nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Tuesday, 21 June 2011 19:41 newsroom
NA HAMIS SHIMYE
BALOZI wa Tanzania nchini Malaysia, Abdul Sisco Mtiro, leo atahojiwa na Baraza la Maadili, kutokana na kutowasilisha tamko la mali na madeni kwa Tume Maadili ya Viongozi wa Umma.
Tangazo lililotolewa jana na tume, lilisema balozi huyo ataanza kujitetea leo asubuhi katika ukumbi wa Karimjee, mjini Dar es Salaam. Sisco atatoa utetezi mbele ya jopo la majaji wa baraza hilo, linaloongozwa na Mwenyekiti Jaji mstaafu, Damian Lubuva.
Baraza hilo jana lilimhoji Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Charles Ochere, kutokana na kushindwa kuwasilisha tamko la mali na madeni kwa tume ya maadili.
Akitoa utetezi, Ochere alisema alishindwa kujaza fomu hizo kutokana na kuchaguliwa kuwemo katika tume ya kuchunguza upotevu wa sh. milioni 500 uliotokea ndani ya halmashauri hiyo.
Nimekuwa nikijaza fomu vizuri tangu mwaka 2005 hadi 2008, lakini 2009 nilishindwa kujaza kutokana na kuwepo ndani ya tume, alisema. Kutokana na hilo, Mwanasheria wa tume, Hassan Mayunga, alidai hoja za mwenyekiti huyo hazina mantiki kwa kuwa ni za hisia.
Jaji Lubuva alisema baraza litatoa uamuzi baada ya kupitia utetezi huo.
NA HAMIS SHIMYE
BALOZI wa Tanzania nchini Malaysia, Abdul Sisco Mtiro, leo atahojiwa na Baraza la Maadili, kutokana na kutowasilisha tamko la mali na madeni kwa Tume Maadili ya Viongozi wa Umma.
Tangazo lililotolewa jana na tume, lilisema balozi huyo ataanza kujitetea leo asubuhi katika ukumbi wa Karimjee, mjini Dar es Salaam. Sisco atatoa utetezi mbele ya jopo la majaji wa baraza hilo, linaloongozwa na Mwenyekiti Jaji mstaafu, Damian Lubuva.
Baraza hilo jana lilimhoji Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Charles Ochere, kutokana na kushindwa kuwasilisha tamko la mali na madeni kwa tume ya maadili.
Akitoa utetezi, Ochere alisema alishindwa kujaza fomu hizo kutokana na kuchaguliwa kuwemo katika tume ya kuchunguza upotevu wa sh. milioni 500 uliotokea ndani ya halmashauri hiyo.
Nimekuwa nikijaza fomu vizuri tangu mwaka 2005 hadi 2008, lakini 2009 nilishindwa kujaza kutokana na kuwepo ndani ya tume, alisema. Kutokana na hilo, Mwanasheria wa tume, Hassan Mayunga, alidai hoja za mwenyekiti huyo hazina mantiki kwa kuwa ni za hisia.
Jaji Lubuva alisema baraza litatoa uamuzi baada ya kupitia utetezi huo.