Bandari kavu Mbezi Beach

pembe

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
2,128
701
Kumezuka wimbi la kujenga bandari kavu huku mbezi beach. Sasa hivi ziko mbili zinajengwa! Cha kushangaza wamiliki hawa hawana vibali kutoka manispaa lakini wanajenga usiku na mchana! Ujenzi wenyewe ni imara kabisa hii ikimaanisha kuna wataalamu wa fani zote wanaosimamia hizo kazi. Kwa hiyo inamaanisha wataalamu hao wanavunja sheria kwani hakuna bango linaloonyesha kinachojengwa.

Viwanja hivi ni kwa ajili ya makazi na hakuna kibali cha wizara ya ardhi kilichotplewa kubadilisha matumizi ya ardhi. Athari za bandari kavu kwenye makzi ya watu ni kama uharibifu wa barabara na mabomba ya maji. Malori yenye kontena kukata nyaya za umeme na vibaka. Vilevile magari mazito husababisha nyufa kwenye nyumba na hasa hasa kuta za uzio (fence).

Je mamlaka husika ziko likizo au ndio rushwa mbele kwa mbele?
 
Kumezuka wimbi la kujenga bandari kavu huku mbezi beach. Sasa hivi ziko mbili zinajengwa! Cha kushangaza wamiliki hawa hawana vibali kutoka manispaa lakini wanajenga usiku na mchana! Ujenzi wenyewe ni imara kabisa hii ikimaanisha kuna wataalamu wa fani zote wanaosimamia hizo kazi. Kwa hiyo inamaanisha wataalamu hao wanavunja sheria kwani hakuna bango linaloonyesha kinachojengwa. Viwanja hivi ni kwa ajili ya makazi na hakuna kibali cha wizara ya ardhi kilichotplewa kubadilisha matumizi ya ardhi. Athari za bandari kavu kwenye makzi ya watu ni kama uharibifu wa barabara na mabomba ya maji. Malori yenye kontena kukata nyaya za umeme na vibaka. Vilevile magari mazito husababisha nyufa kwenye nyumba na hasa hasa kuta za uzio (fence). Je mamlaka husika ziko likizo au ndio rushwa mbele kwa mbele?
usiumize kichwa chako mkuu mamlaka watakua wanajuaa mpango mzima....tanzania hakuna kinachoshindikana
 
usiumize kichwa chako mkuu mamlaka watakua wanajuaa mpango mzima....tanzania hakuna kinachoshindikana

Kwa hiyo wananchi tukae kimya tu kwa vile mamlaka zinajua lakini hazichukui hatua?

Hii bandari kavu ya mtaa wa Simba ndio wanaanza kuchimba! Hii ya mtaa wa Chiriku wameanza kutumia kwa kulaza malori ya kubebea makontena na yanarudi hadi saa site usiku. Kwa hiyo kelele za sauti (noise pollution) ndio basi tena hakuna kulala. Je huu ndi utawala bora na maisha bora kwa kila mtanzania?

Hivi wananchi hatujui haki zetu au tumelogwa? Wengine wanasema mwenye nguvu mpishe na mwisho hata hapo unapoishi utashangaa unaondolewa kupisha bandari kavu!
 
Back
Top Bottom