The Mongolian Savage
JF-Expert Member
- Jul 5, 2018
- 6,191
- 13,614
Mzuka wanajamvi!
Hii dhana ya eti Cameroon majimbo mawili yanayoongea kiingereza North West na South West kujitenga kwasababu ya uonevu inasukumwa sana na Bambekee (Bamilekee).
Bambekee ni semi Bantuskabila maarufu sana Cameroon lenye maendeleo na elimu na pesa. Kwa kifupi ni matajari kama wachaga Tanzania na wakikuyu Kenya. Wanachokosa tu ni madaraka.
Cameroon ina makabila 240 yaliyogawanyika katika makundi matatu Bantus, Semi Bantus, Pygmies na Sudanese (Nitaleta uzi wa hizi kabila siku nyingine).
Cha kushangaza hawa Bambekee asili yao ni majimbo ya yanayoongea kifaransa ila walihamia kwa wingi katika majimbo mawili yanayoongea kiingereza ambalo moja limepakana na Nigeria South West lenye utajiri mkubwa wa mafuta.
Lakini makabila madogo asili ya haya majimbo ya Anglo phone yanayoongea kiingereza hawana shida ya kubaki Cameroun. Ila Bambekee wanawasukuma sana.
Bambekee wana nguvu sana na elimu. Wanajipenda sana na niwafanyabiashara. Wanapenda lugha yao sana na wanapenda kuoana wenyewe kwa wenyewe. Makabila mengine yote Cameroon wanawaogopa na wameapa kamwe hawatashikia madaraka.
Bambekee hata masokoni na kwenye maduka yao wako kivyaovyao na mda wote wanaongea lugha yao ambayo wanaipenda na kuithamini sana. Wengi wa Cameroon Diaspora ni Bambekee.
Bambekee wanamchukia sana Paul Biya. Paul Biya ni kabila la Fung jimbo la kusini mwa Cameroon South Province. Cha kushangaza akina Omar na Ally Bongo wa Gabon ni kabila moja na Paul Biya pia cha kushangaza zaidi Rais wa equatorial Guinea Teodoro Obiang ni kabila moja na Paul Biya ni mipaka tu imewatenga ambapo equatorial guinea ilikuwa koloni la Hispania.
Marekani, Uingereza pamoja na Ufaransa (kichinichini) wanawasupport Bambekee kuleta sintofahamu camerroon. Utashangaa kwanini Ufaransa naye kichinichini anawasupport Bambekee ni kwasababu wameshakosana na Paul Biya.
Makabila mengine Cameroon wanakubali ndio Paul Biya ni dikteta lakini wako radhi aendelee kutawala tu kuliko Bambekee washike madaraka.
Kwenye mpira Bambekee hawapo wengi sana ni Jeremy Njitap tu. Kabila la Bassa ndio wachezaji mpira ni wengi kama etoo Rodger milla na Rigobert Song.
Bambekee ndio tatizo kubwa la kutaka anglophone kujitenga wakisaidiwa na Marekani, Uingereza na Ufaransa ambaye anang'ata na kupuliza. Lakini siyo Wenyeji asili wa hayo majimbo yanayoongea kiingereza.
Source wa Cameroon
Senior JF international political correspondent and analysts
Hii dhana ya eti Cameroon majimbo mawili yanayoongea kiingereza North West na South West kujitenga kwasababu ya uonevu inasukumwa sana na Bambekee (Bamilekee).
Bambekee ni semi Bantuskabila maarufu sana Cameroon lenye maendeleo na elimu na pesa. Kwa kifupi ni matajari kama wachaga Tanzania na wakikuyu Kenya. Wanachokosa tu ni madaraka.
Cameroon ina makabila 240 yaliyogawanyika katika makundi matatu Bantus, Semi Bantus, Pygmies na Sudanese (Nitaleta uzi wa hizi kabila siku nyingine).
Cha kushangaza hawa Bambekee asili yao ni majimbo ya yanayoongea kifaransa ila walihamia kwa wingi katika majimbo mawili yanayoongea kiingereza ambalo moja limepakana na Nigeria South West lenye utajiri mkubwa wa mafuta.
Lakini makabila madogo asili ya haya majimbo ya Anglo phone yanayoongea kiingereza hawana shida ya kubaki Cameroun. Ila Bambekee wanawasukuma sana.
Bambekee wana nguvu sana na elimu. Wanajipenda sana na niwafanyabiashara. Wanapenda lugha yao sana na wanapenda kuoana wenyewe kwa wenyewe. Makabila mengine yote Cameroon wanawaogopa na wameapa kamwe hawatashikia madaraka.
Bambekee hata masokoni na kwenye maduka yao wako kivyaovyao na mda wote wanaongea lugha yao ambayo wanaipenda na kuithamini sana. Wengi wa Cameroon Diaspora ni Bambekee.
Bambekee wanamchukia sana Paul Biya. Paul Biya ni kabila la Fung jimbo la kusini mwa Cameroon South Province. Cha kushangaza akina Omar na Ally Bongo wa Gabon ni kabila moja na Paul Biya pia cha kushangaza zaidi Rais wa equatorial Guinea Teodoro Obiang ni kabila moja na Paul Biya ni mipaka tu imewatenga ambapo equatorial guinea ilikuwa koloni la Hispania.
Marekani, Uingereza pamoja na Ufaransa (kichinichini) wanawasupport Bambekee kuleta sintofahamu camerroon. Utashangaa kwanini Ufaransa naye kichinichini anawasupport Bambekee ni kwasababu wameshakosana na Paul Biya.
Makabila mengine Cameroon wanakubali ndio Paul Biya ni dikteta lakini wako radhi aendelee kutawala tu kuliko Bambekee washike madaraka.
Kwenye mpira Bambekee hawapo wengi sana ni Jeremy Njitap tu. Kabila la Bassa ndio wachezaji mpira ni wengi kama etoo Rodger milla na Rigobert Song.
Bambekee ndio tatizo kubwa la kutaka anglophone kujitenga wakisaidiwa na Marekani, Uingereza na Ufaransa ambaye anang'ata na kupuliza. Lakini siyo Wenyeji asili wa hayo majimbo yanayoongea kiingereza.
Source wa Cameroon
Senior JF international political correspondent and analysts