Balozi zetu bado hazitangazi Utalii na si Msaada

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Nimepata habari hizi muda na mtu mmoja kwa kuniandikia mail .Lakini pia huu ni uzoefu wangu wa miaka madhaa niliyo kuwa nakaa Ughabuni kwamba mabalozi wetu watumishi wao wamejaa dharau , majivuno na maneno machafu.Watu wamekuwa wakilalama kila mara na utawaona wanafanya kazi kama watasikia Rais ama Makamo wa rais anapita ama waziri vinginevyo hakuna lolote

Nimepata habari za watu 3 Watanzania , wazungu kibao wanalalamikia huduma katika balozi zetu .Mtu wa mwisho ameenda Ubalozini kwetu zaidi ya miezi 3 anaomba info za utalii wa Tanzania lakini hadi sasa hajapewa na kakata tamaa .Balozo zinafanya kazi kwa kujisikia na kejeli wakati wanaishi kwa pesa yetu .Balozi hizi sasa zinashindwa hata kumuunga mkono Rais kwa juhudi za kuitangaza Tanzania , Utalii na vivutio vyake .

JK kwanza anza na Japan ujue kuna shida gani .Ukitaka ushahidi ninao na sasa nitakupe skendo za kila Balozi na hasa kwenye kuitangaza Nchi .Hawakusaidii wewe wala mimi wala Nchi yetu wao wana maringo yako na kujivuta vuta .

Ni kweli Ubalozi wa Japan hauna posters wala DVD za Utalii hadi Wajapan wanaaanza ku haha kutafuta info kivyao ?
 
Hakuna watu wenye habari za balozi zetu hapa jamani ? Ama aliye karibu na Membe amweleze ?
 
nadhani ni muhimu kujua kama balozi zimewasiliana
na taasisi husika na kuomba machapisho, vipeperushi
na hata dvd zinazohusu utalii. kama hazijafanya hivyo
hayo ni mapungufu/uzembe wa balozi zetu. kama
balozi zimeomba taasisi husika na hizo taasisi hazija
wajibika basi taasisi huzika zitakuwa hazijatimiza wajibu
wao na zimefanya uzembe.

je hizo taasis husika zimefanya juhudi zozote za kuwasiliana
na kutuma hizo taarifa kwa balozi zetu na kisha balozi
zetu zikarudisha hizo taarifa au kukataa?

je wizara ya mambo ya nje inao mfuko wa kutengeneza
vipeperushi, machapisho, filamu n.k. za kutangaza utalii
na wameshindwa kutumia huo mfuko/bajeti?

kweli balozi zetu zinaendeshwa kwa kodi zetu, je kuna mtu
anayejua kama hizi balozi zinapelekewa hiyo mishahara kila
mwezi au kuna wakati jamaa wanakaa bila mishahara kwa
miezi zaidi ya miwili? mimi nafahamu kuna wakati maafisa
wa ubalozi walikuwa wanakaa bila mishahara hata kwa miezi
mitatu. sasa pengine huko kuzembea kwa hao maofisa kunatokana
na mawazo ya kutokuwa na mishahara?

dharau, kujiona n.k. hizo ni hulka za baadhi ya watu. naamini
kwenye balozi zetu wapo watu wenye ubinaadamu sana tu.
 
Machapisho yana kwenda kote ndiyo jambo mojawapo ambalo balozi zinahusika nazo .Kwa taarifa yako ni kwamba kila Ubalozi una mtu wa kushughulila na tourism.Mishahara ni soo hapa naongea nawe kuna balozi hawajapata mishahara na hata mambo yao ya likizo yako on hold .Nimeuliza wanasema hakuna pesa na hata bills kulipa ni shida lakni bado watu wana vijisenti na Serikali na hata watumishi wana njaa .

Lakini wakiwa ofisini lazima kusimamia kazi zao maana waliweka mkataba na kama wanagoma basi watangaze .Tabia za njoo kesho zinachosha sana kila ni tourism info na wageni wanataka kuja Tanzania .Je hawaoni wanajinyima mishara wenyewe ? maana serikal ikusanye walipwe wao .

Naomba Ubalozi wa Japan umulikwe sasa .Kuna shida pale kubwa kwenye Dept ya Utalii .
 
Balozi Zetu hazina budget/Fedha za kutosha

Inatakiwa Serikali iwekeze sana kwenye balozi kama Marekani, Urusi, UK, German, Spain, Saudi Arabia, China na France.

Kuongeza wafanyakazi kama Tourism Consultants, Lawyers and Economists

Kwa Sasa waanze na Tourism Consultants

Serikali iwekeze kwenye Balozi na itavuna pesa mingi sana...Na hakuna kuibiwa kama Madini
 
Kama waliyo shindwa uchaguzi wa ubunge na uchaguzi ndani ya chama wanapewa ubalozi kama fadhila wht fo you expect,
Balozu anatakiwa kuwa na sifa ya kusaidia raifa katika vita ya kiuchumi kakini tz mavalozi ni wale walioshindwa kuchaguliwa na wananchi kupewa mapumziko nje ya nchi.
 
Jukumu la kutangaza nchi sio la balozi pekee, hata wananchi tunatakiwa kutangaza nchi yetu. Badala ya kushirikiana na majambazi na matapeli kuiba rasilimali zetu tuwekeze muda kwa kulifanyia taifa letu mambo ya msingi kama hayo.
 
Jukumu la kutangaza nchi sio la balozi pekee, hata wananchi tunatakiwa kutangaza nchi yetu. Badala ya kushirikiana na majambazi na matapeli kuiba rasilimali zetu tuwekeze muda kwa kulifanyia taifa letu mambo ya msingi kama hayo.

Wananchi na wafanyabiashara wanatimiza wajibu sana kuliko TTB hata Serikali kutangaza nchi. Wizara ya Mali asili na Utalii ndio hawajui biashara ya Utalii na wamezubaa.

Wananchi na wafanyabiashara wanalipa kodi, wanalipa Tourism development na kodi nyingine....Ni Aibu hata zile pesa za Tourism development, serikali imezipeleka kwenye matumizi mengine....

Hii pesa ya Tourism development (inalipwa na Tour operators/Hotels) peke yake inatosha kuweka Tour consultants kila balozi, especially balozi kubwa kubwa zenye soko la utalii

stroke-----Tafuta muda ujifunze kidogo....Nenda hata TTB watakupa DATA...acha kuropoka....No Research...No right to speak..

better shut your mouth
 
Nimepata habari hizi muda na mtu mmoja kwa kuniandikia mail .Lakini pia huu ni uzoefu wangu wa miaka madhaa niliyo kuwa nakaa Ughabuni kwamba mabalozi wetu watumishi wao wamejaa dharau , majivuno na maneno machafu.Watu wamekuwa wakilalama kila mara na utawaona wanafanya kazi kama watasikia Rais ama Makamo wa rais anapita ama waziri vinginevyo hakuna lolote

Nimepata habari za watu 3 Watanzania , wazungu kibao wanalalamikia huduma katika balozi zetu .Mtu wa mwisho ameenda Ubalozini kwetu zaidi ya miezi 3 anaomba info za utalii wa Tanzania lakini hadi sasa hajapewa na kakata tamaa .Balozo zinafanya kazi kwa kujisikia na kejeli wakati wanaishi kwa pesa yetu .Balozi hizi sasa zinashindwa hata kumuunga mkono Rais kwa juhudi za kuitangaza Tanzania , Utalii na vivutio vyake .

JK kwanza anza na Japan ujue kuna shida gani .Ukitaka ushahidi ninao na sasa nitakupe skendo za kila Balozi na hasa kwenye kuitangaza Nchi .Hawakusaidii wewe wala mimi wala Nchi yetu wao wana maringo yako na kujivuta vuta .

Ni kweli Ubalozi wa Japan hauna posters wala DVD za Utalii hadi Wajapan wanaaanza ku haha kutafuta info kivyao ?
Waziri wa habari na utalii ndio anatakiwa kutayarisha hizo information na kuwapa mabalozi na sio balozi.

Ukija kwenye huduma za kibalozi kwa kweli hata Office za kibalozi zipo kimasikini sana tofauti na balozi za nje zilizopo hapa tz.
 
Jukumu la kutangaza nchi sio la balozi pekee, hata wananchi tunatakiwa kutangaza nchi yetu. Badala ya kushirikiana na majambazi na matapeli kuiba rasilimali zetu tuwekeze muda kwa kulifanyia taifa letu mambo ya msingi kama hayo.
Saa ngapi mkuu wakati ugaibuni bampa to bampa watu wapo kwenye box...
 
Wako Busy kuongeza mikodi tu

Hawajui kuwa Tourism ni Export product business (FOREX income)
 
Back
Top Bottom