Banki ya Dunia: Mpango wa Serikali ya Tanzania Kukopa ni 'Bomu'

Ifilisike mara ngapi tena!? Rasilimali zetu tunazigawa bure kwa "Wachukuaji" ambao tumeamua kuwaita "Wawekezaji" kumbe hakuna chochote wanachowekeza bali ni WIZI MTUPU! Tulipunguziwa madeni kwa kiasi kubwa sana wakati wa awamu ya Mkapa sasa hii awamu ya Kikwete madeni hayo yamerudi tena kwa kiasi kikubwa. Wanaona kabisa nchi haina mapato ya kuweza kujiendesha badala ya kutafuta namna ya kubana matumizi ili kupunguza budget tegemezi sasa wameamua kuanza kukopa mikopo yenye riba kubwa sana ambayo nchi haiwezi kuimudu. Tuna vichwa vya wendawazimu ambao hawaangalii mbali na kama wasiposikia onyo la WB katika mkopo huu mkubwa wanaotaka kuchukua basi itafika wakati hata kukopa itakuwa haiwezekani tena maana nchi itakuwa imezidiwa na madeni makubwa mno.
Nchi haijawahi kuwa tajiri kwahiyo haiwezi kufilisika. Pia nchi haina uwezo wa kulipa madeni zaidi tunapunguza na wakiona tumewalipa na riba kiasi fulani wanasamehe. Ila wakikopa kwenye capital markets shughuli yake wataijua. Ingawa miaka ya sasa hivi wanaweza wasielewe, kiongozi atakayefuata ndiyo atajua joto lake.
 
Kuna link hii imeelezea advantages na disadvantages ya serikali kuamua kuchukua mikopo toka mabenki binafsi badala ya serikali kuuza treasury bonds (dhamana za serikali) kupitia Benki Kuu Ya Tanzania. MwanaJF tuendelee kujielewesha yanayoweza kututoke kwa uamuzi huu wa serikali kutokana na uchambuzi wa kina wa wataalamu wa masuala ya fedha na mabenki hususan iki-focus case hii ya Tanzania:

''It is not clear how the Treasury by borrowing directly from commercial banks can avoid triggering a rise in local interest rates, but the strategy makes political sense in an election year because commercial banks will not make tough demands. The East African: ''
 
In reality bado bajeti yetu ni ndogo sana kwa kulinganisha mahitaji ya taifa na zaidi kwenye umeme, barabara, reli, elimu na kilimo. Haya ni maeneo ambayo hata kama bajeti yote iende kuyandeleza bado haitoshi. Mfano mdogo tu mahitaji ya umeme kwa Tanzania kwa ukuaji wa sasa tutahitaji kuwekeza zaidi ya tsh 12 trillion kwa miaka mitano mpaka kumi ijayo. Sasa hi ni zaidi ya bajeti nzima ya mwaka ujao na huu ni umeme tu bado mambo mengine.

Kwa wale ambao wanafuatalia mwenendo wa kiuchumi wa Keynesian wana support matumizi makubwa ya serikali kwenye nchi ambazo sekta yao binafsi bado ni ndogo mfano hapa kwetu, au kwenye nchi zilizoendelea baada ya mishtuko ya kiuchumi ambapo biashara binafsi hazina hela au zinabana matumizi.

Sasa hii ni kinyume na imani za hizi Bretton woods ambazo siku zote wao wanataka serikali iwe na matumizi madogo. Hivo basi ni wazi WB watapinga mpango wa serikali kukopa nje ya mikopo yao ingawa ni kweli riba yao ni ndogo. Lakini ni kweli vilevile Mkullo anavyosema kuwa sio miradi yote hufadhiliwa na WB na tukisubiri hivyo hatutaendelea.

Ni vyema serikali ikaangalia namna mbadala za kupata mtaji sio kutegemea WB na wafadhili siku zote. Tunahitaji miundo mbinu mingi ambayo hapa kwetu haipo. Na hii itasaidia kukuza uchumi na hayo ndio mamlaka na jukumu la serikali, kukusanya mapato na kuendeleza miundombinu ili wananchi wapate urahisi wa kufanya shughuli zao, bajeti yetu ni muhimu iendelee kukuwa hadi angalao tufikie trillion 50...kwa sasa ukiangalia bajeti ya trillion 11.5 kwa watu million 40 ni kama Tsh 287,000 kwa kila raia au tsh 24,000 kwa mwezi haifiki hata dola moja kwa siku! sasa kweli tutafika bila kuanza mchakato muhimu wa kuongeza bajeti na hivyo pato la taifa?

Hii ndio analysis iliyokwenda shule, haina chuki za siasa wala jazba. Wolrd bank, IMF, IFC na taasisi zote za kimataifa sio rafiki wa nchi masikini hata siku moja. They are lions in a sheep skin.

Alafu director mzima wa world bank anatumia lugha ya ujanja ujanja badala ya lugha ya kisomi: "The World Bank Country Director for Tanzania, Uganga and Burundi, Mr John McIntyre, told a news conference that borrowing from local commercial banks could be counterproductive if interest rates were too high."

Nilipopigia mstari manake anakubali kwamba kuna uwezekano kwamba Tz inaweza ikanufaika na mkopo wa commercial bank; lakini hakutaka kutueleza itanufaika vipi maana kufanya hivyo kutasababisha hasara kwenye world bank. Alafu angalia anapojaribu kutufanya vilaza, kwenye nyekundu anasema endapo interest itakuwa too high mkopo utakuwa counterproductive. What is too high? Too high to whom? Mbona hatuelezi faida za kiuchumi zinatokana na interests zinapokuwa high? Mbona hatuelezi trickledown effects za high interest rates zitakazotokana na mkopo kutoka local bank vis-a-vis zile zitokanazo kwenye mikopo ya world bank? Director mzima anatumia subjective language katika kuhalalisha uharamia wa world bank kwa nchi masikini kama Tz.

Hivi waafrika tutaendelea kutafunwa na Bretton wood institutions hadi lini? Mungu bariki Tz, bariki na vichaa wake.
 
Nchi haijawahi kuwa tajiri kwahiyo haiwezi kufilisika. Pia nchi haina uwezo wa kulipa madeni zaidi tunapunguza na wakiona tumewalipa na riba kiasi fulani wanasamehe. Ila wakikopa kwenye capital markets shughuli yake wataijua. Ingawa miaka ya sasa hivi wanaweza wasielewe, kiongozi atakayefuata ndiyo atajua joto lake.

Nchi iwe tajiri mara ngapi tena!? Tuna rasilimali chungu nzima ambazo zinayavutia makampuni makubwa ya Kimataifa kuja kuchuma rasilimali zetu mbali mbali kuanzia Dhahabu, Almasi, Gas, Tanzanite, Uranium n.k. Kama hizi rasilimali tulizojaliwa na Mungu si utajiri sijui ni kitu gani tena!!!! zinawanufaisha wageni badala ya Watanzania. Hivi unafikiri kampuni kama Barrick wangefunga safari toka kwao kama si kuja kuvuna utajiri tuliojaliwa na Mungu!? Wafuate kitu gani Tanzania nchi ambayo ni maskini ya tatu duniani?
 
Ni kweli issue hii inahitaji watu waliokwenda shule kutupatia a VIABLE FINANCIAL AND ECONOMIC ANALYSIS vinginevyo tutaendelea kutoleana shutuma tu. Oh WB,IMF,ADB, ect. Vs Local Financial institutions, NANI HASA ANAFAA KUTUPATIA MKOPO???. Mimi na uelewa wangu mdogo kuhusu mikopo hii na Tanzania kukopa either WB or Local Banks, sioni kama ni Tatizo. Shida kwangu hapa inakuja inapoonekana kama kwamba hii pesa inahitajika tu kwa ajili ya ELECTION CAPAIN - OCTOBER, 2010 na kana kwamba hawa WB nao wameona wakitoa pesa zao nyingi zitakwenda kwenye Masuala ya Uchaguzi badala ya Miradi ya maendeleo.
Swali la kujiuliza hapa ni kwamba "JE NI KWELI SIE TUMESHINDWA KUDHIBITI MATUMIZI YETU AMBAYO SIYO YA LAZIMA??? mfano: Utumiaji wa Magari ya kifahari, Safari nyingi za Nje ya Nchi za Mhe. Rais na wapambe wake, Matumizi mabaya ya Ofisi za Serikali kwa kununua Thamani za ofisi kila mwaka (Perishable goods but expensive - meza,viti, na....), Semina, warsha na Makongamano, Mianya ya Rushwa na utendaji mbovu wa watumishi wa UMMA, kutokuwa na Mipango thabiti ya kuibua maeneo mapya ya KODI, Kuwa na Viongozi Makini wa kuongoza Mashirika yetu kama vile ATC, Bandari zetu, Bunga zetu, Bahati yetu, Maziwa yetu na Rasilimali zetu.....ect. " A combination of all these can make us move so many steps ahead of the third world countries. Let us talk about these and how i we going eliminate UFISADI.
Nimekuwa mpensi sana wa SERA za President Kagame wa Rwanda anavyoibadili Rwada na kuifanya iwe hub and Business centre for all EAC na anavyo pambana na UFISADI na kupunguza Matumizi ya Serikali (Government expenditure) kwani huu ndio mzingo wa WALIPA KODI....! Kukopa hakuna shida kama utakuja lipa na utatumia vizuri mkopo.... ila kama unakopa ukijua fulani atajijua na deni hili atakapokuwa analilipa, kwanza mie sitakuwepo na usiangalie Modality ya hilo deni kwa kuangalia riba na hata timeframe ya kulipa hilo deni.... hapo ndio watanzania tunatakiwa tuwe makini na ndio hapo tunahitaji ECONOMICS AND FINANCIAL POINT OF VIEW.

Asanteni sana na hii ndio makala yangu ya kwanza hapa Jamii forum
Ni mimi wenu "Igembe Nsabo - Jembe ni Mali"
 
Nchi iwe tajiri mara ngapi tena!? Tuna rasilimali chungu nzima ambazo zinayavutia makampuni makubwa ya Kimataifa kuja kuchuma rasilimali zetu mbali mbali kuanzia Dhahabu, Almasi, Gas, Tanzanite, Uranium n.k. Kama hizi rasilimali tulizojaliwa na Mungu si utajiri sijui ni kitu gani tena!!!! zinawanufaisha wageni badala ya Watanzania. Hivi unafikiri kampuni kama Barrick wangefunga safari toka kwao kama si kuja kuvuna utajiri tuliojaliwa na Mungu!? Wafuate kitu gani Tanzania nchi ambayo ni maskini ya tatu duniani?
BAK utajiri sio kuwa na rasilimali ambazo sio productive. Zipo jamii za wafugaji mtu anamiliki zaidi ya ng'ombe 2000 lakini anaishi kwenye kibanda cha nyasi au maisha ya kutangatanga. Utajiri wetu ungesemeka vizuri kama ungeonekana kwenye kipato cha watu binafsi, miundombinu ya barabara, afya, maji, umeme nk. Pia hatuna mtaji wa kutufanya kuzitumia hizo rasilimali ndiyo maaana wenye pesa zao wanatafuta opportunity na kujaribu kuexploit. Kwahiyo sisi si tajiri, km wewe mwenyewe ulivyohitimisha kwamba Tanzania nchi ambayo ni maskini ya tatu duniani.
 
Back
Top Bottom