Bango lenye lugha ya Ki-mandarin Dar

Tusker Bariiiidi

JF-Expert Member
Jul 3, 2007
5,520
2,091
Bango hili lipo katika Barabara ya Garden karibu kabisa na nyumba za TPDC Mikocheni. Kwangu mimi nimeona hii ni too much!!! Je inawezekana walengwa ndio wanatakiwa wajue lugha hii??? Nini kinafichwa???
Mswahili akienda hapo hatatimuliwa kweli???

Kariakoo kuna Hotel kubwa tuu nayo pia imeandikwa lugha hii ya Kimandarin??? sema hiyo angalau... imeandikwa Sichuan Hotel...

Kesho kutwa Wachina (Sijajua kama wataruhusu jamii nyingine kushiriki??? wanafanya maandamano ya amani kupinga Mauaji ya mwenzao hapa Dar... Sasa Tukiacha mambo haya yaende kiholela holela... Tutavuna mabua (aliwahi kughani Mrisho Mpoto)
Au ni kweli kwamba tunafanywa SHAMBA LA BIBI???

3926d1237485246-bango-lenye-lugha-ya-ki-mandarin-dar-untitled-4-.jpg
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mbona wameshahamia?? si ndio 'globu' hiyo inaangaza, juzi wamekamatwa wanajiuza, nenda stend ya mkoa wanapiga debe, uwanja wa taifa walipga kazi mpaka ya kufagia, achilia mbali kubeba zege! Kariakoo wamejaa! No problem at all, TULISHACHELEWA MKUU, HUWA NASEMA HATUISHI KARN YA 21, kwa namna nyingine, hatuwezi kushindana nao, maana serikali yao wanatupa misaada! nchi za dunia ya tatu zilitakiwa kujiyatarisha kabla ya kuingia kwenye globalisation! huwawezi hao , best way ni sisi kumka, kuungana na kupambana! kuwa competent kila kona!
 
Sheria za kazi zipo na wapo watu wanalipwa mishahara kwa kuhakikisha sheria hiyo inafanya kazi lakini wamechapa usingizi.
 
The board says: ' Please go ahead for 400meters ,then you can see a dinner room named hai tian mei shi.

Lakini ukienda huko hivyo vyakula utaviweza? Nyoka, kobe, konokono etc
 
Sioni ubaya wa kuwa na Bango limeandikwa kwa lugha yao. Ila nakushangaa kwanini ujawahi kulalamika kuwa kuna mabango mengi yameandikwa kwa lugha ya kiingereza, kiarabu na nyinginezo au unadhani hizi ni lugha zetu?

Kama utakuwa ni wa umri wangu, utakumbuka mwaka 1972 Tanzania ilipigana vita fupi na Uganda. Wahindi waliokuwa wanaishi Bukoba Mjini, ilibidi wahame mji na kukimbilia vijijini, tatizo lao ilikuwa ni lugha. Baada ya hapo Wahindi walioendelea kuishi Bukoba walijifunza Kihaya na wengine walikimbia kimoja. Hapa ninachotaka kusisitiza ni kuwa wageni WOTE wanaoingia hapa kwetu Tanzania tufanye juhudi za kuwafundisha kiswahili na siyo wao kutufundisha lugha zao.
Ilo bango, kama lilivyotafsiriwa na Kitia,linaweza kuendelea kuwepo kama limefuata taratibu za kuwepo, lakini kama halina manufaa kwa mtu yoyote, basi mwenye kulimiliki hatokuwa na sababu ya kuliweka. Kwani wote tunaongea kiswahili basi litabadilika kuwa Kiswahili - Iwapo tutafanya ulazima wa kuwafundisha wageni Kiswahili. Sasa hivi Tanzania kuna vijana wengi wamesahau kuwa Kingereza na lugha nyinginezo ni vi-lugha tu kama Kichagga, Kinyamwezi n.k

Mpenzi wangu A, wa UK, nakupa ongera kwa kuendelea kuwaelimisha vijana juu ya Lugha yetu, japokuwa umeishi nje ya nchi kwa muda mrefu kuliko umri wa mtoto wa darasa la saba.
 
Mabadikiko yanawezekana. Mwanzilishi wa mabadiliko si mwingine ... ni mimi na wewe. Kwa kweli watanzania tunahitaji kuamka usingizini na si wale waliokabidhiwa dhamana tu ... Sidhani kama mtu atasinzia ukumbini kama ngoma inachezwa kwa nguvu zote.
 
Sioni tatizo, si wanataka wakamate market fulani. Kama wanabagua kuserve mtu hapo ni issue nyingine.
 
Kwa hiyo hilo la Shule ni la Watanzania? Watanzania wanajua Kiingereza? Mbona hamsemi wangeandika kiswahili katika hilo la shule?
Sipendi ubishi ila suala ni rahisi sana, ya kaisari mpe kaisari. Hiyo ni ya wanaoweza kusoma hiyo. Ni sawa na jambo forum, ni lazima ujue kiingereza uweze kujiunga na kushiriki.
Kumbukeni pia walengwa hawajui kiswahili na kiingereza, la sivyo mnataka mabango yote yawe na lugha kadhaa. Si lazima.
Kuhusu kukaliwa naona kama mnamanisha tufanye walichofanya waafrika kusini, natamani ungejua ni namna gani watanzania walibyogurika nchi za watu, nenda Jberg ukutane na machinga wa kitanzania, je, wafukuzwe kwa maana kuna siku watafika ikulu.
Lets be positive....
 
Hivi bado wadau hamjajiuliza kwa nini hizi kampuni za DINI Tanzania zote zina majina ya kiinglish Mf. true christian church, Tanzania Asseblies of God, Winners Chappel, Full Gospel al so forth? labda ina maana kumuabudu Mungu ina uzito sana kwa lugha ya kigeni....
Haya mabango ya kimandarin ni mwendelezo wa msingi ulioanzia mahala fulani....

NB
Kuna siku nilikuwa Dar nikapita barabara ya morogoro maeneo ya Kagera Manzese, Ukiwa unaelekea Nzese upande wa kushoto kuna garaje moja imeandikwa KITUTU ktk gate, walah kwa watani zangu wanyakyusa hili ni neno baya sana kulitumia public.... Najiuliza kama hakuna utaalam au utaratibu wa kuratibu mabango ya matangazo ili kupunguza public conflicts ktk definitions inaweza kuwa balaa siku za usoni... Bila kusahau kule Mkuranga kuna Duka la dawa lipo pale mjini linaitwa DENGANA pharmacy.... Najua kwa wapare ni kasheshe hapo....
 
Wahusika wenye majukumu ya kuhakikisha wageni wakiwepo wachina hawaingii nchini kinyume cha sheria au wasifanye vitu wasivyotakiwa kufanya either wamelala au wamezawadiwa vizawadi na kusahau kuwa wanauza nchi yetu.mimi nipo China and
I see nchi yetu haijaweka mikakati thabiti ya kuhakikisha wana exploit all potentials za wachina na kujikuta wachina wengi wanao ingia Tanzania ni wale wenye hali mbaya kimaisha hapa China.Lakini wale ambao ndo muhimu kabisa kwa China wengi hawaji huko...
Kwa hiyo inabidi turekebishe urasimu wetu tukitaka to maximize kuifaidi China!
 
haswa mabadiliko yataletwa na watanzania wenyewe,tusibweteke kila mmoja atimize wajibu wake
 
Hebu tupatieni maana ya hayo maneno (KITUTU, DENGANA). They sound very nice to my ears! :)
Nataka kuwa na kampuni yangu someday, nina lengo la kuipa jina la kibantu. "Kitutu garage" sounds very cool :) Hali kadhalika DENGANA; ina sound kama jambo linalofanywa na watu wawili hivi au zaidi (to each other).

Wenzetu wameanza kuhodhi maneno ya Kiswahili kwenye biashara zao: kijiji.com
tizama:[ame=http://en.wikipedia.org/wiki/Kijiji]Wikipedia[/ame]

Wahusika wenye majukumu ya kuhakikisha wageni wakiwepo wachina hawaingii nchini kinyume cha sheria au wasifanye vitu wasivyotakiwa kufanya either wamelala au wamezawadiwa vizawadi na kusahau kuwa wanauza nchi yetu.mimi nipo China and
I see nchi yetu haijaweka mikakati thabiti ya kuhakikisha wana exploit all potentials za wachina na kujikuta wachina wengi wanao ingia Tanzania ni wale wenye hali mbaya kimaisha hapa China.Lakini wale ambao ndo muhimu kabisa kwa China wengi hawaji huko...
Kwa hiyo inabidi turekebishe urasimu wetu tukitaka to maximize kuifaidi China!


Kweli kabisa!
 
Back
Top Bottom