Mdakuzi
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 3,459
- 4,229
Hivi juzi kati nilisikia Anti Ezekiel na Jacob Steven au JB walitangazwa kuwa mabalozi wa ving'amuzi vya Zuku, lakini kwa haya mambo yanayooneshwa na mabalozi hawa kwenye matamasha ya Fiesta, sidhani kama kunaiweka pazuri bidhaa hiyo.
Tangu kuanza matamasha hayo mabalozi hawa wamekuwa wakipanda majukwaani huku wakiwa hoi kwa vilevi na mbaya zaidi Anti amekuwa akikata mauno yake kwa mtindo wa kuonesha kichupi chake au makalio yake.
Nadhani huu ni wakati wa watoaji wa ving'amuzi vya Zuku kujiuliza kama uamuzi wa kutoa ubalozi kwa wasanii hao ulikuwa sahihi.