myao wa tunduru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2010
- 615
- 234
nataka kufungua saving account tanzania,je ni bank gani nzuri kwa huduma hii na michanganuo yake kwa mwenye uelewa na hili....
CRDB branch yoyote sidhani kama inaweza kuishiwa na hela wateja wakashindwa ku withdraw. Na ATM wanazo za kumwaga.
nataka kufungua saving account tanzania,je ni bank gani nzuri kwa huduma hii na michanganuo yake kwa mwenye uelewa na hili....
Mbona hii imeka ki-promo promo??
Kwa kiasi kikubwa ni kweli, benki zote maumivu. Lakini baada ya kuzunguka, nimeamua ku settle na CRDB.
Nilijaribu viji benki vingine nikashindwa (Bank of Africa, Akiba Commercial Bank etc.)
Kwanza kabisa kwa benki nyingine kupata kadi yenye visa ni ishu! Wana kitu kinaitwa Umoja ndio kama ki-visa chao cha local hapa hapa Bongo kina transact sehemu yoyote yenye nembo ya Umoja. Hiyo Umoja yenyewe nikakuta kikadi changu kinamezwa mezwa bila sababu halafu kikadi kikimezwa mfano Mlimani City unaambiwa usubiri kirudi Makao Makuu halafu wakitume branch ulipofungilia account Buguruni. Wiki tatu!
Ukipoteza kadi wanakula buku kumi kukupa kadi ingine, halafu kwa mfano Bank of Africa wanatoa kitambulisho cha benki na ATM ambayo haina picha, so utembee navyo vyote viwili. Sasa kwa nini msiweke picha kwenye ATM kama CRDB ili kupunguza vikadi vya kubeba kutunisha wallet wakati mtu huna kitu?
Haya kuna hii benki ya posta. Kuna siku tumegandishwa mda mrefu sana bila kuambiwa sababu, nje ATM ime boomer, akaja Mhindi mmoja wakatuomba tumwache apite, akawabwagia deposit ya miburungutu mikubwa pwaaaaa, ndio tukaitwa eti tu withdraw laki laki zetu, hela iliwaishia!
CRDB branch yoyote sidhani kama inaweza kuishiwa na hela wateja wakashindwa ku withdraw. Na ATM wanazo za kumwaga.
nataka kufungua saving account tanzania,je ni bank gani nzuri kwa huduma hii na michanganuo yake kwa mwenye uelewa na hili....
Mkuu kama wadau walivyotangulia kusema hapo juu benki zote za TZ kwa customer care bado sana ila kuna unafuu wa namna fulani katika baadhi ya mabenki. CRDB ni wazuri ila wana bank charges nyingi sana. Exim hawana bank charges nyingi almost ni bure kuweka pesa zako na kuchukua na pia wana MasterCard. Interest rate ya CRDB ni 2% na Exim ni 3 %. NBM na NBC ni wabovu zaidi.
jamani nimezunguka kote nashangaa ata anaefagilia crdb me nimegota azania bank ni mwisho akuna makato ya aina yoyote ile zaidiya interest alafu ukifungua acc ya usd bomba sana wana reti nzuri nawakilisha wakuu
Tatizo la CRDB wana charges nyingi sana kila mwezi wanakata 400, ukiwekewa mshahara wanakata commission charges, ukitumia ATM zao wanakata 500 for each withdraw. Jaribu Barclays hawana ATM withdraw charges.Hata kama imekaa ki-promo promo ni sawa tu maana ukilinganisha benki zote CRDB kwa kweli wako juu mimi binafsi nimewakubali na nikajuta ni kwa nini sikufungua akaunti kwao mapema? Hapa kwetu ukienda benki hukai zaidi ya dk 30. Hebu jaribu benki ya makabwela ukione cha moto, mpaka unashangaa kama hao wafanyakazi wao wanafanya kazi kwa kulipwa au wanajitolea? Yaani ni kero tupu (morale ni zero). Siku zingine ukute msitari wenyewe umepiga kona kama tano hivi na kama mko karibu na barabara basi tegemea huo msitari kuukuta uko barabarani!
Ninakubaliana na aliyesema benki zetu zote ni maumivu tu, lakini hata kwa mbumbumbu kuna mjanja wao!! Basi bila ubishi CRDB ni miongoni mwa wajanja wao!