Linguistic
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 3,671
- 8,237
Sherehe hiyo ilikuwa inafanyika katika boti moja katika mji uliopo karibu na mto wa Shigbanj, wakielekea katika nyumba ya biharusiwakati walipopigwa na radi hiyo. Wakazi wanasema kwamba radi kadhaa zilipiga kundi hilo. Kila mwaka mamia ya watu kusini mwa bara Asia hufariki kutokana na radi.
Mwaka 2016, Bangladesh ilitangaza radi kuwa janga wakati zaidi ya watu 200 walipofariki katika mwezi wa Mei pekee, ikiwemo watu 82 katika siku moja.
Wataalamu wanasema kwamba kukatwa kwa misitu kumesababisha ongezeko la radi kutokana na kutoweka kwa miti mingi mirefu ambayo huzuia radi.
Credit to BBC swahili