara, idadi yake ya watu na rasimali zake sioni uzito wa madai ya bei za umeme na muungano. Tanganyika ina watu zaidi ya millioni 35 na Zanzibar millioni 1. Kwa hesabu za haraka wazanzibar wakilipa sawa na bara, bado hesabu zitakuwa zile zile.

Kama muungano ni between equals hakuna sababu ya mmoja kumbebea mzigo mwenzie. Tatizo lililopo ni kuwa hatujaukubali huu muungano kwa dhati. Kama ingekuwa hivyo, watu wa bara wasingeona tatizo la kuwapiga jeki wenzao na wale wa znz kutingisha kibiriti kwa kudai hata tungetaka bure mngetupa tu! Inabidi kwanza tukubali kuwa huu muungano ni muhimu kwetu sote na kwa hali hiyo tuko tayari kusacrifice kwa ajili yake. Hata kama ZNZ wako milioni moja subsidy yeyote inayofanyika huko inapunguza uwezo wa kuwatendea hivyo hivyo wenzao wa bara. Hili walikubali na wa'appreciate' na sio kubeza kila wakati. Kwa mfano, kwenye hili la umeme. Kwa nini EWURA wasitangaze bei moja kwa pande zote mbili halafu serikali ya ZNZ iwauzie wateja kwa bei nafuu wakilipia wao tofauti hiyo ya bei? Au serikali ya Muungano ilipie hiyo tofauti badala ya kujificha nyuma ya hawa Ewura! Kufanya hivi kutafanya suala zima liwe wazi kwa wote.
 
Kama muungano ni between equals hakuna sababu ya mmoja kumbebea mzigo mwenzie. Tatizo lililopo ni kuwa hatujaukubali huu muungano kwa dhati. Kama ingekuwa hivyo, watu wa bara wasingeona tatizo la kuwapiga jeki wenzao na wale wa znz kutingisha kibiriti kwa kudai hata tungetaka bure mngetupa tu! Inabidi kwanza tukubali kuwa huu muungano ni muhimu kwetu sote na kwa hali hiyo tuko tayari kusacrifice kwa ajili yake. Hata kama ZNZ wako milioni moja subsidy yeyote inayofanyika huko inapunguza uwezo wa kuwatendea hivyo hivyo wenzao wa bara. Hili walikubali na wa'appreciate' na sio kubeza kila wakati. Kwa mfano, kwenye hili la umeme. Kwa nini EWURA wasitangaze bei moja kwa pande zote mbili halafu serikali ya ZNZ iwauzie wateja kwa bei nafuu wakilipia wao tofauti hiyo ya bei? Au serikali ya Muungano ilipie hiyo tofauti badala ya kujificha nyuma ya hawa Ewura! Kufanya hivi kutafanya suala zima liwe wazi kwa wote.

Nadhani Fundi inabidi uelewe kuwa umeme unapotumia nyumbani una gharama nyingi zikiwemo za uzalishaji, uzambaji na maintanance. Hivyo bei ya umeme inalipa vitu vyote hivyo. Sijuhi mchundo umechulia wapi, kama ni Dar basi kamuulize MKUU.

Zanzibar ni Compact hivyo gharama za usambaji na maintanance ni ndogo kuliko za bara. Na hii inatokana na kuwa unauzia shirika la usambaji Zanzibar hivyo gharama za usambaji na maintanance ni ndogo kule. Kwa mtaji huo walaji wa umeme :) wa Zanzibar hawahitajiki kulipa gharama za usambazaji kwa walaji wa umeme bara :) (walaji = watumiaju).

Hesabu za usambaji wa umeme ni sawa na hesabu za bima ya magari. Sehemu yenye wezi wengi wa magari wanalipa bima kubwa kuliko sehemu yenye wezi wachache.
 
TANESCO wanawauzia umeme SHIRIKA LA UMEME ZANZIBAR, na shirika ndilo linawauzia Wazenji kwa bei waitakayo wao, TANESCO haihusiki na usambazaji, ununuzi wa vifaa au metengenezo ya aina yoyote ndani ya Zanzibar, wao wanachojua ni kuuza na malipo yao tu, faida mia kwa mia.
Huko BARA wajameni TANESCO inahusika na madudu yote, tokea wizi, usambazaji na ukarabati na ndio maana mnalipia zaidi kufidia hayo madudu.
Nadhani mtanielewa
 
Ouch, Mkuu Bin Maryam! Naruhusiwa kukosea ndiyo maana sikuupata uhandisi. Unachosema, Bin Maryam kinaelekea isipokuwa kwa kitu kimoja. Kama Ewura wanapanga bei ya kumuuzia msambazaji wa Zanzibar wangesema hivyo, ili bei atakayolipa mteja iwe baina yao na msambazaji wao. Hii itaondoa dhana kuwa Tanesco wanahusika na bei anayolipa mteja. Au Ewura nayo ni ya muungano kwa hiyo wanahusika kuwapangia bei wenzetu wa ZNZ? Mbona inaelekea nguvu zote wamemuelekezea Tanesco? Hilo la wezi lina ukweli, siwezi kupinga. Asante kwa kunielewesha.
 
Nadhani Fundi inabidi uelewe kuwa umeme unapotumia nyumbani una gharama nyingi zikiwemo za uzalishaji, uzambaji na maintanance. Hivyo bei ya umeme inalipa vitu vyote hivyo. Sijuhi mchundo umechulia wapi, kama ni Dar basi kamuulize MKUU.

Zanzibar ni Compact hivyo gharama za usambaji na maintanance ni ndogo kuliko za bara. Na hii inatokana na kuwa unauzia shirika la usambaji Zanzibar hivyo gharama za usambaji na maintanance ni ndogo kule. Kwa mtaji huo walaji wa umeme :) wa Zanzibar hawahitajiki kulipa gharama za usambazaji kwa walaji wa umeme bara :) (walaji = watumiaju).

Hesabu za usambaji wa umeme ni sawa na hesabu za bima ya magari. Sehemu yenye wezi wengi wa magari wanalipa bima kubwa kuliko sehemu yenye wezi wachache.

Hii hoja is so weak!

Zenj wana tofauti gani na mji kama Moshi au Iringa ktk umeme?

You can argue better than this! Acha siasa ktk umeme!

Ukweli Visiwani wanalipia kidogo kwa kubwebwa na walala hoi Bara!

Kwanza garama kuleta tu umeme toka Kidatu/Kihansi to Zanzibar ni kubwa mara nyingi kwani unapiata baharini- which is another cost!

Ukweli ni kuwa Visiwani wanabebwa na kusaidiwa umeme na Bara!

Tupunguze ushabiki na siasa!
 
"As a result of an inquiry conducted, Ewura has concluded that the proposed tariff increase and connection charges were justifiable, save for the unjustifiable increases of some cost items and an unexplainable low level of the energy charges for State Fuel and Power Corporation of Zanzibar," he said.

Kwa wanaojua kimombo, huyu bwana anataka kutueleza nini? Pamoja na majibu mazuri ya Bin Maryam na SiDe naona badop kuna jambo limejificha. SiDe mbona hukujibu hivi tokea mwanzo badala ya lugha ya ubabe ya kuwa hata kama znz wakitaka bure watapewa tuu?
 
Hii hoja is so weak!

Zenj wana tofauti gani na mji kama Moshi au Iringa?

You can argue better than this! Acha siasa ktk umeme!

Ukweli Visiwani wanalipia kidogo kwa kubwebwa ba walala hoi Bara!

Kwanza garama kuleta tu umeme toka Kidatu/Kihansi to Zanzibar ni kubwa mara nyingi kwani unapiata baharini- which is another cost!

Ukweli ni kuwa Visiwani wanabebwa na kusaidiwa umeme na Bara!

Tupunguze ushabiki na siasa!

Kwa uhalali bei ya Moshi na Tanga ni tofauti kabisa. Lakini kwa sababu miji hiyo inategemea msambaji mmoja ni lazima gharama zichangiwe. Na kuna vijiji Tanzania bara ambavyo kuna watumiaji watano tu wa umeme. Watumiaji hawa hawaingizi faida na hili shirika lipate faida basi watumiaji wa miji mingine ni lazima wachangie.

Mkoa wa Kagera unapata umeme kutoka Uganda lakini bei ni sawa na mtu anayetumia wa Kidatu/Kihansi. Piga hesabu hapo. Kwanini asilipe sawa na mtu wa Uganda.
 
Huu Muungano una kasoro nyingi sana mojawapo ni hili la umeme. Wanasiasa hawataki kuliweka wazi ili tuzijadili kwa mapana na marefu kasoro mbali mbali zilizoko katika muungano ili kuuboresha muungano huo (kama itawezekana). Wanataka kuzifukia kasoro zote zinazolalamikiwa pande zote mbili ili muungano uonekane kama uko shwari kabisa, kitu ambacho si cha kweli.
 
Kwa uhalali bei ya Moshi na Tanga ni tofauti kabisa. Lakini kwa sababu miji hiyo inategemea msambaji mmoja ni lazima gharama zichangiwe. Na kuna vijiji Tanzania bara ambavyo kuna watumiaji watano tu wa umeme. Watumiaji hawa hawaingizi faida na hili shirika lipate faida basi watumiaji wa miji mingine ni lazima wachangie.

Mkoa wa Kagera unapata umeme kutoka Uganda lakini bei ni sawa na mtu anayetumia wa Kidatu/Kihansi. Piga hesabu hapo. Kwanini asilipe sawa na mtu wa Uganda.

Thanks,
Unasupport watumiaji wote wa umeme Tanzania walipie sawa- wawe Zenj au Moshi au Tanga! This is fair! Kwa nini Bara waibebe Zenj kulipia umeme? Why?

Sasa swali ni kwa nini Zenj wanalipia kidogo????

Je huu sii upendeleo?

Tuache siasa tuangalie uchumi!
 
Back
Top Bottom