wana jf, apology if this topic has been discussed. Kwa kuwa baadhi ya mabenki hapa nchini yanaaacount under shariah law. Je mabenki hayo yana kopesha wateja (wenye account za shariah law) kwa kufuata shariah law, yaani bila interest?
Kama hawatozi riba nitakwenda kukopa kutumia hiyo Sharia Banking, lakini wasiniwekee masharti mengineyo kama vile niwe Mshariah! I think BoT watatangaza kuwa hizo bank ni Muflis baada ya kuanza kutoa mikopo kishriah shariah.
Ibrah, ikiwa shariah account hazina any interest hata ya 0.1% kwa nini wasiwape mikopo watu wenye account hizo loans zisizo na riba kama account zao zilivyo? au ndiyo kumlazimisha mtu kumtii Mungu kupia technics za kishetani?
Ni kweli hazina riba lakini kuna utaratibu wa kugawana faida au hasara. Sio rahisi kwa sasa ku operate a truly islamic banking (interet- free) sambamba na conventional banking kama baadhi ya mabenki ya hapa nyumbani yanataka tuamini. Kwa mfano, hilo suala unalouliza sio rahisi sana kufanyika katika benki ambayo ni mchanganyiko, yaani islamic na conventional (kama KCB na NBC). Bank haiwezi kuaccept interest bearing deposits na kisha ikopeshe interest-free kwa kutegemea kugawana faida au hasara ya uwekezaji.
so the whole thing ni utapeli wa design fulani hivi.
Alisema hivi. MFUMO HUU WA ISLAMI BANKING KUNAKUWA HAKUNA MTEJA BALI KILA ANAYEWEKA PESA ZAKE ANAKUWA SHARE HOLDER. KWA KUWA SHARE HOLDER UNABIDI BANK IKIFAHAMISHE KILA KITU HUSUSAN MATUMIZI AU UWEKEZAJI WOWOTE UNAOFANYWA NA PESA ZAKO KWA MAANA KUWA MNA SHARE FAIDA NA HASARA.
Hilo linaweza kuwa sawa lakini technically kwa hapa kwetu islamic account holder hawezi kuwa shareholder (in a true sense of it). Kwa mfano KCB na NBC zote sio listed hivyo hawawezi kutreat depositors wa islamic accounts kama shareholders (i.e. they can not sell their shares to the public). Hili peke yake linafanya depositors kukosa maamuzi kwenye uwekazaji wa benki tofauti na unavyotaka tuamini.
Kwa wale wasomaji wazuri wa Jamii forum s Economics.
Dr barubaru alifafanua kwa kina sana katika mada mojawapo. Alisema hivi. MFUMO HUU WA ISLAMI BANKING KUNAKUWA HAKUNA MTEJA BALI KILA ANAYEWEKA PESA ZAKE ANAKUWA SHARE HOLDER.
KWA KUWA SHARE HOLDER UNABIDI BANK IKIFAHAMISHE KILA KITU HUSUSAN MATUMIZI AU UWEKEZAJI WOWOTE UNAOFANYWA NA PESA ZAKO KWA MAANA KUWA MNA SHARE FAIDA NA HASARA.
Inapotokea mteja anataka kukopa basi bank inapitia mchanganuo wake na kama itaridhika nao basi wanampa hizo pesa na BANK TENA INAKUWA NA SHARE HOLDER KATIKA MRADI HUO.bank itasimamia uwekezaji na taratibu zote za kifedha katika mradi huo kwani nayo pia inaweza kupata faida au hasara. bank inakuwa mshauri mkuu wa mradi huo kuhakikisha unaendelea na kama ukiona hauna faida nasi wanaondoa pesa zao(wanajitoa share holding )
vile vile faida katika account hizi haziwi fixed bali zinategemea na uwekezaji katika mwezi huo. wao wanachukua % ndogo tu za uendeshaji.
Someni vizuri mada hiyo ya dr hamza kwani ilifungua wengi sana na kuwafanya waingie katika mfumo huu ambao sana unaingia kwa kasi sana hasa baada ya kuona mfumo wa sasa wa mwenye bank na mteja ulivyoleta mtikisiko wa uchumi duniani